Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

WIMBO 147 Ahadi ya Uzima wa Milele

Unapaswa Kufanya Nini Juu Uishi Milele?

Unapaswa Kufanya Nini Juu Uishi Milele?

“Kila mutu mwenye anakubali Mwana na kumuamini akuwe na uzima wa milele.”YOH. 6:40.

WAZO KUBWA

Namna zabihu ya Yesu inaletea faida watiwa-mafuta na kondoo wengine.

1. Batu mingi banawaza nini kuhusu kuishi milele?

 BATU mingi banakuwaka baangalifu juu ya chakula yenye batakula na banafanyaka mazoezi kwa ukawaida juu baendelee kuwa na afya ya muzuri. Lakini, banajua kama haiko ile njo itafanya basizeeke na kufa. Pengine banawaza kama haiwezekane kuishi milele. Lakini, Yesu alisema kama inawezekana wanadamu wapate “uzima wa milele,” sawa vile Yohana 3:16 na 5:24 inasema.

2. Yohana sura ya 6 inasema nini juu ya uzima wa milele? (Yohana 6:39, 40)

2 Siku moya, Yesu alifanya muujiza kwa kutolea batu mingi mikate na samaki. a Ile ilikuwa jambo ya kushangaza. Lakini jambo yenye alisema kisha pale, ilikuwa ya kushangaza tena zaidi. Bale batu balimufuata Kapernaumu, karibu na bahari ya Galilaya, na kule alibaambia kama inawezekana batu bafufuliwe na kuishi milele. (Soma Yohana 6:39, 40.) Wazia barafiki yako na batu benye unapenda benye bamekufa. Maneno ya Yesu inaonyesha kama batu mingi benye bamekufa banaweza kufufuliwa na kama weye na batu benye unapenda munaweza kuishi milele. Lakini, imekuwa nguvu kwa batu mingi kuelewa maneno yenye Yesu alisema kisha pale yenye iko mu Yohana sura ya 6. Yesu alisema nini?

3. Kulingana na Yohana 6:51 Yesu alifundisha nini juu yake mwenyewe?

3 Batu benye balifuata Yesu Kapernaumu baliona uhusiano kati ya mikate yenye Yesu alibatolea na mana yenye Yehova alitoleaka mababu zao. Hata maandiko inaita ile mana kuwa “mukate kutoka mbinguni.” (Zb. 105:40; Yoh. 6:31) Yesu alizungumuzia mana juu ya kubafundisha jambo fulani ya maana. Hata kama mana ilikuwa chakula yenye Mungu alitoa kwa muujiza, bale benye baliikula balifikia kufa. (Yoh. 6:49) Lakini, Yesu alijiita “mukate wa kweli kutoka mbinguni,” “mukate wa Mungu,” na “mukate wa uzima.” (Yoh. 6:32, 33, 35) Yesu alionyesha tofauti yenye kuwa kati yake na mana. Alisema hivi: “Mimi ni mukate wa uzima wenye ulishuka kutoka mbinguni. Kama mutu yeyote anakula mukate huu ataishi milele.” (Soma Yohana 6:51.) Wale Wayahudi walivurugika. Hawakuelewa juu ya nini Yesu anaweza kusema kama alishuka kutoka mbinguni kama “mukate” ya hali ya juu kupita mana yenye Mungu alitolea mababu zao. Kisha Yesu aliwaambia hivi: “Mukate wenye nitatoa ni mwili wangu.” Yesu alimaanisha nini? Ni muzuri tuelewe jibu ya ile ulizo juu inaonyesha namna siye na batu benye tunapenda tunaweza kuishi milele. Tuone mambo yenye Yesu alimaanisha.

MUKATE WA UZIMA NA MWILI WAKE

4. Juu ya nini maneno ya Yesu ilikwaza batu fulani?

4 Batu fulani benye balikuwa banamusikiliza Yesu balikwazika sana wakati alisema kama atatoa ‘mwili wake kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’ Baliwaza kama atabapatia mwili wake juu baikule, ni kusema bakule nyama ya mutu. (Yoh. 6:52) Kisha Yesu alisema jambo yenye ingebakwaza tena zaidi: “Kama hamukule mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamuna uzima ndani yenu wenyewe.”—Yoh. 6:53.

5. Juu ya nini tuko hakika kama Yesu hakumaanisha kama batu balipaswa kunywa damu yake?

5 Mu siku za Noa, Mungu alikataza banadamu kula damu. (Mwa. 9:3, 4) Yehova alirudilia ile jambo mu Sheria yenye alipatia Waisraeli. Mutu yeyote mwenye angekula damu alipaswa “kuuawa.” (Law. 7:27, maelezo ya chini.) Yesu aliheshimia ile Sheria. (Mt. 5:17-19) Kwa hiyo haingewezekana atie moyo Wayahudi wakule mwili wake na wakunywe damu yenye kuwa mu mishipa yake. Lakini, kupitia ile maneno yenye kushangaza, Yesu alikuwa nafundisha batu namna ya kupata uzima, ni kusema “uzima wa milele.”—Yoh. 6:54.

6. Tunapaswa kuelewa namna gani maneno ya Yesu kuhusu kula mwili wake na kunywa damu yake?

6 Yesu alipenda kufundisha nini? Ni wazi kama Yesu alikuwa natumia maneno ya mufano, sawa vile alifanya mbele ya pale, wakati aliambia hivi mwanamuke Musamaria: “Kila mutu mwenye atakunywa maji yenye nitamupatia hatasikia kiu hata kidogo, lakini maji yenye nitamupatia yatakuwa chemchemi ya maji ndani yake, yenye kububujika ili kutoa uzima wa milele.” (Yoh. 4:7, 14) b Yesu hakukuwa namaanisha kama ule mwanamuke Musamaria angepata uzima wa milele kwa kunywa tu maji fulani. Vilevile, hakukuwa naambia bale batu mingi katika Kapernaumu kama bangeishi milele kama tu banakula mwili wake na kunywa damu yake sawa vile banakulaka chakula.

TOFAUTI KATI YA MAMBO MBILI

7. Batu fulani banasema nini juu ya maneno yenye kuwa mu Yohana 6:53?

7 Batu fulani banasema kama maneno ya Yesu ya mu Yohana 6:53 inazungumuzia mambo yenye batu banapaswa kufanya wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Banasema vile juu wakati Yesu alianzisha ile tukio, alitumia maneno yenye kufanana na ya mu Yohana sura ya sita. (Mt. 26:26-28) Banasema kila mutu mwenye kuhuzuria Chakula cha Mangaribi cha Bwana anapaswa kula mukate na kunywa divai. Ile mawazo ni ya kweli? Ni jambo ya maana tuelewe muzuri ile mambo juu kila mwaka mamilioni ya batu mu dunia yote banajiunga na siye juu ya kufanya ile tukio. Tuone mambo yenye kuwa tofauti kati ya maneno yenye kuwa mu Yohana 6:53 na maneno yenye Yesu alisema wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana.

8. Kuko tofauti gani kati ya mambo yenye Yesu alisema Galilaya na mambo yenye alisema wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana? (Ona pia picha.)

8 Acha tuzungumuzie tofauti mbili. Kwanza, ni wakati gani na ni wapi njo Yesu alisema maneno yenye kuwa mu Yohana 6:53-56? Yesu aliambia ile maneno kikundi ya Wayahudi katika Galilaya mu mwaka wa 32. Ilikuwa karibu mwaka moya mbele aanzishe Chakula cha Mangaribi cha Bwana katika Yerusalemu. Pili, Yesu aliambia nani ile maneno? Batu mingi benye balikuwa namusikiliza Yesu katika Galilaya balihangaikia sana kutimiza mahitaji yao ya kimwili kuliko kutimiza mahitaji yao ya kiroho. (Yoh. 6:26) Na wakati Yesu alisema jambo yenye habakuelewa, bila kukawia baliacha kumuamini. Na hata, wanafunzi wake fulani waliacha kumufuata. (Yoh. 6:14, 36, 42, 60, 64, 66) Ile mambo iko tofauti sana na mambo yenye ilifanyika mwaka moya kisha pale mu mwaka wa 33, wakati Yesu alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Mu ile tukio, mitume wake waaminifu 11 walikuwa pamoya naye hata kama hawakuelewa muzuri mambo fulani yenye alikuwa nafundisha. Tofauti na batu katika Galilaya, mitume wake waaminifu walikuwa hakika kama Yesu alikuwa Mwana wa Mungu mwenye alitoka mbinguni. (Mt. 16:16) Yesu aliwapongeza kwa kuwaambia hivi: “Ninyi ndio mumeshikamana na mimi katika majaribu yangu.” (Lu. 22:28) Ile tofauti mbili tu inatusaidia kuelewa kama, mu Yohana 6:53 Yesu hazungumuzie mambo ya kufanya wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Lakini haiko ile tu.

Yohana sura ya 6 inazungumuzia mambo yenye Yesu aliambia kikundi ya Wayahudi mu Galilaya (kushoto). Mwaka moya kisha pale alizungumuza na kikundi kidogo ya mitume wake waaminifu mu Yerusalemu (kuume) (Ona fungu ya 8)


MANENO YA YESU INAWEZA KUKULETEA FAIDA GANI?

9. Maneno yenye Yesu alisema wakati Chakula cha Mangaribi cha Bwana ilihusu nani?

9 Wakati ya Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu alipatia mitume wake mukate wenye hauna chachu na kuwaambia kama ule mukate unafananisha mwili wake. Kisha akawapatia divai na kusema kama inafananisha “damu ya agano.” (Mk. 14:22-25; Lu. 22:20; 1 Ko. 11:24) Mambo yenye alisema juu ya agano ni ya maana. Agano jipya haikufanywa na batu yote, lakini ilifanywa tu na “nyumba ya Israeli [ya kiroho]” wenye watakuwa “katika Ufalme wa Mungu.” (Ebr. 8:6, 10; 9:15) Ile wakati mitume hawakuelewa ile jambo. Lakini kisha wakati kidogo wangetiwa mafuta na roho takatifu na kuingia mu agano jipya juu waweze kutawala na Yesu mbinguni.—Yoh. 14:2, 3.

10. Kuko tofauti gani ingine kati ya mambo yenye Yesu alisema Galilaya na mambo yenye alisema wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana? (Ona pia picha.)

10 Ona kama wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu alikuwa nazungumuzia “kundi ndogo.” Mitume wenye walikuwa na Yesu mu ile nyumba wakati alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana, njo walikuwa wa kwanza mu ile kundi ndogo. (Lu. 12:32) Mitume na wengine wenye wangejiunga nao mu kundi ndogo njo wenye walipaswa kula mukate na kunywa divai. Wao njo watatawala mbinguni pamoya na Yesu. Mambo yenye Yesu aliambia mitume wake wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana ilihusu batu kidogo. Lakini maneno yenye alisema katika Galilaya ilihusu batu mingi zaidi.

Ni hesabu kidogo tu ya watu njo wanakula mukate na kunywa divai, lakini “kila mutu” anaweza kuonyesha imani katika Yesu na kupata uzima wa milele (Ona fungu ya 10)


11. Yesu alisema nini Galilaya yenye inaonyesha kama hakukuwa nazungumuzia batu kidogo?

11 Wakati Yesu alikuwa Galilaya mu mwaka wa 32, alikuwa nazungumuza na Wayahudi wenye walikuwa wanamutafuta juu awapatie mukate. Lakini, Yesu alizungumuza nao juu ya jambo fulani ya maana zaidi kupita chakula. Alizungumuzia mupango wenye ungewasaidia kupata uzima wa milele. Yesu alisema pia kama wale wenye walikuwa wamekufa wangefufuliwa siku ya mwisho na kuishi milele. Yesu hakukuwa nazungumuzia batu kidogo, sawa vile alifanya wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Lakini, mu Galilaya Yesu alikuwa nazungumuzia baraka yenye batu yote bangeweza kupata. Alisema hivi: “Kama mutu yeyote anakula mukate huu ataishi milele . . . mukate wenye nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”Yoh. 6:51. c

12. Mutu anapaswa kufanya nini juu apate uzima wa milele?

12 Yesu hakuambia Wayahudi wenye walikuwa Galilaya kama batu yote benye baliishi ku dunia ao benye bataishi ku dunia batapata uzima wa milele. Ni wenye tu ‘wanakula mukate huu,’ ni kusema wenye kuonyesha imani, njo wangepata ile baraka. Batu mingi benye kujiita Bakristo banawaza kama ikiwa tu banamuamini Yesu na kumuona kuwa Bwana na mwokozi wao, bataokolewa. (Yoh. 6:29) Lakini ile haitoshe juu ku mwanzo batu mingi mu Galilaya balimuamini Yesu, lakini kisha wakati baliacha kumufuata. Juu ya nini?

13. Wanafunzi wa kweli wa Yesu wanapaswa kufanya nini?

13 Batu mingi benye Yesu alikulisha balikuwa namufuata juu tu alikuwa nabapatia mambo yenye balipenda. Balifurahia namna Yesu aliponyesha batu kwa muujiza, chakula ya bure, na mafundisho yenye ilipatana na mawazo yao. Lakini, Yesu alionyesha kama wanafunzi wake wa kweli wanapaswa kufanya mambo mingi zaidi. Yesu hakukuya ku dunia juu tu ya kutimiza tamaa za batu. Batu balipaswa kukubali mwaliko wake wakati alisema ‘mukuye kwangu.’ Bangefanya vile kwa kukubali na kutii mambo yote yenye alifundisha.—Yoh. 5:40; 6:44.

14. Tunapaswa kufanya nini juu mwili na damu ya Yesu ituletee faida?

14 Yesu aliambia ile kikundi ya batu kama ni jambo ya lazima waonyeshe imani. Kuonyesha imani katika nini? Balipaswa kuonyesha imani katika uwezo wa kukomboa wa mwili na damu ya Yesu, wakati ingetolewa kuwa zabihu. Ilikuwa jambo ya lazima Wayahudi waamini vile, na ni jambo ya lazima kwetu pia. (Yoh. 6:40) Kwa kweli, sawa vile Yohana 6:53 inaonyesha, juu mwili na damu ya Yesu ituletee faida tunapaswa kuonyesha imani katika bei ya ukombozi. Na batu mingi sana banaweza kufanya vile.—Efe. 1:7.

15-16. Tumejifunza mambo gani ya maana mu Yohana sura ya 6?

15 Mambo yenye Biblia inasema mu Yohana sura ya 6 ni ya maana sana kwetu na kwa wapendwa wetu. Inaonyesha wazi namna Yesu anahangaikia sana batu. Wakati alikuwa Galilaya, aliponyesha bagonjwa, alifundisha juu ya Ufalme, na alitimiza mahitaji ya kimwili ya batu kwa kubapatia chakula. (Lu. 9:11; Yoh. 6:2, 11, 12) Na jambo ya maana zaidi, alifundisha batu kama yeye ni “mukate wa uzima.”—Yoh. 6:35, 48.

16 Wale wenye Yesu aliita “kondoo wengine” hawapaswe kula mukate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho, tukio yenye tunafanya kila mwaka. (Yoh. 10:16) Wanakula mwili na damu ya Yesu mu njia ya mufano. Wanafanya vile kwa kuonyesha imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu na baraka zote zenye tutapata kupitia ile zabihu. (Yoh. 6:53) Lakini, wenye wanakula mukate na divai wanaonyesha kama wako katika agano jipya na wako na tumaini ya kutawala pamoya na Yesu mbinguni katika Ufalme. Kwa hiyo, ikuwe tuko watiwa-mafuta ao kondoo wengine, habari yenye kuwa mu Yohana sura ya 6 inatufundisha mambo mingi. Inaonyesha kama ni jambo ya maana sana kuonyesha imani ili kupata uzima wa milele.

WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe

a Yohana sura ya 6:5-35 inazungumuziwa mu habari yenye kutangulia.

b Maji yenye Yesu alizungumuzia inafananisha mipango yenye Yehova alikamata juu wanadamu waweze kuishi milele.

c Yohana sura ya 6 inatumia neno yenye inaweza kutafsiriwa “kila mutu” kuhusu wale wenye wataishi milele.—Yoh. 6:35, 40, 47, 54, 56-58.