Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA

Watu Waaminifu Wanatimizaka Naziri Zao

Watu Waaminifu Wanatimizaka Naziri Zao

Soma Waamuzi 11:30-40 juu uone mambo yenye mufano wa Yefta na mutoto wake mwanamuke inaweza kukufundisha kuhusu kutimiza naziri.

Chunguza habari yote. Waisraeli waaminifu waliona namna gani naziri zenye walimutolea Yehova? (Hes. 30:2) Namna gani Yefta na mutoto wake mwanamuke walionyesha kama walikuwa na imani kwa Yehova?—Amu. 11:9-11, 19-24, 36.

Ujifunze mambo mingi zaidi. Inawezekana Yefta alikuwa nafikiria nini wakati alifanya naziri? (w16.04 7 fu. 12) Yefta na mutoto wake walijiima mambo gani juu ya kutimiza naziri? (w16.04 7-8 fu. 14-16) Leo Wakristo wanaweza kufanya naziri gani?—w17.04 5-8 fu. 10-19.

Umejifunza nini? Ujiulize hivi:

  • ‘Ni nini inaweza kunisaidia niendelee kutimiza naziri yangu ya kujitoa kwa Mungu?’ (w20.03 13 fu. 20)

  • ‘Ninaweza kujiima mambo gani juu ya kumutumikia Yehova zaidi?’

  • ‘Nini inaweza kunisaidia niendelee kuheshimia naziri yangu ya ndoa?’ (Mt. 19:5, 6; Efe. 5:28-33)