Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 47

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

Ndugu—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Wazee?

Ndugu—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Wazee?

“Kama mwanaume anajikaza ili akuwe mwangalizi, anatamani kazi ya muzuri.”1 TI. 3:1.

WAZO KUBWA

Mambo yenye Maandiko inaomba ndugu atimize juu afikie kuwa muzee.

1-2. Ni “kazi ya muzuri” gani yenye wazee wanafanya?

 KAMA kulishapita wakati fulani tangu uko mutumishi wa huduma, pengine uko mu njia ya kutimiza mambo yenye inaombwa juu ya kuwa muzee. Unaweza kujikaza juu ufikie ile “kazi ya muzuri”?—1 Ti. 3:1.

2 Muzee anafanyaka kazi gani? Anahubiri kwa bidii, anafanya kazi ya uchungaji na ya kufundisha, na anatia nguvu kutaniko kupitia maneno na mufano wake. Njo maana Biblia inaita bale banaume benye kutumika sana kuwa “zawadi katika wanadamu.”—Efe. 4:8.

3. Ndugu anaweza kufanya nini juu astahili kuwa muzee? (1 Timoteo 3:1-7; Tito 1:5-9)

3 Unaweza kufanya nini juu ustahili kuwa muzee? Mambo yenye mutu anapaswa kutimiza juu afikie kuwa muzee ni tofauti na mambo yenye mutu anapaswa kutimiza juu apate kazi fulani. Mu ulimwengu kama uko na ufundi wenye mukubwa wa kazi iko natafuta unaweza kupata kazi. Lakini kama unapenda kuwa muzee haitoshe tu kuwa na ufundi wa kuhubiri na kufundisha. Unapaswa kutimiza mambo yenye Maandiko inaomba ndugu watimize juu wakuwe wazee. Ile mambo iko mu 1 Timoteo 3:1-7 na Tito 1:5-9. (Soma.) Mu hii habari tutazungumuzia mambo yenye Maandiko inaomba ndugu watimize juu wastahili kuwa wazee: (1) kujulikana kuwa mutu muzuri inje na ndani ya kutaniko, (2) kuwa kichwa ya familia mwenye ni mufano muzuri, na (3) kuwa tayari kutumikia kutaniko.

UJULIKANE KUWA MUTU MUZURI

4. “Kuwa bila lawama” maana yake nini?

4 Juu ufikie kuwa muzee unapaswa “kuwa bila lawama.” Maana yake bengine mu kutaniko banapaswa kukujua kuwa mutu muzuri juu ya tabia yako ya muzuri. Zaidi ya ile, kunapaswa kuwa “ushuhuda muzuri kutoka kwa watu wa inje” juu yako. Batu benye habiko Mashahidi banaweza kusema mubaya juu ya imani yako, lakini habapaswe kuwa na sababu yoyote ya kusema kama hauko munyoofu ao hauna mwenendo muzuri. (Da. 6:4, 5) Ujiulize hivi: ‘Inje na ndani ya kutaniko ninajulikana kuwa mutu muzuri?’

5. Namna gani unaweza kuonyesha kama uko “mwenye kupenda wema”?

5 Kama uko “mwenye kupenda wema,” unaona sifa za muzuri za bengine na unabapongeza juu ya zile sifa. Unafurahia pia kufanyia bengine mambo ya muzuri hata kama haulazimike kufanya vile. (1 Te. 2:8; Tit. 1:8) Juu ya nini ni jambo ya maana sana wazee wakuwe na ile sifa? Juu ile itafanya bafurahie kupitisha wakati mingi mu kazi ya uchungaji na mu migao yao ingine. (1 Pe. 5:1-3) Furaha yenye banapata wakati banatumikia bengine ni ya mingi kupita mambo yenye banajiima.—Mdo. 20:35.

6. Ni mu njia gani fulani muzee anaweza kuwa “mukaribishaji-wageni”? (Waebrania 13:2, 16; ona pia picha.)

6 Unaonyesha kama uko “mukaribishaji-wageni” wakati unafanyia bengine mambo ya muzuri, hata benye habiko barafiki yako ya karibu. (1 Pe. 4:9) Kitabu fulani inasema hivi juu ya mwanaume mwenye ni mukaribishaji-wageni: “Mulango wa nyumba yake na wa moyo wake unapaswa kuwa wazi kwa ajili ya batu benye hajue.” Ujiulize hivi: ‘Najulikana kuwa mutu mwenye anakaribishaka bageni?’ (Soma Waebrania 13:2, 16.) Mwanaume mwenye ni mukaribishaji-wageni anachangia kidogo yenye iko nayo pamoya na bengine. Kwa mufano anaalika Wakristo wenye hawana bitu mingi na Wakristo wenye kutumika kwa bidii, sawa vile waangalizi wa muzunguko na wasemaji wageni.—Mwa. 18:2-8; Mez. 3:27; Lu. 14:13, 14; Mdo. 16:15; Ro. 12:13.

Bibi na bwana wakaribishaji-wageni wanakaribisha mwangalizi na bibi yake (Ona fungu ya 6)


7. Namna gani muzee anaweza kuonyesha kama haiko“mutu mwenye kupenda feza”?

7 “Hapaswe kuwa . . . mutu mwenye kupenda feza.” Maana yake makuta na bitu ya kimwili haiko njo mambo ya maana sana kwako. Ukuwe tajiri ao maskini unatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza mu sehemu zote za maisha yako. (Mt. 6:33) Unatumia wakati, nguvu, na bitu yako juu ya kumuabudu Yehova, juu ya kuhangaikia familia yako, na juu ya kutumikia kutaniko. (Mt. 6:24; 1 Yo. 2:15-17) Ujiulize hivi: ‘Niko na mawazo gani juu ya makuta? Ninatosheka na bitu ya lazima ao ninapenda sana kutafuta makuta na kuwa na bitu mingi ya kimwili?’—1 Ti. 6:6, 17-19.

8. Ni mu njia gani fulani unaweza kuonyesha kama uko “mwenye kiasi katika tabia” na uko “mwenye kujizuia”?

8 Kama uko “mwenye kiasi katika tabia” na “mwenye kujizuia,” uko na usawaziko mu sehemu zote za maisha yako. Ile inamaanisha kuepuka kula na kunywa kupita kiasi, kujikaza kuwa na kiasi mu mambo ya kuvala na kujipamba na mu mambo ya kujifurahisha. Haupaswe kufuatilia namna ya kuishi ya watu wa mu hii ulimwengu. (Lu. 21:34; Yak. 4:4) Unapaswa kuwa mwenye kutulia hata wakati wanakuchokoza. ‘Usikuwe mulevi’ ao kujulikana kuwa mutu mwenye anakunywaka sana. Ujiulize hivi: ‘Najulikana kuwa mutu mwenye kiasi na mwenye kujizuia?’

9. Kuwa na “akili ya muzuri” na kuwa na “utaratibu” maana yake nini?

9 Kama uko na “akili ya muzuri,” unachunguza mambo kwa uangalifu kwa kutumia kanuni za Biblia. Unachunguza sana zile kanuni za Biblia, na ile inafanya ukuwe na hekima na uelewaji. Haukamate maamuzi haraka-haraka. Lakini unahakikisha kama unajua muzuri mambo yote. (Mez. 18:13) Ile inafanya ukamate maamuzi ya muzuri yenye kupatana na mawazo ya Yehova. Kama uko na “utaratibu,” ni kusema unajipanga muzuri na unaheshimia wakati. Unajulikana kuwa mutu mwenye kutumainika na mwenye kufuata maagizo. Zile sifa zitafanya ujulikane kuwa mutu muzuri. Tuone sasa mambo yenye Maandiko inasema yenye inaweza kukusaidia kuwa kichwa ya familia muzuri.

UKUWE KICHWA YA FAMILIA MUZURI

10. Namna gani mwanaume anaweza kusimamia “muzuri nyumba yake mwenyewe”?

10 Kama uko bwana na unapenda kuwa muzee, familia yako pia inapaswa kuwa mufano muzuri. Kwa hiyo unapaswa “kusimamia muzuri nyumba [yako] mwenyewe.” Unapaswa kujulikana kuwa kichwa ya familia mwenye upendo na mwenye kuhangaikia familia yake. Ile inamaanisha usaidie familia yako imuabudu Yehova muzuri. Juu ya nini ni jambo ya maana kufanya vile? Mutume Paulo alisema hivi: “Kama mutu hajue namna ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atatunza namna gani kutaniko la Mungu?”—1 Ti. 3:5.

11-12. Kama ndugu anapenda kuwa muzee, juu ya nini ni jambo ya maana batu ya familia yake bakuwe na mwenendo muzuri? (Ona pia picha.)

11 Kama uko baba unapaswa kuhakikisha kama “watoto [wako wenye wangali wadogo ni] watiifu na wenye kuchukua mambo kwa uzito.” Unapaswa kuwafundisha na kuwazoeza kwa upendo. Kusema kweli, sawa batoto bote nabo batapenda kucheka na kucheza. Lakini juu unabazoeza muzuri, batakuwa batiifu, batakuwa na adabu na tabia ya muzuri. Pia, unapaswa kujikaza kusaidia batoto yako bakuwe na uhusiano wa muzuri pamoya na Yehova, batumikishe kanuni za Biblia mu maisha yao, na bafanye maendeleo juu bafikie kubatizwa.

12 “Kuwa na watoto wenye kuamini na wenye hawashitakiwe kuwa wapotovu ao waasi.” Kama mutoto mwenye kubatizwa mwenye angali ku nyumba anafanya zambi nzito ile inaweza kuwa na matokeo gani juu ya baba yake? Kama baba aliachilia mambo na hakumutolea mazoezi na nizamu yenye alistahili, ile itafanya ule baba asistahili kuwa muzee.—Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 10 , 1996, uku. 21, fu. 6-7.

Kichwa ya familia iko nasaidia batoto yake bafanye mambo yenye kumufurahisha Yehova na kusaidia kutaniko (Ona fungu ya 11)


TUMIKIA KUTANIKO

13. Namna gani unaweza kuonyesha kama uko “mwenye usawaziko” na hauko “kichwa-nguvu”?

13 Ndugu wenye kuwa na sifa za Kikristo wanasaidia sana kutaniko. Mwanaume “mwenye usawaziko” anafuatilia amani. Kama unapenda kujulikana kuwa mutu mwenye usawaziko, sikiliza bengine na ukuwe tayari kukubali mawazo yao. Mu mukutano utakuwa tayari kukubali uamuzi wa batu mingi kama hakuna sheria ao kanuni fulani ya Biblia yenye inavunjwa. ‘Usikuwe kichwa-nguvu’ maana yake haupaswe kukazia mambo ikuwe tu vile weye unapenda. Unajua kama ni jambo ya lazima kusikiliza mawazo ya bengine (Mwa. 13:8, 9; Mez. 15:22) ‘Haupaswe kuwa mugomvi’ ao “mwenye kukasirika haraka.” Kuliko kuwa mukali ao kubishana na bengine ubatendee kwa busara na kwa upole. Juu unapenda amani unakamata hatua ya kufanya amani hata kama hali iko nguvu. (Yak. 3:17, 18) Maneno yako yenye upendo inaweza kutuliza bengine, hata bapinzani.—Amu. 8:1-3; Mez. 20:3; 25:15; Mt. 5:23, 24.

14. “Hapaswe kuwa muamini mupya” na anapaswa kuwa “mushikamanifu” maana yake nini?

14 Ndugu mwenye iko najikaza juu akuwe muzee “hapaswe kuwa muamini mupya.” Hata kama haiombe ukuwe umebatizwa kwa miaka mingi, uko na lazima ya wakati juu ufikie kuwa Mukristo mwenye kukomala kiroho. Mbele ya kuwekwa kuwa muzee unapaswa kuonyesha sawa Yesu kama uko munyenyekevu, na kama uko tayari kumungojea Yehova akupatie mugao kwa wakati wenye kufaa. (Mt. 20:23; Flp. 2:5-8) Unaweza kuonyesha kama uko “mushikamanifu” kwa kushikamana na Yehova na kanuni zake na kwa kufuata muongozo wa tengenezo.—1 Ti. 4:15.

15. Ni lazima muzee akuwe musemaji muzuri sana? Fasiria.

15 Maandiko inaonyesha wazi kama mwangalizi anapaswa kuwa na “uwezo wa kufundisha.” Ni kusema ni lazima muzee akuwe musemaji muzuri sana? Hapana. Wazee wengi wenye uzoefu, hata kama hawako wasemaji wazuri sana, wanafundishaka muzuri mu mahubiri na mu ziara za uchungaji. (Linganisha na 1 Wakorinto 12:28, 29 na Waefeso 4:11.) Lakini, unapaswa kuendelea kujikaza juu ya kukomalisha ufundi wako wa kufundisha. Unaweza kufanya vile namna gani?

16. Unaweza kufanya nini juu ukuwe mufundishaji muzuri zaidi? (Ona pia picha.)

16 “Mwenye kushikamana kabisa na neno la uaminifu.” Juu ukuwe mufundishaji muzuri, mafundisho na mashauri yako itegemee Neno ya Mungu. Ukuwe unajifunza sana Biblia na vichapo vyetu. (Mez. 15:28; 16:23) Wakati uko najifunza, ukuwe muangalifu juu uone namna ya kutumia muzuri Maandiko. Na wakati uko nafundisha ujikaze sana juu ya kugusa moyo wa basikilizaji bako. Unaweza kuongeza ufundi wako wa kufundisha kama unaomba wazee wenye uzoefu mashauri na unajikaza kuitumikisha. (1 Ti. 5:17) Wazee wanapaswa kuwa na [uwezo wa] kutia moyo” ndugu na dada. Lakini, wanapaswa pia kuwatolea mashauri na hata ‘kuwakaripia.’ Lakini wazee wanapaswa kufanya ile mambo yote kwa upole. Kama uko mupole na uko na upendo na mafundisho yako inategemea Neno ya Mungu, utakuwa mufundishaji muzuri juu utakuwa unaiga Mwalimu Mukubwa, Yesu.—Mt. 11:28-30; 2 Ti. 2:24.

Wakati mutumishi wa huduma iko na muzee mwenye uzoefu anatumia ile nafasi juu ya kujifunza namna ya kufundisha kwa kutumia Biblia. Pia anarudilia mbele ya kioo hotuba yenye atatolea kutaniko (Ona fungu ya 16)


ENDELEA KUJIKAZA

17. (a) Nini njo inaweza kusaidia watumishi wa huduma waendelee kujikaza? (b) Wazee wanapaswa kukumbuka nini wakati wako nachunguza ikiwa ndugu anastahili? (Ona kisanduku “ Mukuwe na Kiasi Wakati Muko Nachunguza Bengine.”)

17 Kisha kuchunguza mambo yenye mutu anapaswa kufanya juu akuwe muzee, watumishi wa huduma fulani wanaweza kuwaza kama hawatafikiaka kuwa wazee. Lakini ukumbuke kama Yehova na tengenezo yake hawatazamie kama utatimiza zile sifa kwa ukamilifu. (1 Pe. 2:21) Na ni roho takatifu ya Yehova yenye nguvu njo itakusaidia kutimiza ile mambo. (Flp. 2:13) Kuko sifa fulani yenye ungependa kufanyia maendeleo? Sali kwa Yehova juu ya ile jambo. Tafuta habari, na uombe muzee fulani akupatie mashauri yenye inaweza kukusaidia.

18. Watumishi wa huduma wote wanatiwa moyo kufanya nini?

18 Siye wote, hata ndugu wenye walishakuwa wazee tujikaze kuendelea kukomalisha sifa zenye tumezungumuzia mu hii habari. (Flp. 3:16) Uko mutumishi wa huduma? Endelea kujikaza! Umuombe Yehova akuzoeze juu umutumikie zaidi na utumikie zaidi kutaniko. (Isa. 64:8) Yehova abariki mambo yote yenye uko najikaza kufanya juu ufikie kuwa muzee.

WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja