Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

Yehova Anaona Machozi Yako

Yehova Anaona Machozi Yako

“Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi. Je, hayaandikwe katika kitabu chako?”ZB. 56:8.

WAZO KUBWA

Yehova anaelewa namna tunajisikia wakati tuko na magumu na anatufariji.

1-2. Ni mambo gani yenye inaweza kufanya tutoshe machozi?

 WAKATI fulani, siye bote tunatoshaka machozi. Tunaweza kutosha machozi ya furaha wakati mambo ya muzuri inatufikia. Pengine ulilia wakati jambo fulani ya maana ao ya pekee ilitokea, kwa mufano wakati mutoto wako alizaliwa, wakati ulikumbuka jambo fulani ya muzuri, ao wakati ulionana tena na rafiki yako mwenye ulionaka zamani sana.

2 Lakini, mara mingi tunaliaka juu ya huzuni mingi yenye tuko nayo mu moyo. Kwa mufano tunaweza kulia wakati mutu anatuvunja moyo tunaweza kulia, sababu ya maumivu ya ugonjwa wa muda murefu, ao wakati mupendwa wetu anakufa. Wakati za vile, tunaweza kujisikia sawa vile nabii Yeremia alijisikia wakati Wababiloni walishambulia Yerusalemu. Yeremia alisema hivi: “Mito midogo ya maji inatiririka kutoka kwenye macho yangu . . . Macho yangu yanalia bila kuacha, bila kupumuzika.”—Omb. 3:48, 49.

3. Yehova anajisikiaka namna gani wakati anaona watumishi wake wako nateseka? (Isaya 63:9)

3 Yehova anajua machozi yote yenye tulishakatosha kwa sababu ya magumu. Biblia inatuhakikishia kama Yehova anajua hali zote za nguvu zenye watumishi wake wanapambana nazo, na anatusikiliza wakati tunamulilia atusaidie. (Zb. 34:15) Ni kweli kama Yehova anaonaka na kutusikiliza wakati tunamulilia, lakini haishiake tu pale. Kama muzazi mwenye upendo, anasikiaka mubaya sana wakati anaona watoto wake wako nalia, na ile inamuchocheaka afanye jambo fulani juu ya kuwasaidia.—Soma Isaya 63:9.

4. Mifano fulani ya mu Biblia inaweza kutufundisha nini juu ya Yehova?

4 Biblia inaonyesha vile Yehova alitenda wakati watumishi wake walitosha machozi. Tutaona vile alitenda kwa kuchunguza mufano wa Hana, Daudi, na Mufalme Hezekia. Juu ya nini walilia? Yehova alitenda namna gani wakati walimulilia awasaidie? Namna gani mufano wao unaweza kutufariji wakati tunalia kwa sababu ya huzuni, kwa sababu ya kusalitiwa, ao kwa sababu ya kukosa tumaini?

MACHOZI YA HUZUNI

5. Hana alijisikia namna gani kwa sababu ya magumu yake?

5 Hana alipata magumu ya mingi yenye ilimufanya alie kwa huzuni. Bwana yake alikuwa na bibi mwingine mwenye kuitwa Penina, na ule bibi alikuwa anamutendea Hana mubaya. Zaidi ya ile magumu, Hana hakukuwa nazala, lakini Penina alikuwa na batoto mingi. (1 Sa. 1:1, 2) Penina alikuwa anamuzarau Hana kila wakati juu hakukuwa anazala. Ungekuwa Hana, ungejisikia namna gani? Hana alihuzunika sana mupaka “alikuwa analia na hakukuwa anakula. . . . Alikuwa na uchungu mwingi sana” mu moyo wake.—1 Sa. 1:6, 7, 10.

6. Hana alifanya nini juu apate faraja?

6 Nini njo ilimufariji Hana? Jambo moya yenye ilimusaidia ni kuenda kuabudu Yehova ku tabenakulo. Kule, inawezekana alienda pembeni ya muingilio wa uwanja wa tabenakulo na “akaanza kusali kwa Yehova na kulia bila kujizuia.” Alimulilia Yehova hivi: “[Ona] mateso ya mutumishi wako na kunikumbuka.” (1 Sa. 1:10b, 11) Hana alimufungulia Yehova moyo wake katika sala. Bila shaka Yehova aliguswa sana kuona machozi ya ule mutoto yake mwanamuke mwenye alipenda sana!

7. Hana alijisikia namna gani kisha kumufungulia Yehova moyo?

7 Hana alijisikia namna gani kisha kumufungulia Yehova moyo wake katika sala na kisha Kuhani Mukubwa Eli kumuhakikishia kama Yehova atamusikiliza? Biblia inasema hivi: “Mwanamuke huyo akaenda zake na akakula, na uso wake haukukuwa tena na huzuni.” (1 Sa. 1:17, 18) Hata kama hali yake ilikuwa haiyabadilika, Hana alitulia. Alikuwa amemutupia Yehova muzigo wake. Yehova aliona huzuni yake, alisikia kilio yake, na kisha alimubariki kwa kumupatia mutoto.—1 Sa. 1:19, 20; 2:21.

8-9. Kulingana na Waebrania 10:24, 25, juu ya nini tunapaswa kujikaza kufika ku mikutano? (Ona pia picha.)

8 Mambo yenye tunajifunza. Uko na magumu yenye inafanya utoshe machozi ya huzuni? Pengine uko na huzuni juu mutu wa familia yako ao rafiki yako amekufa. Mu hali za vile, ni kawaida mutu kupenda kuwa peke yake. Lakini sawa tu vile Hana alifarijiwa na kutiwa moyo wakati alienda ku tabenakulo, unaweza kufarijiwa wakati unaenda ku mikutano hata kama haujisikie muzuri. (Soma Waebrania 10:24, 25.) Ku mikutano utasikia maandiko ya Biblia yenye kutia moyo na yenye kufariji. Ile ni njia yenye Yehova anatumia juu ya kukusaidia kukazia akili mawazo ya muzuri na kuachana na mawazo yenye kuvunja moyo. Ile inaweza kukusaidia ujisikie muzuri hata kama hali yako haibadilike palepale.

9 Ku mikutano yetu, ndugu na dada zetu wanatuonyesha huruma na tunajisikia muzuri wakati tunaona namna wanatuhangaikia na wanatupenda. (1 Te. 5:11, 14) Ona mufano wa ndugu fulani painia wa pekee mwenye bibi yake alikufa. Alisema hivi: “Ningali nalia. Wakati fulani, naikalaka pembeni miye peke na kuanza kulia. Lakini mikutano inanisaidiaka sana. Maneno yenye kutia moyo ya ndugu na dada zangu inanituliza kabisa. Hata kama niko na wasiwasi ao mahangaiko mbele ya kuenda ku mikutano, kisha mikutano najisikiaka tu muzuri.” Ku mikutano yetu, Yehova anaweza kutumia ndugu na dada zetu juu ya kutusaidia.

Waabudu wenzetu wanaweza kutufariji (Ona fungu ya 8-9)


10. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Hana wakati tuko na maumivu ya moyo?

10 Jambo ingine yenye ilimufariji Hana ni kumufungulia Yehova moyo wake katika sala. Na weye unaweza ‘kumutupia [Yehova] mahangaiko,’ na kuwa hakika kama atakusikiliza. (1 Pe. 5:7) Dada fulani mwenye bamwizi baliua bwana yake alisema hivi: “Nilijisikia sawa vile moyo wangu unavunjika vipande-vipande na hautaponaka tena. Kusali kwa Yehova, Baba yangu mwenye upendo, njo kulinifariji. Wakati fulani, nilikosa maneno ya kusema mu sala lakini alinielewa. Wakati nilikuwa na huzuni sana na mahangaiko, nilimuomba anipatie amani ya moyo. Kisha kusali, moyo na akili yangu vilitulia na niliweza kuendelea na mambo ingine.” Wakati unamulilia Yehova na kumuambia mahangaiko yako yote, Yehova anahuzunika kuona machozi yako na anaelewa maumivu yenye uko nayo. Hata kama magumu yako haiishe, Yehova anaweza kukutuliza na kukusaidia ukuwe na amani kwa kiasi fulani. (Zb. 94:19; Flp. 4:6, 7) Na atakubariki juu unaendelea kuvumilia kwa uaminifu.—Ebr. 11:6.

MACHOZI YA KUSALITIWA

11. Daudi alijisikia namna gani wakati bengine balimutendea mubaya?

11 Daudi alipata magumu mingi sana mu maisha yake yenye ilifanya alie. Batu balimuchukia na hata batu benye alitumainia balimusaliti. (1 Sa. 19:10, 11; 2 Sa. 15:10-14, 30) Wakati fulani, aliandika hivi: “Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu; usiku wote ninalowanisha kitanda changu kwa machozi.” Juu ya nini Daudi alijisikia vile? Anasema hivi: “Kwa sababu ya wale wote wenye kunisumbua.” (Zb. 6:6, 7) Matendo ya bengine ililetea Daudi maumivu mingi sana mupaka machozi yake ilikuwa tu inamwangika.

12. Kulingana na Zaburi 56:8, Daudi alikuwa hakika na jambo gani?

12 Hata kama Daudi alipata magumu mingi, alikuwa hakika kama Yehova alimupenda. Aliandika hivi: “Yehova atasikia sauti ya kilio changu.” (Zb. 6:8) Wakati ingine Daudi aliandika maneno ya kugusa moyo yenye kuwa mu Zaburi 56:8. (Soma.) Ile maneno inaonyesha wazi namna Yehova anatupenda na kutuhangaikia sana. Daudi alisikia sawa vile Yehova iko anakusanya machozi yake mu chupa ao kuiandika mu kitabu. Daudi alikuwa hakika kama Yehova aliona na alikumbuka maumivu yake. Alikuwa hakika kama Baba yake wa mbinguni mwenye upendo alijua magumu yenye alipita ndani, lakini pia alijua maumivu yenye ile magumu ilimuletea.

13. Wakati wengine wanatuvunja moyo, tunapaswa kukumbuka nini? (Ona pia picha.)

13 Mambo yenye tunajifunza. Uko najisikia mubaya juu mutu fulani alikuvunja moyo ao mutu fulani mwenye ulikuwa natumainia alikusaliti? Pengine roho iko nakuluma juu ulikuwa nachumbiana na mutu fulani lakini urafiki wenu uliisha bila kutazamia, ao pengine ndoa yako ilivunjika kwa kushitukia; ao tena pengine mutu mwenye unapenda ameacha kumutumikia Yehova. Ndugu mwenye bibi yake alifanya uzinifu na ule bibi akamuacha, anasema hivi: “Sikuitika kama ile mambo iko nanifikia, niliishiwa kabisa! Nilijiona wa bure, nilihuzunika, na nilikasirika.” Kama kuko mutu mwenye amekusaliti na kukuvunja moyo, ujue kama Yehova hawezi kukuacha hata kidogo. Ule ndugu alisema hivi: “Nimeelewa kama batu banaweza kutuacha lakini Yehova yeye ni mwamba wetu. Hata kutokee nini, iko tu pale. Hataacha watumishi wake waaminifu.” (Zb. 37:28) Ujue pia kama Yehova anatupenda kupita mwanadamu yeyote. Haiko juu mutu fulani alitusaliti njo Yehova ataacha kutuhangaikia. (Ro. 8:38, 39) Jambo ya kukumbuka ni hii: Hata mutu akutendee namna gani, Baba yako wa mbinguni yeye anakupenda tu.

Kitabu ya Zaburi inatuhakikishia kama Yehova iko karibu na wenye kuvunjika moyo (Ona fungu ya 13)


14. Zaburi 34:18 inatusaidia tukuwe hakika na nini?

14 Wakati banatusaliti, tunaweza kufarijiwa na maneno yenye kutia moyo yenye Daudi alisema mu Zaburi 34:18. (Soma.) Kitabu fulani inasema kama benye “kupondwa roho” banaweza kuwa “benye habatumainie kama kuko jambo yoyote ya muzuri yenye itabafikia.” Yehova anasaidia namna gani bale benye banajisikia vile kwa sababu bamevunjwa moyo? Sawa vile muzazi mwenye upendo anabebaka mutoto wake na kumufariji wakati mutoto iko nalia, Yehova “iko karibu na” siye wakati mutu fulani anatusaliti ao anatuacha. Yehova anasikia maumivu yenye tuko nasikia na anatusaidia bila kukawia. Iko tayari kutufariji wakati tuko na maumivu mu moyo na wakati tunajiona kuwa wa bure. Na anatuahidi mambo mingi ya muzuri yenye inatusaidia tuvumilie magumu yetu ya leo.—Isa. 65:17.

MACHOZI YA KUKOSA TUMAINI

15. Nini njo ilimulilisha Hezekia?

15 Wakati alikuwa na miaka 39, Mufalme Hezekia wa Yuda alifikia kujua kama iko na magonjwa yenye haitapona. Nabii Isaya alimuambia Mufalme Hezekia ujumbe wa Yehova wenye ulionyesha kama atakufa juu ya ile magonjwa. (2 Fa. 20:1) Ilionekana sawa vile hakuna tena tumaini. Wakati Hezekia alisikia ile habari, alihuzunika na alilia sana. Alimulilia Yehova sana katika sala juu amusaidie.—2 Fa. 20:2, 3.

16. Yehova alimufanyia nini Hezekia?

16 Wakati Yehova alisikia sala ya Hezekia, na wakati aliona machozi yake, Yehova alimusikilia huruma na alimuambia hivi: “Nimesikia sala yako. Nimeona machozi yako. Angalia, ninakuponyesha.” Kupitia Isaya, Yehova alimuahidi Hezekia kama atarefusha maisha yake na ataokoa Yerusalemu kutoka mu mikono ya Waashuru.—2 Fa. 20:4-6.

17. Yehova anatutegemeza namna gani wakati tuko na magonjwa ya nguvu? (Zaburi 41:3) (Ona pia picha.)

17 Mambo yenye tunajifunza. Uko na magonjwa yenye inaonekana kama haitapona? Sali kwa Yehova. Atakusikiliza hata kama uko nalia wakati uko nasali. Biblia inatuhakikishia kama “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote” atatufariji mu magumu yetu yote. (2 Ko. 1:3, 4) Hatuwezi kutazamia kama Yehova atatosha magumu yetu yote kwa sasa, lakini tunaweza kuwa hakika kama atatutegemeza. (Soma Zaburi 41:3.) Kupitia roho yake takatifu, Yehova anatupatia nguvu, hekima, na amani ya moyo ili tuweze kuvumilia. (Mez. 18:14; Flp. 4:13) Pia anatutegemeza kupitia tumaini yenye kuwa mu Biblia yenye inaonyesha kama magonjwa yote itaisha.—Isa. 33:24.

Yehova atajibia sala zetu kwa kutupatia nguvu, hekima, na amani ya moyo (Ona fungu ya 17)


18. Ni andiko gani inakufariji wakati uko mu hali ya nguvu? (Ona kisanduku “ Maneno ya Kutuliza Yenye Inaweza Kutupanguza Machozi.”)

18 Maneno ya Yehova ilimufariji Hezekia. Neno ya Mungu inaweza kutufariji na siye. Mu Biblia muko maneno yenye Yehova aliandikisha, yenye inaweza kutufariji wakati tuko napambana na hali za nguvu. (Ro. 15:4) Wakati dada moya wa mu Afrika ya Mangaribi alipata habari kama iko na ugonjwa wa cancer, alilia mara mingi. Anasema hivi: “Andiko moya yenye ilinifariji sana ni Isaya 26:3. Hata kama hatuwezi kuamua ni magumu gani itatupata, ile andiko ilinihakikishia kama Yehova anaweza kutupatia amani ya moyo yenye itatusaidia kuamua namna tutatenda wakati tunapata magumu.” Kuko andiko yenye inakutulizaka wakati uko mu hali ya nguvu, pengine mu hali yenye unaona kama hakuna jambo ya kufanya?

19. Tunangoya baraka gani?

19 Tuko ku mwisho-mwisho wa siku za mwisho, kwa hiyo tunaweza kutazamia kama mambo ya kuleta machozi itaongezeka. Lakini sawa vile tumejifunza kupitia mufano wa Hana, Daudi, na Mufalme Hezekia, Yehova anaona machozi yetu na ile inamufanya ahuzunike. Anatupenda na hasahau machozi yetu. Kwa hiyo, wakati tuko mu hali za nguvu, tukuwe tayari kumufungulia Yehova moyo wetu mu sala. Tusijitenge hata siku moya na ndugu na dada zetu wenye wanatupenda. Na maneno yenye kutuliza yenye kuwa mu Biblia iendelee kutufariji. Tunaweza kuwa hakika kama tukiendelea kuvumilia kwa uaminifu, Yehova atatubariki. Atatupanguza machozi yetu yote yenye tunalia kwa sababu ya huzuni, kusalitiwa, na kukosa tumaini. Ile ni kati ya baraka zenye ametuahidi. (Ufu. 21:4) Ku mwisho, machozi yetu yote itakuwa tu ya furaha.

WIMBO 4 “Yehova Ni Muchungaji Wangu”