Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

WIMBO 18 Tuko na Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

Bei ya Ukombozi Inatufundisha Nini?

Bei ya Ukombozi Inatufundisha Nini?

“Kwa jambo hili upendo wa Mungu ulifunuliwa.”1 YO. 4:9.

WAZO KUBWA

Mambo yenye bei ya ukombozi inatufundisha juu ya sifa za Yehova Mungu na za Yesu Kristo.

1. Juu ya nini ni jambo ya maana kwetu kufika ku Ukumbusho wa kila mwaka wa kifo ya Kristo?

 SIYE wote tunakubali kama zabihu ya ukombozi ni zawadi ya bei sana! (2 Ko. 9:15) Juu Yesu alitoa maisha yake ya kibinadamu kwa ajili yetu, tunaweza kuwa na urafiki wa karibu sana pamoya na Yehova Mungu. Tuko pia na tumaini ya kupata uzima wa milele. Inafaa kabisa tuonyeshe shukrani juu ya bei ya ukombozi na tumushukuru Yehova juu upendo wake ulimuchochea atupatie ile zawadi! (Ro. 5:8) Ili kutusaidia tuendelee kuonyesha shukrani na tuendelee kukamata kwa uzito bei ya ukombozi, Yesu alianzisha Ukumbusho wa kila mwaka wa kifo yake.—Lu. 22:19, 20.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Hii mwaka Ukumbusho utafanywa Siku ya Posho, tarehe 12, Mwezi wa 4, 2025. Ni wazi kama siye wote tuko napanga kuenda ku ile tukio. Mu kipindi ya Ukumbusho tutapata faida sana kama kila mumoya wetu anakamata wakati wa kutafakari a juu ya mambo yenye Yehova na Yesu wametufanyia. Mu hii habari tutaona mambo yenye bei ya ukombozi inatufundisha juu ya Yehova na juu ya Mwana wake. Habari yenye kufuata itatusaidia kuelewa namna tunaweza kufaidika na bei ya ukombozi na namna tunaweza kuonyesha shukrani.

MAMBO YENYE BEI YA UKOMBOZI INATUFUNDISHA JUU YA YEHOVA

3. Namna gani kifo ya mutu moya inaweza kukomboa mamilioni ya watu? (Ona pia picha.)

3 Bei ya ukombozi inatufundisha kama Yehova ni mwenye haki. (Kum. 32:4) Namna gani? Fikiria hii jambo. Juu Adamu hakumutii Mungu, tuliriti zambi na kifo. (Ro. 5:12) Ili kutukomboa kutoka mu zambi na kifo, Yehova alifanya mipango juu Yesu atoe zabihu ya ukombozi. Namna gani zabihu ya mutu moya mukamilifu ingeweza kukomboa mamilioni ya watu? Mutume Paulo alifasiria hivi: “Kama vile kupitia kukosa kutii kwa ule mutu mumoja [Adamu] wengi walifanywa kuwa watenda-zambi, vilevile pia kupitia kutii kwa mutu mumoja [Yesu] wengi watafanywa kuwa wenye haki.” (Ro. 5:19; 1 Ti. 2:6) Mu maneno ingine, ni kupitia mwanadamu moya mukamilifu mwenye hakutii njo tulifikia kuwa watumwa wa zambi na kifo. Njo maana, kupitia mwanadamu moya mukamilifu mwenye kutii tunaweza kukombolewa.

Mwanaume moya alifanya tukuwe watumwa wa zambi na kifo. Vilevile mwanaume moya alituweka huru (Ona fungu ya 3)


4. Juu ya nini Yehova hakuacha tu watoto watiifu wa Adamu waishi milele?

4 Iliomba kabisa Yesu akufe juu tuweze kukombolewa? Yehova hangeacha tu watoto wa Adamu wenye wanamutii waishi milele? Mwanadamu mwenye hakamilike anaweza kuona kama ile njo ingekuwa namna ya muzuri ya kumaliza ile mambo. Lakini kuwaza vile ni kusahau kama haki ya Yehova ni kamilifu. Juu Yehova ni mwenye haki, hangefanya sawa vile Adamu hakufanya zambi wakati alikatala kutii.

5. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama sikuzote Yehova atatenda kwa haki?

5 Mambo ingekuwa namna gani kama Yehova angetia haki pembeni na kuacha watoto wa Adamu wenye hawakamilike waishi milele? Ile ingefanya watu wajiulize ikiwa Mungu angeweza kuacha haki yake pembeni mu mambo ingine pia. Kwa mufano, watu wangejiuliza ikiwa Mungu atatimiza kabisa ahadi zake zote. Lakini hatuna sababu ya kuwaza vile. Yehova alitenda kwa haki hata kama kufanya vile kulimuomba afanye jambo ya nguvu sana, ni kusema atoe Mwana wake mupendwa. Ile inatuhakikishia kama sikuzote atatenda kwa haki.

6. Bei ya ukombozi inaonyesha namna gani kama Yehova anatupenda sana? (1 Yohana 4:9, 10)

6 Bei ya ukombozi inatusaidia kuelewa kama Yehova ni mwenye haki, lakini inatusaidia zaidi sana kuelewa kama Yehova iko na upendo. (Yoh. 3:16; Soma 1 Yohana 4:9, 10.) Mafundisho kuhusu bei ya ukombozi inaonyesha kama Yehova anapenda tukuwe na maisha ya milele, lakini pia tukuwe mu familia yake. Fikiria hii jambo: Wakati Adamu alifanya zambi, Yehova alimufukuza mu familia ya waabudu wake. Matokeo ni kama, siye wote tumezaliwa inje ya familia yake. Lakini kwa sababu ya bei ya ukombozi, Yehova anasamehe zambi zetu na atapatia kila mutu mwenye anaonyesha imani na mwenye anamutii nafasi ya kuingia tena mu familia yake. Hata leo tunaweza kuwa na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova na pamoya na waamini wenzetu. Kwa kweli Yehova anatupenda sana!—Ro. 5:10, 11.

7. Mateso yenye Yesu alipata inatusaidia namna gani kuelewa kama Yehova anatupenda sana?

7 Tunaweza kuelewa muzuri zaidi namna Yehova anatupenda sana kama tunafikiria mambo yenye ilimuomba afanye juu atutolee ile zabihu. Shetani anasema kama hakuna mutumishi wa Yehova mwenye atabakia muaminifu wakati iko mu hali ya nguvu. Juu ya kuonyesha kama Shetani anasema uongo, Yehova aliruhusu Yesu ateseke mbele ya kufa. (Yob. 2:1-5; 1 Pe. 2:21) Yehova alijionea namna wakubwa wa dini walimucheka Yesu, aliona namna maaskari walimupiga, na namna walimupigilia misumari kwenye muti. Kisha Yehova alijionea namna mutoto wake mupendwa alikufa kisha kuteseka sana. (Mt. 27:28-31, 39) Yehova alikuwa na uwezo wa kusimamisha ile magumu kwa wakati wowote. Kwa mufano, wakati watu walisema: “Muache sasa Mungu amuokoe,” palepale Yehova angeweza kumuokoa. Lakini kama angefanya vile, bei ya ukombozi haingelipwa na hatungekuwa na tumaini ya kukombolewa. Kwa hiyo Yehova aliruhusu Mwana wake avumilie ile mateso yote mupaka wakati alikata roho.

8. Unawaza Yehova alijisikia mubaya wakati aliona mutoto wake iko nateseka? Fasiria. (Ona pia picha.)

8 Juu Yehova ni Mweza-Yote, tusiwaze kama yeye hasikiake huzuni. Tuliumbwa kwa mufano ya Mungu na tunasikiaka huzuni, ni wazi kwamba Yehova naye anasikiaka huzuni. Biblia inasema kama Yehova naye ‘anahuzunikaka.’ (Zb. 78:40, 41) Fikiria pia habari ya Abrahamu na Isaka. Kumbuka kama Yehova alimuambia Abrahamu atoe mutoto wake mumoya tu kuwa zabihu. (Mwa. 22:9-12; Ebr. 11:17-19) Wazia namna Abrahamu alijisikia mubaya sana wakati alikuwa najitayarisha juu ya kuua mutoto wake Isaka. Bila shaka Yehova alijisikia mubaya sana kupita Abrahamu wakati aliona watu wako natesa na kuua mutoto wake!—Ona ku jw.org video Tuige Imani Yao—Abrahamu, Sehemu ya 2.

Yehova alisikia mubaya sana kuona Mwana wake iko anateseka (Ona fungu ya 8)


9. Waroma 8:32, 38, 39 inakusaidia kuelewa nini juu ya namna Yehova anakupenda sana weye na waabudu wenzako?

9 Bei ya ukombozi inatufundisha kama hakuna mutu mwenye anatupenda sana kupita Yehova. Hata marafiki ao watu wa familia wa karibu sana hawatupendi kupita vile Yehova anatupenda. (Soma Waroma 8:32, 38, 39.) Yehova anatupenda kupita hata vile tunajipenda. Unapenda kuishi milele? Yehova anapenda hata zaidi uishi milele. Unapenda zambi zako zisamehewe? Yehova anapenda hata zaidi kusamehe zambi zako. Anakuomba jambo moya tu: Ukubali zawadi ya bei ya ukombozi kwa kuonyesha imani na kwa kumutii. Bila shaka, bei ya ukombozi inaonyesha kabisa kama Yehova anatupenda. Mu dunia mupya tutajifunza mambo mingi zaidi juu ya upendo wake.—Muh. 3:11.

MAMBO YENYE BEI YA UKOMBOZI INATUFUNDISHA JUU YA YESU

10. (a) Nini njo ilimuhuzunisha sana Yesu? (b) Namna gani Yesu alitakasa jina ya Yehova? (Ona pia kisanduku “ Ushikamanifu wa Yesu Ulitakasa Jina ya Yehova.”)

10 Yesu anahangaikia sana mawazo yenye watu wako nayo juu ya Baba yake. (Yoh. 14:31) Yesu alihuzunika sana wakati walimushitaki kama ni muasi na alimutukana Mungu, juu ile ingechafua jina ya Baba yake. Njo maana alisali hivi: “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kipite mbali na mimi.” (Mt. 26:39) Juu Yesu alibakia muaminifu mupaka kifo, alitakasa kabisa jina ya Baba yake.

11. Namna gani Yesu alionyesha kama anapenda sana watu? (Yohana 13:1)

11 Bei ya ukombozi inatufundisha pia kama Yesu anahangaikia sana watu, zaidi sana wanafunzi wake. (Mez. 8:31; soma Yohana 13:1.) Kwa mufano, Yesu alijua kama angepata magumu mingi mu utumishi wake ku dunia na angekufa kifo ya maumivu. Lakini alitimiza utumishi wake ku dunia, haiko juu alilazimika kufanya vile, lakini juu alipenda watu. Alihubiri, alifundisha, na kusaidia wengine kwa moyo wake wote. Hata siku ya kifo yake, Yesu alikamata wakati wa kusafisha migulu ya mitume wake, kuwafundisha mambo mingi, na kuwafariji. (Yoh. 13:12-15) Kisha, wakati alikuwa ku muti wa mateso, Yesu alikamata wakati fulani juu ya kupatia tumaini mutenda-maovu mwenye alikuwa pembeni yake. Alikamata pia mipango juu kukuwe mutu wa kuhangaikia mama yake. (Lu. 23:42, 43; Yoh. 19:26, 27) Yesu alikuwa na upendo mingi sana, ule upendo ulionekana kupitia kifo yake lakini pia kupitia maisha yake yote ku dunia.

12. Ni mu njia gani Yesu anaendelea kutumika kwa ajili yetu?

12 Hata kama Yesu alikufa “mara moja kwa wakati wote,” angali anatumika sana kwa ajili yetu. (Ro. 6:10) Namna gani? Anaendelea kutumia wakati na nguvu yake juu tupate baraka zenye bei ya ukombozi inatuletea. Fikiria mambo yenye iko nafanya: Iko natawala mbinguni akiwa Mufalme wetu, Kuhani Mukubwa, na kichwa cha kutaniko. (1 Ko. 15:25; Efe. 5:23; Ebr. 2:17) Anasimamia kazi ya kukusanya watiwa-mafuta na kundi kubwa, na anapaswa kumaliza ile kazi mbele taabu kubwa imalizike. b (Mt. 25:32; Mk. 13:27) Anahakikisha pia kama watumishi wake waaminifu wanapata chakula ya kiroho yenye wako nayo lazima mu hizi siku za mwisho. (Mt. 24:45) Na hata mu Utawala wake wa Miaka Elfu ataendelea kututumikia. Kwa kweli, Yehova alitoa Mwana wake haiko tu juu akufe kwa ajili yetu lakini pia juu aendelee kutufanyia mambo ingine ya mingi!

USIACHE KUJIFUNZA

13. Namna gani kutafakari kunaweza kukusaidia uendelee kujifunza juu ya namna Mungu na Kristo wanatupenda?

13 Unaweza kuendelea kujifunza juu ya namna Yehova Mungu na Kristo Yesu wanakupenda kwa kuendelea kutafakari juu ya mambo yenye wamekufanyia. Kwa mufano, mu kipindi ya Ukumbusho, unaweza kusoma kwa uangalifu kitabu moya ya Injili ao zaidi. Usisome mambo mingi sana mara moya lakini uende polepole na utafute sababu zingine zenye zinapaswa kutuchochea tumupende Yehova na Yesu. Na ujikaze kuambia wengine mambo yenye umejifunza.

14. Kulingana na Zaburi 119:97 na maelezo ya chini, namna gani kufanya utafiti kunaweza kutusaidia tuendelee kujifunza juu ya bei ya ukombozi na juu ya mafundisho ingine? (Ona pia picha.)

14 Kama ulishafanya miaka mingi mu kweli, unaweza kujiuliza ikiwa kuko mambo fulani ya mupya yenye unaweza kujifunza kuhusu haki ya Yehova, upendo wake, na bei ya ukombozi. Kusema kweli, mambo ya kujifunza juu ya bei ya ukombozi na mambo ingine haitaishaka. Kwa hiyo utafanya nini? Soma na kujifunza habari mingi zenye kuwa mu vichapo vyetu. Fanya utafiti wakati unapata andiko yenye hauelewe muzuri. Kisha utafakari juu ya mambo ya mupya yenye umepata, na ujiulize kama inakufundisha nini juu ya Yehova, juu ya Mwana wake, na namna inaonyesha kama wanakupenda.—Soma Zaburi 119:97 na maelezo ya chini.

Hata kama tulishafanya miaka mingi mu kweli, tunaweza kujifunza mambo ya mupya yenye itafanya tukuwe wenye shukrani zaidi juu ya bei ya ukombozi (Ona fungu ya 14)


15. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kujifunza mambo ya mupya mu Biblia?

15 Usivunjike moyo kama haupate jambo fulani ya mupya ao jambo fulani ya ajabu kila wakati unajifunza na kufanya utafiti. Uko sawa mutu mwenye iko natafuta zahabu. Mutu mwenye iko natafuta zahabu anapitishaka saa mingi ao hata masiku mingi mbele apate hata kalijiwe ka kidogo ka zahabu. Lakini anaendelea kutafuta juu kila kalijiwe ka zahabu kenye anapata ni ka maana sana. Kweli ya Biblia ni ya maana hata zaidi kupita zahabu! (Zb. 119:127; Mez. 8:10) Kwa hiyo, ukuwe muvumilivu na uheshimie programu yako ya kusoma Biblia.—Zb. 1:2.

16. Namna gani tunaweza kuiga Yehova na Yesu?

16 Wakati uko najifunza, tafuta namna ya kutumikisha mambo yenye uko najifunza. Kwa mufano uige haki ya Yehova kwa kutendea wengine bila upendeleo. Kama Yesu, uonyeshe kama unamupenda Yehova na wengine kwa kuwa tayari kuteseka kwa ajili ya jina ya Yehova na kwa kujitoa juu ya kusaidia Wakristo wenzako. Pia, umuige Yesu kwa kuhubiria wengine juu nao wapate nafasi ya kukubali zawadi ya Yehova ya maana sana, bei ya ukombozi.

17. Tutaona nini mu habari yenye kufuata?

17 Wakati unaelewa mambo mingi zaidi juu ya bei ya ukombozi unakuwa mwenye shukrani juu ya ile zawadi. Ni vile upendo wako kwa Yehova na Mwana wake utaongezeka, kisha nao pia watakupenda sana. (Yoh. 14:21; Yak. 4:8) Kwa hiyo tuendelee kutumia mambo yote yenye Yehova anatupatia ili tuendelee kujifunza juu ya bei ya ukombozi. Habari yenye kufuata itazungumuzia baraka fulani zenye bei ya ukombozi inatuletea na tutaona namna tunaweza kuonyesha shukrani juu ya upendo wenye Yehova ametuonyesha.

WIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu

a MAFASIRIO YA MANENO FULANI: “Kutafakari” maana yake kukazia akili habari fulani na kuifikiria sana.

b Kukusanywa kwa “vitu vyenye kuwa mbinguni” yenye Paulo anazungumuzia mu Waefeso 1:10, ni tofauti na kukusanywa kwa “watu wenye kuchaguliwa” yenye Yesu anazungumuzia mu Matayo 24:31 na Marko 13:27. Paulo anazungumuzia wakati wenye Yehova anachagua wale wenye watatawala pamoya na Yesu kwa kuwatia mafuta kwa roho takatifu. Yesu yeye anazungumuzia wakati wenye mabaki ya watiwa-mafuta wenye kuwa ku dunia watakusanywa pamoya mbinguni mu kipindi ya taabu kubwa.