Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 8

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

Endelea Kufuata Muongozo wa Yehova

Endelea Kufuata Muongozo wa Yehova

“Mimi, Yehova [njo] . . . mwenye anakuongoza.”ISA. 48:17.

WAZO KUBWA

Mu hii habari tutaona namna Yehova anaongoza watu wake leo na baraka yenye tunapata wakati tunafuata muongozo wake.

1. Juu ya nini tunapaswa kufuata muongozo wa Yehova? Toa mufano.

 WAZIA unapotea mu pori. Hatari iko fasi yote: Wanyama wa pori, vidudu vyenye kuambukiza magonjwa, mimea yenye sumu, na fasi za majiwe-majiwe. Utakuwa mwenye shukrani sana kama uko na mutu wa kukuongoza mwenye anajua fasi kwenye kuko hatari na namna ya kukuepusha nayo! Dunia iko sawa vile ile pori. Inajaa hatari zenye zinaweza kuharibu hali yetu ya kiroho. Lakini tuko na Kiongozi mukamilifu, Yehova. Anatuongoza ili tuepuke hatari na ili tufike kwenye tuko naenda, ni kusema mu dunia mupya, kwenye tutapata uzima wa milele.

2. Yehova anatuongoza namna gani?

2 Namna gani Yehova anatuongoza? Kwanza, anatumia Neno yake Biblia. Lakini, wakati fulani anatumia pia wanadamu wenye kumuwakilisha. Kwa mufano, anatumia “mutumwa muaminifu na mwenye busara” ili atutolee chakula ya kiroho yenye itatusaidia kukamata maamuzi ya hekima. (Mt. 24:45) Yehova anatumia pia wanaume wenye uzoefu ili kutuongoza. Kwa mufano, anatumia waangalizi wa muzunguko na wazee wa kutaniko ili watutie moyo na kututolea mafundisho yenye itatusaidia wakati wa magumu. Tuko wenye shukrani sana juu tuko na muongozo wenye kutumainika mu hizi siku za mwisho zenye kuwa nguvu sana! Ule muongozo unatusaidia tuendelee kukubaliwa na Yehova na tuendelee kutembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Lakini, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kufuata muongozo wa Yehova, zaidi sana wakati unatolewa na wanaume wenye hawakamilike. Juu ya nini? Pengine hatufurahie muongozo wenye wanatupatia. Ao tunaweza kuona kama muongozo wenye tunapewa hauko wa muzuri na kuwaza kama hautoke kwa Yehova. Mu hali za vile, tunapaswa kuwa hakika kabisa kama Yehova njo iko naongoza watu wake, na kama kufuata muongozo wake kunaleta baraka. Juu tukuwe kabisa hakika na ile jambo, mu hii habari tutazungumuzia (1) namna Yehova aliongoza watu wake zamani, (2) namna iko natuongoza leo, na (3) faida yenye tunapata wakati tunaendelea kufuata muongozo wake.

Kuanzia zamani mupaka leo, Yehova ametumia wanadamu ili kuongoza watu wake (Ona fungu ya 3)


NAMNA YEHOVA ALIONGOZA TAIFA YA ISRAELI

4-5. Namna gani Yehova alionyesha kama alikuwa natumia Musa ili kuongoza Waisraeli? (Ona picha ku jalada.)

4 Yehova alimuweka Musa ili aongoze Waisraeli mu safari yao ya kutoka Misri. Na alipatia Waisraeli ushuhuda wenye kuonyesha kama ni yeye alikuwa nawaongoza kupitia Musa. Kwa mufano, aliweka nguzo ya wingu muchana na nguzo ya moto usiku. (Kut. 13:21) Musa alifuata ile nguzo yenye ilimuongoza yeye na Waisraeli mupaka ku Bahari Nyekundu. Watu waliogopa sana wakati waliwaza kama hawana kwa kukimbilia juu walikuwa kati ya bahari na jeshi ya Wamisri yenye ilikuwa nawafuata. Walisema kama Musa alikosea kwa kuwaleta kwenye Bahari Nyekundu, lakini Musa hakukosea. Ni Yehova mwenyewe njo aliongoza watu wake pale, kupitia Musa. (Kut. 14:2) Kisha Mungu aliwaokoa mu njia ya ajabu sana.—Kut. 14:26-28.

Musa alitegemea nguzo ya wingu ili kuongoza watu wa Mungu mu jangwa (Ona fungu ya 4-5)


5 Kwa miaka 40 kisha pale, Musa aliendelea kutegemea nguzo ya wingu ili kuongoza watu wa Mungu mu jangwa. a Kwa kipindi fulani, Yehova alitia ile wingu juu ya hema ya Musa, kwenye Waisraeli wote wangeweza kuiona. (Kut. 33:7, 9-10) Yehova alizungumuza na Musa kupitia ile wingu, na kisha Musa aliambia watu maagizo ya Yehova. (Zb. 99:7) Waisraeli walikuwa na ushuhuda wenye kuwa wazi, wenye ulionyesha kama Yehova alikuwa anatumia Musa ili kuwaongoza.

Musa na Yoshua mwenye alikamata nafasi yake (Ona fungu ya 5, 7)


6. Waisraeli walitenda namna gani kuhusu muongozo wa Yehova? (Hesabu 14:2, 10, 11)

6 Jambo ya kuhuzunisha ni kama, Waisraeli wengi walikatala ule ushuhuda wenye kuwa wazi, wenye ulionyesha kama Yehova alikuwa natumia Musa ili kumuwakilisha. (Soma Hesabu 14:2, 10, 11.) Mara kwa mara, hawakukubali daraka yenye Musa alikuwa nayo. Matokeo ilikuwa nini? Yehova hakuruhusu ile kizazi ya Waisraeli iingie mu Inchi ya Ahadi.—Hes. 14:30.

7. Zungumuzia watu fulani wenye walifuata muongozo wa Yehova. (Hesabu 14:24) (Ona pia picha.)

7 Lakini, Waisraeli fulani walifuata muongozo wa Yehova. Kwa mufano, Yehova alisema hivi: “Kalebu . . . aliendelea kunifuata kwa moyo wote.” (Soma Hesabu 14:24.) Yehova alimubariki Kalebu, na hata alimuacha achague eneo yenye alipenda mu Kanaani. (Yos. 14:12-14) Kizazi yenye ilifuata ya Waisraeli iliweka pia mufano muzuri kuhusu kufuata muongozo wa Yehova. Wakati Yoshua alikamata nafasi ya Musa ya kuongoza, Waisraeli ‘walimuheshimia sana sikuzote za maisha yake.’ (Yos. 4:14) Matokeo ilikuwa nini? Yehova aliwabariki kwa kuwaingiza mu Inchi ya Ahadi.—Yos. 21:43, 44.

8. Fasiria namna Yehova aliongoza watu wake wakati wa wafalme. (Ona pia picha.)

8 Miaka fulani kisha pale, Yehova aliweka waamuzi ili waongoze watu wake. Kisha, Yehova aliweka manabii ili waongoze watu wake wakati wa wafalme. Wafalme waaminifu walisikiliza mashauri ya manabii. Kwa mufano, Mufalme Daudi alikubali kwa unyenyekevu wakati nabii Natani alimurekebisha. (2 Sa. 12:7, 13; 1 Ny. 17:3, 4) Mufalme Yehoshafati alifuata muongozo wa nabii Yahazieli na alitia moyo watu wa Yuda ‘wakuwe na imani katika manabii [wa Mungu].’ (2 Ny. 20:14, 15, 20) Wakati Mufalme Hezekia alikuwa mu hali ya nguvu, alitafuta muongozo wa nabii Isaya. (Isa. 37:1-6) Kila wakati wenye wafalme walitafuta muongozo wa Yehova, walibarikiwa na Yehova alilinda taifa. (2 Ny. 20:29, 30; 32:22) Watu wote walipaswa kuona waziwazi kama Yehova alikuwa natumia manabii ili kuongoza watu wake. Lakini, wafalme wengi na pia watu walikatala kusikiliza manabii wa Yehova.—Yer. 35:12-15.

Mufalme Hezekia na nabii Isaya (Ona fungu ya 8)


NAMNA YEHOVA ALIONGOZA WAKRISTO WA KWANZA-KWANZA

9. Yehova alitumia nani ili kuongoza Wakristo mu karne ya kwanza? (Ona pia picha.)

9 Yehova alianzisha kutaniko ya Kikristo mu karne ya kwanza. Namna gani aliongoza wale Wakristo wa kwanza-kwanza? Alimuweka Yesu kuwa kichwa cha kutaniko. (Efe. 5:23) Lakini Yesu hakuongoza yeye mwenyewe moja kwa moja kila mwanafunzi wake. Alitumia mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu ili wawaongoze. (Mdo. 15:1, 2) Pia, wazee waliwekwa ili kuongoza makutaniko.—1 Te. 5:12; Tit. 1:5.

Mitume na wazee katika Yerusalemu (Ona fungu ya 9)


10. (a) Wakristo wengi wa kwanza-kwanza walitenda namna gani wakati walipewa muongozo? (Matendo 15:30, 31) (b) Juu ya nini watu fulani wa zamani hawakukubali wale wenye walimuwakilisha Yehova? (Ona kisanduku “ Juu ya Nini Watu Fulani Wanakatala Ushuhuda Wenye Kuwa Wazi?”)

10 Wakristo wa mu karne ya kwanza walitenda namna gani? Wengi wao walifurahia kufuata muongozo wenye walipewa. Kwa kweli, ‘walifurahi sana juu ya kitia-moyo’ yenye walipewa. (Soma Matendo 15:30, 31.) Sasa, namna gani Yehova iko naongoza watu wake leo?

NAMNA YEHOVA IKO NATUONGOZA LEO

11. Toa mufano wenye unaonyesha kama Yehova anaongoza wale wenye kusimamia kazi leo.

11 Yehova anaendelea kuongoza watu wake leo. Anafanya vile kupitia Neno yake na kupitia Mwana wake, kichwa cha kutaniko. Tuko na ushuhuda wenye kuonyesha kama Yehova anaendelea kutumia wanadamu ili kumuwakilisha? Ndiyo. Kwa mufano, fikiria mambo fulani yenye ilitokea ku mwisho-mwisho wa miaka ya 1800. Charles Taze Russell na wenzake walielewa kama mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka wa maana sana kwa ajili ya Ufalme wa Mungu. (Da. 4:25, 26) Kuchunguza maunabii ya Biblia, njo kuliwasaidia waelewe vile. Yehova alikuwa naongoza utafiti wenye walikuwa nafanya mu Biblia? Ndiyo kabisa. Mambo yenye ilitokea mu mwaka 1914 ilionyesha wazi kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala ile mwaka. Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilitokea, kisha magonjwa ya kuambukiza, matetemeko ya inchi, na upungufu wa chakula. (Lu. 21:10, 11) Kwa kweli, Yehova alikuwa natumia wale wanaume Wakristo waaminifu ili kusaidia watu wake.

12-13. Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu ni mipango gani ilikamatwa ili kazi ya kuhubiri na kufundisha ifanywe sana?

12 Pia, fikiria mambo yenye ilitokea wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Kisha kuchunguza Ufunuo 17:8, ndugu wenye walikuwa wanaongoza ku makao makubwa walielewa kama ile vita haingeongoza ku Armagedoni. Kungekuwa kipindi ya amani yenye ingetutolea nafasi ya kuhubiri sana. Njo maana ndugu walianzisha Masomo ya Gileadi, hata kama ile wakati ile ilionekana kuwa haipatane na akili. Walianzisha ile masomo ili kuzoeza wamisionere kuhubiri na kufundisha mu inchi mbalimbali mu dunia yote. Wamisionere walitumwa hata wakati wa vita. Zaidi ya ile, mutumwa-muaminifu alianzisha Mazoezi Katika Huduma ya Kiteokrasi b ili kuzoeza wote mu kutaniko wakuwe wahubiri na walimu wazuri zaidi. Watu wa Mungu walitayarishwa mu njia mbalimbali kwa ajili ya kazi kubwa yenye ilikuwa mbele yao.

13 Wakati tunafikiria ile mambo, tunaona waziwazi kama Yehova alikuwa naongoza watu wake mu ile wakati ya nguvu. Tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu, watu wa Yehova mu inchi za mingi, wanafurahia amani na uhuru kwa kiasi fulani, na ile inawasaidia waendelee kufanya kazi ya kuhubiri. Kwa kweli, kazi ya kuhubiri imekuwa na matokeo ya muzuri kabisa.

14. Juu ya nini tunaweza kutumainia muongozo wenye tengenezo ya Yehova inatupatia na wenye wazee wanatupatia? (Ufunuo 2:1) (Ona pia picha.)

14 Leo ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanaendelea kufuata muongozo wa Kristo. Wanapenda muongozo wenye wanatolea ndugu na dada upatane na mawazo ya Yehova. Na wanatumia waangalizi wa muzunguko na wazee ili kutolea makutaniko ule muongozo. c Wazee watiwa-mafuta wako katika “mukono [wa Kristo ] wa kuume.” (Soma Ufunuo 2:1.) Kwa kweli, wale wazee ni watu wenye hawakamilike na wanafanyaka makosa. Musa na Yoshua na hata mitume, walifanya pia makosa wakati fulani. (Hes. 20:12; Yos. 9:14, 15; Ro. 3:23) Lakini, Yesu anaendelea kuongoza mutumwa muaminifu na mwenye busara, na wazee wenye wamewekwa, na ataendelea kufanya vile “sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 28:20) Kwa hiyo, tuko na sababu za muzuri sana za kutegemea muongozo wenye anatupatia kupitia wale wenye ameweka ili watuongoze.

Baraza Yenye Kuongoza ya leo (Ona fungu ya 14)


TUNAPATA FAIDA WAKATI TUNAFUATA MUONGOZO WA YEHOVA

15-16. Mufano wa wale wenye walifuata muongozo wa Yehova unakufundisha nini?

15 Wakati tunaendelea kufuata muongozo wa Yehova tunapata baraka mingi hata leo. Kwa mufano, Andy na Robyn walifuata mashauri ya mutumwa ya kufanya maisha kuwa mwepesi. (Mt. 6:22) Matokeo ni kwamba, waliweza kujitolea ili kutumika mu kazi fulani ya ujenzi. Robyn anasema hivi: “Tunaishi mu nyumba za kidogo sana na mara mingi hatukuwake hata na mafiga. Na nilipaswa kuuzisha vitu vya mingi vyenye nilitumia ili kupiga picha, jambo yenye ninapendaka sana. Ile ilifanya machozi initoke. Lakini kama Sara, bibi ya Abrahamu, niliazimia kuangalia mbele hapana nyuma.” (Ebr. 11:15) Ule bibi na bwana wamepata faida gani? Robyn anasema hivi: “Tunajisikia kuwa wenye kutosheka sana juu tunajua kama tuko namupatia Yehova kila kitu yenye tuko nayo. Kutumika mu kazi mbalimbali za ujenzi zenye kufanywa na tengenezo, kunatusaidia tuwazie kwa kiasi fulani namna maisha itakuwa mu dunia mupya.” Andy anakubaliana naye, anasema hivi: “Tunatosheka kwa sababu tunatumia nguvu yetu yote ili kuunga mukono kazi ya Ufalme.”

16 Tunapata faida gani ingine wakati tunafuata muongozo fulani wa Yehova? Kisha kumaliza masomo ya segondere, Marcia alipenda kabisa kufuata shauri ya kufanya utumishi wa wakati wote. (Mt. 6:33; Ro. 12:11) Anasema hivi: “Nilipewa nafasi ya kusoma masomo ya juu kwa miaka ine bila kulipa. Lakini nilipenda kufuatia miradi ya kiroho. Kwa hiyo, niliamua kufuata mazoezi yenye ingenisaidia kujua kazi fulani, yenye ingenitegemeza mu utumishi wangu. Ile ni moya kati ya maamuzi ya muzuri yenye nimekamata. Sasa niko nafurahia kazi ya upainia, na juu kazi yangu hainikamate wakati yote, nimeweza kujitolea ili kusaidia ku Beteli siku fulani, na nimepata mapendeleo ingine ya pekee.”

17. Tunapata baraka gani zingine wakati tunaendelea kufuata muongozo wa Yehova? (Isaya 48:17, 18)

17 Wakati fulani, tunapewa mashauri yenye inatulinda ili tusiangukie mu mutego wa kupenda vitu vya kimwili na tuepuke mambo yenye inaweza kufanya tuvunje sheria za Mungu. Wakati tunafuata ile miongozo yenye Yehova anatutolea, tunapata baraka mingi. Tunaendelea kuwa na zamiri safi, na tunaepuka mahangaiko ya mingi. (1 Ti. 6:9, 10) Matokeo inakuwa nini? Tunaendelea kumuabudu Yehova kwa moyo wote. Ile inafanya tukuwe na furaha na amani ya moyo na tutosheke kabisa.—Soma Isaya 48:17, 18.

18. Juu ya nini unaazimia kuendelea kufuata muongozo wa Yehova?

18 Bila shaka Yehova ataendelea kutumia wanadamu wenye wanamuwakilisha ili kututolea muongozo wakati wa taabu kubwa na hata mu Utawala wa Miaka Elfu. (Zb. 45:16) Je! Tutaendelea kufuata muongozo wake hata wakati inaomba tufanye jambo fulani yenye hatufurahie? Itakuwa mwepesi kufanya vile ikiwa tuko najikaza kufuata muongozo wenye Yehova anatutolea leo. Kwa hiyo, tuendelee kufuata muongozo wenye Yehova anatutolea, hata muongozo wenye anatutolea kupitia wanaume wenye ameweka ili kutuongoza. (Isa. 32:1, 2; Ebr. 13:17) Na wakati tuko nafanya vile, tutumainie kabisa Kiongozi wetu Yehova mwenye iko natuongoza ili tuepuke hatari zenye zinaweza kuharibu hali yetu ya kiroho. Pia Yehova iko natuongoza ili tufike kwenye tuko naenda, ni kusema mu dunia mupya kwenye tutapata uzima wa milele.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Namna gani Yehova aliongoza taifa ya Israeli?

  • Namna gani Yehova aliongoza Wakristo wa kwanza-kwanza?

  • Tunapata faida gani wakati tunafuata muongozo wa Yehova leo?

WIMBO 48 Tutembee na Yehova Kila Siku

a Yehova aliweka pia malaika “mwenye alikuwa anaenda mbele ya kambi” ili kuongoza taifa ya Israeli mu Inchi ya Ahadi. Inawezekana ule malaika alikuwa Mikaeli, ni kusema Yesu mbele akuye ku dunia.—Kut. 14:19; 32:34.

b Ilifikia kuitwa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Leo ile mazoezi ni sehemu ya mukutano wetu wa katikati ya juma.

c Ona kisanduku “Daraka la Baraza Lenye Kuongoza” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2021 uku. 18.