Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

WIMBO 132 Sasa Tunakuwa Mwili Mumoja

Bwana, Onyesha Bibi Yako Heshima

Bwana, Onyesha Bibi Yako Heshima

“Ninyi bwana, . . . muwapatie heshima.”1 PE. 3:7.

WAZO KUBWA

Namna bwana anaweza kuonyesha bibi yake heshima kupitia maneno na matendo.

1. Juu ya nini Yehova alianzisha ndoa?

 YEHOVA ni “Mungu mwenye furaha,” na anapenda na siye tukuwe na furaha. (1 Ti. 1:11) Ametupatia zawadi za mingi juu tufurahie maisha. (Yak. 1:17) Ndoa iko kati ya zile zawadi. Wakati mwanamuke na mwanaume wanaoana, wanafanya naziri kama watapendana na kuheshimiana. Kama bibi na bwana wanaendelea kupendana sana, watakuwa na furaha ya kweli.—Mez. 5:18.

2. Ndoa mingi ziko namna gani leo?

2 Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, mu dunia ya leo bibi na bwana wengi wanasahau naziri yenye walifanya siku yenye walioana. Ile inafanya wasikuwe na furaha. Ripoti fulani ya hivi karibuni ya OMS inaonyesha kama bwana wengi wanapiga bibi zao, wanawatukana, na kuwatendea mubaya mu njia zingine za mingi. Bwana anaweza kuwa anatendeaka bibi yake muzuri wakati wako mbele ya watu, lakini anamutendea mubaya wakati wako ku nyumba. Zaidi ya ile, bwana wengi wanaangaliaka pornografia na ile inafanya bibi zao wajisikie kuwa hawapendwe na hawaheshimiwe.

3. Ni mambo gani inaweza kufanya bwana atendee bibi yake mubaya?

3 Nini inaweza kufanya bwana atendee bibi yake mubaya? Pengine mu familia yenye bwana alikomalia, baba yake alikuwa na jeuri na ile inaweza kufanya awaze kama ni jambo ya kawaida kutendea bibi mubaya. Ao kwenye anaishi watu wanawaza kama “mwanaume wa kweli” anapaswa kutumia nguvu juu ya kuonyesha bibi yake kama yeye njo shefu. Ao pengine hakufundishwa kujizuia, hata kuzuia kasirani yake. Na juu wanaume fulani wanazoea kuangalia pornografia, ile inafanya wakuwe na mawazo ya mubaya, wanawaza kama wanamuke wako tu pale juu ya kuwatimizia tamaa yao ya ngono. Zaidi ya ile, ripoti zinaonyesha kama tangu ugonjwa wa Korona, ile matatizo imeongezeka. Lakini ile mambo yote haipatie bwana sheria ya kutendea bibi yake mubaya.

4. Bwana Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu juu ya jambo gani, na juu ya nini?

4 Bwana Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu juu wasikuwe na mawazo yenye haifae kuhusu wanamuke. a Juu ya nini? Sababu moya ni kwamba mambo yenye mutu anawaza njo yenye anafanyaka. Mutume Paulo alionya hivi Wakristo watiwa-mafuta wa Roma: “Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.” (Ro. 12:1, 2) Wakati Paulo aliandikia kutaniko ya Roma, inaonekana kulikuwa kulishapita wakati fulani tangu ile kutaniko ianzishwe. Lakini, maneno ya Paulo inaonyesha kama watu fulani mu ile kutaniko walikuwa wangali wanachochewa na desturi na mawazo ya ulimwengu. Njo maana aliwashauria wabadilishe mawazo na tabia yao. Ile mashauri inahusu pia bwana Wakristo leo. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, bwana fulani Wakristo wamechochewa na mawazo ya ulimwengu na hata wametendea mubaya bibi zao. b Yehova anapenda bwana atendee bibi yake namna gani? Jibu ya hii ulizo iko mu andiko ya musingi ya hii habari.

5. Kulingana na 1 Petro 3:7, bwana anapaswa kutendea bibi yake namna gani?

5 Soma 1 Petro 3:7. Yehova anaomba bwana waonyeshe bibi zao heshima. Bwana mwenye anaheshimia bibi yake anamutendea kwa upole na kwa upendo. Mu hii habari tutaona namna bwana anaweza kuonyesha bibi yake heshima. Lakini, tuzungumuzie kwanza tabia zenye zinashushia bibi heshima.

EPUKA TABIA ZENYE ZINASHUSHIA BIBI HESHIMA

6. Yehova anaona namna gani mwanaume mwenye anapiga bibi yake? (Wakolosai 3:19)

6 Kupiga bibi. Yehova anachukia kila mutu mwenye jeuri. (Zb. 11:5) Anachukia sana wakati bwana anapiga bibi yake. (Mal. 2:16; soma Wakolosai 3:19.) Kulingana na andiko yetu ya musingi, 1 Petro 3:7, kama bwana hatendee bibi yake muzuri, ile inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya uhusiano wake pamoya na Yehova. Yehova anaweza hata kukatala kusikiliza sala zake.

7. Kulingana na Waefeso 4:31, 32, bwana anapaswa kuepuka maneno ya namna gani? (Ona pia “Mafasirio ya Maneno Fulani.”)

7 Kutukana bibi. Bwana fulani wanatendea bibi zao mubaya kwa kuwaambia maneno makali na yenye kuumiza. Lakini Yehova anachukia “hasira, kasirani kali, kufoka, [na] matukano.” c (Soma Waefeso 4:31, 32.) Yehova anasikiaka kila kitu. Anasikia namna bwana anazungumuza na bibi yake, hata wakati wako wao wawili tu. Bwana mwenye anazungumuza na bibi yake kwa ukali, anaharibisha ndoa yake lakini pia urafiki wake pamoya na Mungu.—Yak. 1:26.

8. Yehova anaona namna gani tabia ya kuangalia pornografia, na juu ya nini?

8 Kuangalia pornografia. Yehova anaona namna gani tabia ya kuangalia pornografia? Anaichukia. Kwa hiyo, bwana mwenye anaangalia picha chafu anaharibisha urafiki wake pamoya na Yehova, na anashushia bibi yake heshima. d Yehova anapenda bwana aendelee kuwa mushikamanifu kwa bibi yake, hapana tu mu matendo lakini pia mu mawazo. Yesu alisema kama mwanaume mwenye anaangalia mwanamuke kwa kumutamani, tayari amefanya naye uzinifu “katika moyo wake.” eMt. 5:28, 29.

9. Juu ya nini Yehova anachukia wakati bwana anakaza bibi yake kufanya matendo ya ngono yenye inamushushia heshima?

9 Kukaza bibi kufanya matendo ya ngono ya kumushushia heshima. Bwana fulani wanakaza bibi zao kufanya matendo ya ngono yenye inawashushia heshima na yenye inawafanya wajisikie kuwa hawapendwe ao hawako safi. Yehova anachukia tabia ya vile ya kukosa upendo na ya kujifikiria mwenyewe. Anaomba bwana apende bibi yake na aheshimie zamiri yake. (Efe. 5:28, 29) Sasa tuseme nini kama tayari bwana Mukristo haheshimie bibi yake, ao anamutendea mubaya, ao tena anaangaliaka pornografia? Namna gani anaweza kubadilisha mawazo na matendo yake?

NAMNA BWANA ANAWEZA KUACHANA NA TABIA ZA MUBAYA

10. Mufano wa Yesu unaweza kusaidia namna gani bwana?

10 Ni nini inaweza kusaidia bwana aache kumutendea bibi yake mubaya na kumushushia heshima? Anapaswa kujikaza kumuiga Yesu. Hata kama Yesu hakukuwa na bibi, namna alitendea wanafunzi wake ni mufano wenye unaweza kusaidia bwana ajue namna ya kutendea bibi yake. (Efe. 5:25) Kwa mufano, tuone mambo yenye bwana anaweza kujifunza kupitia namna Yesu alitendea mitume wake na namna alizungumuza nao.

11. Yesu alitendea mitume wake namna gani?

11 Yesu alitendea mitume wake kwa upole na heshima. Hakuwatendea kwa ukali. Hata kama Yesu alikuwa na nguvu kupita mitume wake, hakutumia ile nguvu juu ya kuwaogopesha. Lakini, aliwatumikia kwa unyenyekevu. (Yoh. 13:12-17) Aliambia wanafunzi wake hivi: “Mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu.” (Mt. 11:28-30) Yesu alikuwa na tabia ya upole. Mutu mupole haiko muzaifu, lakini ni mutu mwenye iko na nguvu ya kujizuia. Wakati wanamuchokoza, anabakia mwenye kutulia.

12. Namna gani Yesu alizungumuza na wengine?

12 Yesu alitumia maneno yake juu ya kufariji na kutia moyo wengine. Hakuzungumuza na wafuasi wake kwa ukali. (Lu. 8:47, 48) Hata wakati wapinzani walimutukana na kujaribu kumukasirisha “hakujibu kwa matukano.” (1 Pe. 2:21-23) Wakati fulani, Yesu alibakia kimya kuliko kujibu kwa ukali. (Mt. 27:12-14) Yesu ni mufano muzuri sana kwa bwana Wakristo!

13. Sawa vile Matayo 19:4-6 inasema, namna gani bwana anaweza ‘kushikamana na bibi yake’? (Ona pia picha.)

13 Yesu alisema kama bwana wanapaswa kubakia washikamanifu kwa bibi zao. Alirudilia maneno ya Baba yake, mwenye alisema kama mwanaume anapaswa ‘kushikamana na bibi yake.’ (Soma Matayo 19:4-6.) Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa ‘kushikamana na’ yenye inatumiwa mu hii andiko, inamaanisha neno kwa neno “kubanisha vitu mbili kwa kutumia kolo.” Kwa hiyo, uhusiano kati ya bibi na bwana unapaswa kuwa nguvu sana sawa vile wamebananishwa na kolo. Wakiwaachanisha, wote wawili watalumia. Bwana mwenye anajikaza kuwa na uhusiano wa vile na bibi yake ataepuka kuangalia aina yoyote ya pornografia. Bila kukawia, atageuza macho yake juu “yasiangalie mambo yenye hayana mafaa yoyote.” (Zb. 119:37) Ni sawa vile anafanya agano na macho yake juu asiangalie kwa njia ya kutamani mwanamuke yeyote mwenye haiko bibi yake.—Yob. 31:1.

Bwana mushikamanifu anakatala kuangalia pornografia (Ona fungu ya 13) g


14. Bwana mwenye alikuwa natendea bibi yake mubaya anapaswa kufanya mambo gani juu atengeneze tena urafiki wake pamoya na Yehova na pamoya na bibi yake?

14 Bwana mwenye anapigaka bibi yake ao kumutukana anapaswa kufanya mambo ingine zaidi ya mambo yenye tumeona ili atengeneze tena urafiki wake pamoya na Yehova na pamoya na bibi yake. Anapaswa kufanya mambo gani? Kwanza, anapaswa kutambua kama iko na tatizo kubwa. Yehova anaonaka mambo yote, anaona mambo yote yenye anasema na kufanya. (Zb. 44:21; Muh. 12:14; Ebr. 4:13) Pili, anapaswa kuacha kutendea bibi yake mubaya na anapaswa kubadilika. (Mez. 28:13) Tatu, anapaswa kumuomba bibi yake na Yehova huruma na kutafuta musamaha wao. (Mdo. 3:19) Anapaswa pia kumuomba Yehova amupatie hamu ya kubadilika na amusaidie kuzuia mawazo, maneno, na matendo yake ya mubaya. (Zb. 51:10-12; 2 Ko. 10:5; Flp. 2:13) Ine, anapaswa kutenda kulingana na sala zake kwa kujifunza namna ya kuchukia kila aina ya jeuri na maneno makali. (Zb. 97:10) Tano, anapaswa kutafuta bila kukawia musaada wa wazee wa kutaniko. (Yak. 5:14-16) Sita, anapaswa kukamata mipango juu asiangukie tena mu zile tabia. Bwana mwenye anaangaliaka pornografia anapaswa pia kufuata hii mambo yote sita. Yehova atabariki bidii yake ya kupenda kubadilisha tabia yake. (Zb. 37:5) Lakini, zaidi ya kuachana na tabia zenye zinamushushia bibi yake heshima, bwana anapaswa pia kujifunza namna ya kuonyesha bibi yake upendo na heshima. Anaweza kufanya vile namna gani?

NAMNA YA KUONYESHA BIBI UPENDO NA HESHIMA

15. Namna gani bwana anaweza kuonyesha bibi yake upendo?

15 Umuonyeshe upendo. Ndugu fulani wenye kuwa mu ndoa yenye furaha wanazoea kufanyia bibi zao kila siku jambo fulani yenye inaonyesha kama wanawapenda. (1 Yo. 3:18) Bwana anaweza kuonyesha bibi yake kama anamupenda kupitia mambo ya kidogo-kidogo sawa vile kumukamata mukono ao kumukumbatia. Anaweza kumutumia ka ujumbe ku telefone na kumuambia kwa mufano “niko nakuwaza” ao kumuuliza “mambo ni sawa?” Wakati fulani, anaweza kumuandikia bibi yake maneno fulani ku karatasi ili kumuonyesha kama anamupenda, ao anaweza kumupatia zawadi. Wakati bwana anafanya hii mambo, anamuonyesha bibi yake heshima na anafanya ndoa yao ikuwe nguvu zaidi.

16. Juu ya nini bwana anapaswa kumupongeza bibi yake?

16 Umuonyeshe shukrani. Bwana mwenye anaheshimia bibi yake anamutia moyo na anamuambia juu ya nini ni wa maana kwake. Bwana anaweza kufanya vile kwa kukumbuka kumushukuru bibi yake juu ya mambo yote yenye anafanya ili kumutegemeza. (Kol. 3:15) Wakati bwana anapongeza bibi yake kwa moyo wote, anamufanya ajisikie muzuri. Bibi anajisikia kuwa salama, kuwa anapendwa, na anaheshimiwa.—Mez. 31:28.

17. Namna gani bwana anaweza kuonyesha bibi yake heshima?

17 Umutendee kwa upole na kwa heshima. Bwana mwenye anapenda bibi yake anamuona kuwa wa maana. Anamuona kuwa zawadi kutoka kwa Yehova. (Mez. 18:22; 31:10) Kwa hiyo, anamutendea kwa upole na kwa heshima, hata wakati wa kitendo cha ndoa. Hatamukaza kufanya matendo ya ngono yenye inafanya ajisikie mubaya, yenye inamushushia heshima, ao yenye inachafua zamiri yake. f Bwana pia atajikaza kuendelea kuwa na zamiri safi mbele ya Yehova.—Mdo. 24:16.

18. Bwana anapaswa kuazimia kufanya nini? (Ona pia kisanduku “ Njia Ine za Kuonyesha Bibi Yako Heshima.”)

18 Bwana, ukuwe hakika kama Yehova anaona na anafurahia namna uko najikaza kumutendea bibi yako kwa heshima mu mambo yote. Azimia kuepuka matendo ya kushushia bibi yako heshima. Umutendee kwa upole, kwa heshima na kwa upendo. Ukifanya vile, utamuonyesha kama unamupenda na unamuona kuwa wa maana. Onyesha bibi yako heshima na utalinda uhusiano wa maana zaidi wenye uko nao, uhusiano wako pamoya na Yehova.—Zb. 25:14.

WIMBO 131 “Kile Chenye Mungu Ameunganisha”

a Habari “Unatendea Wanamuke Vile Yehova Anawatendea?” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 1, 2024 inaweza kusaidia bwana.

b Habari “Msaada kwa Wanaotendewa kwa Jeuri Nyumbani” yenye kuwa mu sehemu “Habari Zingine” ku jw.org inaweza kusaidia wale wenye wanatendewa mubaya ku nyumba.

c MAFASIRIO YA MANENO FULANI: “Kutukana” inatia ndani kupanga mutu majina ya kumushushia heshima, kutumia maneno ya makali, na maneno ya kuzarau mutu. Maneno yoyote ya kuumiza, ya kuzarau mutu, ao ya kumuchambua, ni matukano.

d Ona ku jw.org habari “Ponografia Inaweza Kuiharibu Ndoa Yako.”

e Mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 8, 2023 muko habari “Kama Bibi ao Bwana Yako Anaangaliaka Pornografia.” Ile habari inaweza kusaidia bibi mwenye bwana yake anaangaliaka pornografia.

f Biblia haitaye liste ya matendo ya ngono kati ya bibi na bwana yenye inaweza kuonwa kuwa safi ao machafu. Bibi na bwana Wakristo wanapaswa kukamata maamuzi yenye inaonyesha kama wanaheshimia Yehova, yenye inaonyesha kama kila mumoja wao anapenda kumufurahisha mwenzake, na yenye itawasaidia kuendelea kuwa na zamiri safi. Kwa kawaida, bibi na bwana hawapaswe kuzungumuzia ile mambo ya kipekee ya mu ndoa yao pamoya na watu wengine.

g MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu iko pamoya na wafanyakazi wenzake wenye hawako Mashahidi, wanajaribu kumuchochea aangalie picha za pornografia.