Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

“Malaika wenye walichaguliwa” wenye kuzungumuziwa mu 1 Timoteo 5:21 ni nani?

Mutume Paulo aliandikia hivi Timoteo muzee mwenzake: “Ninakuagiza kwa uzito mbele ya Mungu na Kristo Yesu na malaika wenye walichaguliwa, kwamba ushike maagizo haya bila upendeleo wala ubaguzi wowote.”—1 Ti. 5:21.

Kwanza, tuzungumuzie wale wenye haiwezekane wakuwe wale malaika wenye walichaguliwa. Ni wazi kama, hawako kati ya wale 144000. Wakati Paulo alimuandikia Timoteo, Wakristo watiwa-mafuta walikuwa hawayaanza kufufuliwa juu waende mbinguni. Mitume na Wakristo wengine watiwa-mafuta walikuwa hawayakuwa viumbe wa roho, kwa hiyo haiwezekane wakuwe “malaika wenye walichaguliwa.”—1 Ko. 15:50-54; 1 Te. 4:13-17; 1 Yo. 3:2.

Pia, “malaika wenye walichaguliwa” hawawezi kuwa malaika wenye hawakumutii Mungu wakati wa Garika. Wale malaika walijiunga na Shetani na wakakuwa pepo wachafu, na walikuwa maadui wa Yesu. (Mwa. 6:2; Lu. 8:30, 31; 2 Pe. 2:4) Wakati wenye kuya, watafungwa katika abiso kwa miaka 1000 na kisha wataharibiwa milele pamoya na Shetani.—Yud. 6; Ufu. 20:1-3, 10.

“Malaika wenye walichaguliwa” wenye Paulo alizungumuzia wanapaswa kuwa malaika waaminifu wenye kuwa mbinguni wenye wanategemeza “Mungu na Kristo Yesu.”

Kuko maelfu ya maelfu ya malaika waaminifu. (Ebr. 12:22, 23) Hatupaswe kuwaza kama wote wanakuwaka na mugao uleule wakati moya. (Ufu. 14:17, 18) Kumbuka kama wakati fulani malaika moya alipewa mugao wa kuharibu maaskari wa Ashuru 185000. (2 Fa. 19:35) Inawezekana malaika wengi wamepewa mugao wa ‘kukusanya kutoka katika Ufalme [wa Yesu] vitu vyote vyenye vinafanya watu wakwazike na pia watu wenye matendo ya kuvunja sheria.’ (Mt. 13:39-41) Inawezekana wengine wako na mugao wa ‘kukusanya watu wake wenye kuchaguliwa’ juu waende mbinguni. (Mt. 24:31) Na wengine wanapewa mugao wa ‘kutulinda katika njia zetu zote.’—Zb. 91:11; Mt. 18:10; linganisha na Matayo 4:11; Lu. 22:43.

Inawezekana “malaika wenye walichaguliwa” wenye kuzungumuziwa mu 1 Timoteo 5:21 walipewa mugao wa pekee wa kuhangaikia mambo yenye kuhusu kutaniko. Kama tunasoma ile habari yote, tunaona kama Paulo alitoa mashauri ya hekima kuhusu wazee, wenye kutaniko inapaswa kuonyesha heshima. Wazee pia, wanapaswa kutimiza migao yao “bila upendeleo wala ubaguzi wowote” na hawapaswe kukamata maamuzi ao kuhukumu bila kufikiri sana. Jambo ya maana sana yenye inapaswa kuwachochea wafuate mashauri ya Paulo yeye iliongozwa na roho ya Mungu, ni juu wanatumika “mbele ya Mungu na Kristo Yesu.” Ni wazi kama malaika fulani wamepewa mugao wa kushugulikia mambo yenye kuhusu kutaniko, sawa vile kulinda kutaniko, kusimamia kazi ya kuhubiri, na kutoa ripoti kwa Yehova.—Mt. 18:10; Ufu. 14:6.