Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Siyaachaka Kujifunza

Siyaachaka Kujifunza

NINAMUSHUKURU Yehova juu yeye ni ‘Mufundishaji wangu Mukubwa.’ (Isa. 30:20) Anafundisha waabudu wake kupitia Neno yake Biblia, uumbaji wake wa ajabu, na tengenezo yake. Pia anatumia wanadamu wenzetu, ni kusema ndugu na dada zetu wa kiroho, juu ya kutusaidia. Hata kama ninakaribia miaka 100, ninaendelea kujifunza kupitia zile njia zote zenye Yehova ananitolea. Acha niwaelezee namna gani.

Pamoya na familia yangu mu 1948

Nilizaliwa mu 1927 mu muji wa kidogo karibu na Chicago, Illinois, katika Amerika. Bazazi yetu balikuwa na batoto tano: Jetha, Don, miye, Karl, na Joy. Siye bote tuliazimia kumutumikia Yehova kwa moyo wote. Mu 1943 Jetha alisoma darasa ya pili ya Gileadi. Don alienda ku Beteli ya Brooklyn mu New York mu 1944, Karl mu 1947, na Joy mu 1951. Mufano wao muzuri na mufano wa bazazi yangu, ulinigusa sana.

FAMILIA YETU INAJIFUNZA KWELI

Baba na mama balikuwa nasoma Biblia na balimupenda Mungu, na balitusaidia na siye tufanye vile. Baba yangu alikuwa askari mu Vita ya Pili ya Ulimwengu katika Ulaya. Kisha kutoka ku vita, hakutumainia tena makanisa. Mama yangu alifurahi sana kuona vile baba alirudia muzima, alimuambia hivi: “Karl, tuende ku kanisa vile tulizoea kufanya.” Baba akajibia hivi: “Nitakusindikiza, lakini sitaingia.” Mama akamuuliza: “Juu ya nini?” Akajibu: “Wakati wa vita, viongozi wa dini ileile, wenye walikuwa ngambo mbili tofauti, walibariki maaskari wa upande wao! Mungu, aliunga mukono pande zote mbili?”

Kisha, wakati mama alikuwa ku kanisa, Mashahidi wa Yehova wawili walifika kwetu. Walipatia baba yangu buku mbili ya kitabu Mwangaza (katika Kiingereza), yenye ilikuwa nazungumuzia kitabu ya Ufunuo. Baba alipendezwa na akakubali vile vitabu. Wakati mama aliona vile vitabu, akaanza kuvisoma. Kisha, siku fulani mama aliona tangazo mu gazeti fulani ya kutoa habari, yenye inaalika watu wenye wanapenda kujifunza Biblia kupitia vitabu Mwangaza. Aliamua kuenda. Wakati alifika, mwanamuke fulani mwenye kukomala alifungula mulango. Mama alionyesha vile vitabu na akauliza hivi: “Hapa njo muko munajifunza hivi vitabu?” Akajibia: “Ndiyo, karibu ndani.” Juma yenye ilifuata, mama alienda na siye bote batoto tano, na kisha pale tulianza kukusanyika kila juma.

Ku mukutano moya, mwenye alikuwa naongoza aliniomba nisome Zaburi 144:15, yenye inasema kama wale wenye kumuabudu Yehova wako na furaha. Ile andiko ilinigusa sana, pamoya na maandiko ingine mbili, 1 Timoteo 1:11 yenye inasema kama Yehova ni “Mungu mwenye furaha,” na Waefeso 5:1 yenye inatutia moyo tukuwe “waigaji wa Mungu.” Niliamua kama ninapaswa kufurahia mambo yenye niko nafanya juu ya muumbaji wangu na kumushukuru kwa ile pendeleo. Nimejikaza kufanya vile mu maisha yangu yote.

Kutaniko ya karibu ilikuwa ku kilometre 32 mu muji wa Chicago. Hata vile, tulikuwa nakusanyika, na niliendelea kujifunza mambo mingi juu ya Biblia. Ninakumbuka siku moya, mwenye alikuwa naongoza alipatia Jetha ajibie. Wakati nilikuwa namusikiliza Jetha, niliwaza hivi: ‘Nilijua ile jibu, na miye ningeweka mukono yulu na kujibia.’ Nilianza kutayarisha mikutano na kutoa majibu. Na jambo ya maana zaidi, miye na ndugu zangu tulikomala kiroho. Nilibatizwa mu 1941.

KU MIKUSANYIKO NILIJIFUNZA JUU YA YEHOVA

Nakumbukaka sana mukusanyiko wa mu 1942 wenye tulifanya mu Cleveland, Ohio. Maeneo zaidi ya 50 ya mu Amerika ilijiunga na siye kupitia telefone juu ya kufuata ile mukusanyiko. Familia yetu pamoya na mafamilia ingine, tulilala mu mahema karibu na fasi ya mukusanyiko. Vita ya Pili ya Ulimwengu ilikuwa naendelea, na upinzani juu ya Mashahidi wa Yehova ulikuwa naongezeka. Busiku, niliona kikundi ya ndugu wanasimamisha magari yao na tala zao zilikuwa na angalia inje ya kiwanja. Wote walisikilizana kama mu gari mulipaswa kubakia mutu moya wa kutuchunga busiku. Kama kungetokea fujo, ndugu wangewasha tala za magari juu watu wenye kutushambulia wasione muzuri na wangepiga pi-pii. Kisha wengine wangeenda mbio kusaidia. Nilijiambia hivi: ‘Watu wa Yehova wanajitayarisha muzuri kwa ajili ya kila kitu!’ Nilijisikia kuwa salama, nililala muzuri, na hakuna jambo ya mubaya yenye ilitokea.

Kisha miaka, wakati nilikuwa nafikiria ile mukusanyiko, nilitambua kama mama yangu hakuhangaika ao kuogopa hata kidogo. Alimutumainia kabisa Yehova na tengenezo yake. Siwezi kusahau mufano wake muzuri.

Muda kidogo mbele ya mukusanyiko, mama yangu alijaza ombi ya kuwa painia. Kwa hiyo alifuata kwa uangalifu hotuba zenye zilikuwa nazungumuzia utumishi wa wakati wote. Wakati tulikuwa narudia ku nyumba, alisema hivi: “Ninapenda kuendelea kuwa painia, lakini sitaweza kufanya vile na wakati uleule kuhangaikia nyumba yetu.” Kisha akauliza kama tunaweza kumusaidia. Tuliitika, na akapatia kila mumoja wetu chumba moya ao mbili ya kusafisha mbele ya kutumia chakula ya asubui. Kisha siye kuenda ku masomo, aliangalia kama nyumba iko safi kisha alienda mu mahubiri. Alikuwa natumika sana, lakini hakukosa wakati ya kuhangaikia batoto yake. Wakati tulikuwa narudia kula chakula ya muchana na kisha masomo, sikuzote alikuwa pale kwa ajili yetu. Siku fulani kisha masomo, tulikuwa tunamusindikiza mu mahubiri, na ile ilitusaidia kuelewa kazi ya upainia.

KUANZA UTUMISHI WA WAKATI WOTE

Nilianza kazi ya upainia wakati nilikuwa na miaka 16. Hata kama baba yangu alikuwa hayakuwa Shahidi, alihangaikia namna mambo ilikuwa naniendekea mu mahubiri. Mangaribi moya, nilimuambia kama hata kama nimejikaza sana, siyapata mutu wa kujifunza naye Biblia. Nikanyamaza kidogo, kisha nikamuuliza, “utapenda nijifunze na weye Biblia?” Aliwaza kidogo kisha akajibia hivi: “Hakuna sababu yenye inaweza kufanya nikatale.” Kwa kweli, baba yangu njo alikuwa mwanafunzi wangu wa kwanza wa Biblia. Ile ilikuwa pendeleo kubwa!

Tulijifunza kitabu “Kweli Itawaweka Huru.” Wakati nilikuwa nafundisha baba yangu Biblia, nilitambua kama alikuwa nanisaidia nikuwe mwanafunzi muzuri wa Biblia na mwalimu muzuri zaidi. Kwa mufano, mangaribi fulani, kisha kusoma fungu alisema hivi: “Ninaona mambo yenye kitabu inasema. Lakini unajua namna gani kama kitabu kinasema kweli?” Nilikuwa siyajitayarisha juu ya ile, nilisema: “Saa hii sina jibu. Wakati tutajifunza tena nitakuwa nilishapata jibu.” Na nilipata jibu. Nilipata maandiko yenye iliunga mukono jambo yenye tulikuwa nazungumuzia. Kuanzia pale, nilitayarisha muzuri funzo yetu ya Biblia, na nilijifunza kufanya utafiti. Ile ilifanya nikomale kiroho na baba yangu pia akomale kiroho. Alitumikisha mambo yenye alikuwa najifunza na alibatizwa mu 1952.

KU BETELI NILIENDELEA KUJIFUNZA

Nilitoka kwetu wakati nilikuwa na miaka 17. Jetha a akakuwa misionere, na Don, akaenda ku Beteli. Wote wawili walipenda migao yao, ile ilinitia moyo sana. Kwa hiyo nilijaza fomu ya kuenda ku Beteli na ya kusoma masomo ya Gileadi, kisha nikaacha mambo mu mikono ya Yehova. Matokeo ilikuwa nini? Balinialika ku Beteli mu 1946.

Kwa miaka mingi, nimetumikia migao mbalimbali ku Beteli, na ile imeniwezesha kujifunza mambo mingi ya mupya. Mu miaka 75 ku Beteli, nimejifunza namna ya kusaidia kuchapisha vitabu na namna ya kufanya hesabu. Pia nilijifunza namna ya kuuza na kusafirisha vitu mbalimbali. Zaidi ya yote, nimefurahia mafundisho ya kiroho yenye tunapata ku Beteli mu ibada ya asubui na kupitia hotuba zenye kutegemea Biblia.

Niko nafundisha ku masomo ya wazee wa kutaniko

Pia kuko mambo yenye nimejifunza kupitia mudogo yangu, Karl, mwenye alikuya ku Beteli mu 1947. Alikuwa mwanafunzi na mwalimu muzuri wa Biblia. Nilikuwa na hotuba fulani na nilimuomba anisaidie. Nilimuambia Karl kama nilikuwa nimekusanya habari za mingi lakini sikujua namna ya kuzitumikisha. Alinisaidia nijue jambo ya kufanya wakati aliniuliza hivi: “Joel, hotuba yako inazungumuzia nini?” Mara moya nilielewa alipenda kusema nini; wazo yake ilikuwa nizungumuzie tu habari yenye inahusu hotuba yangu, na niache habari zingine pembeni. Ninaendelea kukumbuka ile jambo.

Juu ya kuwa na furaha ku Beteli, ni jambo ya maana tukuwe nahubiri kwa bidii. Kama tunafanya vile tunaweza kujionea mambo mingi yenye kutia moyo. Jambo moya yenye nakumbukaka ni yenye ilitokea mangaribi fulani mu Bronx mu muji wa New York. Miye na ndugu mwengine tulitembelea mwanamuke fulani mwenye aliitika Munara wa Mulinzi na Amuka! Tulijitambulisha kwa kusema hivi: “Hii mangaribi tuko nasaidia batu bajifunze mambo ya muzuri yenye kutoka mu Biblia.” Ule mwanamuke alijibu hivi: “Kama ni juu ya Biblia, muingie.” Tulisoma na kuzungumuzia maandiko mbalimbali kuhusu Ufalme wa Mungu na dunia mupya. Ile mambo ilimugusa sana, kwa hiyo alialika barafiki yake fulani bajiunge na siye mu juma yenye ilifuata. Kisha ule mwanamuke na bwana yake wakakuwa watumishi waaminifu wa Yehova.

KUJIFUNZA KUTOKA KWA BIBI YANGU

Mbele nikutane na bibi yangu, nilikuwa nilishafanya miaka 10 na niko natafuta mutu wa kuoana naye. Nini njo ilinisaidia nipate bibi muzuri? nilisali sana na kufikiri juu ya hii ulizo, ‘Nini njo ninapenda kufanya kisha ndoa?’

Niko na Mary mu kazi ya muzunguko

Kisha mukusanyiko wenye ulifanywa mu 1953 mu Yankee Stadium, nilikutana na dada mwenye kuitwa Mary Aniol. Yeye na Jetha balisomaka pamoya darasa ya pili ya masomo ya Gileadi na yangu balitumika fasi moya mu kazi yao ya umisionere. Mary alinielezea kwa furaha juu ya kazi yake ya umisionere mu Karibea na juu ya mafunzo ya Biblia yenye aliongoza kwa miaka mingi. Vile tuliendelea kujuana muzuri zaidi, tulitambua kama tulikuwa na miradi ileile. Tukapendana sana na tukaoana mu Mwezi wa 4, 1955. Mu njia mingi, Mary alionyesha kuwa alikuwa zawadi kutoka kwa Yehova na alikuwa mufano muzuri wa kuiga. Alifurahia mugao wote wenye alipewa. Alitumika kwa bidii, alihangaikia bengine kwa moyo wote na sikuzote alitia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Tulitumika mu kazi ya muzunguko kwa miaka tatu na mu 1958, tulialikwa ku Beteli.

Nilijifunza mambo mingi kutoka kwa Mary. Kwa mufano, ku mwanzo-mwanzo wa ndoa yetu, tuliamua kama tutakuwa nasoma Biblia pamoya. Tulikuwa tunasoma mistari karibu 15, kisha mumoya wetu kusoma sehemu, tulikuwa tunazungumuzia ile maandiko na namna ya kuitumikisha mu maisha yetu. Mara mingi Mary aliniambia mambo yenye alijifunza ku Gileadi ao mu kazi yake ya umisionere. Ile mazungumuzo ilifanya hotuba zangu zikuwe za muzuri zaidi na ilinisaidia nijue namna ya kutia moyo dada.—Mez. 25:11.

Bibi yangu mupendwa Mary alikufa mu 2013. Ninangoya kwa hamu kumuona tena mu dunia mupya! Lakini mbele ile wakati ifike, ninaazimia kuendelea kujifunza na kumutumainia Yehova kwa moyo wangu wote. (Mez. 3:5, 6) Wakati ninafikiria mambo yenye batu ya Yehova batafanya mu dunia mupya, ile inanifariji na kuniletea furaha. Bila shaka kati ya ile mambo, tutajifunza mambo mingi kutoka kwa Mufundishaji wetu Mukubwa na juu yake! Kwa kweli, nakosa maneno ya kumushukuru juu ya mambo yenye amenifundisha kufikia hapa na juu ya namna amenionyesha fazili zake zenye hazistahiliwe mu njia mingi.

a Ona habari juu ya maisha ya Jetha Sunal mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 3, 2003, uku. 23-29.