Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ushuhuda

Ushuhuda

Kuonyesha Huruma Watu Wote

Siku moya, dada fulani katika Nouvelle-Zélande aliangalia video Muhangaikiane,” yenye inazungumuzia namna Yehova hasikiake tu huruma lakini anafanyaka pia jambo fulani juu ya kusaidia. (Isa. 63:​7-9) Ule dada aliamua kutumikisha mambo yenye alijifunza mu ile video kwa kutafuta nafasi ya kusaidia mutu fulani. Baadaye ile siku, wakati alienda kununua chakula, alikutana na mwanamuke fulani mwenye hana fasi ya kuishi na ule dada akamuuliza kama anaweza kumununulia kitu fulani ya kula. Ule mwanamuke alikubali. Wakati ule dada alirudia na chakula, alimuhubiria kwa muda mufupi kwa kutumia trakte Kuko Siku Mateso Itaisha?

Ule mwanamuke alianza kulia. Alisema kama alikomalia mu familia ya Mashahidi lakini kumepita miaka mingi tangu aache kweli. Hivi karibuni, alikuwa anasali kwa Yehova ili amusaidie kumurudilia. Dada alipatia ule mwanamuke Biblia na akafanya mipango kwa ajili ya funzo. a

Kama Yehova, tunaweza kuonyesha watu huruma, kutia ndani watu wa familia na ndugu na dada mu kutaniko. Na tunaweza pia kuonyesha huruma kwa kutafuta nafasi ya kuhubiria wengine.

a Ili kujua namna ya kusaidia wenye hawatende tena, soma habari “Munirudilie” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 6, 2020.