Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 1

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

Piganisha Woga kwa Kumutegemea Yehova

Piganisha Woga kwa Kumutegemea Yehova

ANDIKO YA MWAKA WA 2024: “Wakati ninaogopa, ninakutegemea wewe.”ZB. 56:3.

WAZO KUBWA

Ona namna tunaweza kumutumainia zaidi Yehova na kupiganisha woga.

1. Juu ya nini tunaweza kuogopa wakati fulani?

 KILA mutu anaogopaka wakati fulani. Kusema kweli, kujifunza Biblia kumetusaidia tusiogope wafu, tusiogope mambo ya uchawi, na tusiogope mambo yenye inaweza kutokea wakati wenye kuya. Lakini tungali tunaishi mu wakati wenye kuwa na “mambo yenye kuogopesha,” sawa vile vita, jeuri, na magonjwa. (Lu. 21:11) Tunaweza pia kuogopa wanadamu, sawa vile wakubwa wa serikali wenye kututesa ao watu wa familia yetu wenye wanapinga ibada safi. Watu fulani wanaweza kuogopa kama hawataweza kuvumilia magumu yenye wako nayo leo ao yenye wanaweza kupata wakati wenye kuya.

2. Daudi alijikuta mu hali gani wakati alikuwa Gati? Fasiria.

2 Daudi naye aliogopa wakati fulani. Kwa mufano, wakati Mufalme Sauli alikuwa namutafuta ili kumuua, Daudi aliamua kukimbilia mu muji wa Wafilisti wenye kuitwa Gati. Bila kukawia, Mufalme Akishi wa Gati alipata habari kama Daudi alikuwa ule mupiganaji-vita mwenye nguvu mwenye watu walikuwa nasifu kwa kuimba kama aliua “makumi . . . ya maelfu” ya Wafilisti. Daudi ‘aliogopa sana.’ (1 Sa. 21:10-12) Alikuwa na wasiwasi juu ya mambo yenye Akishi angemutendea. Namna gani alipiganisha woga wake?

3. Kulingana na Zaburi 56:1-3, 11, namna gani Daudi alipiganisha woga wake?

3 Mu Zaburi ya 56, Daudi anaonyesha namna alijisikia wakati alikuwa mu muji wa Gati. Ile zaburi inaonyesha namna Daudi alikuwa na woga. Lakini pia inaonyesha namna alipiganisha woga wake. Wakati Daudi aliogopa alimutegemea Yehova. (Soma Zaburi 56:1-3, 11.) Alikuwa na sababu za muzuri za kufanya vile. Kwa musaada wa Yehova alipata wazo yenye haiko ya kawaida, lakini ilikuwa na matokeo ya muzuri. Alijifanya kuwa mwenda-wazimu. Ile ilifanya Akishi amufukuze kuliko kumuua. Kwa hiyo, Daudi aliweza kuponyoka.—1 Sa. 21:13–22:1.

4. Tunaweza kufanya nini ili tumutegemee Yehova zaidi? Leta mufano.

4 Siye pia tunaweza kupiganisha woga wetu kwa kumutegemea Yehova. Lakini namna gani tunaweza kumutegemea zaidi Yehova, zaidi sana wakati tunaogopa? Fikiria hii mufano: Ikiwa wanakuambia kama uko na ugonjwa fulani, ku mwanzo unaweza kuogopa. Lakini, unaweza kutulia kama unatumainia munganga wako. Pengine ameweza kuponyesha watu wengi wenye walikuwa na ule ugonjwa. Anaweza kukusikiliza kwa uangalifu na kukuhakikishia kama anaelewa namna uko najisikia. Anaweza kupendekeza matunzo fulani yenye iliweza kusaidia watu wengine. Vilevile, tunaweza kumutegemea zaidi Yehova kama tunafikiria mambo yenye alishafanya, mambo yenye iko nafanya leo, na mambo yenye atatufanyia wakati wenye kuya. Ni vile Daudi alifanya. Wakati tutakuwa nachunguza maneno fulani yenye kuongozwa na roho ya Mungu yenye Daudi aliandika mu Zaburi ya 56, fikiria namna weye pia unaweza kumutegemea zaidi Yehova na kupiganisha woga wako.

YEHOVA ALISHAFANYA NINI?

5. Ili kupiganisha woga wake, Daudi alitafakari juu ya mambo gani? (Zaburi 56:12, 13)

5 Wakati uzima wa Daudi ulikuwa mu hatari alikazia mambo yenye Yehova alikuwa alishafanya. (Soma Zaburi 56:12, 13.) Ni vile Daudi alizoea kufanya mu maisha yake yote. Kwa mufano, wakati fulani alitafakari juu ya uumbaji wa Yehova, wenye ulimukumbusha kama Yehova iko na nguvu ya mingi sana na anahangaikia sana wanadamu. (Zb. 65:6-9) Alitafakari pia juu ya mambo yenye Yehova alikuwa amefanyia wengine. (Zb. 31:19; 37:25, 26) Na alitafakari zaidi sana juu ya mambo yenye Yehova alikuwa amemufanyia kipekee. Tangu wakati Daudi alikuwa mutoto, Yehova alimutegemeza na kumulinda. (Zb. 22:9, 10) Wazia namna kutafakari juu ya ile mambo kulimufanya Daudi amutegemee Yehova hata zaidi!

Daudi alimutumainia zaidi Yehova kwa kukazia akili mambo yenye alikuwa alishafanya, mambo yenye alikuwa nafanya, na mambo yenye angefanya (Ona fungu ya 5, 8, 12) d


6. Wakati tunaogopa nini njo itatusaidia tumutegemee Yehova?

6 Wakati unaogopa, ujiulize hivi: ‘Yehova alishafanya nini?’ Fikiria vitu vyenye aliumba. Kwa mufano, wakati ‘tunaangalia kwa uangalifu’ namna Yehova anahangaikia ndege na maua, vitu vyenye havikuumbwa kwa mufano wake na vyenye haviwezi kumuabudu, ile inafanya tukuwe hakika zaidi kama atatuhangaikia pia. (Mt. 6:25-32) Fikiria pia mambo yenye Yehova amefanyia watumishi wake. Unaweza kujifunza juu ya mutu fulani mwenye kuzungumuziwa mu Biblia mwenye alionyesha imani ya ajabu, ao unaweza kusoma habari kuhusu mutumishi fulani wa Yehova wa wakati wetu. a Zaidi ya ile, tafakari juu ya namna Yehova amekuhangaikia. Alikusaidia kupata kweli namna gani? (Yoh. 6:44) Amejibia namna gani sala zako? (1 Yo. 5:14) Namna gani zabihu ya Mwana wake mupendwa iko nakuletea faida kila siku?—Efe. 1:7; Ebr. 4:14-16.

Tunamutumainia zaidi Yehova wakati tunakazia akili mambo yenye alishafanya, mambo yenye iko nafanya, na mambo yenye atafanya (Ona fungu ya 6, 9-10, 13-14) e


7. Namna gani mufano wa Danieli ulimusaidia Vanessa kupiganisha woga wake?

7 Vanessa, b dada wa Haiti, alipambana na hali yenye kuogopesha. Mwanaume fulani wa mu eneo yao alimutumia ujumbe kila siku na kumukaza ili aanzishe uhusiano pamoja naye. Vanessa alikatala kabisa. Lakini ule mwanaume akakuwa makali zaidi na hata akamuogopesha kama atamutendea mubaya. Vanessa anasema hivi: “Niliogopa.” Namna gani Vanessa aliweza kupiganisha woga wake? Alikamata hatua za kujilinda. Muzee fulani alimusaidia juu ajulishe wakubwa wa serikali wa mu eneo yao ile tatizo. Lakini alikazia pia namna Yehova alilinda watumishi wake zamani. Vanessa anasema hivi: “Mutu wa kwanza mwenye nilifikiria alikuwa nabii Danieli. Alitupwa mu shimo ya simba wenye njaa hata kama hakukuwa na kosa. Lakini Yehova alimuhangaikia. Nilimuomba Yehova ashugulikie ile hali. Na kisha kufanya vile, sikuogopa tena.”—Da. 6:12-22.

YEHOVA IKO NAFANYA NINI LEO?

8. Daudi alikuwa hakika juu ya jambo gani? (Zaburi 56:8)

8 Hata kama uzima wa Daudi ulikuwa mu hatari wakati alikuwa mu muji wa Gati, hakuacha woga umumalize nguvu. Lakini aliamua kufikiria mambo yenye Yehova alikuwa namufanyia ile wakati. Daudi alitambua kama Yehova alikuwa namuongoza na kumulinda na kama alielewa namna alikuwa najisikia. (Soma Zaburi 56:8.) Daudi alikuwa pia na marafiki washikamanifu wenye walimutegemeza sawa vile Yonatani, na alipata musaada kutoka kwa Kuhani Mukubwa Ahimeleki. (1 Sa. 20:41, 42; 21:6, 8, 9) Na hata wakati Mufalme Sauli alipenda kumuua, Daudi aliponyoka. Alikuwa hakika kama Yehova alijua muzuri jaribu yenye alikuwa napambana nayo na namna ile jaribu ilifanya ajisikie.

9. Yehova anajua nini kuhusu kila mumoja wetu?

9 Wakati unapambana na jaribu yenye inakufanya uogope, kumbuka kama Yehova anajua jaribu yenye uko napambana nayo na namna ile jaribu inakufanya ujisikie. Kwa mufano, Yehova hakuona tu namna Waisraeli walitendewa mubaya mu Misri, lakini pia aliona “maumivu yenye [walikuwa nayo].” (Kut. 3:7) Daudi aliimba kama Yehova aliona “mateso” yake na “taabu” mingi yenye alikuwa nayo. (Zb. 31:7) Na wakati watu wa Mungu waliteseka, hata kwa sababu ya maamuzi yao ya mubaya, “alitaabika.” (Isa. 63:9) Wakati unaogopa, Yehova anaelewa namna unajisikia, na anapenda sana kukusaidia upiganishe woga wako.

10. Juu ya nini uko hakika kama Yehova anakuhangaikia na kama atakusaidia upambane na jaribu yoyote?

10 Lakini wakati uko napambana na majaribu yenye kuogopesha, inaweza kuwa nguvu kwako kutambua namna Yehova iko nakutegemeza. Unaweza kufanya nini? Omba Yehova akusaidie kuona namna iko nakutegemeza. (2 Fa. 6:15-17) Kisha ufikirie hii mambo: Kuko hotuba fulani ao maelezo fulani yenye ilitolewa ku mikutano yenye imekutia nguvu? Kichapo, video, ao nyimbo fulani imekutia moyo? Mutu fulani alizungumuza na weye kuhusu wazo fulani ao andiko fulani yenye kutia moyo? Inaweza kuwa mwepesi kusahau namna upendo wa ndugu na dada zetu na chakula ya kiroho yenye tunapata, vinatusaidia sana. Tusisahau kama ile mambo ni zawadi ya pekee sana kutoka kwa Yehova. (Isa. 65:13; Mk. 10:29, 30) Inaonyesha kama Yehova anakuhangaikia. (Isa. 49:14-16) Na inaonyesha kama Yehova anastahili kutumainiwa.

11. Nini njo ilisaidia Aida kupiganisha woga wake?

11 Aida, mwenye kuishi Senegal, aliona namna Yehova alimutegemeza wakati wa majaribu. Juu yeye njo mutoto wa kwanza kwao, wazazi wake walitazamia kama atatafuta makuta ya mingi ili atimize mahitaji yake na mahitaji yao pia. Lakini, kisha kufanya maisha yake kuwa mwepesi juu akuwe painia, Aida alikuwa na magumu ya kupata makuta. Watu wa familia yake walimuchambua na kumusema mubaya. Aida anasema hivi: “Niliogopa kama sitaweza kusaidia wazazi wangu na kama kila mutu ataniachilia. Na hata nilimulaumu Yehova juu aliruhusu mambo iharibike sana vile.” Kisha, Aida alisikia hotuba yenye ilitolewa ku mukutano. Anasema hivi: “Musemaji alitukumbusha kama hata tukuwe na vidonda vya namna gani mu moyo wetu, Yehova anavijua. Pole kwa pole kupitia mashauri ya wazee na ya wengine, nilifikia kuwa hakika kama Yehova ananipenda. Nilianza kusali kwa Yehova nikiwa hakika zaidi kama atanisaidia. Na nilijisikia kuwa mwenye amani kabisa wakati niliona anajibia sala zangu.” Kisha wakati fulani, Aida alipata kazi yenye ilimusaidia atimize mahitaji yake mu kazi ya upainia, lakini pia ilimusaidia kutimiza mahitaji ya wazazi wake na ya watu wengine. Anasema hivi: “Nimejifunza kumutegemea Yehova kabisa. Sasa wakati ninasali, mara mingi woga wangu unaisha kabisa.”

YEHOVA ATAFANYA NINI WAKATI WENYE KUYA?

12. Kulingana na Zaburi 56:9, Daudi alikuwa hakika juu ya jambo gani?

12 Soma Zaburi 56:9. Hii andiko inaonyesha jambo ingine yenye ilisaidia Daudi kupiganisha woga wake. Hata wakati maisha yake ilikuwa ingali mu hatari, alitafakari juu ya mambo yenye Yehova angemufanyia. Daudi alijua kama Yehova angemuokoa kwa wakati wenye kufaa. Kwa kweli, Yehova alikuwa amesema kama ni Daudi njo angekuwa mufalme wa Israeli kisha Sauli. (1 Sa. 16:1, 13) Daudi alijua kama mambo yote yenye Yehova aliahidi, ingetimia kabisa-kabisa.

13. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atafanya nini?

13 Yehova ameahidi kukufanyia nini? Hatutazamie kama Yehova atazuia tusipatwe na magumu yote. c Lakini, hata tupatwe na magumu ya namna gani mu huu ulimwengu, Yehova ataitosha mu dunia mupya. (Isa. 25:7-9) Bila shaka, Muumbaji wetu iko na uwezo wa kufufua wafu, wa kutuponyesha, na wa kuharibu wapinzani wote.—1 Yo. 4:4.

14. Tunaweza kutafakari juu ya mambo gani?

14 Wakati unaogopa, utafakari juu ya mambo yenye Yehova atafanya wakati wenye kuya. Fikiria namna utajisikia wakati Shetani hatakuwa tena. Wakati watu wenye haki watakamata nafasi ya watu wabaya, na wakati hali ya kutokamilika itaisha pole kwa pole kila siku. Onyesho fulani ku mukusanyiko wa eneo wa 2014, ulionyesha namna tunaweza kutafakari juu ya tumaini yetu. Baba fulani alikuwa nazungumuza na familia yake juu ya namna 2 Timoteo 3:1-5 inaweza kusomwa mu njia tofauti ikiwa ilikuwa inatabiri namna mambo itakuwa mu Paradiso: “Mu ulimwengu mupya mutakuwa nyakati za furaha. Kwa maana watu watakuwa wenye kupendana, wenye kupenda mambo ya kiroho, wenye kiasi, wanyenyekevu, wenye kumusifu Mungu, wenye kutii wazazi, wenye shukrani, washikamanifu, wenye kupenda sana watu wa familia yao, wenye kupenda makubaliano, wenye kusema mambo ya muzuri juu ya wengine, wenye kujizuia, wapole, wenye kupenda wema, wenye kutumainika, wenye kuwa tayari kusikia, wenye kujishusha, wenye kumupenda Mungu kuliko kupenda raha, wenye wanachochewa na ushikamanifu kwa Mungu; na weye ushikamane na watu wa namna ile.” Unazungumuzaka na watu wa familia yako ao waamini wenzako juu ya namna maisha itakuwa mu ulimwengu mupya?

15. Hata kama Tanja aliogopa, nini njo ilimusaidia kupiganisha woga wake?

15 Dada Tanja, wa mu Makedonia ya Kaskazini, alipiganisha woga wake kwa kutafakari juu ya baraka za wakati wenye kuya. Wazazi wake walimupinga kwa ukali wakati alianza kujifunza Biblia. Anasema hivi: “Mambo fulani yenye niliogopa kama itatokea, ilifikia kutokea. Mama yangu alinipiga kisha kila mukutano. Wazazi wangu waliniogopesha kama wataniua ikiwa ninakuwa Shahidi wa Yehova.” Ku mwisho, Tanja alifukuzwa kwao. Alitenda namna gani? Anasema hivi: “Nilikazia akili furaha yenye ningekuwa nayo milele juu ninajikaza kuendelea kuwa muaminifu. Pia nilifikiria juu ya namna Yehova atanibariki mu ulimwengu mupya na kunirudishia hata zaidi mambo yote yenye nimepoteza mu hii dunia. Nilifikiria pia namna tutasahau mambo yote ya mubaya.” Tanja aliendelea kuwa muaminifu, na kwa musaada wa Yehova alipata fasi ya kuishi. Leo, Tanja ameolewa na ndugu muaminifu na wako natumika kwa furaha mu utumishi wa wakati wote.

UJIFUNZE KUMUTEGEMEA YEHOVA ZAIDI LEO

16. Nini njo itatusaidia tuendelee kuwa hodari wakati matukio yenye ilitabiriwa mu Luka 21:26-28 itatokea?

16 Mu kipindi ya taabu kubwa, watu wengi “watazimia kwa woga.” Lakini watu wa Mungu watabakia imara na wenye uhodari. (Soma Luka 21:26-28.) Juu ya nini hatutaogopa? Juu tutakuwa tayari tumejifunza kumutegemea Yehova. Tanja mwenye tumezungumuzia anasema kama mambo yenye ilimufikia zamani, iko namusaidia kupambana na hali zingine za nguvu. Anasema hivi: “Nimejifunza kama mu hali yoyote Yehova anaweza kutusaidia na kutubariki. Kusema kweli, jambo yoyote yenye wengine wanafikia kufanya, wanaifanya juu tu Yehova anawaruhusu. Na hata jaribu ikuwe nguvu namna gani, itafikia tu mwisho.”

17. Andiko yetu ya mwaka wa 2024 itatusaidia namna gani? (Ona picha ku jalada.)

17 Leo ni jambo ya kawaida kuogopa. Lakini kama Daudi, tunaweza kuamua kama hatutaacha woga ututawale. Andiko ya mwaka wa 2024 ni sala yenye Daudi alimutolea Yehova. Alisali hivi: “Wakati ninaogopa, ninakutegemea wewe.” (Zb. 56:3) Sawa vile kitabu fulani yenye kuzungumuzia Biblia inasema juu ya ile andiko, Daudi “haendelee kufikiria juu ya mambo yenye inamuogopesha, ao juu ya magumu yake, lakini anakazia akili mukombozi wake mwenye atamuokoa.” Mu miezi yenye kuya fikiria juu ya andiko yetu ya mwaka, zaidi sana wakati uko napambana na hali zenye kuogopesha. Kamata wakati wa kutafakari juu ya mambo yenye Yehova alishafanya, juu ya mambo yenye iko nafanya leo, na juu ya mambo yenye atafanya wakati wenye kuya. Kisha, kama Daudi unaweza kusema: “Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.”—Zb. 56:4.

Wakati wa musiba, dada fulani iko nafikiri juu ya andiko ya mwaka (Ona fungu ya 17)

NAMNA GANI UNAWEZA KUPIGANISHA WOGA KWA KUFIKIRIA . . .

  • mambo yenye Yehova alishafanya?

  • mambo yenye Yehova iko nafanya leo?

  • mambo yenye Yehova atafanya?

WIMBO 33 Umutupie Yehova Muzigo Wako

a Unaweza kupata habari zenye zitatia imani yako nguvu ku jw.org kwa kuandika “tuige imani yao” ao “ushuhuda” mu sehemu tafuta. Mu JW Library®, angalia mu sehemu “Tuige Imani Yao” ao “Habari juu ya Maisha ya Watu.”

b Majina fulani imebadilishwa.

d MAFASIRIO YA PICHA: Daudi iko nafikiri namna Yehova alimupatia nguvu ya kuua dubu, namna alikuwa anamusaidia kupitia Ahimeleki, na namna angemufanya kuwa mufalme.

e MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye amefungwa kwa sababu ya imani yake, iko nafikiri juu ya namna Yehova alimusaidia aache kuvuta tumbako, namna iko namutia moyo kupitia barua za wapendwa wake, na namna atamupatia uzima wa milele mu Paradiso.