Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Ni mwanadamu alianzisha dini?

WATU FULANI WANAAMINI kwamba ni mwanadamu alianzisha dini; wengine wanawaza kwamba Mungu anatumia dini ili kusaidia watu wamukaribie. Wewe unawaza namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Kuna “ibada [ao, dini] iliyo safi na isiyotiwa unajisi [ao, uchafu] kwa maoni ya Mungu wetu na Baba.” (Yakobo 1:27) Dini safi ao ya kweli inatoka kwa Mungu.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Ili tumupendeze Mungu, dini yetu inapaswa kutegemea kweli ya Biblia.—Yohana 4:23, 24.

  • Dini zenye kutegemea mawazo ya watu hazina faida yoyote.—Marko 7:7, 8.

Ni jambo la maana kuwa katika dini fulani?

UNAWEZA KUJIBU NINI?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Inalingana na hali

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja.” (Waebrania 10:24, 25) Mungu anataka waabudu wake wakusanyike pamoja katika kikundi chenye kupangwa muzuri.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Wale wenye wanaabudu Mungu wanapaswa kuungana katika imani.—1 Wakorintho 1:10, 11.

  • Wale wenye kuwa katika dini yenye Mungu anakubali wanafanya familia moja ya ndugu na dada duniani pote.—1 Petro 2:17.