Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo

Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo

WAKATI wenye kuja, hakuna mutu mwenye atagonjwa, kuzeeka, ao kufa. Wewe pia unaweza kuwa na maisha ya vile! Lakini leo, maisha inajaa magumu na matatizo. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe na maisha yenye furaha leo? Biblia iko na mashauri yenye inaweza kukusaidia ukuwe mwenye furaha na ujisikie mwenye kutosheka hata leo. Tuzungumuzie matatizo fulani yenye kutokea mu maisha na tuone namna Biblia inaweza kutusaidia.

NAMNA YA KUWA MWENYE KUTOSHEKA

Shauri la Biblia: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.”​Waebrania 13:5.

Leo, kuko vitu mingi vyenye watu wanasema kama tunapaswa kuwa navyo. Lakini Biblia inasema kama tunaweza ‘kutosheka na vitu vya sasa.’ Namna gani?

Epuka “kupenda feza.” Juu tu ya “kupenda feza,” watu wanaweza kutia katika hatari afya yao, familia, urafiki, ao hata kupoteza mwenendo na heshima yao. (1 Timoteo 6:10) Lakini kufanya vile ni kujidanganya! Ku mwisho, mwenye kupenda mali “hatashiba.”​—Muhubiri 5:10.

Ona watu kuwa wa maana kuliko vitu. Ni kweli kwamba vitu vya kimwili vinaweza kutusaidia. Lakini haviwezi kutupenda ao kutushukuru; ni watu tu njo wanaweza kufanya vile. Kuwa na “rafiki wa kweli” kunaweza kutusaidia tukuwe wenye kutosheka katika maisha.​—Mezali 17:17.

TUNAWEZA KUFANYA MAISHA YETU IKUWE YENYE FURAHA HATA LEO KWA KUFUATA MASHAURI YA BIBLIA

NAMNA YA KUVUMILIA WAKATI UKO MUGONJWA

Shauri la Biblia: “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri.”​Mezali 17:22.

Kama vile “dawa ya muzuri,” kuwa mwenye furaha kunaweza kutusaidia kuvumilia magonjwa. Lakini, namna gani tunaweza kuwa wenye furaha hata kama tuko wagonjwa?

Ukuwe mwenye shukrani. Kama tunakaza akili juu ya magumu yetu, tutaona “siku zote” kuwa tu za mubaya. (Mezali 15:15) Lakini Biblia inasema, ‘ujionyeshe kuwa mwenye shukrani.’ (Wakolosai 3:15) Ujifunze kufurahia mambo ya muzuri mu maisha, hata kama ni ya kidogo. Mwangaza wenye kupendeza wakati jua linashuka, upepo wenye kutuliza, sura yenye furaha ya mutu mwenye unapenda; ile mambo inafanyaka maisha ikuwe yenye kufurahisha.

Fanya mambo kwa faida ya wengine. Hata kama afya yetu haiko muzuri, tunaweza kupata “furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Matendo 20:35) Wakati wengine wanatushukuru kwa sababu tunajikaza kufanya jambo fulani, ile inafanya tujisikie wenye kutosheka, na inafanya tusahau kwanza magumu yetu. Tunaweza kufanya maisha yetu ikuwe muzuri zaidi kwa kusaidia wengine wafanye maisha yao kuwa ya muzuri zaidi.

NAMNA YA KUFANYA NDOA IKUWE YENYE NGUVU

Shauri la Biblia: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​Wafilipi 1:10.

Bibi na bwana wenye wanapitisha pamoja wakati kidogo tu wanaweza kuharibisha uhusiano wao. Njo maana ni jambo lenye hekima bibi na bwana watie ndoa yao pa nafasi ya kwanza; ni kusema, waione kuwa kitu cha maana zaidi mu maisha yao.

Mufanye mambo pamoja. Kuliko kila mutu kufanya mambo yake mwenyewe, mupange kufanya mambo pamoja. Biblia inasema hivi: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja.” (Muhubiri 4:9) Munaweza kupika chakula pamoja, kuenda ku shamba, kunywa kinywaji fulani, kufanya mazoezi ya mwili, ao kucheza muchezo fulani pamoja.

Onyesha kama unapenda mwenzako. Biblia inatia moyo bibi na bwana wapendane na kuheshimiana. (Waefeso 5:28, 33) Sura yenye furaha, kukumbatiana kwa upendo, ao zawadi ya kidogo vinaweza kusaidia sana ili ndoa ikuwe yenye nguvu. Lakini, ni bibi ao bwana yako tu njo mwenye unapaswa kuonyesha mapenzi.​—Waebrania 13:4.