Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hakuna Mwenye Anaweza Kuepuka Kifo

Hakuna Mwenye Anaweza Kuepuka Kifo

WAZIA uko unafuata video kuhusu mutu fulani mwenye kujulikana, pengine ni muchezaji wa muziki mwenye unapendaka sana. Inaanza kwa kuonyesha maisha yake ya utoto wakati iko anajifunza namna ya kupiga chombo fulani cha muziki, na namna anajizoeza mara mingi. Kisha unamuona katika maonyesho ya muziki, anaanza kuenda mu inchi mingi, na kisha anakuwa mutu mwenye kujulikana sana mu dunia yote. Lakini bila kukawia, video inamalizika kwa kuonyesha vile anazeeka na kufa.

Ile video haiko ya kuwazia; ni hadisi ya kweli yenye kuonyesha mutu mwenye aliishi kabisa lakini mwenye amekwisha kufa. Ikuwe ule mutu alikuwa muchezaji wa muziki, mwanasayansi, muchezaji wa muchezo fulani, ao mutu mwingine mwenye kujulikana sana, hali ni ileile. Pengine ule mutu alifanya mambo mingi, lakini angeweza kufanya mambo mingi zaidi kama hangezeeka na kufa.

Hata kama ile inahuzunisha, ni hali yenye itapata kila mumoja wetu. (Muhubiri 9:5) Hata tujikaze namna gani, tutafikia kuzeeka na kufa. Haiko tu ile, maisha yetu inaweza kufupishwa na aksidenti ao ugonjwa fulani hatari. Kama vile Biblia inaonyesha, tuko kama kunguku ya asubui yenye “inatokea kwa wakati kidogo na kisha inapotea.”​—Yakobo 4:14.

Juu hatujue namna maisha yetu itakuwa kesho, watu fulani wanafuata maisha ya “tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.” (1 Wakorinto 15:32) Lakini watu wanachagua maisha ya vile, juu wanajua kama wanaweza kufa wakati wowote na juu hawana tumaini kwa ajili ya wakati wenye kuja. Wakati fulani mu maisha, zaidi sana wakati unapatwa na magumu, unaweza kujiuliza, ‘Hakuna maisha ingine?’ Ni wapi kwenye unaweza kupata jibu?

Leo, watu mingi wanawaza kama sayansi inaweza kuleta majibu. Maendeleo katika mambo ya sayansi na matunzo imefanya iwezekane kuishi wakati murefu. Na wanasayansi fulani wako wanatafuta namna ya kusaidia watu waishi wakati murefu zaidi. Wapate matokeo ya muzuri ao hapana, tunaendelea kujiuliza hivi: Juu ya nini watu wanazeeka na kufa? Kuko tumaini kuwa adui wetu kifo hatakuwa tena? Habari zenye kufuata zitazungumuzia ile maulizo, na zitajibu ulizo hili: Hakuna Maisha Ingine?