Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, kurekebisha chembe za uriti kumesaidia kurefusha maisha ya watu?

Tamaa ya Wanadamu ya Kuishi Wakati Murefu

Tamaa ya Wanadamu ya Kuishi Wakati Murefu

“Nimeona kazi yenye Mungu amepatia wana wa binadamu wafanye. Amefanya kila kitu kuwa kizuri kwa wakati wake. Hata ametia umilele katika moyo wao.”​Muhubiri 3:10, 11.

ILE maneno ya zamani yenye hekima ya Mufalme Sulemani inaonyesha muzuri namna watu wanajisikia kuhusu uzima. Kwa mamia ya miaka, watu wametamani sana kuishi wakati murefu; pengine ni juu maisha ni ya mufupi na hakuna mwenye anaweza kuepuka kifo. Hadisi mingi za kweli na za kuwazia zinaonyesha kama, kwa miaka mingi watu wametafuta njia ya kusaidia watu waishi miaka mingi zaidi.

Tuzungumuzie Gilgameshi, mufalme wa Sumeria. Hadisi mingi za kuwazia zilizungumuzia maisha yake. Moja kati ya zile hadisi, yenye kupatikana mu Maandishi ya Gilgameshi inaonyesha kama, ule mufalme alifanya safari yenye hatari ili ajue namna ya kuepuka kifo. Lakini alishindwa kujua namna ya kuepuka kifo.

Katika Ulaya ya kuanzia miaka ya 500 K.K.Y.​— 1500 K.K.Y., fundi wa kutengeneza dawa iko katika chumba chake cha kufanyia kazi

Katika karne ya ine mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, mafundi wa kutengeneza dawa katika China walijaribu kutengeneza dawa fulani yenye waliamini kuwa inaweza kurefusha maisha. Walipata ile dawa kwa kuchanganya madini ya mercure na arsenic. Watu wanawaza kama ile dawa njo iliua watawala mingi wa China. Katika kipindi cha kuanzia miaka ya 500 K.K.Y. mupaka 1500 K.K.Y., mafundi fulani wa kutengeneza dawa katika Ulaya walijaribu kugeuza zahabu (ao, or) mu njia yenye ingeweza kufanya watu waweze kuikula. Waliamini kama juu zahabu haiharibikake, ingeweza kusaidia kurefusha maisha ya watu.

Leo, wanasayansi wenye kujifunza vitu vyenye kuishi na wenye kujifunza chembe za uriti wamejikaza sana ili wajue sababu yenye kuleta uzee. Kama vile tu wale wenye walitafuta dawa ya kurefusha maisha, bidii ya wale wanasayansi inaonyesha kama watu wangali wanatumaini sana kuwa wanaweza kupata njia yenye inaweza kuwasaidia wasizeeke na kufa. Lakini bidii yao imeleta matokeo gani?

MUNGU “AMETIA UMILELE KATIKA MOYO WAO.”​—MUHUBIRI 3:10, 11

KUTAFUTA SABABU ZENYE KUFANYA WATU WAZEEKE

Leo, wanasayansi wenye kujifunza chembe za mwili wa mwanadamu wametoa maelezo zaidi ya 300 ili kufasiria sababu zenye kufanya tuzeeke na kufa. Katika miaka ya hivi karibuni, wanasayansi wenye kujifunza molekuli wameweza kurekebisha chembe za uriti na protini (ao, protéines) ili kupunguza mwendo wa kuzeeka wa chembe za wanyama na za wanadamu. Ile maendeleo imechochea matajiri fulani wachangie feza ili kusaidia wanasayansi wajue “kile kinaletaka kifo.” Wale wanasayansi wamefanya nini?

Kujaribu kuongeza urefu wa maisha. Wanasayansi fulani wanawaza kama tunazeeka kwa sababu kuko jambo fulani lenye kufanyika ku télomères. Télomères ni sehemu zenye kuwa ku mwisho wa kromozome. Télomères zinalindaka habari zenye kuwa mu chembe za uriti wakati chembe zinatokeza chembe za mupya. Lakini, kila wakati wenye chembe zinatokeza chembe za mupya, télomères zinakuwa mufupi. Kisha wakati fulani, zile chembe zinaacha kutokeza chembe za mupya na mutu anaanza kuzeeka.

Elizabeth Blackburn, mwenye alipata tuzo ao zawadi ya Nobeli mu mwaka wa 2009, alivumbua pamoja na watu wenye alikuwa anatumika nao, kimengenya (ao, enzyme) yenye inasaidia télomères isifupike haraka; juu kufupika kwa télomères njo kunafanyaka chembe zizeeke. Lakini walikubali kama télomères hazisaidie wanadamu kuishi wakati murefu zaidi.

Kupanga upya chembe ni njia ingine yenye wanasayansi wanatumia ili kujaribu kuzuia uzee. Wakati chembe zetu zinashindwa kutokeza chembe za mupya kwa sababu zimezeeka, zile chembe zinaweza kutuma habari zenye hazifae ndani ya chembe zenye kukinga mwili; na ile inafanya mwili uvimbe, ukuwe na maumivu yenye kuendelea, na kuleta magonjwa. Hivi karibuni, wanasayansi katika Ufaransa walikamata chembe za watu wenye kuzeeka na kuzipanga upya; na wamoja kati ya wale wazee walikuwa na zaidi ya miaka 100. Profesa Jean-Marc Lemaître, kiongozi wa kikundi cha wale wenye walikuwa wanafanya utafiti, alisema kama kazi yao ilionyesha kuwa inawezekana “kubadilisha mwendo wa kuzeeka” kwa chembe.

JE, SAYANSI INAWEZA KUREFUSHA MAISHA YETU?

Wanasayansi mingi wanasema kuwa hata kama kuko njia mingi za kuzuia uzee, wanadamu hawataweza kuishi wakati murefu zaidi kuliko zamani. Ni kweli, tangu miaka ya 1800 watu wamesaidiwa kuishi miaka mingi. Lakini imekuwa vile zaidi sana juu watu wanaheshimia kanuni za usafi, wanakamata mipango ya muzuri juu ya kupiganisha magonjwa yenye kuambukiza, wanatumia dawa zenye kuua mikrobe, na dawa za kujikinga na magonjwa (ao, vaccins). Watu fulani wenye kujifunza chembe za uriti wanaamini kama urefu wa maisha ya mwanadamu umepunguka ao kuongezeka kidogo.

Musa, muandikaji mumoja wa Biblia, alisema maneno yenye kufuata kumepita karibu miaka 3 500: “Urefu wa maisha yetu ni miaka makumi saba (70), ao makumi munane (80) kama mutu iko na nguvu za pekee. Lakini imejaa taabu na huzuni; na inapita haraka, na tunaenda zetu.” (Zaburi 90:10) Hata kama mwanadamu amejikaza ili arefushe maisha yetu, maisha iko tu kama vile Musa alisemaka.

Tofauti na maisha ya mwanadamu, wanyama fulani wanaweza kuishi mamia ya miaka na miti fulani inaweza kuishi maelfu ya miaka. Wakati tunalinganisha urefu wa maisha yetu na wa viumbe vingine, tunaweza kujiuliza, ‘maisha yetu ni miaka 70 ao 80 tu?’