Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uone Pombe Vile Mungu Anaiona

Uone Pombe Vile Mungu Anaiona

BILA shaka unafurahia zawadi mingi zenye Mungu ametupatia, kutia ndani uhuru wa kuchagua namna utatumia zile zawadi. Biblia inasema kama divai ni zawadi kutoka kwa Mungu, hata inasema: “Mukate unafanywa ili kuleta kicheko, na divai inafanya maisha yafurahishe.” (Muh. 10:19; Zb. 104:15) Lakini, inawezekana umeona kama watu fulani hawajue namna ya kutumia pombe. Tena, watu mu dunia yote wako na maoni na kanuni tofauti-tofauti juu ya namna ya kutumia pombe. Sasa, ni nini inaweza kusaidia Wakristo wakamate maamuzi ya hekima kuhusu kunywa pombe?

Ikuwe tunaishi wapi ao tulikomalishwa mu desturi gani, kuacha mawazo ya Mungu iongoze mawazo yetu na maamuzi yetu, kutafanya tupate matokeo ya muzuri.

Pengine umejionea kama watu wengi mu dunia wanakunywa pombe mara mingi na wanakunywa pombe ya mingi. Watu fulani wanakunywa pombe juu ya kujifurahisha na wengine wanakunywa juu ya kusahau magumu yao. Na mu maeneo ingine, mutu mwenye anakunywa pombe mingi anaonekana kama iko na nguvu mingi ao ni mwanaume kabisa.

Lakini Wakristo wako na muongozo wenye hekima wa Muumbaji wao mwenye upendo. Kwa mufano, Mungu ametuonya juu ya matokeo ya mubaya ya kunywa pombe sana. Pengine ulishakasoma Mezali 23:​29-35 yenye inazungumuzia namna mutu mwenye anakunywa pombe sana anapata matokeo ya mubaya. a Daniel, muzee Mukristo katika Ulaya, anakumbuka vile maisha yake ilikuwa mbele akuwe Mukristo wa kweli, anasema hivi: “Kunywa pombe sana kulinifanya nikamate maamuzi ya mubaya na nikutane na mambo ya mubaya sana mu maisha yangu. Na wakati ninafikiria ile mambo najisikia mubaya sana.”

Namna gani tunaweza kukamata maamuzi ya hekima kuhusu kunywa pombe na kuepuka matokeo ya mubaya ya kunywa sana? Jambo ya kufanya ni kuacha maoni ya Mungu iongoze mawazo na matendo yetu.

Acha tuzungumuzie mambo yenye Biblia inasema kuhusu pombe na sababu fulani zenye zinachochea watu kunywa.

KANUNI ZA BIBLIA

Neno ya Mungu haikataze kunywa pombe kwa kiasi. Biblia inaonyesha kama kunywa pombe inaweza kufurahisha. Inasema hivi: “Ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo muchangamufu, kwa sababu tayari Mungu wa kweli amefurahia kazi zako.” (Muh. 9:7) Wakati fulani Yesu alikunywa divai. Na watumishi wengine waaminifu wa Yehova walifanya vile pia.—Mt. 26:​27-29; Lu. 7:34; 1 Ti. 5:23.

Lakini, Neno ya Mungu inaonyesha kama kuko tofauti kubwa kati ya kunywa pombe kidogo na kulewa. Biblia inasema waziwazi hivi: “Musilewe divai.” (Efe. 5:18) Na hata Biblia inasema kama “walevi . . . hawatariti Ufalme wa Mungu.” (1 Ko. 6:10) Kwa kweli, Yehova anakataza kabisa kunywa pombe kupita kiasi na ulevi. Kuliko kufuata mambo yenye desturi yetu inasema juu ya pombe, ni jambo ya maana kufuata maoni ya Mungu.

Watu fulani wanawaza kama wanaweza kunywa pombe ya mingi bila kulewa. Lakini, kufanya vile kuko hatari sana. Maandiko inaonyesha wazi kama kuwa “watumwa wa divai nyingi,” kunaweza kuharibisha hali ya kiroho na mwenendo wa mwanaume ao wa mwanamuke. (Tit. 2:3; Mez. 20:1) Yesu alifikia hata kusema kama “kunywa sana” kunaweza kufanya mutu akose kuingia mu dunia mupya ya Mungu. (Lu. 21:​34-36) Sasa ni nini inaweza kusaidia Mukristo aepuke matatizo yenye inatokana na kunywa pombe sana?

CHUNGUZA JUU YA NINI UNAKUNYWA NA UNAKUNYWA KADIRI GANI

Ni hatari kwa mutu kuacha desturi ya kwenye alikomalia ichochee maoni yake kuhusu kunywa pombe. Wakristo wanachagua kwa hekima kumufurahisha Yehova mu mambo yenye inahusu kula na kunywa. Biblia inatukumbusha hivi: “Ikuwe munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Ko. 10:31) Tuone maulizo fulani na kanuni fulani za Biblia za kufikiria:

Ninakunywa pombe juu tu ya kufurahisha wengine? Kutoka 23:2 inasema hivi: “Haupaswe kufuata watu wengi.” Mu hii andiko Yehova alikuwa naonya Waisraeli wasifuate watu wenye hawamufurahishe. Ile shauri inahusu pia Wakristo leo. Kama tunaacha wengine njo wachochee maoni yetu na maamuzi yetu kuhusu pombe, pole kwa pole tunaweza kuacha kufuata kanuni za Yehova na kujitenga naye.—Ro. 12:2.

Ninakunywa pombe juu ya kujionyesha kama niko mutu mwenye nguvu? Mu desturi fulani, kunywa pombe mara mingi na kunywa sana ni mambo ya kawaida na inakubaliwa. (1 Pe. 4:3) Lakini ona mambo yenye 1 Wakorinto 16:13 inatutia moyo tufanye: “Mukae macho, musimame imara katika imani, muendelee kuwa kama wanaume, mukuwe na nguvu.” Pombe inaweza kusaidia mutu kuwa na nguvu? Hapana kabisa, haiwezekane. Pombe inaweza kufanya mutu asikuwe na uwezo wa kufikiri muzuri na asikamate maamuzi ya muzuri. Kwa hiyo, kunywa pombe mingi hakufanye mutu akuwe na nguvu, lakini kunaonyesha kama ni muzaifu. Isaya 28:7 inaonyesha kama wale wenye wanapotea kwa sababu ya pombe wanayumba-yumba na wanajikwaa.

Nguvu ya kweli inatoka kwa Yehova, na ile inaomba kuendelea kuwa macho na kusimama imara katika imani. (Zb. 18:32) Tunafanya vile kwa kuwa waangalifu ili tuepuke kukamata maamuzi yenye inaweza kuharibisha uhusiano wetu pamoja na Yehova. Yesu alionyesha kama alikuwa na ile nguvu kabisa, na watu wengi walimuheshimia na walimuona kuwa mwanaume mwenye bidii mwenye aliazimia kabisa kufanya mambo ya muzuri.

Ninakunywa pombe juu ya kusahau magumu yangu? Muandikaji mumoja wa zaburi aliongozwa kuandika hivi: “Wakati mahangaiko yalinilemea, [Yehova] Ulinifariji na kunituliza.” (Zb. 94:19) Kama uko na magumu mingi, tafuta musaada kwa Yehova hapana mu pombe. Njia moya ya muzuri ya kutafuta musaada kwa Yehova ni kusali tena na tena. Pia, wengi wameona kama kutafuta shauri kwa rafiki mwenye kukomaa kiroho mu kutaniko kunasaidia. Kwa kweli, kunywa pombe ili kusahau magumu, kunaweza kufanya mutu akose nguvu ya kupambana na ile magumu, na kunaweza kufanya asikuwe na nguvu ya kuazimia kufanya mambo yenye kuwa sawa. (Hos. 4:11) Daniel, mwenye tulizungumuzia anasema hivi: “Nilikuwa na wasiwasi na nilikuwa najilaumu. Nilikunywa juu ya kupambana na ile hali lakini ile iliniongezea magumu. Nilifikia kupoteza marafiki na nilijiona kuwa wa bure.” Ni nini ilifikia kumusaidia Daniel? Anasema hivi: “Nilielewa kama nilikuwa na lazima ya musaada wa Yehova, hapana pombe. Kwa musaada wa Yehova niliweza kupambana na magumu yangu.” Ukweli ni kwamba kila siku Yehova iko tayari kutusaidia, hata kama inaonekana hakuna tumaini.—Flp. 4:​6, 7; 1 Pe. 5:7.

Kama unakunywaka pombe, ujichunguze kupitia maulizo yenye kufuata: ‘Kuko mutu fulani wa mu familia yangu ao rafiki yangu wa karibu mwenye iko na wasiwasi juu ya namna yangu ya kunywa?’ Kama ni vile ile inaonyesha kama umeanza kukomalisha tabia ya mubaya bila weye mwenyewe kujua. ‘Nimeanza kunywa pombe mingi kupita vile nilikuwa nakunywa zamani? Ile inaweza kuwa hali ya mutu mwenye anawaza kama haiko mutumwa wa pombe lakini alishaanza kuwa mutumwa wa pombe. ‘Ni nguvu kwangu kufanya masiku fulani ao wakati murefu bila kunywa?’ Kama ni vile ni kusema ulishakuwa na zoezi ya kunywa pombe ao ulishakuwa mutumwa wa pombe. Ile inaweza kumaanisha kama uko na lazima ya musaada wa munganga ili uache ile tabia.

Juu kunywa pombe kunaweza kuleta matatizo, Wakristo fulani wameamua kama hawatakunywa pombe yoyote. Wengine wanaweza kuamua kama hawatakunywa pombe juu tu wanaona kama pombe haina utamu. Kama rafiki yako fulani anachukua ule uamuzi unaweza kumuonyesha upendo kwa kuheshimia uamuzi wake na kwa kuepuka kumulaumu.

Pengine umeona kama ni jambo ya hekima kujiwekea mipaka fulani. Mukristo anaweza kujiwekea mipaka kuhusu kiasi ya pombe yenye atakunywa. Ao anaweza kujiwekea sheria kuhusu mara ngapi atakunywa, pengine mara moja kwa juma ao kunywa kidogo wakati wa chakula. Wengine wamejiwekea mipaka kuhusu aina ya pombe yenye wanaweza kunywa. Kwa mufano wanaweza kunywa divai ao bia kwa kiasi, lakini wanakatala kunywa pombe za makali sana ao hata pombe za makali zenye kuchangwa na vinywaji vya sukari. Wakati mutu anajiwekea mipaka yenye kuwa wazi kuhusu kunywa pombe itakuwa mwepesi kwake kuheshimia ile mipaka. Mukristo wenye kukomaa kiroho hatakuwa na wasiwasi kuhusu namna watu wengine watawaza juu yake kwa sababu amejiwekea mipaka na anaazimia kabisa kuheshimia ile mipaka.

Ni jambo ya lazima pia kufikiria maoni ya wengine. Waroma 14:21 inasema: “Ni muzuri zaidi kuacha kula nyama ao kunywa divai ao kufanya jambo lolote lenye linamukwaza ndugu yako.” Namna gani tunaweza kutumikisha ile shauri? Kwa kuonyesha ndugu zetu upendo. Kama unaona kuwa mutu fulani atakwazika ukikunywa pombe, je, upendo hautakuchochea usikunywe pombe hata kama uko na haki ya kufanya vile? Ukifanya vile utaonyesha kama unahangaikia wengine na unaheshimia mawazo yao wakati uko natafuta faida zao, hapana tu faida yako mwenyewe.—1 Ko. 10:24.

Kwa upande mwingine, wakubwa wa serikali wanaweza kutia sheria zenye zinaweza kusaidia Wakristo kukamata maamuzi. Kwa mufano, kunaweza kuwa sheria zenye zinakataza kunywa pombe mbele ya kufikia umri fulani ao inaweza kukataza kutembeza gari ao kutumikisha mashini fulani kama mutu alishakunywa pombe. —Ro. 13:​1-5.

Yehova ametupatia uhuru wa kufurahia zawadi mbalimbali zenye ametupatia. Moya kati ya zile zawadi ni uhuru wa kuchagua vitu vyenye tutakula na vyenye tutakunywa. Maamuzi yenye tunakamata ionyeshe basi kama tunaona ile zawadi kuwa ya maana kwa kuchagua kumufurahisha Baba yetu wa mbinguni.

a Shirika fulani yenye inahusika na mambo ya afya mu Amerika inaonyesha kama kunywa pombe kupita kiasi hata mara moja kunaweza kuwa na matokeo ya mubaya sawa vile kuua mutu, kujiua, kutendea wengine mubaya kingono, jeuri mu familia, matendo ya kingono yenye kuwa hatari, na mimba kutoka.