Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

Furahia Tumaini Yenye Haikatishe Tamaa

Furahia Tumaini Yenye Haikatishe Tamaa

“Tumaini halikatishe tamaa.”— Ro. 5:5.

WIMBO 142 Tusiache Tumaini Yetu

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini tunaweza kusema kama Abrahamu alikuwa na sheria ya kuwa na tumaini?

 YEHOVA alimuahidi rafiki yake Abrahamu kama mataifa yote ya ku dunia itajibariki kupitia uzao wake. (Mwa. 15:5; 22:18) Juu Abrahamu alikuwa na imani ya nguvu kwa Mungu, alikuwa hakika kama ile ahadi ya Mungu itatimia. Hata vile, wakati Abrahamu alikuwa na miaka 100 na Sara miaka 90, wale bibi na bwana waaminifu walikuwa tu hawajapata mutoto. (Mwa. 21:​1-7) Lakini Biblia inasema: “Kwa kutegemea tumaini, [Abrahamu] alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi kulingana na yale yenye yalikuwa yamesemwa.” (Ro. 4:18) Tunajua kama mambo yenye Abrahamu alitumainia ilitimia. Alifikia kuwa baba ya Isaka, mutoto mwenye kwa miaka mingi alitumaini kama atapata. Ni nini njo ilifanya Abrahamu akuwe hakikia kwamba Yehova atatimiza ahadi yake?

2. Juu ya nini Abrahamu alikuwa hakika kama ahadi ya Yehova itatimia?

2 Juu Abrahamu alikuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova, alikuwa “amesadikishwa kabisa kwamba kile chenye Yeye [Mungu] aliahidi” kitatimia. (Ro. 4:21) Yehova alimukubali Abrahamu na akamutangaza kuwa mwenye haki kwa sababu ya imani yake. (Yak. 2:23) Vile Waroma 4:18 inasema, Abrahamu alikuwa na imani na alikuwa na tumaini pia. Tuone sasa maneno yenye mutume Paulo anasema juu ya tumaini, maneno yenye inapatikana mu Waroma sura ya 5.

3. Paulo anafasiria nini kuhusu tumaini?

3 Paulo anafasiria sasa juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama “tumaini [letu] halikatishe tamaa” ao halivunje moyo. (Ro. 5:5) Anatusaidia pia kuelewa namna tumaini yetu ya Kikristo inaweza kuwa nguvu zaidi. Wakati tuko nazungumuzia Waroma 5:​1-5, fikiria namna tumaini yako ya wakati wenye kuja imekuwa nguvu zaidi kadiri wakati umepita. Hii habari itakusaidia pia ujue namna unaweza kufanya tumaini yako ikuwe nguvu zaidi kuliko leo. Kwanza, tuzungumuzie tumaini ya muzuri yenye Paulo alisema kama haiwezi kutukatisha tamaa.

TUMAINI YA MUZURI YENYE TUKO NAYO

4. Waroma 5:​1, 2 inazungumuzia nini?

4 Soma Waroma 5:​1, 2. Paulo aliandikia hii maneno kutaniko yenye ilikuwa Roma. Kule, ndugu na dada walikuwa wamejifunza kuhusu Yehova na Yesu, walionyesha imani, na walifikia kuwa Wakristo. Kwa hiyo Mungu ‘aliwatangaza kuwa wenye haki kupitia imani’ na aliwatia mafuta kwa roho takatifu. Kwa kweli, walipata tumaini ya muzuri sana.

5. Watiwa-mafuta wako na tumaini gani?

5 Kisha Paulo aliandikia Wakristo watiwa-mafuta wa Efeso kuhusu tumaini yenye Mungu alikuwa amewapatia. Ile tumaini ilitia ndani uriti kwa ajili ya watakatifu. (Efe. 1:18) Pia, Paulo aliambia Wakolosai fasi kwenye tumaini yao itatimia kwa kusema hivi: “Tumaini lenye linawekwa kwa ajili yenu mbinguni.” (Kol. 1:​4, 5) Tumaini ya Wakristo watiwa-mafuta ni kwamba watafufuliwa ili waishi milele mbinguni, kwenye watatawala pamoya na Kristo.—1 Te. 4:​13-17; Ufu. 20:6.

Ndugu F. W. Franz alieleza muzuri uhakika wenye Wakristo watiwa-mafuta wako nao kuhusu tumaini yao (Ona fungu ya 6)

6. Ndugu fulani mutiwa-mafuta alisema nini kuhusu tumaini yake?

6 Wakristo watiwa-mafuta wanafurahia sana ile tumaini. Moya kati yao ni Ndugu Frederick Franz. Alisema hii maneno yenye kutoka ku moyo: “Tumaini yetu ni jambo ya hakika, na itatimizwa kikamili kwa kila mumoja wa wale 144 000 wa kundi ndogo mu namna yenye inapita vile tunaweza kuwazia.” Kisha kumutumikia Mungu kwa uaminifu kwa miaka mingi, Ndugu Franz alihakikisha hivi mu 1991: “Tunaendelea kuona ile tumaini yetu kuwa ya maana sana. . . . Tunaiona kuwa ya maana hata zaidi kadiri tunaedelea kuingojea. Ni jambo yenye inastahili kungojewa, hata kama ingeomba tuingojee kwa miaka milioni moja. Ninaona tumaini yetu kuwa ya maana zaidi kuliko wakati mwingine wowote.”

7-8. Wengi kati ya waabudu wa Yehova leo wako na tumaini gani? (Waroma 8:​20, 21)

7 Wengi kati ya waabudu wa Yehova leo wako na tumaini tofauti na ya watiwa-mafuta. Wako na tumaini yenye Abrahamu alikuwa nayo. Ile tumaini ni kuishi milele ku dunia chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu. (Ebr. 11:​8-10, 13) Paulo aliandika kuhusu ile tumaini ya muzuri sana. (Soma Waroma 8:​20, 21.) Wakati ulijifunza kwa mara ya kwanza juu ya tumaini ya wakati wenye kuja yenye kuzungumuziwa mu Biblia, nini njo ulipenda sana? Ni kujua kama siku moya utakuwa mukamilifu, na hautakuwa tena na muelekeo wa kufanya zambi? Ao ulifurahia kujua kama wapendwa wako wenye walishakufa wataishi tena mu dunia yenye itakuwa paradiso? “Kwa musingi wa tumaini,” tuko na mambo mengi yenye tunangojea kwa hamu.

8 Ikuwe tumaini yetu ni kuishi milele mbinguni ao ku dunia, tuko na tumaini ya muzuri na yenye kufurahisha. Na ile tumaini inaweza kuendelea kuwa nguvu zaidi. Mambo yenye Paulo aliandika inatuonyesha namna ile inawezekana. Tuzungumuzie basi mambo yenye Paulo aliandika kuhusu tumaini. Kufanya vile kutatuhakikishia kama tumaini yetu itaendelea kuwa nguvu zaidi na haitatukatisha tamaa ao kutuvunja moyo.

NAMNA TUMAINI INAKUWA NGUVU ZAIDI

Wakristo wote wanaweza kutazamia kama watapata aina fulani ya taabu (Ona fungu ya 9-10)

9-10. Vile mufano wa Paulo unaonyesha, Wakristo wanaweza kutazamia nini? (Waroma 5:3) (Ona pia picha.)

9 Soma Waroma 5:3. Ona kwamba taabu inaweza kufanya tumaini ya mutu ikuwe nguvu zaidi. Ile inaweza kutushangaza. Kwa kweli, wafuasi wote wa Yesu wanaweza kutazamia kama watapata mateso. Tuone mufano wa Paulo. Aliambia hivi Watesalonike: “Wakati tulikuwa pamoja na ninyi, tulikuwa tunawaambia mbele ya wakati kwamba tutapata taabu, na ni vile mambo yametokea.” (1 Te. 3:4) Na aliandikia hivi Wakorinto: “Hatutaki mukose kujua, ndugu, juu ya taabu yenye tulipata . . . Hatukukuwa na uhakika kabisa hata juu ya uzima wetu.”—2 Ko. 1:8; 11:​23-27.

10 Leo pia Wakristo wanaweza kutazamia kama watapata aina fulani ya taabu. (2 Ti. 3:12) Halafu weye? Kadiri unamuamini Yesu na kuendelea kumufuata, ni vile pia uko naendelea kupata taabu? Pengine marafiki na watu wa familia wamekuchekelea. Pengine hata wamekutendea mubaya. Je, umepata matatizo ku kazi juu unaazimia kuendelea kuwa munyoofu mu mambo yote? (Ebr. 13:18) Umepata upinzani kutoka kwa wakubwa wa serikali juu unahubiria wengine kuhusu tumaini yako? Ikuwe unapambana na taabu ya namna gani, kumbuka kama Paulo alisema kwamba tunapaswa kufurahi. Juu ya nini?

11. Juu ya nini tunapaswa kuazimia kuvumilia taabu yoyote?

11 Tunaweza kufurahi wakati tunapambana na taabu juu tunajua kama taabu inaweza kuwa na matokeo ya muzuri. Vile Waroma 5:3 inasema, “taabu inatokeza uvumilivu.” Wakristo wote watapambana na taabu, kwa hiyo Wakristo wote wanapaswa kuwa na uvumilivu. Tunapaswa kuazimia kuvumilia majaribu yoyote yenye tunaweza kupambana nayo. Ni kama tu tunafanya vile njo tunaweza kuona utimizo wa tumaini yetu. Hatupendi kuwa sawa wale wenye Yesu alikuwa nafikiria wakati alizungumuzia mbegu yenye inaanguka kwenye majiwe. Ku mwanzo walikubali neno kwa furaha lakini “kisha taabu ao mateso” kutokea, walianguka. (Mt. 13:​5, 6, 20, 21) Kusema kweli, hakuna mwenye anafurahiaka mateso ao majaribu, lakini kuivumilia kuko na matokeo ya muzuri. Namna gani?

12. Tutapata matokeo gani ya muzuri kama tunavumilia majaribu?

12 Yakobo alizungumuzia matokeo ya muzuri ya kuvumilia majaribu. Aliandika hivi: “Muache uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili mukuwe kamili na bila kosa katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yak. 1:​2-4) Hapa, Yakobo anasema kama uvumilivu uko na kazi ya kufanya ao ya kukamilisha. Ni kazi gani yenye uvumilivu unapaswa kukamilisha? Unaweza kutusaidia tukomalishe sifa sawa vile subira, imani, na kumutegemea Mungu. Lakini, kuko faida ingine ya muzuri yenye tutapata kama tuko wavumilivu.

13-14. Uvumilivu unatokeza nini, na ile inafanya tumaini yetu ikuwe namna gani? (Waroma 5:4)

13 Soma Waroma 5:4. Paulo alionyesha kama uvumilivu unatokeza “hali ya kukubaliwa.” Uvumilivu wako unafanya Yehova akukubali. Ile haimaanishe kama Yehova anafurahi wakati unapata majaribu ao magumu. Lakini ni weye njo Yehova anafurahia. Uvumilivu wako unatokeza hali ya kukubaliwa. Ile ni baraka ya ajabu!—Zb. 5:12.

14 Kumbuka kama Abrahamu alivumilia majaribu na ile ilifanya Yehova amukubali. Yehova alimuona kuwa rafiki yake na alimuona kuwa mwenye haki. (Mwa. 15:6; Ro. 4:​13, 22) Na siye anaweza kutuona vile. Haiko juu ya kazi mingi yenye tunafanya mu utumishi wake, ao juu tuko na madaraka ya mingi njo Yehova anatukubali. Yehova anatukubali juu tunavumilia kwa uaminifu. Siye wote tunaweza kuvumilia ikuwe tuko na miaka ngapi, tuko mu hali gani, ao tuko na uwezo gani. Je, kwa sasa kuko jaribu fulani yenye uko unavumilia kwa uaminifu? Kama ni vile, usisahau kama Yehova anakukubali. Kujua vile kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri sana. Kunaweza kutia nguvu tumaini yetu.

TUMAINI YA NGUVU ZAIDI

15. Paulo anaendelea kwa kuzungumuzia nini, na juu ya nini ile inaweza kuvuruga mutu?

15 Vile Paulo alifasiria, Yehova anatukubali wakati tunavumilia magumu kwa uaminifu. Ona vile Paulo anaendelea na maelezo yake: “Hali ya kukubaliwa inatokeza tumaini, na tumaini halikatishe tamaa.” (Ro. 5:​4, 5) Hii maneno ya Paulo inaweza kuvuruga mutu. Juu ya nini? Juu mbele ya pale, mu Waroma 5:​2, Paulo aliandika kama Wakristo wa Roma walikuwa tayari na tumaini, “tumaini la utukufu wa Mungu.” Kwa hiyo mutu anaweza kujiuliza: ‘Kama wale Wakristo tayari walikuwa na tumaini, juu ya nini Paulo anataya tena tumaini mu mazungumuzo yake?’

Tumaini ya Kikristo yenye ilikuvutia sana ku mwanzo, imekomaa na imekuwa nguvu zaidi (Ona fungu ya 16-17)

16. Namna gani tumaini ya mutu inaanza kuwa nguvu zaidi? (Ona pia picha.)

16 Ili kuelewa maneno ya Paulo ni muzuri tukumbuke kama tumaini inaweza kukomaa ao kuwa nguvu zaidi. Tuchukue mufano: Unakumbuka wakati ulisikia kwa mara ya kwanza kuhusu tumaini ya ajabu yenye kuwa mu Neno ya Mungu? Pengine ile wakati uliwaza kama ile ni tumaini ya muzuri sana, lakini haukukuwa hakika kama itatimia. Lakini, kadiri uliendelea kumujua Yehova muzuri, na ahadi zenye kuwa mu Biblia, ulifikia kuwa hakika zaidi kama ile tumaini itatimia.

17. Namna gani tumaini yako inaendelea kuwa nguvu zaidi kisha kujitoa kwa Yehova na kubatizwa?

17 Hata kisha kujitoa kwa Mungu na kubatizwa, tumaini yako iliendelea kuwa nguvu zaidi kadiri uliendelea kujifunza na kukomaa kiroho. (Ebr. 5:13–6:1) Ni sawa vile ulijionea mu maisha yako mambo yenye kuandikwa mu Waroma 5:​2-4. Ulipata taabu mbalimbali, lakini ulivumilia na ukakubaliwa na Mungu. Na juu uko hakika kama Mungu anakupenda na anakufurahia, uko sasa na sababu mingi zaidi ya kuamini kama mambo yenye Yehova aliahidi itatimia. Tumaini yako inakuwa nguvu zaidi kuliko vile ilikuwa ku mwanzo. Ile tumaini imekuwa ya kweli kabisa kwako, imekuwa tumaini yako. Ile tumaini inakugusa sana. Inachochea kila sehemu ya maisha yako na inabadilisha namna unatendea familia yako, namna yako ya kukamata maamuzi, na hata namna yako ya kutumia wakati.

18. Yehova anatupatia uhakikisho gani?

18 Mutume Paulo anazungumuzia pia jambo fulani ya maana sana kuhusu tumaini yenye unakuwa nayo kisha kukubaliwa na Mungu. Anakuhakikishia kama tumaini yako itatimia. Juu ya nini unapaswa kuwa hakika kabisa na ile jambo? Paulo anataja huu uhakikisho wenye kutoka kwa Mungu: “Tumaini halikatishe tamaa; kwa sababu upendo wa Mungu umemwangwa ndani ya mioyo yetu kupitia roho takatifu, yenye tulipewa.” (Ro. 5:5) Uko na sababu zote za kuamini kama tumaini yako ni ya kweli.

19. Unaweza kuwa na uhakika gani kuhusu tumaini yako?

19 Fikiria ahadi yenye Yehova alimupatia Abrahamu na namna alimukubali na kumuona kuwa rafiki yake. Tumaini ya Abrahamu haikukuwa ya bure. Biblia inasema hivi: “Kisha Abrahamu kuonyesha uvumilivu, alipata ahadi hiyo.” (Ebr. 6:15; 11:​9, 18; Ro. 4:​20-22) Tumaini ya Abrahamu haikumukatisha tamaa. Na weye unaweza kuwa hakika kama ukibakia muaminifu, tumaini yako itatimia. Tumaini yako ni ya kweli; ni jambo yenye kuleta furaha, hapana jambo ya kuvunja moyo! (Ro. 12:12) Paulo aliandika: “Mungu mwenye anatoa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani kwa sababu munamutegemea, ili muongezeke katika tumaini kwa nguvu za roho takatifu.”—Ro. 15:13.

WIMBO 139 Wazia Uko mu Dunia Mupya

a Mu hii habari tutaona tumaini yetu siye Wakristo ni nini na juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama itatimia. Waroma sura ya 5 itatusaidia kuona namna tumaini yenye tuko nayo leo iko tofauti na tumaini yenye tulikuwa nayo wakati tulianza kujifunza kweli.