Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Gani Adui Wetu Kifo Ataharibiwa?

Namna Gani Adui Wetu Kifo Ataharibiwa?

HATA kama wanadamu wote waliriti zambi na kifo kwa sababu ya kukosa kutii kwa Adamu na Eva, wazazi wetu wa kwanza, ile haikubadilisha kusudi la Mungu kwa ajili ya familia ya wanadamu. Fasi mingi katika Neno lake lenye kuandikwa, ni kusema, Biblia, Mungu ameonyesha mara mingi kama kusudi lake halijabadilika.

  • “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​Zaburi 37:29.

  • “Atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapanguza machozi kwenye nyuso zote.”​Isaya 25:8.

  • “Adui wa mwisho mwenye ataharibiwa ni kifo.”​1 Wakorinto 15:26.

  • “Kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​Ufunuo 21:4.

Namna gani Mungu “atameza kifo,” na ‘kuharibu’ ule adui? Kama vile tumeona, Biblia inasema waziwazi kama “wenye haki . . . wataishi milele.” Lakini inasema pia kama “hakuna mwenye haki katika dunia mwenye anafanya mema sikuzote na hafanyake zambi.” (Muhubiri 7:20) Ili kuharibu kifo, je, Mungu hataomba tena wanadamu wafuate kanuni zake? Ile haiwezekane! Hawezi hata kidogo kufanya vile, kwa sababu “Mungu . . . hawezi kusema uongo.” (Tito 1:2) Sasa, Mungu atafanya nini ili kutimiza kusudi lake lenye upendo, lenye alikuwa nalo wakati aliumba wanadamu?

MUNGU “ATAMEZA KIFO MILELE.”​—ISAYA 25:8

MUNGU ANAHARIBU KIFO KWA KULIPA BEI YA UKOMBOZI

Yehova Mungu alikamata mupango wenye upendo ili kukomboa wanadamu kutoka katika kifo, kwa kulipa bei ya ukombozi. Wakati Biblia inazungumuzia bei ya ukombozi, inazungumuzia kitu fulani chenye kuwa na samani ao bei ileile, chenye kinaombwa ili kulipa mambo yenye iliharibika ao ili kutimiza mambo yenye kuombwa na haki. Juu wanadamu wote ni watenda-zambi na wamehukumiwa kifo, Biblia inasema hivi waziwazi: “Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza hata kidogo kumukomboa ndugu yake wala kumupatia Mungu bei ya ukombozi kwa ajili yake, (bei ya ukombozi kwa ajili ya uzima wao ni yenye samani sana kiasi ya kwamba hawawezi hata kidogo kuipata).”​—Zaburi 49:7, 8.

Wakati mwanadamu mwenye hakamilike anakufa, anaweza tu kulipia hukumu ya zambi zake mwenyewe; hawezi kujikomboa yeye mwenyewe, wala hawezi kulipia zambi za mutu mwingine. (Waroma 6:7) Tulikuwa na lazima ya mutu mwenye alikuwa mukamilifu na mwenye hakuwa na zambi ili atoe uzima wake, hapana kwa ajili ya zambi zake mwenyewe, lakini kwa ajili ya zambi zetu.​—Waebrania 10:1-4.

Na ni vile kabisa njo Mungu alipanga mambo. Alituma Mwana wake, Yesu, kutoka mbinguni ili azaliwe ku dunia akiwa mwanadamu mukamilifu, na mwenye hana zambi. (1 Petro 2:22) Yesu alisema kama alikuja ili “atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Marko 10:45) Alikufa ili alipie zambi zetu na kutukomboa katika kifo ili tuweze kupata uzima.​—Yohana 3:16.

NI WAKATI GANI KIFO KITAHARIBIWA?

Leo, kama vile Biblia ilisema, tunaishi “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia,” na ile inaonyesha kama tunaishi “siku za mwisho” za huu ulimwengu. (2 Timoteo 3:1) Wakati “siku ya hukumu na ya uharibifu wa watu wenye hawamuogope Mungu” itaanza, ile itaonyesha kama siku za mwisho zimemalizika. (2 Petro 3:3, 7) Lakini watu wenye kumupenda Mungu wataokoka ule uharibifu na Mungu atawabariki kwa kuwapatia “uzima wa milele.”​—Matayo 25:46.

Yesu alikuja ili “atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”​—Marko 10:45

Mamilioni ya watu watakuwa na nafasi ya kuishi milele wakati watafufuliwa. Yesu alifufua mutu mwenye alikuwa amekufa wakati alitembelea muji wa Naini. Mujane mumoja alikuwa na mutoto mumoja tu mwanaume na ule mutoto alikuwa amekufa; Yesu ‘alimusikilia huruma,’ na alimufufua ili aishi tena. (Luka 7:11-15) Mutume Paulo alisema pia hivi: “Niko na tumaini kwa Mungu . . . kwamba kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” Tumaini hilo lenye nguvu, linaonyesha kama Mungu anawapenda sana wanadamu.​—Matendo 24:15.

Mamiliare ya watu wanaweza kungojea kwa hamu kuishi milele. Biblia inasema hivi: “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Ule wakati, kila mumoja wao atafurahi sana na kutiwa moyo wakati atajionea utimizo wa maneno ya mutume Paulo yenye iliandikwa kumepita miaka karibu 2 000, yenye inasema: “Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi uwezo wako wa kuumiza?” (1 Wakorinto 15:55) Kifo, adui mubaya sana wa wanadamu, atakuwa ameharibiwa!