Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | BIBLIA ILIOKOKA NAMNA GANI?

Sababu Gani Biblia Imeokoka

Sababu Gani Biblia Imeokoka

Biblia imeokoka. Ndiyo sababu unaweza kuipata na kuisoma leo. Na wakati unachagua tafsiri ya muzuri ya Maandiko, unaweza kuwa hakika kwamba unasoma Biblia yenye kupatana na maandishi ya kwanza. * Lakini, sababu gani kuna habari nyingi zenye kushangaza juu ya namna Biblia iliokoka hata kama kulikuwa hatari ya kuharibika, upinzani, na hatari ya kutaka kubadilisha kimakusudi ujumbe wake? Biblia iko na jambo gani la pekee?

“Sasa, niko hakika kwamba Biblia yenye niko nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu”

Wanafunzi wengi wa Biblia wamefikia kuwa na mawazo yenye mutume Paulo alikuwa nayo. Aliandika hivi : “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Wanaamini kwamba Biblia imeokoka kwa sababu Biblia tu ndiyo Neno la Mungu na kwa sababu Mungu amelinda Neno lake mupaka leo. Faizal, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza ya gazeti hili alifikia kuamua kuchunguza yeye mwenyewe mawazo yenye watu walisema juu ya Neno la Mungu kwa kujifunza Biblia. Mambo yenye alivumbua yalimushangaza. Kisha, alitambua kwamba Biblia haiunge mukono mafundisho mengi yenye dini nyingi zenye kujiita kuwa za Kikristo zinafundisha. Zaidi ya hilo, moyo wake uliguswa wakati alijifunza kusudi la Mungu juu ya dunia kama vile inaonyeshwa katika Neno Lake.

Anasema hivi: “Sasa, niko hakika kwamba Biblia yenye niko nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu. Tena, Mungu mwenye aliumba ulimwengu wote, ana uwezo wa kutupatia kitabu na kukilinda kwa ajili yetu. Kusema jambo lenye kuwa tofauti na hilo ni kuonyesha kama uwezo wa Mungu Mweza-Yote, uko na mipaka! Na mimi ni nani ili niseme kama uwezo wa Mungu uko na mipaka?”—Isaya 40:8.

^ fu. 3 Ona habari “Jinsi ya Kuchagua Tafsiri Nzuri ya Biblia” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2008.