Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

WIMBO 35 ‘Tuhakikishe Mambo ya Maana Zaidi’

Kamata Maamuzi Yenye Itamufurahisha Yehova

Kamata Maamuzi Yenye Itamufurahisha Yehova

“Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima, na kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi ni uelewaji.”MEZ. 9:10.

WAZO KUBWA

Namna ya kutumia ujuzi, uelewaji, na utambuzi juu ya kukamata maamuzi ya hekima.

1. Ni jambo gani ya nguvu yenye siye wote tunapaswa kufanya?

 KILA SIKU tunapaswa kukamata maamuzi. Maamuzi fulani ni ya mwepesi kukamata, sawa vile kuamua tutakula nini ao tutalala saa gani. Lakini kuko maamuzi yenye inakuwaka nguvu kukamata juu inaweza kuwa na matokeo juu ya afya yetu, juu ya wapendwa wetu, juu ya ibada yetu ao juu inaweza kutuletea ao kutukosesha furaha. Tunapenda kukamata maamuzi yenye itakuwa na matokeo ya muzuri juu yetu na juu ya familia yetu. Na zaidi ya yote, tunapenda kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova.—Ro. 12:1, 2.

2. Ni mambo gani itakusaidia kukamata maamuzi ya hekima?

2 Inawezekana ukamate maamuzi ya hekima kama (1) unatafuta habari zote, (2) unatafuta kujua mawazo ya Yehova juu ya ile jambo (3) unafikiria kwa uangalifu matokeo ya maamuzi yako. Hii habari itazungumuzia ile mambo tatu na itatusaidia pia kuona namna tunaweza kukomalisha sifa ya utambuzi.—Mez. 2:11.

TAFUTA KUJUA HABARI ZOTE

3. Toa mufano wenye kuonyesha juu ya nini unapaswa kutafuta habari zote mbele ya kukamata uamuzi.

3 Jambo ya kwanza yenye unapaswa kufanya juu ukamate uamuzi muzuri ni kutafuta kujua habari zote. Juu ya nini ni jambo ya maana kufanya vile? Wazia mutu mwenye kuwa na ugonjwa wa nguvu anaenda kuona munganga. Unawaza munganga ataamua ni matunzo gani ule mugonjwa anapaswa kupata bila kuchunguza hali yake ao kumuuliza maulizo? Hapana. Na weye utakamata maamuzi ya muzuri kama unatafuta kwanza kujua habari zote zenye zinahusu hali yako. Unaweza kufanya vile namna gani?

4. Kulingana na Mezali 18:13, utafanya nini juu upate habari zote? (Ona pia picha.)

4 Mara mingi kuuliza maulizo kutakusaidia kupata habari zote. Kwa mufano, tuseme wanakualika ku fete fulani. Utaenda? Kama haujue mwenye anakualika ao mipango yenye alikamata juu ya ile fete, itaomba umuulize maulizo sawa vile: “Fete itakuwa wapi na saa gani? Kutakuwa watu mingi ao kidogo? Nani njo ataisimamia? Nani wengine walialikwa? Ni mambo gani itafanywa kule? Kutakuwa pombe?” Majibu ya ile maulizo itakusaidia kukamata uamuzi wa hekima.—Soma Mezali 18:13.

Tafuta kujua habari zote kwa kuuliza maulizo (Ona fungu ya 4) a


5. Kisha kupata habari zote, unapaswa kufanya nini?

5 Kisha kupata habari zote, fikiria namna mambo itapitikana. Turudilie tena mufano yetu ya fete. Utafanya nini ukipata habari kama watu wenye hawaheshimie kanuni za Biblia watakuwa ku ile fete ao kutakuwa pombe na kila mutu atakunywa vile anapenda? Unawaza inawezekana ile fete ipitishe mipaka? (1 Pe. 4:3) Ao tena, utafanya nini kama saa ya ile fete njo saa ya mikutano ao ya kuenda mu mahubiri? Wakati unafikiria ile mambo yote, itakuwa mwepesi kwako kukamata uamuzi wa muzuri. Lakini kuko jambo ingine yenye unapaswa kufanya. Weye tayari uko na mawazo fulani, lakini ujiulize: Yehova yeye anawaza nini?—Mez. 2:6.

TAFUTA KUJUA MAWAZO YA YEHOVA

6. Kulingana na Yakobo 1:5, juu ya nini tunapaswa kumuomba Yehova atusaidie?

6 Umuombe Yehova akusaidie kuelewa mawazo yake. Yehova anaahidi kutupatia hekima yenye itatusaidia kujua ikiwa uamuzi wenye tunakamata unamufurahisha ao hapana. Anatupatia hekima “kwa ukarimu na bila kulaumu.”—Soma Yakobo 1:5.

7. Unaweza kufanya nini juu ujue mawazo ya Yehova? Toa mufano.

7 Kisha kumuomba Yehova muongozo wake, ukuwe muangalifu juu utambue jibu yake. Kwa mufano: Tuseme uko nasafiri, kisha unapotea. Unaweza kuuliza njia mutu wa ile eneo. Lakini, utauliza tu kisha unaenda bila kungoya jibu? Hapana. Utasikiliza kwa uangalifu muongozo wenye ule mutu anakupatia. Vilevile, kisha kumuomba Yehova hekima, tafuta kujua jibu yake kwa kutafuta sheria na kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yako. Kwa mufano, mbele ya kuamua kama utaenda ku fete yenye tulizungumuzia, unaweza kuchunguza mambo yenye Biblia inasema juu ya karamu za kupita kiasi, marafiki wabaya. Unaweza pia kuchunguza juu ya nini ni jambo ya lazima utie faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza kuliko mambo yenye unapenda.—Mt. 6:33; Ro. 13:13; 1 Ko. 15:33.

8. Utafanya nini kama uko na lazima ya musaada juu upate habari zenye uko natafuta? (Ona pia picha.)

8 Lakini, wakati fulani unaweza kuwa na lazima ya musaada juu upate habari zenye uko natafuta. Unaweza kuomba mashauri kwa ndugu ao dada mwenye kukomala kiroho. Lakini, ni muzuri pia kama unatafuta habari weye peke. Kuko habari mingi mu vyombo vyetu vya kutafuta habari, sawa vile kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova na broshua Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo. Kumbuka kama kusudi yako ni kukamata uamuzi wenye utamufurahisha Yehova.

Tafuta kujua mawazo ya Yehova (Ona fungu ya 8) b


9. Tutajua namna gani kama uamuzi wetu utamufurahisha Yehova? (Waefeso 5:17)

9 Tutajua namna gani kama uamuzi wetu utamufurahisha Yehova? Kwanza kabisa, tunapaswa kumujua Yehova muzuri. Biblia inasema hivi: “Kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi ni uelewaji.” (Mez. 9:10) Kwa kweli, kujua sifa za Yehova, kusudi yake na mambo yenye anapenda ao kuchukia, njo uelewaji wa kweli. Ujiulize hivi: ‘Kulingana na mambo yenye ninajua juu ya Yehova, ni uamuzi gani njo ninaweza kukamata wenye utamufurahisha?’—Soma Waefeso 5:17.

10. Juu ya nini kanuni za Biblia ni za maana zaidi kupita mawazo ya watu wa familia yetu ao desturi za mu eneo yetu?

10 Juu ya kumufurahisha Yehova, wakati fulani tunalazimika kukamata maamuzi yenye wengine hawafurahie. Kwa mufano, wazazi fulani wenye kuwa na nia ya muzuri wanaweza kukaza mutoto wao aolewe na mwanaume mwenye kuwa na makuta mingi ao mwenye ataleta mali ya mingi hata kama ule mwanaume hana hali ya muzuri ya kiroho. Ni kweli wanapenda mutoto wao asikose kitu kimwili; lakini nani njo atasaidia mutoto wao aendelee muzuri kiroho? Yehova iko na mawazo gani juu ya ile jambo? Matayo 6:33 inaonyesha mawazo ya Yehova. Mu ile andiko, Yesu anashauria Wakristo waendelee “kutafuta kwanza Ufalme.” Ni kweli kama tunapaswa kuheshimia wazazi wetu na watu wa mu eneo yetu, lakini jambo ya maana zaidi kwetu ni kumufurahisha Yehova.

FIKIRIA MATOKEO YA KILA UAMUZI

11. Wafilipi 1:9, 10 inazungumuzia sifa gani yenye inaweza kukusaidia kufikiria matokeo ya uamuzi wako?

11 Kisha kuchunguza kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yako, ni muzuri kufikiria matokeo yenye maamuzi fulani inaweza kuwa nayo. (Soma Wafilipi 1:9, 10) Utambuzi unaweza kukusaidia utambue matokeo ya kila uamuzi. Wakati fulani inaweza kuwa mwepesi kukamata uamuzi. Lakini haiko maamuzi yote njo inakuwaka mwepesi kukamata. Utambuzi utakusaidia kukamata maamuzi ya hekima hata mu hali za nguvu.

12-13. Namna gani utambuzi unaweza kukusaidia kukamata uamuzi muzuri kuhusu kazi?

12 Fikiria hii hali. Uko natafuta kazi ya kukusaidia kutimiza mahitaji ya familia yako. Unapata kazi mbili. Unatafuta kujua habari zote; kwa mufano ni kazi ya namna gani, programu ya kazi itakuwa namna gani, itakuwa nakamata wakati ngapi juu ya kufika ku kazi, na mambo ingine. Zile kazi zote mbili hazipingane na kanuni za Biblia. Pengine unafurahia zaidi kazi moya kati ya zile kazi mbili juu ni kazi yenye unapendaka ao juu watakuwa nakulipa makuta mingi. Lakini kuko mambo ingine ya kufikiria mbele ya kukamata uamuzi.

13 Kwa mufano, mu zile kazi mbili kuko yenye itakuzuia kukusanyika? Kuko yenye itakukula wakati mingi mupaka ukose wakati wa kupitisha pamoya na familia yako na kuitimizia mahitaji ya kiroho? Kujiuliza maulizo ya vile kutakusaidia utie “mambo ya maana zaidi,” ni kusema ibada na mahitaji ya familia yako, pa nafasi ya kwanza kuliko vitu vya kimwili. Kisha unaweza sasa kukamata uamuzi wenye Yehova atabariki.

14. Namna gani kuwa na utambuzi na kuonyesha upendo kutatusaidia tusikwaze wengine?

14 Utambuzi unatusaidia pia kufikiria matokeo yenye maamuzi yetu inaweza kuwa nayo juu ya wengine, ili tuepuke ‘kuwakwaza.’ (Flp. 1:10) Ile sifa ni ya maana sana wakati tuko nakamata maamuzi yenye inahusu mambo ya kipekee, sawa vile kuvala na kujipamba. Kwa mufano, pengine siye tunapendaka aina fulani ya kuvala na kujipamba. Lakini tutafanya nini kama ile inaweza kukwaza wengine mu kutaniko ao inje ya kutaniko? Utambuzi utatusaidia kuheshimia zamiri yao. Upendo utatusaidia kutafuta faida ya ‘wengine’ na kuwa na kiasi. (1 Ko. 10:23, 24, 32; 1 Ti. 2:9, 10) Kwa hiyo tutakamata uamuzi wenye unaonyesha kama tunapenda na kuheshimia wengine.

15. Inaomba kufanya nini mbele ya kukamata uamuzi juu ya jambo ya maana sana?

15 Kama unataka kukamata uamuzi kuhusu jambo fulani ya maana sana, fikiria mambo yote yenye inaomba ufanye juu utimize ule uamuzi. Yesu alisema kama tunapaswa “kuhesabia garama.” (Lu. 14:28) Kwa hiyo fikiria wakati, vitu, na nguvu yenye itakuomba juu ya kutimiza uamuzi wako. Wakati fulani, ni muzuri uzungumuze na watu ya familia yako juu ya kujua jambo yenye kila mutu mu familia anapaswa kufanya ili kutegemeza ule uamuzi. Juu ya nini ni muzuri kufanya vile? Ile inaweza kukusaidia kujua ikiwa unapaswa kubadilisha mambo fulani mu uamuzi wenye unataka kukamata ao ikiwa ni muzuri zaidi kukamata uamuzi ingine. Kama unazungumuza na watu wa familia yako na kusikiliza mawazo yao, watakuwa tayari kukutegemeza juu ule uamuzi ukuwe na matokeo ya muzuri.—Mez. 15:22.

KAMATA UAMUZI WENYE UTAKUWA NA MATOKEO YA MUZURI

16. Ni mambo gani yenye inaweza kukusaidia ukamate uamuzi wenye utakuwa na matokeo ya muzuri? (Ona pia kisanduku “ Namna ya Kukamata Maamuzi ya Hekima.”)

16 Kama unafuata mambo yenye tumezungumuzia, utakamata uamuzi wenye hekima. Kisha kupata habari zote na kuchunguza kanuni zenye zitakusaidia kukamata uamuzi wenye utamufurahisha Yehova, unaweza sasa kumuomba Yehova akusaidie juu uamuzi wako ukuwe na matokeo ya muzuri.

17. Siri ya kukamata maamuzi ya muzuri ni nini?

17 Hata kama maamuzi mingi yenye unakamataka inakuwaka na matokeo ya muzuri, kumbuka kama siri ya kukamata maamuzi ya muzuri ni kutegemea hekima ya Yehova, hapana akili na uzoefu wako. Yehova tu njo anatoa ujuzi wa kweli, uelewaji, na utambuzi; ile mambo tatu njo hekima. (Mez. 2:1-5) Yehova atakusaidia ukamate maamuzi yenye itamufurahisha.—Zb. 23:2, 3.

WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?

a MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu na dada vijana wako nazungumuzia mualiko wa kuenda ku fete yenye wanapata ku telefone.

b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moya kati yao iko nafanya utafiti mbele ya kuamua ikiwa ataenda ku ile fete.