Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

WIMBO 90 Tutiane Moyo

Namna ya Kupiganisha Mashaka

Namna ya Kupiganisha Mashaka

“Muchunguze mambo yote.”1 TE. 5:21.

WAZO KUBWA

Namna ya kupiganisha mashaka yenye inaweza kufanya usimutumikie Yehova muzuri.

1-2. (a) Watumishi fulani wa Yehova wako na mashaka juu ya mambo gani? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

 SIYE wote tunakuwaka na mashaka a wakati fulani hata tukuwe na miaka ngapi. Kwa mufano, wazia kijana mwenye ni Shahidi mwenye iko najiuliza ikiwa Yehova anamuhangaikia. Ile inaweza kufanya akuwe na mashaka kuhusu kubatizwa. Ao fikiria ndugu mwenye sasa ni mutu muzima, mwenye wakati alikuwa kijana aliamua kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza kuliko kutafuta makuta mingi. Juu sasa familia yake iko na magumu ya kupata makuta, anaweza kuanza kujiuliza ikiwa alikamata uamuzi wa muzuri. Wazia dada mwenye kuzeeka mwenye hana tena nguvu mingi. Anaweza kuvunjika moyo juu hawezi tena kufanya mambo yenye alikuwaka nafanya zamani. Ulishakajiuliza hii maulizo: ‘Yehova ananihangaikia kabisa? Nilifanya muzuri kujiima mambo fulani juu ya kumutumikia Yehova? Yehova angali anaweza kunitumikisha?’

2 Kama hatutafute majibu ya ile maulizo, ile inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya ibada yetu. Mu hii habari tutaona namna tunanaweza kukazia akili kanuni za Biblia wakati (1) tunashakia kama Yehova anatuhangaikia, (2) tunashakia kama maamuzi yenye tulikamataka ilikuwa ya muzuri, ao (3) tuko najiuliza ikiwa Yehova angali anaweza kututumikisha.

NAMNA YA KUMALIZA MASHAKA

3. Tunaweza kufanya nini juu ya kumaliza mashaka yetu?

3 Jambo moya yenye tunaweza kufanya juu ya kumaliza mashaka yetu, ni kujifunza Neno ya Mungu juu ya kupata majibu ya maulizo yenye kutuhangaisha. Kama tunafanya vile tutakuwa nguvu, tutakomala kiroho, na itakuwa mwepesi zaidi ‘kusimama imara katika imani.’—1 Ko. 16:13.

4. Namna gani tunaweza ‘kuchunguza mambo yote’? (1 Watesalonike 5:21)

4 Soma 1 Watesalonike 5:21. Hii andiko inatutia moyo ‘tuchunguze mambo yote.’ Tunaweza kufanya vile namna gani? Tujihakikishie kama mambo yenye tunaamini ni ya kweli kwa kuilinganisha na mambo yenye Biblia inasema. Kwa mufano, fikiria ule kijana mwenye iko najiuliza ikiwa Yehova anamuona kuwa wa maana. Anapaswa tu kuacha ile ulizo vile? Hapana, anapaswa ‘kuchunguza mambo yote’ kwa kutafuta kujua mawazo ya Yehova juu ya ile jambo.

5. Namna gani “tunasikia” majibu ya Yehova ku maulizo yetu?

5 Wakati tuko nasoma Neno ya Mungu “tunasikia” Yehova iko nazungumuza na siye. Lakini ili kujua mawazo yake juu ya jambo fulani, kuko jambo ingine yenye tunapaswa kufanya. Tunapaswa kutafuta maandiko yenye kuzungumuzia mambo yenye kutuhangaisha. Tunapaswa kutafuta habari kwa kutumia vyombo vya kutafuta habari vyenye tengenezo ya Yehova inatupatia. (Mez. 2:​3-6) Tunapaswa kusali kwa Yehova atusaidie wakati tuko natafuta habari kusudi tupate mawazo yake juu ya jambo yenye kutuhangaisha. Kisha tunaweza kutafuta kanuni za Biblia na habari zenye kuhusu hali yetu. Kujifunza habari za Biblia za batu benye balipambana na hali sawa yetu kunaweza pia kutusaidia.

6. Namna gani mikutano inatusaidia kupiganisha mashaka yetu?

6 Pia, “tunamusikia” Yehova ku mikutano yetu. Mu hotuba ao mu maelezo ya mutu fulani, tunaweza kusikia jambo fulani yenye tuko nayo lazima ili kupiganisha mashaka yetu. (Mez. 27:17) Tuone sasa namna tunaweza kupiganisha mashaka fulani.

WAKATI HAUKO HAKIKA KAMA YEHOVA ANAKUHANGAIKIA

7. Watu fulani wanaweza kujiuliza ulizo gani?

7 Ulishakajiuliza hii ulizo: ‘Yehova ananionaka kabisa?’ Kama unajionaka kuwa wa bure, inaweza kuwa nguvu kukubali kama unaweza kuwa rafiki ya Muumbaji wa bitu yote. Inawezekana Mufalme Daudi naye aliwaza vile. Alishangala kuona kama Yehova anahangaikia hata wanadamu, viumbe wa hali ya chini. Aliuliza hivi: “Ee Yehova, mwanadamu ni nini ili umutambue, mwana wa mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umukazie uangalifu?” (Zb. 144:3) Unaweza kupata wapi jibu ya ile ulizo?

8. Kulingana na 1 Samweli 16:​6, 7, 10-12, Yehova anaonaka nini wakati anaangalia batu?

8 Biblia inaonyesha kama Yehova anaona batu benye bengine banaona kuwa ba hali ya chini. Kwa mufano, Yehova alimutuma Samweli ku nyumba ya Yese juu atie mafuta mutoto wake umoya mwenye angefikia kuwa mufalme wa Israeli. Yese alikuwa na batoto banaume munane, lakini aliita batoto saba bakutane na Samweli. Hakuita Daudi mwenye alikuwa mudogo zaidi. b Lakini ni Daudi njo Yehova alichagua. (Soma 1 Samweli 16:​6, 7, 10-12.) Yehova aliona moyo wa Daudi, aliona kama alikuwa kijana mwanaume mwenye alihangaikia mambo ya kiroho.

9. Juu ya nini unapaswa kuwa hakika kama Yehova anakuhangaikia? (Ona pia picha.)

9 Fikiria mambo yenye Yehova amefanya juu ya kuonyesha kama anakujua. Anakupatia mashauri yenye inapatana kabisa na hali yako. (Zb. 32:8) Anaweza kufanya vile namna gani kama hakujue muzuri? (Zb. 139:1) Wakati unatumikisha mashauri ya Yehova na kuona namna inakusaidia, utakuwa hakika kama Yehova anakuhangaikia. (1 Ny. 28:9; Mdo. 17:​26, 27) Yehova anaona mambo yote yenye uko nafanya juu ya kumutii na kumutumikia. Yehova anaona sifa za muzuri zenye uko nazo na anapenda kuwa rafiki yako. (Yer. 17:10) Anapenda na weye ukubali kuwa rafiki yake.—1 Yo. 4:19.

“Kama unamutafuta, atajiacha umupate, lakini kama unamuacha, atakukataa milele.”—1 Ny. 28:9 (Ona fungu ya 9) c


WAKATI UKO NAJIULIZA IKIWA MAAMUZI YENYE ULIKAMATAKA ILIKUWA YA HEKIMA

10. Wakati tunafikiria maamuzi yenye tulikamataka zamani, tunaweza kujiuliza maulizo gani?

10 Kisha miaka, batu fulani banaweza kuangalia nyuma na kujiuliza ikiwa balikamataka maamuzi ya muzuri. Juu ya kumutumikia Yehova zaidi, pengine baliamua kuachana na kazi ao biashara yenye ingebaletea makuta ya mingi. Wakati murefu imepita ao hata kulishapita miaka mingi na pengine banajua batu fulani benye balikamata maamuzi tofauti, na benye sasa banaonekana kuwa na makuta mingi na maisha ya muzuri. Ile inaweza kufanya bajiulize hivi: ‘Nilifanya muzuri kujiima mambo fulani juu ya kumutumikia Yehova? Ao ile maamuzi inafanya nikose mambo fulani ya maana?’

11. Ni nini njo ilihangaisha muandikaji wa Zaburi 73?

11 Kama na weye uko najiuliza maulizo ya vile, fikiria namna muandikaji wa Zaburi 73 alijisikia. Aliona bengine banaonekana kuwa na afya ya muzuri na mali mingi, na banaonekana kuwa habana mahangaiko mu maisha. (Zb. 73:​3-5, 12) Wakati alibaangalia na kuona namna maisha yao ilionekana kuwa ya muzuri, aliona kama bidii yake ya kumutumikia Yehova ilikuwa ya bure. Ile mawazo yenye kuvunja moyo ‘ilimusumbua muchana wote.’ (Zb. 73:​13, 14) Alifanya nini juu ya kupiganisha ile mawazo?

12. Kulingana na Zaburi 73:​16-18, muandikaji wa zaburi alifanya nini juu ya kupiganisha mawazo yenye ilikuwa namuhangaisha?

12 Soma Zaburi 73:​16-18. Muandikaji wa zaburi alienda ku hekalu ya Yehova. Kule aliweza kufikiri muzuri. Alitambua kuwa hata kama bengine balionekana kuwa na maisha ya muzuri, habakukuwa na tumaini ya wakati wenye kuya. Kujua vile kulimusaidia kuwa na amani ya akili juu alijua kama kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza, ilikuwa uamuzi wa muzuri zaidi. Ile ilifanya aazimie tena zaidi kuendelea kumutumikia Yehova.—Zb. 73:​23-28.

13. Unaweza kufanya nini kama unakuwa na mashaka juu ya maamuzi yako ya zamani? (Ona pia picha.)

13 Na weye unaweza kupata ile amani ya akili kupitia Neno ya Mungu. Namna gani? Fikiria baraka zenye uko nazo. Kwa mufano weye uko na hazina mbinguni. Lakini bengine biko tu na mambo yenye hii ulimwengu inabatolea. Banaweza kutegemea sana vitu vyenye bamepata mu hii ulimwengu juu habana tumaini ya kupata kitu ingine wakati wenye kuya. Lakini weye, Yehova amekuahidi kama atakupatia baraka za mingi sana kupita vile unaweza kuwazia. (Zb. 145:16) Pia, fikiria hii jambo: Ni nani anajua maisha yake ingekuwa namna gani kama angekamata maamuzi tofauti? Hakuna. Tuko hakika na hii jambo: Benye banaamua kujiima mambo fulani juu banamupenda Mungu na jirani habakose kitu yoyote ya muzuri.

Kazia akili baraka zenye Yehova ameahidi (Ona fungu ya 13) d


WAKATI UNAWAZA KAMA YEHOVA HAWEZI TENA KUKUTUMIKISHA

14. Wakristo fulani wako mu hali gani, na wanaweza kujiuliza ulizo gani?

14 Batumishi fulani ya Yehova banateseka kwa sababu ya uzee, magonjwa, ao ulemavu. Ile inaweza kufanya bajisikie kuwa Yehova habaone kuwa ba maana. Banaweza kujiuliza hivi: ‘Yehova anaweza tena kunitumikisha?’

15. Muandikaji wa Zaburi 71 alikuwa hakika na jambo gani?

15 Muandikaji wa Zaburi 71 alikuwa pia na ile mahangaiko. Alisali hivi: “Usiniache wakati nguvu zangu zinaisha.” (Zb. 71:​9, 18) Lakini aliendelea kuwa hakika kama, ikiwa anamutumikia Yehova kwa uaminifu, Yehova atamuongoza na kumutegemeza. Sawa vile ule muandikaji wa zaburi alifikia kuelewa, Yehova anafurahia wale wenye wanafanya yao yote juu ya kuendelea kumutumikia hata kama hali yao inawatilia mipaka fulani.—Zb. 37:​23-25.

16. Namna gani Yehova anatumia Wakristo wenye kuzeeka? (Zaburi 92:​12-15)

16 Ndugu na dada wenye kuzeeka, mujione vile Yehova anawaona. Anaweza kuwasaidia kuwa nguvu kiroho hata kama hamuna tena nguvu mingi kimwili. (Soma Zaburi 92:​12-15.) Kuliko kukazia akili mambo yenye hauwezi kufanya, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya. Kwa mufano, unaweza kutia bengine nguvu kupitia mufano wako wa uaminifu na kwa kubaonyesha kama unabahangaikia. Unaweza kubaelezea namna Yehova amekutegemeza kwa miaka mingi na unaweza kuzungumuzia ahadi zenye uko nangoya kwa hamu sana zitimie. Pia usisahau hata siku moya kama sala zenye unatoa kwa ajili ya bengine zinaweza kuwa na matokeo ya muzuri sana. (1 Pe. 3:12) Hata tukuwe mu hali gani, siye wote tuko na jambo yenye tunaweza kumutolea Yehova na kutolea bengine.

17. Juu ya nini hatupaswe kujilinganisha na bengine?

17 Kama unahuzunika juu hauwezi kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova, ukuwe hakika kama Yehova anafurahia jambo yoyote yenye unafanya. Pengine umeanza kujilinganisha na bengine. Uepuke kufanya vile. Juu ya nini? Juu Yehova hatulinganishake na bengine. (Gal. 6:4) Kwa mufano, Maria alimutolea Yesu zawadi ya mafuta yenye marashi ya bei sana. (Yoh. 12:​3-5) Lakini mujane maskini alitoa ku hekalu feza mbili za kidogo zenye zilikuwa na samani ya kidogo sana. (Lu. 21:​1-4) Lakini, Yesu aliona kama wale wanamuke wote wawili walionyesha imani. Yehova Baba yake anafurahia kila kitu yenye unafanya juu umejitoa kwake na unamupenda, hata kama weye unaona ni ya kidogo sana.

18. Ni nini itakusaidia kuacha kuwa na mashaka? (Ona pia kisanduku “ Neno ya Yehova Inaweza Kukusaidia Kupiganisha Mashaka.”)

18 Wakati fulani siye wote tunakuwaka na mashaka, lakini sawa vile tumeona, Biblia Neno ya Mungu yenye kutegemeka na yenye haiseme uongo inaweza kutusaidia kupiganisha ile mashaka. Kwa hiyo, uazimie kupiganisha mashaka yako juu isikuvunje moyo. Kwa kweli, Yehova anakujua weye kipekee. Anaona mambo yote yenye ulijiima juu ya kumutumikia na anaahidi kukubariki. Anaona batumishi yake bote baaminifu kuwa ba maana, anabapenda, na kubahangaikia.

WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

a MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu hii habari tuko nazungumuzia mashaka yenye inafanya tujiulize ikiwa Yehova anatuoa kuwa wa maana, ao ikiwa tulikamata maamuzi yenye hekima. Ile mashaka haiko njo yenye Biblia inasema kama inaweza kuonyesha kuwa mutu hamuamini Yehova na ahadi zake.

b Hata kama Biblia haiseme Daudi alikuwa na miaka ngapi wakati Yehova alimuchagua, inawezekana alikuwa angali kijana.—Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 9, 2011, uku. 29, fu. 2.

c MAFASIRIO YA PICHA : Juu ya kujua mawazo ya Yehova kuhusu hali yake, kijana Shahidi iko natafuta mashauri mu Biblia.

d MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anafanya kazi ya mikono juu ya kutegemeza familia yake. Lakini iko nafikiria baraka zenye tutapata mu Paradiso.