Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 42

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

Onyesha Shukrani Juu ya “Zawadi Katika Wanadamu”

Onyesha Shukrani Juu ya “Zawadi Katika Wanadamu”

“Wakati alipanda juu . . . , alitoa zawadi katika wanadamu.”EFE. 4:8.

WAZO KUBWA

Namna watumishi wa huduma, wazee, na waangalizi wa muzunguko wanatusaidia, na namna tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya mambo yenye wale wanaume waaminifu wanafanya.

1. Yesu ametupatia zawadi gani?

 HAKUNA mwanadamu mwenye amekuwa mukarimu sana sawa Yesu. Wakati alikuwa ku dunia alikuwa tayari kutumia nguvu yake ya kufanya miujiza juu ya kusaidia bengine. (Lu. 9:12-17) Alitutolea zawadi kubwa zaidi wakati alitoa uzima wake kwa ajili yetu. (Yoh. 15:13) Tangu afufuliwe ameendelea kuwa mukarimu. Sawa vile aliahidi, alimuomba Yehova atumwangie roho yake takatifu juu itufundishe na kutufariji. (Yoh. 14:16, 17, maelezo ya chini; 16:13) Na kupitia mikutano yetu, Yesu anaendelea kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima juu ya kufanya wanafunzi mu dunia yote.—Mt. 28:18-20.

2. Ni nani wako kati ya “zawadi katika wanadamu” wenye kuzungumuziwa mu Waefeso 4:7, 8?

2 Yesu ametupatia zawadi ingine. Mutume Paulo aliandika kama kisha Yesu kupanda mbinguni, “alitoa zawadi katika wanadamu.” (Soma Waefeso 4:7, 8.) Paulo alifasiria kama kisha Yesu kupanda mbinguni, alitoa ile zawadi ili isaidie kutaniko mu njia mbalimbali. (Efe. 1:22, 23; 4:11-13) Leo kati ya “zawadi katika wanadamu” kuko watumishi wa huduma, wazee wa kutaniko, na waangalizi wa muzunguko. a Kusema kweli bale banaume habakamilike na banafanyaka makosa. (Yak. 3:2) Lakini Bwana wetu, Yesu Kristo, anabatumia juu ya kutusaidia. Bale banaume ni zawadi yenye Yesu ametupatia

3. Toa mufano wenye kuonyesha namna siye bote tunaweza kutegemeza kazi ya ndugu wenye kuwa “zawadi katika wanadamu.”

3 Yesu aliweka banaume benye kuwa “zawadi katika wanadamu” ili kujenga kutaniko. (Efe. 4:12) Na siye bengine tunaweza kubasaidia kutimiza ile daraka ya maana. Kwa mufano tufikirie kazi ya ujenzi: Bamoya kati yetu banasaidia kujenga Majumba ya Ufalme. Bengine banategemeza kazi ya kujenga kwa kuleta chakula na vitu mbalimbali, ao banategemeza mu njia ingine. Vilevile siye bote tunaweza kutegemeza kazi ya watumishi wa huduma, wazee wa kutaniko, na waangalizi wa muzunguko kupitia mambo yenye tunasema na kufanya. Tuone namna kazi yao inatuletea faida na namna tunaweza kuwaonyesha shukrani, na pia namna tunaweza kuonyesha shukrani Yesu mwenye alitupatia wale “zawadi katika wanadamu.”

WATUMISHI WA HUDUMA WANAFANYA “UTUMISHI WA KUSAIDIA”

4. Taya “utumishi wa kusaidia” wenye watumishi wa huduma walifanya mu karne ya kwanza?

4 Mu karne ya kwanza ndugu fulani waliwekwa kuwa watumishi wa huduma. (1 Ti. 3:8) Inaonekana kama ni wao njo walifanya “utumishi wa kusaidia” ao kazi fulani za kusaidia zenye Paulo alizungumuzia. (1 Ko. 12:28) Ni wazi kama watumishi wa huduma walisaidia kufanya kazi fulani juu wazee wakazie zaidi kazi ya kufundisha na ya uchungaji. Kwa mufano, inawezekana ni watumishi wa huduma njo walisaidia kufanya kopi za Maandiko ao pengine walikuwa naenda kuuza vitu vya kutumia ili kufanya kopi.

5. Ni kazi gani za kusaidia zenye watumishi wa huduma wanafanya leo?

5 Fikiria kazi mbalimbali zenye watumishi wa huduma wanafanya juu ya kusaidia kutaniko yenu. (1 Pe. 4:10) Wanaweza kupewa mugao wa kushugulikia mambo ya makuta ao eneo, kufanya ombi ya vichapo na kuvitolea wahubiri, kutumika ku audio-video, kutumika ku ukaribishaji, ao kusaidia kutunza Jumba ya Ufalme. Zile kazi zote ni za maana juu kutaniko itumike muzuri. (1 Ko. 14:40) Zaidi ya ile watumishi wa huduma fulani wanafanya vipindi ku mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo, na wanatoa hotuba za watu wote. Mutumishi wa huduma anaweza pia kuwekwa kuwa musaidizi wa mwangalizi wa kikundi ya mahubiri. Wakati fulani watumishi wa huduma wenye kustahili wanasindikiza wazee mu ziara za uchungaji.

6. Juu ya nini tuko wenye shukrani sana kwa watumishi wa huduma?

6 Namna gani kazi ya watumishi wa huduma inasaidia kutaniko. Dada Beberly b wa mu inchi ya Bolivia, anaseme hivi: “Juu ya mambo yote yenye watumishi wa huduma wanafanya, ninafurahia mikutano. Ninaweza kuimba, kutoa maelezo, kusikiliza hotuba, na kujifunza kupitia video na picha. Wanahangaikia usalama na wanahangaikia wale wenye wanafuata mikutano kupitia vidéoconférence. Kisha mikutano wao njo wa kwanza kufanya usafi, wanashugulikia visanduku vya michango, na wanahakikisha kama tuko na vichapo vyenye tuko navyo lazima. Niko mwenye shukrani sana juu ya mambo yote yenye wanafanya!” Leslie, mwenye anaishi Kolombia na mwenye bwana yake ni muzee wa kutaniko, anasema hivi: “Musaada wenye watumishi wa huduma wanamutolea bwana yangu inamusaidia atimize muzuri migao yake mbalimbali. Bila watumishi wa huduma, bwana yangu angekuwa na mambo mingi sana ya kufanya. Kwa hiyo, niko mwenye shukrani juu ya bidii yao na roho yao ya kupenda kusaidia.” Bila shaka na weye unakubaliana na ile maneno ya shukrani.—1 Ti. 3:13.

7. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani watumishi wa huduma? (Ona pia picha.)

7 Haitoshe tu kuwa wenye shukrani juu ya mambo yenye watumishi wa huduma wanafanya. Biblia inatushauria hivi: Mujionyeshe  kuwa wenye shukrani.” (Kol. 3:15) Krzysztof, muzee mu inchi ya Finlandi, anasema hivi juu ya namna anaonyeshaka shukrani: “Ninatumiaka mutumishi wa huduma karte ao ujumbe. Ku ile karte ao ujumbe ninatayaka andiko fulani na mambo fulani yenye mutumishi wa huduma alifanya yenye ilinitia moyo, na ninaelezaka juu ya nini niko mwenye shukrani juu ya kazi yake.” Pascal na Jael, wa mu Nouvelle Calédonie, wanasali kwa ukawaida juu ya watumishi wa huduma. Pascal anasema hivi: “Hivi karibuni tulisali sana juu ya watumishi wa huduma. Tulimushukuru Yehova juu ya bale banaume, na tulimuomba abasaidie.” Yehova anasikilizaka sala za vile na zinaletea kutaniko yote faida.—2 Ko. 1:11.

WAZEE WA KUTANIKO “WANAFANYA KAZI KWA BIDII KATI YENU”

8. Juu ya nini Paulo aliandika kama wazee wa mu karne ya kwanza ‘walifanya kazi kwa bidii’? (1 Watesalonike 5:12, 13)

8 Wazee wa mu karne ya kwanza walitumika kwa bidii kwa ajili ya kutaniko. (Soma 1 Watesalonike 5:12, 13; 1 Ti. 5:17) ‘Walisimamia’ kutaniko. Kwa mufano waliongoza mikutano na walikamata maamuzi wakiwa baraza za wazee. ‘Walionya’ ndugu na dada zao kwa kuwapatia mashauri yenye kuwa wazi lakini yenye upendo ili kulinda kutaniko. (1 Te. 2:11, 12; 2 Ti. 4:2) Wale wanaume walitumika pia kwa bidii juu ya kutimiza mahitaji ya familia zao na kuendelea kuwa nguvu kiroho.—1 Ti. 3:2, 4; Tit. 1:6-9.

9. Leo wazee wanafanya kazi gani mbalimbali?

9 Leo wazee wako na mambo mingi ya kufanya. Ni waeneza-injili. (2 Ti. 4:5) Wanafanya kazi ya kuhubiri kwa bidii, wanapanga eneo ya kuhubiri ya kutaniko, na wanatuzoeza kuhubiri na kufundisha muzuri. Wanatumikaka kama waamuzi wenye huruma na wenye hawana upendeleo. Wakati Mukristo anafanya zambi nzito, wazee wanajikaza kumusaidia juu arudishe tena uhusiano wake pamoya na Yehova. Hata vile, ni waangalifu juu waendelee kulinda usafi wa kutaniko. (1 Ko. 5:12, 13; Gal. 6:1) Lakini, wazee wanajulikana zaidi sana kuwa wachungaji. (1 Pe. 5:1-3) Wanatoa hotuba zenye kutegemea Maandiko zenye kutayarishwa muzuri, wanajikaza kujua kila mutu mu kutaniko, na wanafanya ziara za uchungaji. Zaidi ya migao yao ingine, wazee fulani wanasaidia mu kazi ya kujenga na kutunza Majumba ya Ufalme, kupanga mikusanyiko, kutumika mu Halmashauri za Uhusiano na Hopitali na mu Vikundi vya Kutembelea Wagonjwa. Wazee wanatumika kwa bidii kwa ajili yetu!

10. Juu ya nini tuko wenye shukrani kwa sababu ya kazi ya nguvu yenye wazee wanafanya?

10 Yehova alitabiri kama wachungaji wangetuhangaikia na kama ‘hatungeogopa tena wala kutetemeshwa.’ (Yer. 23:4) Johanna, dada wa Finlandi, alijionea ile jambo wakati mama yake alikuwa mugonjwa sana. Anasema hivi: “Hata kama inakuwaka nguvu kwangu kuelezea wengine namna niko najisikia, muzee mwenye sikukuwa najua muzuri, alinivumilia, alisali pamoya na miye, na alinihakikishia kama Yehova ananipenda. Sikumbuke kabisa mambo yenye alisema, lakini ninakumbuka kama nilijisikia kuwa salama. Ninaamini kama Yehova alimutuma juu ya kunisaidia kwa wakati wenye kufaa.” Wazee wa mu kutaniko yako wamekusaidia namna gani?

11. Namna gani tunaweza kuonyesha wazee shukrani? (Ona pia picha.)

11 Yehova anapenda tuonyeshe wazee shukrani “kwa sababu ya kazi yao.” (1 Te. 5:12, 13) Henrietta, mwenye anaishi pia Finlandi, anasema hivi: “Wazee wanapenda kusaidia wengine, lakini ile haimaanishe kama wako na wakati na nguvu mingi kupita wengine. Na haimaanishe kama hawana magumu mu maisha yao. Wakati fulani ninaambiaka muzee, “Unajua, uko muzee muzuri sana. Nilipenda tu ujue vile.” Dada Sera wa Uturuki anasema hivi: “Wazee wako na lazima ya kutiwa moyo juu waendelee na kazi yao. Kwa hiyo, tunaweza kuwaandikia ujumbe, kuwaalika kwa ajili ya chakula, ao kuhubiri pamoya nao.” Kuko muzee mwenye unafurahiaka sana mwenye ungependa kushukuru? Tafuta njia za kufanya vile.—1 Ko. 16:18.

Unaweza kutia moyo wazee ili waendelee kutimiza kazi yao (Ona fungu ya 7, 11, 15)


WAANGALIZI WA MUZUNGUKO WANATUJENGA

12. Ni mupango gani ulisaidia kujenga makutaniko mu karne ya kwanza? (1 Watesalonike 2:7, 8)

12 Yesu alipatia kutaniko “zawadi katika wanadamu” wenye wanatumika mu njia ingine. Chini ya muongozo wake, wazee katika Yerusalemu walituma Paulo na Barnaba na wengine wakuwe waangalizi wenye kusafiri. (Mdo. 11:22) Juu ya nini? Sababu ni ileile yenye inafanya watumishi wa huduma na wazee wawekwe: Ili kujenga kutaniko. (Mdo. 15:40, 41) Bale banaume banajiima mambo mingi na hata banaweka uzima wao mu hatari juu ya kufundisha na kutia moyo bengine.—Soma 1 Watesalonike 2:7, 8.

13. Waangalizi wa muzunguko wanafanya kazi gani mbalimbali?

13 Waangalizi wa muzunguko hawabakiake tu fasi moya. Waangalizi fulani wanafanya safari za murefu juu ya kutembelea makutaniko. Kila juma mwangalizi wa muzunguko anatoaka hotuba mbalimbali, anafanyaka ziara za uchungaji, anaongozaka mukutano wa mapainia, mukutano wa wazee, na mikutano kwa ajili ya mahubiri. Zaidi ya ile, anatayarishaka hotuba mbalimbali na anapangaka mikusanyiko ya mizunguko na ya eneo. Anafundishaka masomo ya mapainia, anapangaka mukutano wa pekee pamoya na mapainia wa mu muzunguko wake, na anafanyaka mambo ingine. Pia wakati fulani tawi inamuombaka ashugulikie mambo fulani ya haraka.

14. Juu ya nini tunapaswa kuonyesha shukrani waangalizi wa muzunguko?

14 Waangalizi wa muzunguko wanasaidia kutaniko namna gani? Ndugu fulani wa Uturuki anasema hivi juu ya ziara ya waangalizi wenye kusafiri: “Kila ziara yao inanichochea nitumie wakati mingi juu ya kusaidia ndugu na dada zangu. Nilishakakutana na waangalizi wengi wa muzunguko, lakini hakuna hata umoya mwenye alionekana kama hana wakati wa kuzungumuza na miye ao alifanya nione kama iko na kazi mingi sana.” Johanna, mwenye tulizungumuzia alihubiri pamoya na mwangalizi wa muzunguko lakini hawakukuta mutu yeyote ku nyumba. Johanna anasema hivi: “Nitaendelea kukumbuka ile siku. Dada zangu walikuwa wamehamia mbali na nilikuwa nawakumbuka. Mwangalizi wa muzunguko alinitia moyo na alinisaidia kuelewa kama mu kazi ya Yehova kuwa mbali na watu wenye tunapenda ni tatizo ya wakati mufupi. Lakini mu dunia mupya tutakuwa na nafasi mingi za kupitisha wakati pamoya.” Wengi kati yetu wanapenda sana waangalizi wa muzunguko wenye wanatutumikia.—Mdo. 20:37–21:1.

15. (a) Kulingana na 3 Yohana 5-8, namna gani tunaweza kuonyesha shukrani waangalizi wa muzunguko? (Ona pia picha.) (b) Juu ya nini tunapaswa kuonyesha shukrani bibi za ndugu wenye kuwa na madaraka, na namna gani tunaweza kufanya vile? (Ona kisanduku “ Mukumbuke Bibi Zao.”)

15 Mutume Yohana alitia moyo Gayo akaribishe muzuri ndugu wenye waliwatembelea na ‘ashugulikie safari yao katika njia yenye inamufaa Mungu.’ (Soma 3 Yohana 5-8.) Tunaweza kufanya vile kwa kualika mwangalizi wa muzunguko kwa ajili ya chakula. Njia ingine ya kufanya vile ni kutegemeza mupango wa mahubiri mu juma ya pekee. Leslie, mwenye tulizungumuzia anaonyeshaka shukrani mu njia ingine. Anasema hivi: “Ninasali Yehova awapatie mambo yenye wako nayo lazima. Pia miye na bwana yangu tunawaandikiaka barua juu ya kuwaambia namna ziara yao ilitusaidia sana.” Kumbuka kama waangalizi wa muzunguko ni watu wa kawaida. Wakati fulani wanagonjwa, wanakuwa na mahangaiko, na hata kuvunjika moyo. Pengine ni maneno yako yenye upendo ao zawadi yako ya kidogo njo jibu ku sala ya mwangalizi wenu wa muzunguko!—Mez. 12:25.

TUKO NA LAZIMA YA “ZAWADI KATIKA WANADAMU”

16. Kulingana na Mezali 3:27, ndugu wanapaswa kujiuliza ulizo gani?

16 Mu dunia yote tuko na lazima ya ndugu wengi zaidi wa kutumikia kama “zawadi katika wanadamu.” Kama uko ndugu mwenye kubatizwa, “uko na uwezo wa kusaidia”? (Soma Mezali 3:27.) Uko tayari kutimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa mutumishi wa huduma? Unaweza kutimiza mambo yenye inaombwa ili ufikie kuwa muzee, juu usaidie kutimiza mahitaji ya ndugu zako? c Unaweza kubadilisha mambo fulani mu maisha yako juu ufikie kujaza fomu ya kuenda ku Masomo ya Waeneza-injili wa Ufalme? Ku ile masomo utajifunza mambo mingi yenye itakusaidia juu Yesu aweze kukutumikisha zaidi. Ikiwa unaona kama haustahili, sali kwa Yehova. Umuombe akusaidie na roho yake takatifu juu utimize muzuri mugao wowote wenye unapewa.—Lu. 11:13; Mdo. 20:28.

17. Juu Mufalme wetu Kristo Yesu ametutolea “zawadi katika wanadamu,” ile inaonyesha nini juu yake?

17 Juu Yesu ametutolea ndugu wenye kuwa “zawadi katika wanadamu,” ile inaonyesha kama iko natuongoza mu hizi siku za mwisho. (Mt. 28:20) Kwa kweli, tuko wenye shukrani juu Mufalme wetu ni mwenye upendo, ni mukarimu, na anatutolea wanaume wenye kustahili juu watimize mahitaji yetu. Kwa hiyo, tutafute nafasi za kuonyesha shukrani wale wanaume wenye bidii. Na tusisahau kumushukuru Yehova mwenye anatoa “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.”—Yak. 1:17.

WIMBO 99 Ndugu na Dada Wote

a Wazee wenye kuwa mu Baraza Yenye Kuongoza, wasaidizi wa Baraza Yenye Kuongoza, wazee wa mu Halmashauri za Tawi, na wazee wenye kutumikia migao ingine ya utumishi, wao pia ni “zawadi katika wanadamu.”

b Majina fulani imebadilishwa.

c Juu ya kupata habari zaidi juu ya namna ya kutimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa mutumishi wa huduma ao muzee, ona habari “Ndugu—Muko Najikaza Juu Mufikie kuwa Watumishi wa Huduma?” na “Ndugu—Muko Najikaza Juu Mufikie Kuwa Wazee?” zenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 11, 2024.