Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Tunazeeka na Kufa?

Juu ya Nini Tunazeeka na Kufa?

MUNGU hakuumba wanadamu ili wakufe. Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, walikuwa na akili na mwili wenye kukamilika wakati waliumbwa; wangelikuwa wazima mupaka leo. Tunaona ile waziwazi wakati tunachunguza mambo yenye Yehova alimuambia Adamu kuhusu muti fulani wenye ulikuwa mu bustani ya Edeni.

Mungu alimuambia Adamu hivi: “Siku yenye utakula matunda [ya ule muti], hakika utakufa.” (Mwanzo 2:17) Ile amri haingekuwa na maana kama Adamu alipaswa tu kuzeeka na kufa. Adamu alijua kama hangekula matunda ya ule muti, angeendelea kuishi.

IMUNGU HAKUUMBA WANADAMU ILI WAKUFE

Adamu na Eva hawakuwa na lazima ya kula matunda ya ule muti ili waendelee kuishi; juu katika bustani, kulikuwa miti mingi yenye kuzaa matunda. (Mwanzo 2:9) Kuepuka kula matunda ya ule muti kungeonyesha kama Adamu na Eva wanamutii Ule mwenye aliwapatia uzima. Kungeonyesha pia kama wanatambua kuwa Mungu njo iko na haki ya kuwaambia kile wanapaswa kufanya.

JUU YA NINI ADAMU NA EVA WALIKUFA?

Ili kuelewa ni juu ya nini Adamu na Eva walikufa, tunapaswa kuchunguza mazungumuzo fulani yenye imekuwa na matokeo juu yetu. Shetani Ibilisi alitumia nyoka ili kusema uongo wenye kuumiza. Biblia inasema hivi: “Basi nyoka alikuwa muangalifu kuliko wanyama wote wa pori wenye Yehova Mungu alikuwa amefanya. Kwa hiyo, akamuuliza mwanamuke: ‘Je, ni kweli kwamba Mungu alisema hamupaswe kula matunda ya kila muti wa bustani?’”​—Mwanzo 3:1.

Eva akamujibu hivi: “Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu matunda ya muti wenye kuwa katikati ya bustani Mungu amesema: ‘Hamupaswe kuyakula, hapana, hamupaswe kuyagusa; mukifanya vile mutakufa.’” Kisha nyoka akamuambia: “Hakika hamutakufa. Kwa sababu Mungu anajua kwamba siku ileile yenye mutakula matunda ya muti huo, macho yenu yatafunguliwa na mutakuwa kama Mungu; mukijua mema na mabaya.” Kwa kusema vile, Shetani alionyesha kama Yehova ni muongo, na kama alificha wazazi wetu wa kwanza jambo fulani la muzuri.​—Mwanzo 3:2-5.

Eva aliamini mambo yenye alisikia. Aliangalia ule muti. Aliona kuwa ule muti ulikuwa wenye kupendeza macho. Alikaribia ule muti, akakamata matunda yake, na akaanza kula. Biblia inaongeza hivi: “Kisha, wakati alikuwa pamoja na bwana yake, akamupatia pia, naye akaanza kuyakula.”​—Mwanzo 3:6.

Mungu alimuambia Adamu hivi: “Siku yenye utakula matunda yake, hakika utakufa.”​—MWANZO 2:17

Bila shaka Mungu aliumia sana kuona vile watoto wake wenye alipenda wanakosa kumutii kimakusudi! Alifanya nini? Yehova alimuambia Adamu hivi: “Utarudia katika udongo, kwa maana ulitoshwa katika udongo. Kwa maana wewe ni mavumbi na utarudia katika mavumbi.” (Mwanzo 3:17-19) Kama vile tu Mungu alisema, “siku zote za maisha ya Adamu zikakuwa miaka mia kenda makumi tatu (930), kisha akakufa.” (Mwanzo 5:5) Adamu hakuenda mbinguni ao kuenda mahali pengine penye kufanana na mbinguni. Hakuwa anaishi mbele Yehova amuumbe kutoka katika mavumbi ya udongo. Kwa hiyo wakati alikufa, alipoteza uzima wake na mwili wake ukakuwa tena mavumbi. Hakuishi tena. Mubaya kabisa!

JUU YA NINI HATUKO WAKAMILIFU?

Kwa sababu Adamu na Eva walikosa kumutii Mungu kimakusudi, walipoteza ukamilifu na tumaini lao la kuishi milele. Hali yao ilibadilika; walipoteza ukamilifu na wakakuwa wenye zambi. Lakini zambi yenye walifanya kwa kukosa kumutii Mungu haikuwa na matokeo juu yao wenyewe tu. Waliambukiza watoto wao hali yao yenye zambi. Waroma 5:12 inasema hivi: “Kupitia mutu mumoja [Adamu] zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”

Biblia inafananisha zambi na kifo na “kitambaa chenye kufunika vikundi vyote vya watu na kifuniko chenye kimesukwa juu ya mataifa yote.” (Isaya 25:7) Kile kitambaa chenye kufunika wanadamu kiko kama kunguku yenye sumu yenye hakuna mutu anaweza kuponyoka. Kwa kweli, “katika Adamu wote wanakufa.” (1 Wakorinto 15:22) Ulizo lenye tunajiuliza na lenye mutume Paulo alijiuliza, ni hili: “Ni nani ataniokoa kutoka katika mwili wenye unapatwa na kifo hiki?” Kuko mwenye anaweza kufanya vile?​—Waroma 7:24.