Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuliumbwa ili Tuishi Milele

Tuliumbwa ili Tuishi Milele

NI NANI mwenye hapendake kuishi maisha ya murefu na yenye furaha? Fikiria namna maisha ingekuwa muzuri ikiwa tungeishi milele kwa furaha na afya ya muzuri! Tungepitisha wakati mingi na watu wenye tunapenda, kuenda fasi mingi katika dunia, na tungejifunza kufanya mambo mingi yenye tunapendaka kufanya.

Ni mubaya kuwa na ile tamaa? Hapana! Biblia inatuambia kama Mungu alitia ile tamaa ndani yetu. (Muhubiri 3:11) Inasema pia kama “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Mungu anatupenda na hangeweza kutia ndani yetu tamaa ya kuishi milele ikiwa hatungeweza kuishi milele.

Ni wazi kuwa, hakuna mwenye anapendaka kufa. Kwa kweli, Biblia inasema kama kifo ni “adui” wetu wa mubaya sana. (1 Wakorinto 15:26) Wamoja wanakufa wakati wangali vijana; na wengine wanakufa kisha kuishi wakati mingi. Hata kama ni vile, kifo kitatupata sisi wote. Watu mingi wanaogopa wakati wanawaza juu ya kifo. Kuko siku ule adui ataharibiwa? Ile inawezekana kabisa?

SABABU ZA KUWA NA TUMAINI

Je, unaweza kushangaa kujua kama Mungu hakuumba wanadamu ili wakufe? Kitabu cha Biblia cha Mwanzo kinaonyesha wazi kama Mungu aliumba wanadamu ili waishi milele ku dunia. Wakati Yehova Mungu aliumba dunia, alitia ndani kila kitu chenye watu wako nacho lazima ili kuishi na kufurahia maisha. Kisha aliumba mwanaume wa kwanza, Adamu, na alimutia mu paradiso, ni kusema, bustani ya Edeni. Kisha kufanya vile, “Mungu akaona kila kitu chenye alikuwa amefanya, na angalia! kilikuwa kizuri sana.”​—Mwanzo 1:26, 31.

Adamu aliumbwa akiwa mukamilifu, kwa mufano wa Mungu. (Kumbukumbu la Torati 32:4) Eva, bibi ya Adamu, hakukuwa pia na kasoro ao kosa lolote; alikuwa na akili na mwili wenye kukamilika. Yehova aliwaambia hivi: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala, na mutawale samaki wa bahari na viumbe vyenye kuruka vya mbinguni na kila kiumbe chenye uzima chenye kutembea juu ya dunia.”​—Mwanzo 1:28.

Ili Adamu na Eva wafikie kujaza dunia, ile ingekamata wakati. Eva angekuwa na watoto, na wale watoto wangekuwa na watoto mupaka dunia ijae kama vile Mungu alipenda. (Isaya 45:18) Kama Mungu alipenda Adamu na Eva wajaze dunia, ingekuwa na maana ikiwa wangeishi tu ili kuona watoto wao na pengine wajukuu wao, bila kujionea vile dunia ingejaa?

Waza pia juu ya kazi yenye walipewa ya kutiisha wanyama. Mungu alimupatia Adamu kazi ya kupatia wanyama majina, na ile ingepaswa kukamata wakati mingi. (Mwanzo 2:19) Lakini ili aweze kuwatiisha alipaswa kujifunza juu ya wale wanyama na kujua namna ya kuwahangaikia. Ile ingeomba wakati mingi zaidi ili aweze kufanya vile.

Kwa hiyo, kazi yenye Mungu aliwapatia ya kujaza dunia na kutiisha wanyama inaonyesha kama Mungu aliumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza juu waishi wakati murefu zaidi. Kwa kweli, Adamu aliishi miaka mingi sana.

MUNGU ALIUMBA WANADAMU ILI WAISHI MILELE MU DUNIA PARADISO

WALIISHI MIAKA MINGI SANA

Adamu, miaka 930

Metusela, miaka 969

Noa, miaka 950

Leo, miaka 70-80

Biblia inaonyesha kama zamani wanadamu waliishi miaka mingi sana kuliko vile iko leo. Inasema hivi: “Siku zote za maisha ya Adamu zikakuwa miaka mia kenda makumi tatu (930).” Kisha, inataja wanaume wengine sita wenye waliishi zaidi ya miaka 900! Wale wanaume ni Seti, Enoshi, Kenani, Yaredi, Metusela, na Noa. Wote waliishi mbele ya Garika ya siku za Noa; na Noa mwenyewe aliishi miaka 600 mbele Garika ikuje. (Mwanzo 5:5-27; 7:6; 9:29) Ni nini ilifanya watu waishi miaka mingi vile?

Wale wanaume wote waliishi karibu na kipindi cha ukamilifu. Bila shaka ile njo sababu kubwa yenye ilifanya waishi miaka mingi. Lakini kuko upatano gani kati ya ukamilifu na kuishi miaka mingi? Na namna gani kifo kitaharibiwa? Ili kupata jibu, tunapaswa kwanza kuelewa ni juu ya nini tunazeeka na kufa.