Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hii Dunia Itaharibika?

Hii Dunia Itaharibika?

Pengine unajua kama Biblia inasema kutakuwa mwisho wa dunia. (1 Yohana 2:17) Ile mwisho, ni mwisho ya wanadamu? Je, hii planete yetu, itakuwaka fasi kwenye hakuna uzima tena, ao itaharibiwa lote?

JIBU YA BIBLIA KU ILE MAULIZO YOTE MBILI NI HAPANA!

Ni nini haitaharibiwa?

WANADAMU

Mambo Biblia inasema: Mungu “hakuumba [dunia] tu bila sababu, lakini aliifanya ili ikaliwe na watu.”​—ISAYA 45:18.

DUNIA, PLANETE YETU

Mambo Biblia Inasema: “Kizazi kinapita, na kizazi kinakuja, lakini dunia inadumu milele.”​—MUHUBIRI 1:4.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Kulingana na Biblia, dunia haitaharibiwa hata siku moja, itaendelea kuikaliwa. Sasa, mwisho wa dunia njo nini?

WAZA KIDOGO: Biblia inalinganisha mwisho wa dunia yenye kuja na mambo yenye ilitokea mu siku za Noa. Ile wakati, dunia “ilijaa jeuri.” (Mwanzo 6:13) Lakini, Noa alikuwa mwenye haki. Njo maana, Mungu alilinda Noa na familia yake, lakini aliharibisha watu wote wabaya kupitia garika ao mvua kubwa. Ikizungumuzia mambo yenye ilitokeaka ile wakati, Biblia inasema hivi: “Ulimwengu (ao, dunia) wa wakati huo, uliharibiwa kwa garika ya maji.” (2 Petro 3:6) Ile ilikuwa mwisho wa dunia ya ile wakati. Lakini, nini njo iliharibiwa? Haiko dunia, hii planete yetu, lakini ni wanadamu wabaya wenye walikuwa wanaishi mu dunia. Kwa hiyo, wakati Biblia inazungumuzia mwisho wa dunia, haipende kusema kama ni kuharibiwa kwa hii planete yetu. Lakini inazungumuzia njo mwisho wa watu wabaya wenye kuishi ku dunia na mwisho wa mambo yote ya mubaya yenye kuwa mu hii dunia.

Nini njo haitakuwa tena?

MAGUMU NA UBAYA

Mambo Biblia inasema: “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena; utaangalia mahali walikuwa, nao hawatakuwa pale. Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”​—ZABURI 37:10, 11.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Garika ya wakati wa Noa, haikumaliza lote ubaya wote. Kisha garika, mara ingine tena watu wabaya walifanya maisha inakuwa mubaya sana kwa wengine. Hata vile, hivi karibuni, Mungu atamaliza matendo yote ya mubaya. Kama vile muandikaji mumoja wa zaburi alisema: “Waovu hawatakuwa tena.” Mungu atamaliza matendo yote ya mubaya kupitia Ufalme wake, ni kusema, serikali ao guvernema yenye itatawala wanadamu wote waaminifu wenye watakuwa hapa ku dunia. Ile serikali, itatawala na iko mbinguni.

WAZA KIDOGO: Wale wenye wako wanaongoza dunia leo, watafurahi kuunga mukono Ufalme wa Mungu? Biblia inasema hapana. Watapinga Ufalme wa Mungu. (Zaburi 2:2) Ile itakuwa na matokeo gani? Ufalme wa Mungu utaondoa serikali zote za wanadamu na “Ufalme huo peke yake utasimama milele.” (Danieli 2:44) Lakini, juu ya nini utawala wa wanadamu unapaswa kuondolewa?

TUNAPENDA​—Mwisho wa utawala wa wanadamu

Mambo Biblia inasema: “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—YEREMIA 10:23.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Wanadamu, hawakuumbwa na uwezo wa kujiongoza wao wenyewe. Hawaongozake watu wengine muzuri, na hawana uwezo wa kumaliza kabisa magumu yao.

WAZA KIDOGO: Kitabu moja inaonyesha kama inaonekana serikali zote hazina “uwezo wa kumaliza umaskini, njaa, magonjwa, misiba ya asili, vita na jeuri.” Kisha ile kitabu inasema tena hivi: “Watu fulani . . . wanaamini kama ni serikali moja tu yenye kutawala dunia yote njo inaweza kumaliza ile magumu yote.” (Britannica Academic) Lakini, hata kama serikali za wanadamu zote zinaungana pamoja, dunia itaendelea tu kutawaliwa na wanadamu wenye ni watenda-zambi na wenye hawana uwezo wa kumaliza magumu yote yenye tunatoka kutaja. Ufalme wa Mungu, njo serikali moja tu yenye iko na nguvu ya kumaliza lote magumu yote yenye iko hapa ku dunia.

Kwa hiyo, kulingana na Biblia, mwisho wa hii dunia haiko jambo yenye watu wazuri wanapaswa kuogopa. Lakini, ni jambo ya muzuri yenye tunapaswa kuchunga kwa hamu, juu Mungu atatosha hii dunia na kutuletea dunia ya mupya!

Ile, itatokea wakati gani? Habari yenye kufuata italeta jibu ya Biblia.