Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza kujitayarisha tangu sasa ili kuishi mu dunia ya muzuri sana yenye iko karibu

Dunia Paradiso Iko Karibu!

Dunia Paradiso Iko Karibu!

Mungu aliumba dunia juu watu wenye haki waishi milele ndani yake. (Zaburi 37:29) Alitia mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, mu bustani ya Edeni na aliwapatia wao na watoto wao daraka ya kuilima na kuitunza.​—Mwanzo 1:28; 2:15.

Leo, dunia iko tofauti kabisa na dunia Paradiso yenye Mungu aliumba. Hata vile Mungu hayabadilisha mawazo yake. Atatimiza namna gani kusudi yake? Kama vile habari zenye zilitangulia zilionyesha, Mungu hataharibu dunia, hii planete yetu. Lakini, ataacha watu wazuri waishi ndani. Wakati Mungu atatimiza ahadi zake, hali itakuwa namna gani ku dunia?

Serikali yenye itatawala dunia yote

Hivi karibuni, wakati serikali ao guvernema ya mupya ya Mungu itaanza kutawala wanadamu wote, dunia itakuwa fasi ya muzuri kwenye watu wanaweza kuishi pamoja kwa upatano na kufanya kabisa kazi ya muzuri. Mungu alichagua Yesu Kristo kuwa mutawala wa dunia yote. Leo, watawala wengi hawahaingaikie kabisa watu. Lakini Yesu yeye iko tofauti nao, juu atakuwa anafanyia watu mambo ya muzuri tu. Atatawala kwa upendo, na atakuwa Mufalme mwema, mwenye huruma na haki.​—Isaya 11:4.

Watu wote mu dunia watakuwa na umoja

Mu dunia mupya watu hawatagawanyika mu taifa ao kabila. Wanadamu wote watakuwa na umoja. (Ufunuo 7:9, 10) Watu wote wenye kuishi ku dunia watamupenda Mungu na majirani wao. Tena watatumika kwa amani ili kutimiza kusudi ya Mungu ya kulinda dunia, makao yao.​—Zaburi 115:16.

Mazingira itakuwa ya muzuri

Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia, Muumbaji atatosha misiba yote ya asili. (Zaburi 24:1, 2) Yesu alitupatia tu wazo kidogo ya nguvu yenye Mungu alimupatia kwa kutuliza upepo mukali. (Marko 4:39, 41) Chini ya utawala wa Kristo hakuna mwanadamu atakuwa na wasiwasi juu ya misiba ya asili. Ufalme wa Mungu utarudisha amani kati ya wanadamu na wanyama lakini pia utafanya mazingira ikuwe ya muzuri sana.​—Hosea 2:18.

Afya kamilifu na chakula mingi

Kila mutu atakuwa na afya kamilifu. Hakuna mwenye atagonjwa, kuzeeka ao kufa. (Isaya 35:5, 6) Watu watafurahia fasi ya muzuri na yenye kuwa safi sawa ile yenye Adamu na Eva walifurahiaka mu bustani ya Edeni. Na sawa vile mu bustani ya Edeni, mu dunia mupya, udongo utatosha chakula mingi na wanadamu wote mu dunia watakuwa na chakula mingi sana. (Mwanzo 2:9) Sawa vile Israeli, yenye ilikuwaka taifa ya Mungu, kila mutu katika Paradiso ‘atakula mukate [wake] na kushiba.’​—Mambo ya Walawi 26:4, 5.

Kutakuwa amani na usalama ya kweli

Chini ya utawala wa Mungu watu wote wataishi kwa amani na watatendeana muzuri sana kati yao. Hakutakuwa vita, hakuna mwenye atatumia mamlaka yake mubaya na kila mutu atakuwa na yenye iko nayo lazima. Biblia inaahidi hivi: “Watakaa, kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini, na hakuna mutu mwenye atawaogopesha.”​—Mika 4:3, 4.

Kila mutu atakuwa na fasi ya muzuri ya kuishi na kazi ya muzuri

Kila familia itakuwa na nyumba ya muzuri na hawatakuwa na wasiwasi ya kuipoteza na kazi yote yenye watafanya itakuwa na matokeo ya muzuri. Sawa vile Biblia inasema, wale wote wenye wataishi mu dunia mupya “hawatafanya kazi ya jasho ya bure.”​—Isaya 65:21-23.

Watu watapata elimu ya muzuri zaidi

Biblia inaahidi hivi: “Dunia hakika itajaa ujuzi juu ya Yehova.” (Isaya 11:9) Watu wenye wataishi mu dunia mupya watajifunza hekima yenye haina mwisho ya Muumbaji wao Yehova na watajifunza juu ya mambo ingine ya muzuri yenye aliumba. Hawatatumia ile ujuzi yenye watapata juu ya kutengeneza bunduki ao juu ya kutendea wanadamu wengine mubaya. (Isaya 2:4) Kuliko kufanya vile, watajifunza namna ya kuishi kwa amani na wengine na namna ya kulinda dunia.​—Zaburi 37:11.

Uzima wa milele

Mungu alitayarisha dunia yetu kwa uangalifu sana juu kila siku tufurahie kabisa maisha. Alipenda wanadamu waishi milele juu ya dunia. (Zaburi 37:29; Isaya 45:18) Juu ya kutimiza ile kusudi yake, Mungu “atameza kifo milele.” (Isaya 25:8) Biblia inaahidi hivi: “Kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” (Ufunuo 21:4) Mungu atapatia wanadamu wote, ni kusema, wale wenye ataokoa wakati ataharibu hii dunia ya mubaya na wengine wengi wenye atafufua mu dunia mupya, nafasi ya kuishi milele.​—Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.

Tayari mamilioni ya watu wako wanajitayarisha ili waishi chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu wenye uko karibu sana. Hata kama hawakamilike, tayari wako wanajikaza kuwa aina ya watu wenye Mungu anapenda waishi mu dunia yake mupya. Wanafanya vile namna gani? Kwa kujifunza juu ya Yehova Mungu na juu ya mwenye alituma, Yesu Kristo.​—Yohana 17:3.

Unaweza kupata habari zaidi kuhusu nini unaweza kufanya ili kuokoka wakati hii dunia itaharibiwa na kuishi mu dunia ya muzuri sana yenye iko karibu. Uombe Shahidi moja wa Yehova ajifunze Biblia pamoja na weye kwa njia ya mazungumuzo mu kitabu Furahia Maisha Milele!