Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 5

WIMBO 108 Mungu Iko na Upendo Mushikamanifu

Faida Yenye Upendo wa Yehova Unatuletea

Faida Yenye Upendo wa Yehova Unatuletea

“Kristo Yesu alikuja katika ulimwengu ili kuokoa watenda-zambi.”1 TI. 1:15.

WAZO KUBWA

Faida yenye bei ya ukombozi inatuletea na namna tunaweza kumuonyesha Yehova shukrani.

1. Tunaweza kufanya nini juu ya kumufurahisha Yehova?

 WAZIA unapatia mutu mwenye unapenda zawadi ya muzuri na yenye itamusaidia. Utahuzunika sana kama ule mutu anaweka tu ile zawadi bila kuitumikisha. Lakini, utafurahi sana kama anaitumikisha muzuri na anakuonyesha shukrani. Ile mufano inapenda kutufundisha nini? Yehova ametoa Mwana wake kwa ajili yetu. Bila shaka anafurahi sana wakati tunaonyesha shukrani juu ya ile zawadi ya muzuri sana, na juu ya upendo wake wenye ulimuchochea atoe bei ya ukombozi!—Yoh. 3:16; Ro. 5:7, 8.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Lakini, vile wakati iko napita, tunaweza kuona ile zawadi ya bei ya ukombozi kuwa jambo ya kawaida tu. Kama hatuendelee kuonyesha shukrani juu ya bei ya ukombozi, itakuwa sawa vile tunaweka tu fasi moya zawadi ya muzuri yenye Mungu alitupatia bila kuitumikisha. Juu ile isitufikie, tunapaswa mara kwa mara kufikiria mambo yenye Mungu na Kristo walifanya kwa ajili yetu. Hii habari itatusaidia tujue namna ya kufanya vile. Tutazungumuzia faida yenye bei ya ukombozi inatuletea leo, na faida yenye itatuletea mu wakati wenye kuya. Tutazungumuzia pia namna tunaweza kuonyesha shukrani juu ya upendo wa Yehova, zaidi sana mu hii kipindi ya Ukumbusho.

FAIDA YENYE TUNAPATA LEO

3. Bei ya ukombozi inatuletea faida gani leo?

3 Hata leo, bei ya ukombozi yenye Yesu alitoa iko natuletea faida. Kwa mufano, kupitia bei ya ukombozi, Yehova anasamehe zambi zetu. Halazimike kutusamehe, lakini anapenda kufanya vile. Mutunga-zaburi aliimba hivi ili kuonyesha shukrani yake: “Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.”—Zb. 86:5; 103:3, 10-13.

4. Yehova alitoa bei ya ukombozi kwa ajili ya nani? (Luka 5:32; 1 Timoteo 1:15)

4 Watu fulani wanaweza kuona kama hawastahili musamaha wa Yehova. Kusema kweli, siye wote hatustahili musamaha wake. Mutume Paulo alielewa kama ‘hastahili kuitwa mutume.’ Hata vile, alisema hivi: “Kwa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu mimi niko kile niko.” (1 Ko. 15:9, 10) Wakati tunatubu zambi zetu, Yehova anatusamehe. Juu ya nini? Haiko juu tunastahili musamaha wake, lakini juu anatupenda. Kama uko nahangaika juu unawaza kama haustahili, kumbuka kama Yehova alitoa bei ya ukombozi kwa ajili ya watenda-zambi wenye kutubu, hapana kwa ajili ya watu wenye hawana zambi.—Soma Luka 5:32; 1 Timoteo 1:15.

5. Kuko mumoya kati yetu mwenye anapaswa kuwaza kama anastahili rehema ya Yehova? Fasiria.

5 Ni kweli kwamba Yehova anafurahia uaminifu wetu, lakini hakuna hata mumoya wetu mwenye anaweza kuwaza kama anastahili rehema ya Yehova hata kama alishafanya miaka mingi mu utumishi wake. (Ebr. 6:10) Alitupatia bei ya ukombozi kwa bure, hapana juu ya kutulipa kwa ajili ya kazi fulani yenye tumefanya. Ikiwa tunawaza kama tunastahili rehema ya Yehova ao tunastahili kutendewa mu njia fulani ya pekee, ni sawa vile tunasema Yesu alikufa tu bure.—Linganisha na Wagalatia 2:21.

6. Juu ya nini Paulo alifanya mambo mingi mu utumishi wake kwa Yehova?

6 Paulo alijua kama, hata afanye nini hatastahili rehema ya Yehova. Sasa, juu ya nini alifanya mambo mingi mu utumishi wa Yehova? Haiko juu ya kuonyesha kama anastahili, lakini juu ya kuonyesha kama iko mwenye shukrani kwa sababu ya fazili zenye hazistahiliwe za Yehova. (Efe. 3:7) Kama Paulo, tunaendelea kumutumikia Yehova kwa bidii, haiko juu tustahili rehema yake, lakini juu ya kumuonyesha shukrani kwa sababu ya rehema yake.

7. Bei ya ukombozi inatuletea faida gani ingine leo? (Waroma 5:1; Yakobo 2:23)

7 Faida ingine yenye bei ya ukombozi inatuletea leo ni hii: Tunaweza kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova. a Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, wakati tulizaliwa hatukukuwa na uhusiano wowote pamoya na Mungu. Lakini kwa sababu ya bei ya ukombozi, tunaweza kuwa na “amani pamoja na Mungu” na kumukaribia.—Soma Waroma 5:1; Yakobo 2:23.

8. Juu ya nini tunapaswa kuwa wenye shukrani juu ya pendeleo ya kusali kwa Yehova?

8 Fikiria hii jambo: Juu tuko na uhusiano wa karibu pamoya na Yehova, tunaweza kusali kwake. Sala ni pendeleo ya ajabu sana. Yehova anasikilizaka sala zenye watumishi wake wanatoa wakati wanakutana pamoya, lakini pia sala zenye kila mumoya wetu anatoa kipekee. Sala inaweza kutuliza moyo wetu na kutupatia amani ya akili, lakini pia inatia nguvu urafiki wetu pamoya na Yehova. (Zb. 65:2; Yak. 4:8; 1 Yo. 5:14) Wakati Yesu alikuwa ku dunia alisali mara kwa mara kwa Yehova juu alijua kama Yehova alikuwa namusikiliza, na alijua kama sala ingefanya uhusiano wake pamoya na Baba yake uendelee kuwa nguvu. (Lu. 5:16) Tuko wenye shukrani sana juu kupitia zabihu ya Yesu tunaweza kuwa marafiki wa Yehova, na hata tunaweza kuzungumuza naye katika sala!

FAIDA YENYE TUTAPATA MU WAKATI WENYE KUYA

9. Bei ya ukombozi italetea waabudu waaminifu faida gani wakati wenye kuya?

9 Bei ya ukombozi italetea waabudu waaminifu wa Yehova faida gani wakati wenye kuya? Yehova atawapatia uzima wa milele. Watu mingi wanawaza kama ile haitawezekana juu tangu zamani watu wanakufaka tu. Lakini wakati Yehova aliumba wanadamu, alipenda waishi milele. Adamu hangefanya zambi, hakuna mwenye angewaza kama haiwezekane kuishi milele. Hata kama uzima wa milele unaonekana kuwa jambo ya ajabu sana leo, inawezekana kuishi milele juu Yehova alilipa bei ya ajabu sana, alitoa Mwana wake mupendwa.—Ro. 8:32.

10. Watiwa-mafuta na kondoo wengine wako nangoya nini?

10 Ni kweli kwamba uzima wa milele ni zawadi yenye tutapata mu wakati wenye kuya. Lakini Yehova anapenda tangu leo tuwazie namna maisha itakuwa mu ile wakati. Watiwa-mafuta wanangoya kwa hamu maisha ya muzuri yenye watakuwa nayo mbinguni wakati watatawala dunia pamoya na Kristo. (Ufu. 20:6) Kondoo wengine wako na tumaini ya kuishi mu dunia paradiso kwenye hakutakuwa maumivu wala huzuni. (Ufu. 21:3, 4) Uko kati ya kondoo wengine wenye wako na tumaini ya kuishi milele ku dunia? Ile haiko tumaini ya hali ya chini! Yehova aliumba wanadamu juu waishi milele ku dunia. Maisha ku dunia itatuletea furaha ya ajabu sana.

11-12. Tunaweza kuanza kufikiria baraka gani zenye tutapata mu Paradiso? (Ona pia picha.)

11 Wazia namna maisha itakuwa mu dunia Paradiso. Hakutakuwa magonjwa ao kifo. (Isa. 25:8; 33:24) Yehova atatimiza kila tamaa yenye kufaa yenye uko nayo. Utapenda kujifunza zaidi juu ya mambo gani? Juu ya wanyama ao juu ya ndege? Utapenda kujifunza kuchapa, ao kupiga chombo fulani ya muziki? Kutakuwa lazima ya wajenzi na walimaji. Kutakuwa pia lazima ya watu wa kufanya kazi zingine mbalimbali sawa vile kupiga chakula, kutengeneza vitu, na watu wa kutunza mabustani yenye kupendeza. (Isa. 35:1; 65:21) Juu utaishi milele, utakuwa na wakati wa kujifunza jambo yoyote yenye unapenda.

12 Tutafurahi sana kukaribisha wenye watafufuliwa! (Mdo. 24:15) Wazia pia furaha yenye utakuwa nayo wakati utajifunza mambo mingi juu ya Yehova kwa kuchunguza vitu mingi vyenye aliumba. (Zb. 104:24; Isa. 11:9) Na zaidi ya yote itafurahisha sana kumutumikia Yehova bila kufanya zambi hata kidogo! Unaweza kuitika kupoteza zile baraka zote juu tu ya “kufurahia zambi kwa muda”? (Ebr. 11:25) Hapana! Tuko tayari kujiima jambo yoyote leo, juu tu tupate zile baraka. Kumbuka kama hatutachunga dunia Paradiso milele! Kuko siku tutaishi ndani. Ile mambo yote haingewezekana kama Yehova hangetupenda sana na kututolea Mwana wake kuwa zawadi!

Ni baraka gani yenye uko nachunga sana kuona mu Paradiso? (Ona fungu ya 11-12)


ONYESHA SHUKRANI JUU YA UPENDO WA YEHOVA

13. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha Yehova shukrani juu ya upendo wake? (2 Wakorinto 6:1)

13 Namna gani tunaweza kumuonyesha Yehova shukrani juu alitutolea bei ya ukombozi? Ni kwa kutia kazi yake pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. (Mt. 6:33) Kwa kweli, Yesu alikufa “ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya ule mwenye alikufa kwa ajili yao na akafufuliwa.” (2 Ko. 5:15) Hatupaswe kusahau juu ya nini Yehova alituonyesha fazili zake zenye hazistahiliwe.—Soma 2 Wakorinto 6:1.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatumainia muongozo wa Yehova?

14 Tunaweza pia kuonyesha shukrani juu ya upendo wa Yehova kwa kutumainia muongozo wenye anatupatia. Namna gani? Mbele ya kukamata maamuzi, kwa mufano mbele ya kuamua ni kiasi gani ya masomo tutasoma ao tutaitika kazi gani, tunapaswa kufikiria mambo yenye Yehova angependa tufanye. (1 Ko. 10:31; 2 Ko. 5:7) Wakati tunaonyesha imani yetu kupitia matendo, jambo fulani ya ajabu inatokea, tunamutumainia Yehova zaidi na urafiki wetu pamaya naye unakuwa nguvu. Tumaini yetu inakuwa nguvu.—Ro. 5:3-5; Yak. 2:21, 22.

15. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu mu kipindi ya Ukumbusho?

15 Kuko mambo ingine yenye tunaweza kufanya ili kumuonyesha Yehova shukrani juu ya upendo wake: Tutumie hii kipindi ya Ukumbusho juu ya kumuonyesha Yehova namna tuko wenye shukrani sana juu ya bei ya ukombozi. Zaidi ya kujikaza kuhuzuria Ukumbusho, tualike wengine. (1 Ti. 2:4) Ambia wenye unaalika mambo yenye itapitikana ku Ukumbusho. Unaweza kuwaonyesha video Sababu Gani Yesu Alikufa? na Tukumbuke Kifo cha Yesu yenye kuwa ku jw.org. Wazee watajikaza kualika wale wenye hawatende tena. Wazia furaha yenye itakuwa mbinguni na ku dunia ikiwa kondoo fulani wa Yehova mwenye alikuwa amepotea, anarudia! (Lu. 15:4-7) Ku Ukumbusho tusisalimie tu wale wenye tunajua, lakini tujitilie muradi wa kusalimia wapya ao wenye walishakawia na hawakusanyike. Tunapenda wajisikie kuwa wanakaribishwa!—Ro. 12:13.

16. Juu ya nini ni muzuri tufikirie kuhubiri sana mu kipindi ya Ukumbusho?

16 Unaweza kuhubiri sana mu kipindi ya Ukumbusho? Kufanya vile ni njia moya ya kuonyesha shukrani juu ya mambo yote yenye Mungu na Yesu wametufanyia. Kadiri tunafanya mambo mingi mu kazi ya Yehova, ni vile tunaona namna anatutegemeza na ile inafanya tumutumainie zaidi. (1 Ko. 3:9) Pia, ujikaze kufuata programu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho yenye kuwa mu broshua Tuchunguze Maandiko Kila Siku ao mu buku ya mukutano. Unaweza hata kujitilia programu ya kujifunza mambo mingi juu ya ile maandiko.

17. Yehova anafurahia nini? (Ona pia kisanduku “ Namna ya Kuonyesha Shukrani Juu ya Upendo wa Yehova.”)

17 Pengine hali yako haitakuruhusu kufanya mambo yote yenye tumezungumuzia mu hii habari. Lakini kumbuka kama Yehova hatalinganisha mambo yenye unafanya na mambo yenye watu wengine wanafanya; Yehova anaona mambo yenye kuwa mu moyo wako. Anafurahi wakati unaonyesha shukrani kutoka ku moyo kwa ajili ya zawadi yake ya muzuri sana, bei ya ukombozi.—1 Sa. 16:7; Mk. 12:41-44.

18. Juu ya nini tuko wenye shukrani kwa Yehova Mungu na Yesu Kristo?

18 Ni kupitia tu bei ya ukombozi njo tunasamehewa zambi zetu, tuko marafiki wa Yehova, na tuko na tumaini ya kuishi milele. Tuendelee basi kuonyesha kila siku shukrani juu ya upendo wa Yehova, wenye ulimuchochea atutolee zile baraka zote. (1 Yo. 4:19) Tuendelee pia kumuonyesha shukrani Yesu, mwenye alitupenda sana mupaka akatoa uzima wake wa kibinadamu kwa ajili yetu!—Yoh. 15:13.

WIMBO 154 Upendo Haushindwe

a Yehova alisamehe watumishi wake waaminifu wenye waliishi ku dunia zamani hata mbele Kristo atoe zabihu ya ukombozi. Yehova alifanya vile juu alikuwa hakika kama Mwana wake ataendelea kuwa muaminifu mupaka kifo. Kwa hiyo, kwa Yehova ilikuwa sawa vile zabihu ya ukombozi ilikuwa ilishatolewa.—Ro. 3:25.