Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Yehova Alitutegemeza mu Wakati wa Vita na wa Amani

Yehova Alitutegemeza mu Wakati wa Vita na wa Amani

Paul: Tulikuwa na furaha sana! Ilikuwa Mwezi wa 11, 1985, tulikuwa naenda mu mugao wetu wa kwanza wa umisionere mu inchi ya Liberia mu Afrika ya Mangaribi. Avion yetu ilisimama Senegal. Anne akasema hivi: “Kunabakia saa moya hivi tufike Liberia!” Kisha tukasikia hii tangazo: “Batu yote benye biko naenda Liberia batoke mu avion, batu fulani bamejaribu kunyanganya serikali mamlaka. Njo maana avion haitafika kule.” Kwa siku kumi tulibakia na wamisionere mu Senegal. Tulikuwa nasikiliza habari juu ya Liberia, zenye zilikuwa nazungumuzia namna magari ilikuwa nayala maiti ya batu na namna serikali ilikataza batu kutoka inje busiku. Na benye habakuheshimia ile sheria balipigwa masasi.

Anne: Tunakuwaka baangalifu. Tangu wakati nilikuwa mutoto nilijulikana kuwa mutu wa boga sana. Ninasikiaka hata boga ya kuvuka barabara. Lakini tuliazimia kuenda mu mugao wetu.

Paul: Miye na Anne tulizaliwa mu eneo moya, mangaribi mwa Uingereza. Siye bote tulianza kazi ya upainia kisha tu kumaliza masomo ya segondere. Bazazi yangu na mama yake na Anne njo balitutia moyo tufanye vile. Baliunga mukono muradi wetu wa kufanya utumishi wa wakati wote mu maisha yetu yote. Wakati nilikuwa na miaka 19 nilipata pendeleo ya kualikwa ku Beteli na Anne alijiunga na miye ku Beteli kisha ndoa yetu mu 1982.

Tunapewa diplome ku Gileadi, tarehe 8, 1985

Anne: Tulipenda Beteli, lakini tangu zamani tulipenda kutumikia kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri. Kutumika na Wanabeteli wenye walikuwa wamisionere zamani, kulifanya na siye tupende sana kuwa wamisionere. Tulisali juu ya ile jambo kila usiku kwa miaka 3. Kwa hiyo, tulifurahi sana wakati mu 1985 tulipata mualiko wa kuenda ku darasa ya 79 ya Masomo ya Gileadi! Tulipewa mugao wa kuenda kutumikia mu inchi ya Liberia, mu Afrika ya Mangaribi.

UPENDO WA NDUGU NA DADA ULITUTIA NGUVU

Paul: Tulipanda mu avion ya kwanza yenye ilikubaliwa kuingia Liberia. Hali haikukuwa muzuri na serikali iliendelea kukataza batu kutoka inje busiku. Batu baliogopa sana. Mu soko hata wakati gari ilifanya makelele ya nguvu kwa kushitukia, batu balilalamika na kuanza kukimbia. Juu ya kutuliza akili yetu, tulisoma pamoya kila usiku maandiko ya mu Zaburi. Lakini tulipenda sana mugao wetu. Anne alikuwa naenda kuhubiri, na miye nilikuwa natumika ku Beteli na ndugu John Charuk. a Alikuwa na uzoefu na alijua muzuri hali ya ndugu na dada. Kwa hiyo alinizoeza muzuri kabisa.

Anne: Juu ya nini tulipenda sana Liberia bila kukawia? Ni juu ya ndugu na dada zetu. Balikuwa na upendo, bachangamufu, na baaminifu. Tulifikia kuwa marafiki; bakakuwa familia yetu ya mupya. Maneno na mashauri yao ilitia nguvu hali yetu ya kiroho. Mahubiri ilikuwa butamu sana. Wenyenyumba hawakufurahi wakati tulizungumuza nao kidogo tu na kuenda. Batu balikuwa nazungumuzia mambo ya Biblia fasi yote. Ulikuwa tu nakuya na weye unaingia mu mazungumuzo. Tulikuwa na mafunzo mingi ya Biblia mupaka ilikuwa nguvu kuingoza yote. Ilifurahisha sana!

TULITIWA NGUVU HATA WAKATI TULIOGOPA

Tuko nahangaikia wakimbizi ku Beteli ya Liberia mu 1990

Paul: Mu 1989 kisha miaka ine ya amani kidogo, kulitokea vita ya wenyewe kwa wenyewe. Waasi walikamata eneo yenye ilikuwa karibu na Beteli tarehe 2 Mwezi wa 7 , 1990. Kwa miezi tatu hatukuweza kuzungumuza na batu ya inje, hata familia yetu na makao makubwa. Kulikuwa muvurugo, chakula ilikosekana, na batu balikuwa nalala banamuke kinguvu. Ile hali iliendelea kwa miaka 14 na ikaenea mu inchi yote.

Anne: Batu ya mu makabila fulani balikuwa napigana na kuua batu ya mu makabila ingine. Maaskari wenye walikuwa navala manguo ya ovyo-ovyo walikuwa na silaha za nguvu na waliyala mu mabarabara. Waliingia mu manyumba ya batu na kukamata kila kitu yenye walipenda. Wamoya walikuwa naona kuua batu sawa vile kuua makuku. Walikuwa nabebanisha maiti ya batu, na ile ilifanyika hata pembeni ya Beteli. Mashahidi waaminifu waliuawa kutia ndani wamisionere wawili.

Mashahidi walitia maisha yao mu hatari juu ya kuficha Mashahidi wenzao wa mu kabila zenye zilichukiwa na kuuawa. Wamisionere na Wanabeteli walificha pia Mashahidi wenzao. Ku Beteli Mashahidi fulani wenye walikuwa wamekimbia walilala mu nyumba ya chini na wengine walilala mu machumba yetu mu nyumba ya yulu. Mu chumba yetu tulikuwa na familia ya batu saba.

Paul: Kila siku wapiganaji walijaribu kuingia mu Beteli juu ya kuangalia kama tulikuwa naficha batu. Batu ine balikuwa nafanya ulinzi. Bawili balikuwa naangalia ku dirisha na bengine bawili balikuwa nachunga mulango ya inje. Kama bale ba ku mulango ya inje banatia mikono yabo mbele, ni kusema mambo ilikuwa sawa. Lakini kama banatia mikono nyuma ni kusema hali haikukuwa muzuri. Kwa hiyo, bale ba ku dirisha balienda mbio kuficha ndugu zetu.

Anne: Kisha majuma mingi kikundi moya ya wapiganaji iliingia mu Beteli kinguvu. Miye na dada mwingine tuliingia fasi ya kunawia. Ule dada alijificha ku sehemu fulani yenye haikukuwa naonekana yenye ilikuwa mu kabati. Wapiganaji walikuwa wamenifuata mu nyumba ya yulu. Kwa kasirani walipiga mulango nguvu sana na walikuwa na silaha. Paul aliwaambia hivi: “Bibi yangu iko mu W.C.” Wakati nilifunga kabati kwenye ule dada alikuwa najificha, ilifanya makelele. Na kurudisha kila kitu fasi yake kulikamata wakati. Wapiganaji wangejiuliza niko nafanya nini. Ile ilifanya nianze kutetemeka kuanzia ku kichwa mupaka ku likucha. Nilipaswa kutulia mbele ya kufungula mulango. Nilisali na kumulilia Yehova anisaidie. Kisha nikafungula mulango na kwa utulivu nikawasalimia. Mumoya wabo akanipita na kuingia mara moya mu W.C, akaanza kufungula-fungula mu kabati na kutosha byenye bilikuwa ndani. Lakini hakuona kitu. Yeye na benzake balitafuta mu chumba zingine na mu sehemu ya yulu ya nyumba lakini habakuona kitu.

KWELI ILIENDELEA KUANGAZA

Paul: Kwa miezi mingi, tulikuwa na chakula kidogo sana. Lakini chakula ya kiroho ilitupatia nguvu ya kuendelea kuvumilia. Ibada ya asubui ya Beteli njo tu ilikuwa chakula yetu ya asubui. Na tulifurahia kuona namna ilitupatia nguvu.

Kama kukosa chakula na mayi kungetulazimisha kutoka mu Beteli, benye tulikuwa naficha bangeuawa. Wakati fulani namna Yehova alishugulikia mahitaji yetu kwa wakati wenye kufaa, ilikuwa sawa vile muujiza. Yehova alitupatia mambo yenye tulikuwa nayo lazima na alitusaidia tutulie.

Hata kama inchi iliendelea kuwa mu giza zaidi na zaidi, ni kusema hali iliendelea kuharibika sana, kweli iliendelea kuangaza. Mara kwa mara, ndugu na dada zetu walikimbia juu ya kuokoa uzima wao, lakini imani yao iliendelea kuwa nguvu na walikuwa wenye kutulia. Ndugu fulani walisema kama namna walipambana na ile hali ya vita “iliwatayarisha juu ya taabu kubwa.” Wazee wenye uhodari na ndugu vijana walifanya yao yote juu ya kusaidia ndugu na dada. Wakati ndugu na dada walikuwa nakimbia walibakia pamoya, walihubiri mu maeneo ya mupya, na walianza kufanya mikutano mu Majumba ya Ufalme yenye walijijengea mu pori. Mikutano na mahubiri ilitia ndugu na dada moyo na iliwapatia tumaini hata kama hali ilikuwa nguvu sana. Wakati tulikuwa natoa misaada, tuliguswa moyo sana kuona namna ndugu na dada walikuwa naomba tuwapatie njo masakoshi ya mahubiri kuliko kuomba manguo. Batu benye huzuni na benye baliogopa sana kwa sababu ya mambo yenye ilibafikia, balisikia habari njema. Balishangala kuona namna Mashahidi walikuwa na furaha, walikuwa kama muangaza mu giza! (Mt. 5:​14-16) Bidii ya ndugu na dada ilifanya hata wapiganaji fulani wafikie kuwa Mashahidi.

TULITIWA NGUVU WAKATI TULILAZIMIKA KUACHA NDUGU ZETU

Paul: Wakati fulani tulipaswa kutoka mu inchi, mara tatu tulitoka kwa wakati mufupi, na mara mbili kwa mwaka muzima. Dada moya misionere anaeleza muzuri namna tulijisikia. “Ku Gileadi tulijifunza kama tunapaswa kutia moyo wetu mu mugao wetu. Na ni vile tulifanya. Kwa hiyo wakati tunaacha ndugu na dada zetu mu hali za vile ni sawa vile moyo wetu unavunjwa-vunjwa.” Jambo ya kufurahisha ni kama tuliendelea kutegemeza bandugu ya mu Liberia wakati tulikuwa mu inchi za karibu-karibu.

Tunarudia Liberia kwa furaha mu 1997

Anne: Mu Mwezi wa 5, 1996, waine kati yetu tuliondoka na gari ya Beteli, yenye ilikuwa na dokima za maana juu ya kazi yetu mu Liberia. Tulipenda kusafiri kilometre 16 juu ya kuenda fasi kwenye kulikuwa salama zaidi. Kisha ileile wakati eneo yetu ikashambuliwa. Wapiganaji wenye kasirani walianza kupiga masasi mu hewa. Wakatusimamisha, wakatosha batatu kati yetu mu gari, wakaenda na gari lakini Paul alikuwa angali ndani. Tulisimama tu fasi moya na tunaishiwa kabisa. Kwa kushitukia tukaona Paul iko nakuya kwenye tuko, damu ilikuwa namutoka ku kichwa. Juu tulivurugika tuliwaza kama balimupiga masasi. Kisha tukaelewa kama ikiwa balimupiga masasi hangekuwa natembea. Mupiganaji mumoya alimupiga wakati alikuwa namusukuma atoke mu gari. Jambo ya kufurahisha ni kama ilikuwa kilonda ya kidogo tu.

Pale kulikuwa gari ya jeshi yenye ilikuwa nayala batu mingi benye balikuwa na boga sana. Juu hakukukuwa tena fasi tulilazimika kubana ku ile gari na mikono tu. Shofere alitembeza mbio sana, karibu tuanguke. Tulimulilia asimame, lakini hakutusikiliza juu alikuwa na boga sana. Hatujue ni kwa muujiza gani, lakini hatukuanguka. Hata vile wakati tulifika, tulikuwa nachoka sana na mwili yote ilikuwa natetemeka juu ya boga.

Paul: Hatukukuwa tena na kitu. Tulikuwa tu na manguo yenye tulikuwa navala ya kupasuka na ya buchafu. Kisha tukaangaliana na kujiuliza namna gani tungali bazima. Tulilala inje pembeni ya helikoptere yenye ilikuwa na matundu ya masasi na ile helikoptere njo ilitupeleka Sierra Leone siku yenye ilifuata. Tulifurahi sana juu tulikuwa tungali bazima, lakini tulihangaika sana juu ya hali ya Wakristo wenzetu wenye walibakia Liberia.

NGUVU YA KUPAMBANA NA HALI YENYE HAIKUTAZAMIWA

Anne: Wakati tulifika ku Beteli ya Freetown, Sierra Leone, tulikuwa salama na balituhangaikia muzuri. Lakini mambo yenye ilitufikia, ilianza kunirudilia. Muchana niliogopa sana. Niliogopa kuwa jambo fulani ya mubaya sana itatufikia. Kila kitu yenye ilituzunguka ilionekana kuwa haiko ya kweli. Busiku nilikuwa nalamuka na niko natetemeka juu ya boga. Niliogopa tena kama jambo fulani ya mubaya itatufikia. Ilikuwa nguvu kwangu kupumua. Paul alinibana na alisali pamoya na miye. Tuliimba nyimbo za Ufalme mupaka wakati niliacha kutetemeka. Nilijisikia sawa vile nitapata bazimu na sitaendelea tena na kazi ya umisionere.

Siwezi hata kidogo kusaabu jambo yenye ilitokea kisha pale. Ileile juma tulipata magazeti mbili. Moya ilikuwa Amuka! ya tarehe 8, Mwezi wa 6, 1996. Ilikuwa na habari yenye kichwa “Kukabiliana na Mishiko ya Hofu ya Ghafula.” Sasa nilielewa tatizo yangu ilikuwa nini. Ya Pili ilikuwa Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 1996, yenye ilikuwa na habari yenye kichwa “Wao Hupata Wapi Nguvu Zao?” Mu ile Munara mulikuwa picha ya kipepeo yenye ilikuwa imeumia. Ile habari ilifasiria kama sawa vile kipepeo inaendelea kuruka hata kama mabawa yake imeharibika sana, kwa musaada wa roho ya Yehova tunaweza kuendelea kusaidia bengine hata kama tuko na maumivu ya moyo. Ile ilikuwa chakula ya kiroho kutoka kwa Yehova yenye ilifika kwa wakati wenye kufaa kabisa. (Mt. 24:45) Kutafuta habari zingine zenye kuzungumuzia hali yangu na kuzitia pamoya kulinisaidia sana. Kisha wakati nilianza kujisikia muzuri.

NGUVU YA KUJIPATANISHA NA MUGAO MUPYA

Paul: Kila wakati wenye tulikuwa narudia Liberia tulifurahi sana. Ku mwisho-mwisho wa mwaka wa 2004 tulikuwa tumefanya miaka karibu 20 mu mugao wetu. Vita ilikuwa ilishaisha. Kulikuwa mupango wa kujenga tawi. Lakini kwa kushitukia walitupatia mugao wa mupya.

Ilikuwa nguvu sana kwetu. Tulikuwa na uhusiano wa karibu sana na familia yetu ya kiroho. Hatukupenda kuwaacha. Juu tuliachaka familia zetu wakati tuliendaka ku Masomo ya Gileadi, tulijioneaka kama kujitia mu mikono ya Yehova kunaletaka baraka. Kwa hiyo tulikubali ile mugao. Tulitumwa karibu na pale mu inchi ya Ghana.

Anne: Tulilia sana wakati tulitoka Liberia. Tulishangala wakati Frank, ndugu muzee-muzee, alituambia hivi: “Mutusaabu!” Kisha akafasiria hivi: “Ninajua kama hamuwezi kutusaabu, lakini munapaswa kutia moyo wenu wote mu mugao wenu wa mupya. Ule mugao unatoka kwa Yehova. Kwa hiyo muhangaikie sana ndugu na dada wa kule.” Ile maneno ilitupatia nguvu ya kuanza kutumikia mu mugao kwenye batu mingi habakutujua na kwenye kila kitu ilikuwa ya mupya kwetu.

Paul: Lakini bila kukawia tulipenda sana familia yetu ya mupya ya kiroho mu inchi ya Ghana. Mu Ghana mulikuwa Mashahidi wengi sana. Ushikamanifu na imani ya marafiki wetu wapya ilitufundisha mambo mingi. Kisha kutumikia Ghana kwa miaka 13, bila kutazamia tulipata mugao mwingine. Tulitumwa ku tawi ya Afrika ya Mashariki mu inchi ya Kenya. Hata kama tulikumbuka sana marafiki wetu wa mu migao yetu ya mbele, bila kukawia tulipata marafiki wapya mu inchi ya Kenya. Na tuko naendelea kutumikia mu hii eneo kubwa mwenye muko pia kazi kubwa ya kufanya.

Tuko na marafiki wapya ku tawi ya Afrika ya Mashariki mu 2023

MAMBO YENYE TUMEJIFUNZA

Anne: Mu maisha yangu nimepambana na hali za nguvu sana na wakati fulani niliogopa sana na kutetemeka. Hali zenye kuwa hatari na zenye kuleta mahangaiko, zinaweza kuwa na matokeo juu ya afya yetu ya kimwili na ya kiakili. Yehova hatulinde kimuujiza. Kama ninasikia mulio wa masasi ao mulio mwingine wenye kufanana wa masasi, ninasikiaka sawa vile nitatapika na ninasikiaka sawa vile mikono inanipooza. Lakini nimejifunza kutegemea njia zenye Yehova anatumia juu ya kututia nguvu, sawa vile musaada wenye ndugu na dada zetu wanatutolea. Na nimeona kama kwa kuendelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho, Yehova anaweza kutusaidia tuendelee kubakia mu mugao wetu.

Paul: Batu fulani banaweza kuuliza, “Unapenda mugao wako?” Inchi zinaweza kuwa za kupendeza, lakini munaweza pia kuwa hali zenye kuwa hatari. Sasa ni nini njo tunapenda sana kupita inchi? Ndugu na dada zetu wapendwa, familia yetu. Hata kama tunatoka fasi tofauti-tofauti tuko na akili moya. Tuliwaza kama walitutuma juu ya kuwatia moyo, lakini kusema kweli wao njo wametutia moyo.

Kila wakati tunahamia fasi ingine, tunakuta familia ya ndugu na dada, ile ni muujiza kabisa. Kama tu tuko mu kutaniko, tuko na familia. Tuko hakika kama ikiwa tunaendelea kumutegemea Yehova, atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima kulingana na hali yetu.—Flp. 4:13.

a Ona habari juu ya maisha ya John Charuk yenye kichwa, “Je suis reconnaissant à Dieu et au Christ,” mu Munara wa Mulinzi wa Kifaransa wa tarehe 1, Mwezi wa 7, 1973.