Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 48

WIMBO 97 Uzima Wetu Unategemea Neno ya Mungu

Muujiza wa Mikate Wenye Yesu Alifanya

Muujiza wa Mikate Wenye Yesu Alifanya

“Mimi ndio mukate wa uzima. Kila mutu mwenye ananifuata hatasikia njaa hata kidogo.”YOH. 6:35.

WAZO KUBWA

Kuchunguza habari yenye kuwa mu Yohana sura ya 6 yenye kuonyesha namna Yesu alikulisha batu mingi kwa kufanya mukate na samaki ikuwe ya mingi, na kuona mambo yenye ile muujiza inatufundisha.

1. Zamani batu balikuwa naona namna gani mukate?

 MUKATE njo chakula yenye batu mingi ba zamani balizoea kula. (Mwa. 14:18; Lu. 4:4) Ilikuwa nakuliwa sana, njo maana wakati fulani Biblia inatumia neno “mukate” juu ya kumaanisha chakula. (Mt. 6:11; Mdo. 20:7) Kati ya miujiza ya Yesu yenye kujulikana sana, kuko miujiza mbili yenye kuhusu mukate. (Mt. 16:9, 10) Yohana sura ya 6 inazungumuzia muujiza moya kati ya ile miujiza mbili. Wakati tutakuwa nazungumuzia ile habari yenye kuwa mu Yohana, tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza na namna tunaweza kuitumikisha leo.

2. Ni hali gani ilifanya batu mingi bakuwe na lazima ya chakula?

2 Kisha mitume wa Yesu kumaliza kuhubiri, Yesu aliingia pamoya nao mu mashua, na wakavuka Bahari ya Galilaya juu wapumuzike. (Mk. 6:7, 30-32; Lu. 9:10) Kisha wakafika fasi fulani ya kimya karibu na Betsaida. Bila kukawia, maelfu ya batu bakafika pale na kuwazunguka. Yesu hakufanya sawa vile hakubaona. Kwa upendo alikamata wakati wa kubafundisha juu ya Ufalme wa Mungu na akaponyesha bagonjwa. Vile saa ilikuwa napita, mitume walikuwa najiuliza ikiwa bale batu bote batapata wapi chakula. Pengine bamoya kati ya bale batu balikuwa na chakula kidogo, lakini bamingi bangekuwa na lazima ya kuenda mu vijiji juu ya kuuza chakula. (Mt. 14:15; Yoh. 6:4, 5) Yesu angefanya nini?

YESU ANATOLEA BATU MUKATE KWA MUUJIZA

3. Yesu alisema nini wakati aliona kama batu balikuwa na lazima ya chakula? (Ona pia picha .)

3 Yesu aliambia hivi mitume wake: “Haiko lazima waende; ninyi muwapatie chakula.” (Mt. 14:16) Lakini ilionekana kuwa ile haitawezekana juu kulikuwa banaume karibu 5000, na kuongeza banamuke na batoto pengine kulikuwa batu 15000. (Mt. 14:21) Kisha Andrea akasema hivi: “Hapa kuko kijana mwanaume mwenye iko na mikate tano (5) ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini vitu hivi ni nini kwa watu hawa wengi?” (Yoh. 6:9) Bamaskini balizoea kula mikate ya shahiri, batu bengine pia balikuwa naikula. Na pengine zile samaki za kidogo zilikuwa zimetiwa chumvi na kukaushwa. Lakini, ile chakula yenye ule kijana alikuwa nayo ilikuwa ya kidogo sana, haingeenea bale batu yote.

Yesu alitimizia batu mahitaji yao ya kiroho na ya kimwili (Ona fungu ya 3)


4. Yohana 6:11-13 inatufundisha nini? (Ona pia picha.)

4 Juu Yesu alipenda kuonyesha bale batu ukarimu, alibaambia baikale chini mu mayani mu bikundi-bikundi. (Mk. 6:39, 40; Soma Yohana 6:11-13.) Biblia inasema kama kisha pale Yesu alitoa shukrani kwa Baba yake kwa ajili ya ile mikate na samaki. Ilifaa kabisa kumushukuru Mungu juu ile chakula ilitoka kwake. Ile inatufundisha kama tunapaswa kufuata mufano wa Yesu kwa kusali mbele ya kula, ikuwe tuko peke yetu ao tuko fasi ya batu mingi. Kisha Yesu akaambia mitume wake wagabulie batu chakula, na batu yote bakakula na kushiba. Na hata chakula ingine ilibakia. Juu Yesu hakupenda iharibike aliambia mitume wake waikusanye, pengine juu ikuliwe wakati ingine. Yesu alituachia mufano juu ya namna ya kutumia vitu vyetu kwa hekima. Kama uko muzazi, hauone kama ni muzuri muzungumuzie hii habari pamoya na batoto yako na muone mambo yenye munaweza kujifunza juu ya sala, ukaribishaji-wageni, na ukarimu?

Ujiulize hivi: ‘Niko nafuata mufano wa Yesu kwa kusali mbele ya kula?’ (Ona fungu ya 4)


5. Batu balitenda namna gani kisha kuona mambo yenye Yesu alifanya ile siku, na Yesu alitenda namna gani?

5 Batu balishangala sana wakati baliona namna ya Yesu ya kufundisha na miujiza yake. Juu balijua kama Musa aliahidi kama Mungu atasimamisha nabii fulani wa pekee, inawezekana balikuwa najiuliza, ‘Yesu njo ule nabii?’ (Kum. 18:15-18) Kama ni vile, pengine baliona kama atakuwa mutawala muzuri sana, pengine ataweza kutolea taifa yote chakula. Kwa hiyo, wale watu walikuwa karibu “kumukamata [Yesu] ili wamufanye kuwa mufalme.” (Yoh. 6:14, 15) Kama Yesu angeacha wamufanye mufalme, angejiingiza mu mambo ya politike ya Wayahudi wenye walikuwa chini ya utawala wa Roma. Lakini Yesu hakufanya vile. Biblia inasema kama Yesu aliamua ‘kuondoka tena na kuenda kwenye mulima.’ Kwa hiyo, hata kama bengine balimushawishi, hakujiingiza mu mambo ya politike. Ile ni somo kwetu!

6. Tunaweza kuonyesha namna gani kama tunafuata mufano wa Yesu? (Ona pia picha.)

6 Batu habatatuomba tufanye miujiza, sawa vile kufanya mikate ikuwe ya mingi ao kuponyesha bagonjwa; na habatajaribu kutufanya tukuwe wafalme ao watawala. Lakini banaweza kutushawishi tujiingize mu mambo ya politike kwa kutuchochea tuchague kiongozi fulani ao tuseme kama tunaunga mukono kiongozi fulani mwenye banaona kama atatengeneza mambo. Lakini, mufano wa Yesu uko wazi. Alikatala kujiingiza mu mambo ya politike, na hata alifikia kusema hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.” (Yoh. 17:14; 18:36) Leo Wakristo wanaiga namna ya Yesu ya kutenda na kuwaza. Tunategemeza Ufalme wa Mungu, tunatoa ushahidi juu ya ule Ufalme, na tunasali juu ya ule Ufalme. (Mt. 6:10) Tuzungumuzie tena muujiza wa Yesu wa kutolea watu mikate na tuone mambo ingine yenye ile habari inaweza kutufundisha.

Yesu aliachia wanafunzi wake mufano kwa kuepuka kujiingiza mu mambo ya politike ya Wayahudi ao ya Waroma (Ona fungu ya 6)


“MAANA YA ILE MIKATE”

7. Yesu na mitume wake walifanya nini? (Yohana 6:16-20)

7 Kisha Yesu kupatia batu chakula, mitume wake waliingia mu mashua juu warudie Kapernaumu. Yesu yeye akaenda ku mulima juu basimufanye kuwa mufalme. (Soma Yohana 6:16-20.) Wakati mitume walikuwa mu bahari, kulitokea zoruba yenye ilileta upepo mukali na mawimbi. Kisha Yesu akaanza kutembea juu ya maji na kuenda kwenye mitume wake walikuwa, na akaambia Petro naye atembee juu ya maji. (Mt. 14:22-31) Wakati Yesu aliingia mu mashua, upepo ukatulia. Ile ilifanya wanafunzi waseme hivi: “Kwa kweli wewe ni Mwana wa Mungu.” a (Mt. 14:33) Lakini, mitume hawakuona uhusiano wenye ulikuwa kati ya muujiza wa Yesu wa kutembea juu ya maji na muujiza wenye alifanya wakati alikuwa na bale batu mingi. Wakati Marko aliandika juu ya ile habari, aliongezea wazo fulani, aliandika hivi: “[Mitume] wakashangaa sana, kwa maana hawakukuwa wameelewa maana ya ile mikate, lakini mioyo yao iliendelea kuwa mizito kuelewa.” (Mk. 6:50-52) Hawakuelewa kama Yehova alikuwa amepatia Yesu nguvu ya mingi sana ya kufanya miujiza. Wakati kidogo kisha pale, Yesu alizungumuzia tena muujiza wa mikate na alionyesha mambo yenye ule muujiza unatufundisha.

8-9. Juu ya nini batu balimufuata Yesu? (Yohana 6:26, 27)

8 Batu benye Yesu alitolea chakula balihangaikia tu kutimiza mahitaji yao ya kimwili na tamaa zao. Juu ya nini tunasema vile? Siku yenye ilifuata, balitambua kama Yesu na mitume wake walishaenda. Kwa hiyo baliingia mu mashua zenye zilifika kutoka Tiberia na bakaenda Kapernaumu kumutafuta Yesu. (Yoh. 6:22-24) Balifanya vile juu balipenda sana kusikia mambo mingi juu ya Ufalme? Hapana. Jambo yenye balikuwa nafikiria sana ni kutimiza mahitaji yao ya kimwili, balikuwa natafuta mukate. Tunajua vile namna gani?

9 Ona mambo yenye ilitokea wakati bale batu balimuona Yesu karibu na Kapernaumu. Yesu alisema waziwazi kama jambo yenye balihangaikia sana ni kutimiza mahitaji yao ya kimwili. Yesu alibaambia hivi: “Mulikula mikate na mukashiba.” Lakini ile ilikuwa “chakula chenye kinaharibikaka.” Alibatia moyo bafanye kazi kwa ajili ya “chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele.” (Soma Yohana 6:26, 27.) Yesu alisema kama Baba yake njo angetoa ile chakula. Inawezekana batu balishangala wakati balisikia kama kuko chakula yenye inaweza kubapatia uzima wa milele! Ni chakula gani yenye ingebapatia uzima wa milele, na namna gani batu benye balikuwa namusikiliza Yesu bangepata ile chakula?

10. “Kazi ya Mungu” yenye batu balipaswa kufanya ni kazi gani?

10 Inaonekana kama wale Wayahudi waliwaza kama walipaswa kufanya matendo ao kazi fulani juu wapate ile chakula. Pengine walikuwa nafikiria “matendo” yenye sheria ya Musa iliomba kufanya. Lakini, Yesu alibaambia hivi: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba ninyi muamini ule mwenye huyo alimutuma.” (Yoh. 6:28, 29) Juu mutu apate “uzima wa milele” anapaswa kuamini ule mwenye Mungu alituma. Yesu alikuwa alishazungumuzia ile jambo mbele ya pale. (Yoh. 3:16-18, 36) Na kisha pale, alizungumuzia tena na tena namna tunaweza kupata uzima wa milele.—Yoh. 17:3.

11. Namna gani Wayahudi walionyesha kama walikuwa tu nahangaikia chakula? (Zaburi 78:24, 25)

11 Wale Wayahudi hawakukubali mafundisho ya Yesu kuhusu “kazi ya Mungu” ya mupya. Walimuuliza hivi Yesu: “Unafanya alama gani, ili tuione na tukuamini? Ni kazi gani yenye unafanya?” (Yoh. 6:30) Walisema kama mu siku za Musa mababu zao walipokea mana, yenye ilikuwa sawa mukate. (Neh. 9:15; Soma Zaburi 78:24, 25.) Ni wazi kama, walikuwa tu wangali nafikiria mukate ya kukula. Na wakati Yesu alizungumuzia “mukate wa kweli kutoka mbinguni” yenye, tofauti na mana, inaleta uzima wa milele, hawakumuuliza anapenda kumaanisha nini. (Yoh. 6:32) Walihangaikia sana mahitaji yao ya kimwili mupaka wakazarau mafundisho ya maana yenye Yesu alipenda kuwafundisha. Hii habari inatufundisha nini?

JAMBO YENYE TUNAPASWA KUHANGAIKIA SANA

12. Yesu alionyesha namna gani jambo yenye inapaswa kuwa ya maana zaidi kwetu?

12 Hii njo somo ya maana sana yenye tunajifunza mu Yohana sura ya 6: Jambo yenye tunapaswa kuhangaikia sana ni kutimiza mahitaji yetu ya kiroho. Kumbuka kama Yesu alikazia ile jambo wakati alipinga majaribu ya Shetani. (Mt. 4:3, 4) Na mu mahubiri yake ya ku mulima, alikazia kama tunapaswa kutambua mahitaji yetu ya kiroho. (Mt. 5:3) Kwa hiyo tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Namna yangu ya kuishi inaonyesha kama ninahangaikia zaidi kutimiza mahitaji yangu ya kiroho kuliko kutimiza tamaa zangu za kimwili?’

13. (a) Juu ya nini haiko mubaya kufurahia chakula? (b) Lakini tunapaswa kufikiria onyo gani? (1 Wakorinto 10:6, 7, 11)

13 Ni muzuri kusali juu ya mahitaji yetu ya kimwili na kufurahia vitu vyenye tuko navyo. (Lu. 11:3) Biblia inasema kama “kula, kunywa” kunaleta furaha, na ile ‘inatoka katika mukono wa Mungu wa kweli.’ (Muh. 2:24; 8:15; Yak. 1:17) Lakini, hatupaswe kutia vitu vya kimwili fasi ya kwanza mu maisha yetu. Mutume Paulo alionyesha ile jambo wakati aliandikia Wakristo wenye waliishi karibu na mwisho wa mupangilio wa mambo wa Wayahudi. Alizungumuzia mufano mubaya wa Waisraeli wakati walikuwa mu jangwa, na mambo yenye ilitokea karibu na Mulima Sinai. Alionya Wakristo ‘wasitamani mambo ya mubaya, kama vile [Waisraeli] waliyatamani.” (Soma 1 Wakorinto 10:6, 7, 11.) Yehova alikuwa ametolea Waisraeli mana kwa muujiza, lakini juu walikuwa na pupa ya chakula, walifikia kuona ule muujiza kuwa “mambo ya mubaya.” (Hes. 11:4-6, 31-34) Na wakati waliabudu kitoto dume cha ngombe cha zahabu, walionyesha kama walihangaikia sana kula, kunywa, na kujifurahisha kuliko kumutii Mungu. (Kut. 32:4-6) Paulo alitumia mufano wa wale Waisraeli juu ya kuonya Wakristo wenye walikuwa naishi karibu na wakati wenye Yerusalemu na hekalu yake ingeharibiwa mu mwaka wa 70 K.K.Y. Leo tunaishi karibu na mwisho wa huu ulimwengu, kwa hiyo ni muzuri tukamate kwa uzito mashauri ya Paulo.

14. Biblia inasema nini juu ya chakula mu dunia mupya?

14 Wakati Yesu alituambia tusali juu ya “mukate wetu kwa ajili ya siku hii,” alituambia pia tusali juu mapenzi ya Mungu ifanyike “duniani kama mbinguni.” (Mt. 6:9-11) Wakati unasikia ile maneno, nini njo inakukuya mu kichwa? Biblia inaonyesha kama mapenzi ya Mungu inatia ndani kufanya dunia itoe chakula mingi. Isaya 25:6-8, inaonyesha kama tutafurahia chakula mingi chini ya Ufalme wa Yehova. Zaburi 72:16 inasema hivi: “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.” Unangoya kwa hamu kutumia nafaka fulani juu ya kufanya aina fulani ya mukate ao kupiga chakula ingine ya mupya? Zaidi ya ile, utafurahia matunda ya shamba yako ya mizabibu. (Isa. 65:21, 22) Na haiko weye tu, batu yote batafurahia ile mambo.

15. Wakati wa ufufuo kutakuwa mupango gani? (Yohana 6:35)

15 Soma Yohana 6:35. Mambo itakuwa namna gani juu ya bale benye balikula mikate na samaki yenye Yesu alitoa kwa muujiza? Pengine utakutana na bamoya kati yao. Hata kama zamani habakuonyesha imani, banaweza kufufuliwa. (Yoh. 5:28, 29) Batakuwa na lazima ya kujifunza maana ya hii maneno ya Yesu: “Mimi ndio mukate wa uzima. Kila mutu mwenye ananifuata hatasikia njaa hata kidogo.” Itaomba waonyeshe imani katika zabihu ya Yesu na waamini kama alitoa uzima wake kwa ajili yao. Ile wakati kutakuwa mupango wa kufundisha batu benye batafufuliwa na batoto benye batazaliwa. Itakuwa furaha sana kusaidia mu ule mupango wa kufundisha! Kufanya vile kutakuletea furaha mingi sana kupita kukula mukate. Kwa kweli, mambo ya kiroho njo itakuwa mambo ya maana zaidi.

16. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

16 Tumezungumuzia sehemu fulani ya habari yenye kuwa mu Yohana sura ya 6, lakini Yesu alifundisha mambo mingi zaidi juu ya “uzima wa milele.” Wale Wayahudi walipaswa kukazia akili ile mambo, na siye pia tunapaswa kuikazia akili. Tutaendelea kuzungumuzia Yohana sura ya 6 mu habari yenye kufuata.

WIMBO 20 Ulimutoa Mwana Wako Mupendwa

a Juu ya kujua mambo mingi zaidi juu ya hii habari, ona kitabu Yesu—Njia, Kweli, na Uzima, uku. 131, na kitabu Tuige Imani Yao, uku. 185.