Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 45

WIMBO 138 Uzuri wa Kichwa Yenye Imvi

Maneno ya Mwisho-Mwisho ya Banaume Baaminifu Inakufundisha Nini?

Maneno ya Mwisho-Mwisho ya Banaume Baaminifu Inakufundisha Nini?

“Je, haiko wazee ndio wenye kuwa na hekima, na je, uelewaji haukuje kwa sababu ya kuishi siku nyingi?”YOB. 12:12.

WAZO KUBWA

Kumutii Yehova Mungu kunaleta baraka mingi leo, na uzima wa milele wakati wenye kuya.

1. Juu ya nini tunaweza kujifunza mambo mingi kutoka kwa batu benye kuzeeka?

 Siye bote tuko na lazima ya muongozo juu ya kukamata maamuzi ya maana mu maisha yetu. Wazee na Wakristo wengine wenye kukomala kiroho wanaweza kutupatia ule muongozo. Kama wako na miaka mingi kutupita, tusiwaze mara moya kama mashauri yao ni ya zamani na haina tena faida leo. Yehova anapenda tujifunze mambo fulani kutoka kwa batu benye kukomala. Bameishi miaka mingi, kwa hiyo biko na uzoefu, uelewaji, na hekima.—Yob. 12:12.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Zamani, Yehova alitumia batu baaminifu benye kuzeeka juu ya kutia moyo batu yake na kubaongoza. Kwa mufano alitumia Musa, Daudi, na mutume Yohana. Bale banaume baliishi mu vipindi tofauti na hali zao zilikuwa tofauti kabisa. Wakati balikaribia kufa, balipatia vijana mashauri yenye hekima. Kila mumoya wao alikazia kama ni jambo ya maana kumutii Mungu. Yehova aliandikisha maneno yao yenye hekima juu itusaidie leo. Ikuwe tuko vijana ao wazee, tunaweza kujifunza mambo mingi kupitia ile mashauri. (Ro. 15:4; 2 Ti. 3:16) Mu hii habari, tutazungumuzia maneno ya mwisho-mwisho ya bale banaume batatu benye kuzeeka na mambo yenye ile maneno inatufundisha.

“UTAFANYA WAKATI MUREFU”

3. Musa alikuwa na migao gani?

3 Musa alimutumikia Yehova kwa moyo wake wote. Alikuwa nabii, muamuzi, kiongozi, na muandikaji. Musa alijionea mambo mingi mu maisha! Aliongoza Waisraeli kutoka mu utumwa Misri na alijionea miujiza mingi ya Yehova. Yehova alimutumikisha juu ya kuandika vitabu tano vya kwanza vya Biblia, Zaburi 90, na inawezekana Zaburi 91. Pia inawezekana ni Musa njo aliandika kitabu ya Yobu.

4. Musa alitia moyo nani, na juu ya nini?

4 Wakati kidogo mbele akufe, wakati alikuwa na miaka 120, Musa aliita Waisraeli wote juu ya kuwakumbusha mambo yenye walikuwa wameona. Wamoya Waisraeli wenye walikuwa namusikiliza Musa, walijionea, wakati balikuwa vijana namna Yehova alifanya miujiza mingi na namna alihukumu Wamisri. (Kut. 7:​3, 4) Walitembea ku inchi kavu wakati mayi ya Bahari Nyekundu iliachanishwa, na waliona namna maaskari wa Farao waliharibiwa. (Kut. 14:​29-31) Wakati walikuwa mu jangwa, waliona vile Yehova aliwalinda na kuwahangaikia. (Kum. 8:​3, 4) Taifa ya Israeli ilikuwa sasa karibu kuingia mu inchi ya ahadi na Musa alitumia ile nafasi ya mwisho juu ya kuwatia moyo. a

5. Maneno ya mwisho-mwisho ya Musa yenye kuwa mu Kumbukumbu la Torati 30:​19, 20 ilihakikishia nini Waisraeli?

5 Musa alisema nini? (Soma Kumbukumbu la Torati 30:​19, 20.) Musa aliambia Waisraeli kama wangeweza kuwa na maisha ya muzuri mu siku zenye kuya. Yehova angewabariki na wangeishi wakati murefu mu inchi yenye aliwaahidi. Ilikuwa inchi ya muzuri sana na ilitoa chakula mingi! Musa aliwaambia hivi juu ya ile inchi: “Miji mikubwa na yenye kupendeza yenye haukujenga, nyumba zenye kujaa vitu vya muzuri vya namna mbalimbali vyenye haukufanya kazi ili kuvipata, matangi yenye haukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni yenye haukupanda.”—Kum. 6:​10, 11.

6. Juu ya nini Mungu aliruhusu mataifa ingine ipate ushindi juu ya Israeli?

6 Musa alipatia pia Waisraeli onyo. Juu waendelee kuishi mu ile inchi ya muzuri sana, walipaswa kutii amri za Yehova. Musa aliwashauria ‘wachague uzima’ kwa kumusikiliza Yehova na kwa “kushikamana naye.” Lakini, Waisraeli hawakumutii Yehova. Kwa hiyo kisha wakati, Yehova aliruhusu Waashuru na kisha Wababiloni wapate ushindi juu yao na kuwapeleka mu uhamisho.—2 Fa. 17:​6-8, 13, 14; 2 Ny. 36:​15-17, 20.

7. Maneno ya Musa inaweza kutufundisha nini? (Ona pia picha.)

7 Tunajifunza nini? Kutii kunaleta uzima. Kama Waisraeli wenye walikuwa karibu kuingia mu inchi ya ahadi, tuko karibu kuingia mu ulimwengu mupya wenye Mungu ameahidi, dunia yote itageuzwa kuwa paradiso. (Isa. 35:1; Lu. 23:43) Shetani na pepo wake wachafu hawatakuwa tena. (Ufu. 20:​2, 3) Hakutakuwa dini za uongo za kufanya watu wasimukaribie Yehova. (Ufu. 17:16) Hakutakuwa serikali za wanadamu zenye kutesa batu. (Ufu. 19:​19, 20) Mu paradiso hamutakuwa waasi. (Zb. 37:​10, 11) Fasi yote batu batatii sheria zenye haki za Yehova, na ile itafanya kukuwe umoja na amani. Kwa hiyo, batu batapendana na kutumainiana. (Isa. 11:9) Ile ni tumaini ya ajabu sana! Zaidi ya ile, kama tunamutii Yehova, tutaendelea kuishi mu paradiso, hapana tu mamia ya miaka, lakini milele.—Zb. 37:29; Yoh. 3:16.

Kama tunamutii Yehova, tutaishi mu paradiso, hapana tu mamia ya miaka, lakini milele (Ona fungu ya 7)


8. Namna gani ahadi ya kuishi milele ilisaidia ndugu moya mwenye amekuwa misionere kwa miaka mingi? (Yuda 20, 21)

8 Kama tunaendelea kufikiria ahadi ya kuishi milele yenye Mungu ametupatia, tutapenda kushikamana naye hata tupambane na magumu gani. (Soma Yuda 20, 21.) Ile ahadi inaweza pia kutupatia nguvu ya kupiganisha uzaifu wetu. Ndugu moya mwenye amekuwa misionere kwa miaka mingi mu Afrika, mwenye alipiganisha uzaifu fulani kwa wakati murefu, anasema hivi: “Juu nilitambua kama uzaifu wangu ungefanya nipoteze tumaini yangu ya kuishi milele, niliazimia kabisa kuupiganisha na kumulilia Yehova anisaidie. Kwa musaada wa Yehova, niliweza kupiganisha uzaifu wangu.”

“UTAPATA MATOKEO YA MUZURI”

9. Daudi alipata magumu gani mu maisha yake?

9 Daudi alikuwa mufalme, mwanamuziki, mutunga-mashahiri, mupiganaji-vita, na nabii. Alipata magumu mingi. Kwa miaka fulani alikuwa mukimbizi; alikuwa nakimbia Mufalme Sauli, mwenye alikuwa namusikilia wivu. Kisha kuwa mufalme, Daudi alikimbia tena juu ya kuokoa uzima wake wakati mwana wake Absalomu alijaribu kumunyanganya ufalme. Hata kama alipata Daudi ile magumu yote na alifanya makosa fulani, aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu mupaka mwisho wa maisha yake. Na hata Yehova alimuita kuwa “mutu mwenye kufurahisha moyo [wake].” Bila shaka mashauri ya Daudi inaweza kutusaidia!—Mdo. 13:22; 1 Fa. 15:5.

10. Juu ya nini Daudi alipatia mwana wake Sulemani mashauri mbele akuwe mufalme?

10 Kwa mufano, fikiria mashauri yenye Daudi alipatia mwana wake Sulemani, mbele akuwe mufalme. Yehova alichagua kijana Sulemani juu aendeleshe ibada safi na ajenge hekalu yenye ingemuletea sifa. (1 Ny. 22:5) Sulemani angepambana na magumu. Daudi alimuambia nini? Acha tuone.

11. Mu 1 Wafalme 2:​2, 3, Daudi alimuhakikishia Sulemani nini, na namna gani ile maneno ilionekana kuwa ya kweli kabisa? (Ona pia picha.)

11 Daudi alisema nini? (Soma 1 Wafalme 2:​2, 3.) Daudi alimuambia mwana wake kama ikiwa anamutii Yehova, atapata matokeo ya muzuri mu maisha. Na kwa miaka mingi, Sulemani alipata matokeo ya muzuri. (1 Ny. 29:​23-25) Alijenga hekalu ya ajabu, na hata aliandika vitabu fulani vya Biblia. Alijulikana sana juu ya hekima na utajiri wake. (1 Fa. 4:34) Lakini sawa vile Daudi alisema, Sulemani angeendelea kupata matokeo ya muzuri kama tu anaendelea kumutii Yehova Mungu. Jambo ya kuhuzunisha ni kama, ku mwisho-mwisho wa maisha yake, Sulemani alianza kuabudu miungu ingine. Yehova hakumukubali tena, na Sulemani alipoteza hekima ya kuongoza taifa mu njia ya muzuri na ya haki.—1 Fa. 11:​9, 10; 12:4.

Maneno ya mwisho-mwisho yenye Daudi aliambia mwana wake Sulemani inatusaidia kuelewa kama ikiwa tunamutii Yehova, atatupatia hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri (Ona fungu ya 11-12) b


12. Maneno ya Daudi inaweza kutufundisha nini?

12 Tunajifunza nini? Kutii kunaleta matokeo ya muzuri. (Zb. 1:​1-3) Kusema kweli, Yehova hatuahidi kama atatupatia utajiri na utukufu sawa Sulemani. Lakini kama tunatii Mungu wetu, atatupatia hekima yenye itatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. (Mez. 2:​6, 7; Yak. 1:5) Kanuni zake zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri mu mambo sawa vile kazi, masomo, mambo ya kujifurahisha, na makuta. Kutumikisha hekima yenye kutoka kwa Yehova kunaweza kutulinda juu tusipate matokeo ya mubaya yenye inaweza kutukosesha uzima wa milele. (Mez. 2:​10, 11) Tutapata marafiki wazuri na tutapata muongozo wenye utatusaidia tukuwe na furaha mu familia.

13. Ni nini ilimusaidia Carmen apate matokeo ya muzuri mu maisha?

13 Carmen, mwenye anaishi mu Mozambique, aliwaza kama kusoma masomo ya juu njo kutamusaidia akuwe na maisha ya muzuri. Alijiandikisha ku masomo ya juu na akaanza kusoma mambo yenye kuhusu majengo. Aliandika hivi: “Nilipenda mambo yenye nilikuwa najifunza. Lakini ilinikamata wakati mingi na nguvu mingi. Nilikuwa ku masomo kuanzia saa moya na nusu ya asubui (7h30) mupaka saa kumi na mbili ya mangaribi (18h00). Ilikuwa nguvu kwangu kuenda ku mikutano, na hali yangu ya kiroho iliharibika. Mu moyo wangu, nilianza kuona kama nilikuwa najaribu kutumikia mabwana wawili.” (Mt. 6:24) Carmen alisali juu ya hali yake na alitafuta habari mu bichapo. Alisema tena hivi: “Kisha kupata mashauri ya muzuri kutoka kwa ndugu wenye kukomala kiroho na kutoka kwa mama yangu, niliamua kuacha masomo ya juu ili nimutumikie Yehova wakati wote. Ile ilinisaidia kukamata maamuzi ya muzuri mu maisha yangu, na ninafurahi juu nilifanya vile.”

14. Mashauri ya Musa na Daudi ilikazia jambo gani?

14 Musa na Daudi walimupenda sana Yehova na walijua kama ni jambo ya maana kumutii. Mu maneno yao ya mwisho-mwisho, walitia moyo wasikilizaji wao wafuate mufano wao kwa kushikamana na Yehova Mungu. Wote wawili walionya wasikilizaji wao kama wakimuacha Yehova, Yehova naye hatawakubali tena na watapoteza baraka zenye alikuwa amewaahidi. Mashauri yao ni ya maana kwetu leo. Miaka mingi kisha, mutumishi mwingine wa Yehova alionyesha pia kama ni jambo ya maana kuendelea kuwa muaminifu kwa Mungu.

“FURAHA KUBWA”

15. Mutume Yohana alijionea nini mu maisha yake?

15 Yohana alikuwa mutume mwenye Yesu alipenda sana. (Mt. 10:2; Yoh. 19:26) Alikuwa na Yesu mu utumishi wake, alijionea miujiza yake, na alibakia naye wakati wa magumu. Aliona namna Yesu aliuawa na alimuona kisha kufufuliwa kwake. Pia aliona namna Ukristo ulienea mu karne ya kwanza, kutoka ku kikundi kidogo ya Wakristo waaminifu mupaka namna habari njema “ilihubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.”—Kol. 1:23.

16. Barua za Yohana zimeletea nani faida?

16 Karibu na mwisho wa maisha yake, Yohana alipata pendeleo ya kuandika vitabu fulani vya Biblia. Aliandika “ufunuo kupitia Yesu Kristo.” (Ufu. 1:1) Yohana aliandika kitabu ya Injili yenye iko na jina yake. Aliandika pia barua tatu zenye ziliongozwa na roho ya Mungu. Barua yake ya tatu aliiandikia Mukristo muaminifu mwenye aliitwa Gayo, mwenye aliona kuwa mutoto wake wa kiroho. (3 Yo. 1) Ile wakati, inawezekana kulikuwa Wakristo wengi wenye Yohana aliona kuwa watoto wake wa kiroho. Mambo yenye ule mwanaume mwenye kuzeeka na muaminifu aliandika, ilitia moyo wanafunzi wa Yesu zamani na inaendelea kutia moyo wanafunzi wa Yesu leo.

17. Kulingana na 3 Yohana 4, nini njo inaletaka furaha kubwa?

17 Yohana aliandika nini? (Soma 3 Yohana 4.) Yohana aliandika kuhusu furaha yenye tunapata wakati tunamutii Mungu. Wakati Yohana aliandika barua yake ya tatu, watu fulani walikuwa naeneza mafundisho ya uongo na kuleta migawanyiko mu kutaniko. Lakini, wengine waliendelea “kutembea katika kweli.” Walimutii Yehova na ‘waliendelea kutembea kulingana na amri zake.’ (2 Yo. 4, 6) Wale Wakristo waaminifu walimufurahisha Yohana, lakini pia walimufurahisha Yehova.—Mez. 27:11.

18. Maneno ya Yohana inatufundisha nini?

18 Tunajifunza nini? Uaminifu unaletaka furaha. (1 Yo. 5:3) Kwa mufano, kujua kama tuko namufurahisha Yehova, kunatuletea furaha. Yehova anafurahi wakati anaona tunashinda majaribu ya mu huu ulimwengu na tunakubali kweli. (Mez. 23:15) Malaika mbinguni wanafurahi pia. (Lu. 15:10) Siye pia tunafurahi wakati tunaona bengine banaendelea kuwa baaminifu, zaidi sana wakati banapambana na magumu na majaribu. (2 Te. 1:4) Wakati huu ulimwengu utapita, tutakuwa na furaha juu tuliendelea kuwa baaminifu kwa Yehova hata wakati Shetani alikuwa natawala dunia.

19. Dada Rachel anasema nini kuhusu kufundisha bengine kweli? (Ona pia picha.)

19 Tunafurahi hata zaidi wakati tunafundisha bengine kweli. Rachel, mwenye anaishi mu République Dominicaine, anaona kama kufundisha mutu juu ya Mungu wa ajabu mwenye tunatumikia, ni pendeleo kubwa sana. Alisema hivi kuhusu watoto wake wa kiroho, ni kusema watu wenye alisaidia kujua kweli: “Ni nguvu kuelewa furaha yenye ninasikiaka wakati ninaona wale wenye ninafundisha wanakomala kiroho na kufikia kumupenda Yehova, kumutegemea, na kubadilisha maisha yao juu ya kumufurahisha. Ile furaha inapita mambo yote yenye nilifanya ao yenye nilijiima juu ya kuwafundisha.”

Tunapata furaha wakati tunafundisha bengine kumupenda na kumutii Yehova sawa siye (Ona fungu ya 19)


UTUMIKISHE MANENO YA MWISHO-MWISHO YA BANAUME BAAMINIFU

20. Ni mu njia gani tunafanana na Musa, Daudi, na Yohana?

20 Musa, Daudi, na Yohana waliishi mu vipindi na mu hali zenye kuwa tofauti kabisa na zetu. Lakini tunafanana mu mambo ya mingi. Sawa siye, balimutumikia Mungu wa kweli, balisali kwa Yehova, balimutegemea, na balitafuta muongozo wake. Na kama bale banaume ya zamani, tuko hakika kama Yehova atabariki sana benye kumutii.

21. Bale benye banasikiliza mashauri ya banaume baaminifu sawa vile Musa, Daudi na Yohana batapata baraka gani?

21 Tuazimie basi kusikiliza maneno ya mwisho-mwisho ya bale banaume kwa kutii amri za Yehova. Tukifanya vile tutapata matokeo ya muzuri mu mambo yote yenye tutafanya. Tutapata uzima na kuishi “wakati murefu,” ni kusema milele! (Kum. 30:20) Na tutakuwa na furaha juu tunamufurahisha Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, mwenye anatimizaka ahadi zake mu njia yenye hatuwezi hata kuwazia.—Efe. 3:20.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

a Waisraeli wengi wenye waliona miujiza ya Yehova ku Bahari Nyekundu, walikufa mbele ya kuingia mu inchi ya ahadi. (Hes. 14:​22, 23) Yehova alisema kama Waisraeli wenye walikuwa na miaka 20 na zaidi, wenye walikuwa wameandikishwa, wangekufa mu jangwa. (Hes. 14:29) Lakini, Yoshua, Kalebu, na Waisraeli wengi wenye walikuwa wangali wadogo na batu mingi ba mu kabila ya Walawi baliendelea kuishi, na baliona namna Yehova alitimiza ahadi yake wakati balivuka Muto Yordani na kuingia mu inchi ya Kanaani.—Kum. 1:​24-40.

b MAFASIRIO YA PICHA : Kushoto: Daudi iko naambia Sulemani maneno ya mwisho-mwisho yenye hekima. Kuume: Banafunzi biko najifunza hekima ya Yehova ku masomo ya mapainia.