Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 53

Ndugu Vijana​—⁠Mujikaze Kuwa Wakristo Wenye Kukomaa Kiroho

Ndugu Vijana​—⁠Mujikaze Kuwa Wakristo Wenye Kukomaa Kiroho

“Ukuwe na nguvu na ujionyeshe kuwa mwanaume.”—1 FA. 2:2.

WIMBO 135 Yehova Anakuomba “Ukuwe na Hekima”

KIFUPI YA HABARI a

1. Mwanaume Mukristo anapaswa kufanya nini?

 MUFALME Daudi alimuambia Sulemani hivi: “Ukuwe na nguvu na ujionyeshe kuwa mwanaume.” (1 Fa. 2:​1-3) Ni muzuri wanaume wote Wakristo leo watumikishe ile shauri. Ili waweze kufanya vile, wanapaswa kujifunza kutii Sheria ya Mungu na kutumikisha kanuni za Biblia mu sehemu zote za maisha yao. (Lu. 2:52) Juu ya nini ni jambo ya maana sana kwa ndugu vijana kuwa Wakristo wenye kukomaa kiroho?

2-3. Juu ya nini ni jambo ya lazima ndugu vijana wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho?

2 Wanaume Wakristo wanatimiza madaraka mingi ya maana sana mu familia na mu kutaniko. Ndugu kijana, bila shaka umefikiria madaraka yenye unaweza kuwa nayo mu wakati wenye kuya. Unaweza kuwa na muradi wa kuwa mutumishi wa wakati wote, mutumishi wa huduma, na baadaye muzee wa kutaniko. Unaweza pia kupenda kuoa na kuwa na watoto. (Efe. 6:4; 1 Ti. 3:1) Ili kufikia ile miradi na kupata matokeo ya muzuri, uko na lazima ya kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho. b

3 Ni nini inaweza kukusaidia kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho? Kuko ufundi mbalimbali wa lazima wenye unapaswa kujifunza. Unapaswa kufanya nini leo juu ya kujitayarisha ili uweze kutimiza muzuri madaraka yenye unaweza kuwa nayo mu wakati wenye kuya?

MAMBO YA KUFANYA JUU UFIKIE KUWA MUKRISTO MWENYE KUKOMAA KIROHO

Kuiga sifa za Yesu kunaweza kukusaidia kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho (Ona fungu ya 4)

4. Unaweza kupata wapi mifano mizuri ya kuiga? (Ona pia picha.)

4 Chagua mifano mizuri ya kuiga. Mu Biblia muko mifano mingi ya muzuri ya vijana wenye unaweza kuiga. Wale wanaume wenye waliishi zamani walimupenda Mungu na walikuwa na madaraka mbalimbali, na walihangaikia watu wa Mungu mu njia mbalimbali. Leo pia unaweza kupata mu familia yako na mu kutaniko mifano ya muzuri ya wanaume wenye kukomaa kiroho. (Ebr. 13:7) Uko pia na mufano mukamilifu wa Yesu Kristo. (1 Pe. 2:21) Wakati uko nachunguza kwa uangalifu mifano yao, fikiria pia sifa zao za muzuri. (Ebr. 12:​1, 2) Kisha uone namna unaweza kuwaiga.

5. Namna gani unaweza kuwa na uwezo wa kufikiri, na juu ya nini ni ya maana kuwa na ile sifa? (Zaburi 119:9)

5 Ukomalishe na ‘ulinde . . . uwezo wa kufikiri.’ (Mez. 3:21) Mwanaume mwenye kuwa na uwezo wa kufikiri hatendake haraka-haraka ao mbiombio, lakini anafikiri mbele ya kutenda. Kwa hiyo, fanya yako yote ili ukomalishe na ulinde ule uwezo. Juu ya nini? Juu mu hii dunia vijana wengi wanaongozwa na mawazo yao wenyewe, ao wanatenda tu kwa kutegemea namna wanajisikia. (Mez. 7:7; 29:11) Pia televizyo, Enternete na site za kupashana habari zinaweza kuchochea sana namna yako ya kuwaza. Namna gani unaweza kukomalisha uwezo wa kufikiri? Anza kwa kujifunza kanuni za Biblia na ujiulize utapata faida gani kama unazifuata. Kisha utumie zile kanuni ili kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova. (Soma Zaburi 119:9.) Kama unakomalisha ule uwezo, utakuwa umefanya hatua ya maana sana ili kufikia kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho. (Mez. 2:​11, 12; Ebr. 5:14) Fikiria namna uwezo wa kufikiri unaweza kukusaidia mu hizi hali mbili: (1) uhusiano wako pamoya na dada wa mu kutaniko na (2) kuchagua namna ya kuvaa na kujipamba.

6. Uwezo wa kufikiri utasaidia namna gani ndugu kijana aonyeshe dada heshima?

6 Uwezo wa kufikiri utakusaidia uonyeshe wanamuke heshima. Ndugu kijana anaweza kupenda akuwe na urafiki pamoja na dada fulani; ile haiko mubaya. Lakini, kijana mwenye kuwa na uwezo wa kufikiri hatasema, kuandika, ao kufanya jambo yenye itafanya dada awaze kama anapendezwa naye kimapenzi ijapokuwa hana nia ya kuoa ule dada. (1 Ti. 5:​1, 2) Kama iko nachumbia dada fulani, ataepuka kujikuta peke yake na ule dada bila mutu mwingine wa kuwasindikiza, juu asimuharibishie ule dada sifa.—1 Ko. 6:18.

7. Uwezo wa kufikiri unaweza kusaidia namna gani ndugu kijana kuchagua namna ya kuvaa na kukata nywele?

7 Kuchagua muzuri namna ya kuvaa na ya kukata nywele kunaonyesha pia kama ndugu kijana iko na uwezo wa kufikiri. Kwa kawaida, wale wenye wanachochea watu mu namna ya kuvaa hawaheshimie kanuni za Yehova na pengine wanaishi maisha machafu. Mawazo yao machafu inaonekana mu namna yao ya kuvaa. Wanaume wanavaa nguo za kubana sana zenye zinawafanya waonekane sawa wanamuke. Mwanaume mwenye anapenda kukomaa kiroho anaongozwa na kanuni za Biblia na mifano mizuri mu kutaniko wakati anachagua nguo yenye atavaa. Anaweza kujiuliza hivi: ‘Namna yangu ya kuvaa inaonyesha kama niko na akili ya muzuri na kama ninahangaikia maoni ya wengine? Namna yangu ya kuvaa inafanya ikuwe mwepesi kwa wengine kukubali kama niko mutumishi wa Mungu?’ (1 Ko. 10:​31-33; Tit. 2:6) Ndugu mwenye kuwa na uwezo wa kufikiri ataheshimiwa na ndugu na dada lakini pia atapendwa na Yehova.

8. Ndugu kijana anaweza kujifunza namna gani kuwa mwenye kutumainika?

8 Ukuwe mutu mwenye kutumainika. Kijana mwenye kutumainika anatimiza muzuri kabisa migao yake yote. (Lu. 16:10) Fikiria mufano mukamilifu wa Yesu. Hakuna siku Yesu alizarau migao yake. Lakini, alitimiza migao yenye Yehova alimupatia, hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile. Alipenda watu, zaidi sana wanafunzi wake, na alitoa uzima wake kwa kupenda kwa ajili yao. (Yoh. 13:1) Ili kumuiga Yesu, ujikaze sana kutimiza mugao wowote wenye wanakupatia. Kama haujue muzuri namna ya kutimiza mugao fulani, ukuwe munyenyekevu na uombe musaada kwa ndugu wenye kukomaa kiroho. Usifanye tu mambo kidogo, ujikaze kufanya yote yenye unaweza. (Ro. 12:11) Timiza mugao wako, kama “kwa ajili ya Yehova, na hapana kwa ajili ya wanadamu.” (Kol. 3:23) Juu haukamilike, ukuwe munyenyekevu na ukubali makosa yote yenye umefanya.—Mez. 11:2.

UJIFUNZE UFUNDI FULANI WA MAANA

9. Juu ya nini ndugu kijana anapaswa kujifunza ufundi fulani?

9 Ili kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho, uko na lazima ya kujifunza ufundi fulani wa maana. Ile itakusaidia kutimiza migao yako mu kutaniko, kupata kazi ya kukutegemeza weye na familia yako, na kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na wengine. Tuzungumuzie ufundi fulani wa maana.

Kusoma na kuandika muzuri kunaweza kukuletea faida weye na kutaniko yote (Ona fungu ya 10-11)

10-11. Kama ndugu kijana anajua kusoma na kuandika muzuri, ile itamusaidia namna gani yeye na kutaniko? (Zaburi 1:​1-3) (Ona pia picha.)

10 Ujifunze kusoma na kuandika muzuri. Biblia inasema kama mutu mwenye furaha na mwenye anapata matokeo ya muzuri anapitisha wakati kila siku na iko anasoma na kufikiri sana juu ya Neno ya Mungu. (Soma Zaburi 1:​1-3.) Kwa kusoma Biblia kila siku, atafikia kujua namna ya Yehova ya kuona mambo, na ile inaweza kumusaidia kufikiri muzuri. (Mez. 1:​3, 4) Tuko na lazima ya wanaume wa vile mu kutaniko. Juu ya nini?

11 Ndugu na dada wako na lazima ya wanaume wenye uzoefu wa kuwapatie maagizo na mashauri yenye kutegemea Biblia. (Tit. 1:9) Kujua kusoma na kuandika muzuri kunaweza kukusaidia utayarishe hotuba na maelezo yenye kujenga. Ile inaweza pia kukusaidia kuandika maelezo fulani ya maana wakati uko unajifunza Biblia, na wakati uko unasikiliza hotuba ku mikutano na ku mikusanyiko. Mambo yenye uliandika inaweza kukusaidia kujenga imani yako na kutia wengine moyo.

12. Ni nini itakusaidia kujua kuzungumuza muzuri?

12 Ujifunze kuzungumuza muzuri. Mwanaume Mukristo anapaswa kujifunza kuzungumuza muzuri. Mwanaume mwenye anajua kuzungumuza muzuri anasikiliza na anaelewa mawazo ya wengine na namna wengine wanajisikia. (Mez. 20:5) Anaweza kujifunza kutambua maoni ya mutu kupitia sauti ya ule mutu, sura yake, ao ishara zake za mwili. Hauwezi kujifunza kufanya mambo hayo kama haupitishe wakati pamoya na watu. Kama unazoea zaidi kuongea na watu kwa kuwatumia ujumbe ku telefone ao ku ordinatere, ile itakufanya usijue kuzungumuza muzuri na watu uso kwa uso. Kwa hiyo, ujikaze kutafuta nafasi za kuongea na watu uso kwa uso.—2 Yo. 12.

Ni muzuri kujifunza ufundi wenye utakusaidia kupata kazi (Ona fungu ya 13)

13. Ndugu kijana anapaswa kujifunza jambo ingine gani? (1 Timoteo 5:8) (Ona pia picha.)

13 Ujifunze kujitimizia mahitaji yako weye mwenyewe. Mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho anapaswa kuwa na uwezo wa kuhangaikia mahitaji yake na ya familia yake. (Soma 1 Timoteo 5:8.) Mu inchi fulani, baba ao mutu fulani wa mu familia anaweza kufundisha ndugu kijana kazi. Mu fasi zingine, kijana anaweza kujifunza kazi ao ufundi fulani wakati angali ku masomo ya segondere. Ikuwe utatumia njia gani, ni jambo ya maana ujifunze ufundi fulani wenye unaweza kukusaidia kupata kazi. (Mdo. 18:​2, 3; 20:34; Efe. 4:28) Ujulikane kuwa mutu mwenye anatumikaka sana na mwenye anatumika mupaka amalize kazi yenye alianza. Ukifanya vile, inaweza kuwa mwepesi kwako kupata kazi na kuilinda. Sifa na ufundi wenye tumezungumuzia inaweza pia kusaidia mwanaume Mukristo kutimiza madaraka yenye atakuwa nayo mu wakati wenye kuya. Acha tuzungumuzie madaraka fulani.

UJITAYARISHE KWA AJILI YA MADARAKA YA WAKATI WENYE KUYA

14. Ndugu kijana anaweza kujitayarisha namna gani juu ya kuingia mu utumishi wa wakati wote?

14 Mutumishi wa wakati wote. Wanaume Wakristo wengi wenye kukomaa kiroho walianza utumishi wa wakati wote wakati walikuwa wangali vijana. Kuwa painia kunasaidia kijana kujua namna ya kutumika muzuri pamoja na watu tofauti-tofauti. Pia kunamusaidia kujua kutumikisha makuta yake muzuri. (Flp. 4:​11-13) Hatua ya kwanza ya kujitayarisha kuingia mu utumishi wa wakati wote ni kuwa painia musaidizi. Wengi walikuwa mapainia wasaidizi kwa wakati fulani, na ile iliwasaidia kufikia kuwa mapainia wa kawaida. Upainia unaweza pia kufungua mulango kwa ajili ya aina yengine ya utumishi wa wakati wote, kutia ndani kutumika mu ujenzi ao ku Beteli.

15-16. Ndugu kijana anaweza kufanya nini juu astahili kutumikia kutaniko?

15 Mutumishi wa huduma ao muzee. Wanaume Wakristo wanapaswa kutimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa wazee wa kutaniko, juu waweze kutumikia ndugu na dada zao. Mwanaume mwenye iko anajikaza kufikia ile pendeleo “anatamani kazi ya muzuri.” (1 Ti. 3:1) Mbele ya kuwa muzee, ndugu anapaswa kutimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa mutumishi wa huduma. Watumishi wa huduma wanasaidia wazee mu kazi mingi mbalimbali. Wazee na watumishi wa huduma wanatumikia ndugu na dada zao kwa unyenyekevu na wanahubiri kwa bidii. Ndugu vijana wanaweza kustahili kuwa watumishi wa huduma hata wakati wako tu na miaka 17. Watumishi wa huduma wenye uzoefu wanaweza kuwekwa kuwa wazee hata wakati wako tu na miaka 20.

16 Unaweza kufanya nini ili kufikia ile mapendeleo? Kuko sifa zenye unapaswa kukomalisha. Zile sifa zote zinategemea Biblia, upendo wako kwa Yehova, kwa familia yako, na kwa kutaniko. (1 Ti. 3:​1-13; Tit. 1:​6-9; 1 Pe. 5:​2, 3) Ujikaze kuelewa kila sifa yenye inaombwa. Na umuombe Yehova akusaidie ili ukomalishe zile sifa. c

Yehova anapenda bwana apende bibi na watoto wake, awahangaikie kimwili, akuwe rafiki yao na zaidi ya yote awahangaikie kiroho (Ona fungu ya 17)

17. Ndugu kijana anaweza kujitayarisha namna gani kuwa bwana na kichwa cha familia? (Ona pia picha.)

17 Bwana na kichwa cha familia. Sawa vile Yesu alionyesha, wanaume fulani Wakristo wenye kukomaa kiroho wanabakia bila kuoa. (Mt. 19:12) Lakini kama unachagua kuoa, madaraka ingine itaongezeka. Ni kusema, utakuwa bwana na kichwa cha familia. (1 Ko. 11:3) Yehova anatazamia kwamba bwana amupende bibi yake na ahangaikie mahitaji yake ya kiroho, ya kimwili, na akuwe rafiki muzuri kwake. (Efe. 5:​28, 29) Ufundi na sifa zenye tumezungumuzia, sawa vile kuwa na uwezo wa kufikiri, kuheshimia wanamuke, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia kuwa bwana muzuri. Utakuwa umejitayarisha muzuri ili kuwa kichwa na bwana muzuri.

18. Namna gani ndugu kijana anaweza kujitayarisha kuwa baba?

18 Baba. Kisha kuoa, munaweza kuwa na watoto. Mufano wa Yehova unaweza kukufundisha nini kuhusu kuwa baba muzuri? Kuko mambo mingi yenye unaweza kujifunza. (Efe. 6:4) Yehova aliambia waziwazi Yesu, mwana wake, kama anamupenda na anamukubali. (Mt. 3:17) Kama unakuwa baba, uhakikishie watoto wako kwa ukawaida kama unawapenda. Ukuwe na zoea ya kuwapongeza juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Baba wenye wanamuiga Yehova wanasaidia watoto wao wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya ile daraka kwa kupenda na kuhangaikia watu wa familia yako na wa mu kutaniko, na kwa kujifunza kuwaonyesha kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana. (Yoh. 15:9) Ile itakusaidia kutimiza daraka ya kuwa bwana na baba yenye unaweza kuwa nayo mu wakati wenye kuya. Na wakati uleule, utakuwa wa maana sana kwa Yehova, na baraka kwa familia yako na kwa kutaniko.

UNAWEZA KUFANYA NINI SASA?

Vijana wengi wanaume wenye walifundishwa kupitia Maandiko na walitumikisha mambo yenye walijifunza, wamekuwa Wakristo wenye kukomaa kiroho (Ona fungu ya 19-​20)

19-20. Nini itasaidia ndugu kijana akuwe Mukristo mwenye kukomaa kiroho? (Ona picha ku jalada.)

19 Ndugu kijana, hauwezi kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho kama haujikaze. Unapaswa kuchagua mifano mizuri ya kuiga, kukomalisha uwezo wa kufikiri, kujifunza ufundi fulani wa maana, na kujitayarisha kwa ajili ya madaraka ya wakati wenye kuya.

20 Wakati unafikiria mambo yote yenye unapaswa kufanya, unaweza kuwaza kama iko nguvu kwako. Lakini utaweza. Kumbuka kama Yehova iko tayari kukusaidia. (Isa. 41:​10, 13) Ndugu na dada mu kutaniko watakusaidia pia. Wakati utafikia kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho, utakuwa na maisha yenye kufurahisha sana. Ndugu kijana, tunakupenda! Yehova na akubariki sana wakati uko unafanya yako yote ili kufikia kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho.—Mez. 22:4.

WIMBO 65 Fanya Maendeleo!

a Mu kutaniko ya Kikristo tuko na lazima ya wanaume wenye kukomaa kiroho. Mu hii habari, tutaona namna nyiye ndugu vijana munaweza kufikia kuwa wanaume wenye kukomaa kiroho.

b Ona sehemu “Mafasirio ya Maneno Fulani” ya habari yenye kutangulia.

c Ona kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova, sura ya 5-6.