Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu magazeti ya Munara wa Mulinzi ya hii mwaka? Kama ni vile, pima kujibia hii maulizo:

‘Kufanya upya akili yetu’ maana yake nini? (Ro. 12:2)

Hatupaswe tu kufanya matendo fulani ya muzuri mu maisha yetu. Lakini, tunapaswa pia kuchunguza mutu mwenye tuko kwa ndani na kufanya mabadiliko yote yenye inaombwa ili tutii muzuri zaidi kanuni za Yehova.—w23.01, uku. 8-9.

Namna gani tunaweza kuwa na usawaziko wakati tuko tunaona mambo yenye kufanyika mu dunia?

Tunafurahi kuona namna mambo yenye kufanyika leo mu dunia iko natimiza unabii. Kuliko kuwazia kama tukio fulani inatimiza unabii fulani, jambo yenye inaweza kufanya kutaniko ikose kuwa na umoja, ni muzuri mazungumuzo yetu itegemee habari yenye kutolewa na tengenezo ya Yehova. (1 Ko. 1:10)—w23.02, uku. 16.

Kuko tofauti gani kati ya ubatizo wa Yesu na ubatizo wa wanafunzi wake?

Juu alizaliwa mu taifa yenye ilikuwa ilishatolewa kwa Mungu, Yesu hakukuwa na lazima ya kujitoa kwa Yehova sawa vile siye tunafanyaka. Na juu alikuwa mukamilifu, ni kusema, hakukuwa na zambi, hakukuwa na lazima ya kutubu zambi.—w23.03, uku. 5.

Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia wengine watoe maelezo ku mikutano?

Tutoe maelezo ya mufupi juu tupatie pia wengine nafasi ya kutoa maelezo. Tunaweza pia kuepuka kuzungumuzia mawazo mingi sana. Ile itafanya kubakie mambo ingine yenye wengine watazungumuzia.—w23.04, uku. 23.

“Njia ya Utakatifu” yenye kuzungumuziwa mu Isaya 35:8 inamaanisha nini?

Ile njia kubwa ya mufano, kwanza ilimaanisha safari yenye Wayahudi walifanya ya kutoka Babiloni ili kurudia kwao. Halafu mu wakati wetu? Mamia ya miaka mbele ya 1919, kazi ya kutayarisha ile njia ilikuwa inafanywa, ni kusema kazi ya kutafsiri na kuchapisha Biblia, na kazi zingine. Watu wa Mungu wanasafiri mu “njia ya utakatifu” ili kuenda mu paradiso ya kiroho yenye inaongoza kwenye baraka za Ufalme wa Mungu.—w23.05, uku. 15-19.

Sura ya 9 ya kitabu ya Mezali inatupatia mashauri kutokana na wanamuke gani mbili wa mufano?

Kitabu ya Mezali inazungumuzia “mwanamuke mujinga” mwenye mualiko wake unaongoza kwenye “Kaburi,” na “hekima ya kweli” yenye inafananishwa na mwanamuke mwenye mualiko wake unaongoza kwenye “njia ya uelewaji” na ya uzima. (Mez. 9:​1, 6, 13, 18)—w23.06, uku. 22-24.

Namna gani unyenyekevu na usawaziko wa Mungu ulionekana wazi mu namna alimutendea Loti?

Yehova alimuagiza Loti atoke Sodoma na akimbilie mu eneo ya milima. Lakini Loti yeye aliomba akimbilie Soari, na Yehova alikubali ombi lake.—w23.07, uku. 21.

Bibi anaweza kufanya nini kama bwana yake anaangalia pornografia?

Anapaswa kukumbuka kama hapaswe kujihukumu. Anapaswa kukazia akili yake juu ya urafiki wake pamoya na Yehova na kutafakari juu ya habari fulani zenye kuwa mu Biblia zenye kuzungumuzia wanamuke fulani wenye walikuwa na magumu wenye Yehova alifariji. Anaweza kumusaidia bwana yake aepuke hali zenye zinaweza kumuchochea kuangukia tena mu ile mutego.—w23.08, uku. 14-17.

Namna gani ufahamu unaweza kutusaidia kuwa wapole wakati wengine wanapinga mambo yenye tunaamini?

Tunaweza kuona ulizo yao kuwa nafasi ya kujua mambo yenye wanaona kuwa ya maana na mambo yenye wanawaza. Ile inaweza kutusaidia kujibu kwa upole.—w23.09, uku. 17.

Mufano wa Maria unatufundisha nini kuhusu kutiwa nguvu?

Wakati alijua kama atakuwa mama ya Masiya, Maria alitiwa nguvu kupitia wengine. Gabrieli na Elizabeti walimutia Maria moyo kupitia Maandiko. Siye pia tunaweza kutiwa nguvu kupitia waamini wenzetu.—w23.10, uku. 15.

Yehovah anaweza kujibia sala zetu namna gani?

Anaahidi kama atasikiliza sala zetu na anaangalia namna mambo yenye tunamuomba inapatana na kusudi yake. (Yer. 29:12) Anaweza kujibia mu njia tofauti ombi za kufanana, lakini kila siku iko tayari kututegemeza.—w23.11, uku. 21-22.

“Tumaini” inazungumuziwa mu Waroma 5:​2, sasa juu ya nini inazungumuziwa tena mu mustari wa 4?

Wakati mutu anasikia habari njema, anaweza kuwa na tumaini ya kuishi milele mu dunia yenye itakuwa paradiso. Lakini kisha kupata taabu, kuivumilia, na kukubaliwa na Mungu, tumaini yake inakuwa nguvu hata zaidi.—w23.12, uku. 12-13.