Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

Yehova Atakusaidia Wakati wa Magumu

Yehova Atakusaidia Wakati wa Magumu

“[Yehova] ndiye anafanya nyakati zako kuwa imara.”ISA. 33:6.

WAZO KUBWA

Mambo yenye tunaweza kufanya juu tufaidike na musaada wa Yehova mu wakati wa magumu.

1-2. Watumishi waaminifu wa Yehova wanaweza kupambana na magumu gani?

 KWA kushitukia, mambo ya mubaya sana inaweza kubadilisha Maisha yetu. Kwa mufano, ndugu muaminifu mwenye kuitwa Luis a aliambiwa kama alikuwa na aina fulani ya kansere ya nguvu sana. Munganga alimuambia kama alibakia tu na miezi kidogo ya kuishi. Monika na bwana yake walikuwa nafanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Kisha siku moya Monika alijua kama bwana yake, mwenye alikuwa muzee wa kutaniko, alikuwa naishi maisha ya unafiki kwa miaka mingi. Olivia, dada mwenye hayaoelewa, alilazimika kutoka mu nyumba yake kwa sababu ya upepo mukali wenye ungetokea. Wakati alirudia alikutana nyumba yake imeharibiwa kabisa na upepo. Mu wakati kidogo tu, maisha ya wale watu wote ilibadilika kabisa-kabisa. Ulishakajikuta mu hali ya vile? Ulishakakutana na jambo fulani ya mubaya yenye ilibadilisha maisha yako kwa kushitukia?

2 Siye watumishi waaminifu wa Yehova tunapambana na magumu yenye watu wote wanapataka. Tunaweza pia kupambana na upinzani ao mateso kutoka kwa wale wenye wanachukia watu wa Mungu. Hata kama Yehova hazuie ile magumu isitupate, anatuahidi kama atatusaidia. (Isa. 41:10) Kwa musaada wake tunaweza kuendelea kuwa na furaha, kukamata maamuzi ya muzuri, na kuendelea kuwa washikamanifu, hata mu hali za nguvu sana. Mu hii habari tutaona njia ine zenye Yehova anatumia ili kutusaidia wakati tuko napambana na hali za nguvu mu maisha yetu. Tutaona pia mambo yenye tunapaswa kufanya ili tufaidike na musaada wenye Yehova anatutolea.

YEHOVA ATAKULINDA

3. Wakati jambo ya mubaya sana inatupata inaweza kuwa nguvu kufanya nini?

3 Tatizo. Wakati tunapatwa na jambo fulani ya mubaya sana, inaweza kuwa nguvu kwetu kuwaza muzuri na kukamata maamuzi. Juu ya nini? Tunaweza kuwa na maumivu ya nguvu sana mu moyo. Akili yetu inaweza kulemewa na mahangaiko. Tunaweza kujisikia sawa vile tuko natembea mu giza na hatujue tuende wapi. Ona namna wale dada wawili wenye tulizungumuzia walijisikia wakati walipambana na ile magumu. Olivia anasema hivi: “Kisha kupoteza nyumba yangu, nilichanganyikiwa na niliishiwa kabisa.” Monika anasema hivi juu ya namna bwana yake alimusaliti: “Nilivunjika moyo sana. Maumivu yenye nilisikia ilikuwa sawa vile mutu ananiingiza kisu mu moyo. Sikujua tena namna ya kuishi. Jambo yenye singewaziaka, ilinifikia.” Yehova anaahidi kutusaidia namna gani wakati tunalemewa?

4. Kulingana na Wafilipi 4:6, 7, Yehova anatuahidi nini?

4 Namna Yehova anatusaidia. Anaahidi kutupatia jambo yenye Biblia inaita “amani ya Mungu.” (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Ile amani ni utulivu wa akili na wa moyo wenye mutu anakuwaka nao kwa sababu ya uhusiano muzuri wenye iko nao pamoja naye. Ile amani ‘inapita uelewaji wote’; inapita jambo yoyote yenye tunaweza kuwazia. Ulishakasikia utulivu wa ajabu kisha kusali kwa Yehova? Ile yenye ulisikiaka njo “amani ya Mungu.”

5. Namna gani amani ya Mungu inalinda akili yetu na moyo wetu?

5 Ileile andiko inasema kama amani ya Mungu “italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.” Neno ya kwanza-kwanza yenye inatafsiriwa “kulinda,” ilikuwa neno ya kijeshi yenye ilitumiwa ili kuzungumuzia maaskari wenye walikuwa nalinda muji ili usishambuliwe. Watu wenye waliishi mu muji wenye kulindwa, walilala kwa amani juu walijua kama maaskari walikuwa kwenye milango mikubwa ya muji. Vilevile, wakati amani ya Mungu inalinda moyo wetu na akili yetu, tunatulia juu tunajua kama tuko salama. (Zb. 4:8) Kama vile habari ya Hana inaonyesha, hata kama hali yetu haibadilike palepale tunaweza kuwa na amani kwa kadiri fulani. (1 Sa. 1:16-18) Na wakati tunatulia, mara mingi inakuwaka mwepesi zaidi kufikiri na kukamata maamuzi yenye hekima.

Usali mupaka usikie “amani ya Mungu” inalinda moyo wako na akili yako (Ona fungu ya 4-6)


6. Tunaweza kufanya nini ili tupate amani ya Mungu? (Ona pia picha.)

6 Mambo yenye tunapaswa kufanya. Wakati uko na mahangaiko, tafuta mulinzi wa mufano. Namna gani? Sali mupaka wakati utapata amani ya Mungu. (Lu. 11:9; 1 Te. 5:17) Luis, mwenye tulizungumuzia anaeleza namna yeye na bibi yake Ana waliweza kupambana na mahangaiko yao wakati walipata habari kama alibakia tu na miezi fulani ya kuishi. Alisema hivi: “Mu hali ya vile ni nguvu sana kukamata maamuzi kuhusu mambo ya matunzo na mambo ingine. Lakini sala imetusaidia sana kuwa na amani mu hii kipindi yote.” Luis na bibi yake walisema kama walisali sana tena na tena, na kumuomba Yehova awapatie amani ya akili, moyo wenye kutulia, na hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri. Na waliona kama aliwasaidia. Kama uko napambana na magumu, endelea kusali na utaona namna amani ya Yehova italinda moyo wako na akili yako.—Ro. 12:12.

YEHOVA ATAKUFANYA KUWA IMARA

7. Tunaweza kujisikia namna gani wakati tunapambana na jaribu ya nguvu?

7 Tatizo. Wakati tuko napambana na majaribu ya nguvu, tunaweza kujisikia, kuwaza, ao kutenda mu njia yenye haiko ya kawaida. Sawa vile upepo mukali unaweza kurusha mashua ngambo na ngambo, hisia zetu zinaweza kubadilika-badilika. Ana mwenye tulizungumuzia alisema kama alikuwa na hisia mbalimbali kisha kifo ya bwana yake. Alisema hivi: “Wakati nilishuka moyo, nilianza kufikiria tu magumu yangu. Pia nilikasirika kwa sababu bwana yangu hakukuwa tena.” Zaidi ya ile, Ana alijisikia kuwa peke yake na alihuzunika juu alipaswa kukamata maamuzi kuhusu mambo yenye Luis alikuwa nashugulikia muzuri sana. Wakati fulani alijisikia sawa vile alikuwa mu upepo mukali katika bahari. Yehova anatusaidia namna gani wakati hisia za vile zinatulemea?

8. Sawa vile Isaya 33:6, inaonyesha Yehova anatuhakikishia nini?

8 Namna Yehova anatusaidia. Anatuhakikishia kama atatufanya kuwa imara. (Soma Isaya 33:6.) Wakati mashua inakutana na upepo, inaweza kusukumwa nguvu sana ngambo na ngambo. Ili kupambana na ile hali, ku sehemu ya mashua yenye kuwa chini ya maji, kunakuwaka vifaa vyenye vinaisaidiaka isiyumbe-yumbe sana. Ile inafanya hali ikuwe salama zaidi, na watu wasafiri muzuri zaidi. Lakini vifaa mingi vyenye vinasaidia mashua, vinatumikaka muzuri zaidi wakati mashua iko natembea. Vilevile, Yehova atatufanya kuwa imara ikiwa tunaendelea kusonga mbele kwa uaminifu wakati wa magumu.

Utumie vyombo vya kusaidia kutafuta habari ili ukuwe imara (Ona fungu ya 8-9)


9. Namna gani vyombo vyetu vya kusaidia kutafauta habari vinaweza kutusaidia ili tusiyumbe-yumbe? (Ona pia picha.)

9 Mambo yenye tunapaswa kufanya. Wakati unalemewa na hisia mbalimbali, fanya yako yote ili kuendelea na programu yako ya kiroho. Kusema kweli, pengine hautaweza kufanya mambo mingi sawa vile ulikuwa nafanya zamani. Lakini kumbuka kama Yehova ni Mungu mwenye usawaziko. (Linganisha na Luka 21:1-4.) Ku programu yako ya kiroho, weka wakati wa kufanya funzo ya kipekee na kutafakari. Juu ya nini? Kupitia tengenezo yake, Yehova ametupatia habari mingi zenye kutegemea Maandiko, zenye zinaweza kutusaidia tusiyumbe-yumbe. Ili kupata habari zenye uko nazo lazima, unaweza kutumia vyombo vya kusaidia kutafuta habari vyenye kuwa mu luga yako sawa vile JW Library®, Index des publications des Témoins de Jéhovah, na Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Monika, mwenye tulishazungumuzia, alisema kama wakati alikuwa na hisia zenye kuumiza, alitafuta mashauri mu vyombo vya kutafuta habari. Kwa mufano, alitafuta neno “kasirani.” Wakati ingine alitafuta neno “kusaliti” ao “ushikamanifu.” Kisha alikuwa nasoma mupaka ajisikie muzuri. Anasema hivi: “Ku mwanzo nilikuwa na mahangaiko ya mingi. Lakini kadiri niliendelea kusoma, nilijisikia sawa vile Yehova ananikumbatia. Wakati nilikuwa nasoma, nilitambua kama Yehova alikuwa naelewa namna nilikuwa najisikia na alikuwa ananisaidia.” Musaada kutoka kwa Yehova unaweza kukusaidia weye pia usiyumbe-yumbe mupaka wakati utatulia.—Zb. 119:143, 144.

YEHOVA ATAKUTEGEMEZA

10. Tunaweza kujisikia namna gani wakati jambo ya mubaya sana inatupata?

10 Tatizo. Kisha tukio ya mubaya sana, kuko siku zenye tunaweza kukosa nguvu na kujisikia mubaya sana. Tunaweza kujisikia sawa vile mukimbiaji mwenye alikuwaka nakimbia mbio sana, lakini iko sasa natembea kama mutu mwenye kuteuka. Inaweza kuwa nguvu kufanya kazi zenye zamani zilikuwaka mwepesi kwetu, ao tunaweza kukosa nia ya kufanya mambo fulani yenye tulikuwaka nafurahia. Kama Eliya, tunaweza kujisikia kama hatuna nguvu ya kulamuka. Tunapenda tu kulala. (1 Fa. 19:5-7) Yehova anaahidi kutufanyia nini wakati tunajisikia kuwa zaifu?

11. Yehova anatumia njia gani ingine ili kutusaidia? (Zaburi 94:18)

11 Namna Yehova anatusaidia. Anaahidi kututegemeza. (Soma Zaburi 94:18.) Sawa vile mukimbiaji mwenye kuumia anaweza kuwa na lazima ya mutu wa kumutegemeza ili aendelee kusonga mbele, tunaweza pia kuwa na lazima ya musaada ili tuendelee kumutumikia Yehova. Mu hali za vile, Yehova anatuhakikishia hivi: “Mimi, Yehova Mungu wako, ninashika mukono wako wa kuume, ni mimi mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’” (Isa. 41:13) Mufalme Daudi alijionea musaada wa Yehova. Wakati alipambana na majaribu na maadui, alimuambia Yehova hivi: “Mukono wako wa kuume unanitegemeza.” (Zb. 18:35) Sasa namna gani Yehova anatutegemeza?

Ukubali musaada wa watu wa familia, marafiki, na wazee (Ona fungu ya 11-13)


12. Yehova anaweza kutumia nani ili watusaidie wakati tuko zaifu?

12 Mara mingi, Yehova anatutegemeza kwa kuchochea wengine watusaidie. Kwa mufano, wakati fulani Daudi alijisikia kuwa zaifu. Rafiki yake Yonatani alimutembelea ili kumutia moyo na kumutia nguvu. (1 Sa. 23:16, 17) Vilevile, Yehova alimuchagua Elisha ili amusaidie Eliya. (1 Fa. 19:16, 21; 2 Fa. 2:2) Leo, Yehova anaweza kutumia familia, marafiki, ao wazee ili kututegemeza. Lakini wakati tuko na huzuni tunaweza kupenda wengine wasitukaribie. Tunaweza tu kupenda kubakia peke yetu. Ile ni jambo ya kawaida. Sasa, tunaweza kufanya nini ili Yehova atutegemeze?

13. Tunaweza kufanya nini ili Yehova atutegemeze? (Ona pia picha.)

13 Mambo yenye tunapaswa kufanya. Ujikaze sana juu usipende kubakia weye pake. Wakati tunajitenga na wengine, tunaweza kuanza kujifikiria siye wenyewe na magumu yenye tuko nayo. Mawazo ya vile inaweza kufanya tukamate maamuzi ya mubaya. (Mez. 18:1) Ni kweli kwamba siye wote tunapendaka kubakia peke yetu wakati fulani, zaidi sana wakati tuko napambana na hali za nguvu. Lakini kama tunajitenga na wengine kwa muda murefu, inaweza kuwa sawa vile tuko natia pembeni njia yenye Yehova anatumia ili kututegemeza. Kwa hiyo, hata kama inaweza kuwa nguvu sana, kubali musaada wa watu wa familia yako, marafiki, na wazee. Uwaone kuwa njia yenye Yehova iko natumia ili kukutegemeza.—Mez. 17:17; Isa. 32:1, 2.

YEHOVA ATAKUFARIJI

14. Tunaweza kupambana na hali gani za kuogopesha?

14 Tatizo. Wakati fulani tunaweza kupambana na hali za kuogopesha. Mu Biblia watumishi fulani waaminifu wa Mungu wanaeleza namna wakati fulani walisikia mubaya sana na kutetemeka kwa sababu ya maadui wao ao kwa sababu ya mikazo ingine. (Zb. 18:4; 55:1, 5) Vilevile, tunaweza kupambana na upinzani ku masomo, ku kazi, kutoka kwa watu wa familia yetu, ao wakubwa wa serikali. Tunaweza hata kuogopa kama tutakufa kwa sababu ya ugonjwa fulani. Mu wakati ya vile, tunaweza kujisikia sawa mutoto mudogo mwenye hajue afanye nini. Yehova anatusaidia namna gani mu wakati ya vile?

15. Kulingana na Zaburi 94:19 Yehova atatufanyia nini?

15 Namna Yehova anatusaidia. Anatufariji na kututuliza. (Soma Zaburi 94:19.) Hii zaburi inatufanya tufikirie mutoto mudogo mwenye anaogopa na anashindwa kulala kwa sababu ya mvua kubwa yenye kuwa na radi. Wazia baba yake anakuya, anamukamata, na kumubeba mupaka wakati anapata usingizi. Hata kama ile mvua kubwa ingali inanyesha, ule mutoto anajisikia kuwa salama mu mikono ya baba yake mwenye kufariji. Wakati tunapambana na magumu yenye kuogopesha, tunaweza kuwa na lazima Baba yetu wa mbinguni atukumbatie kwa njia ya mufano mupaka wakati tutajisikia muzuri. Namna gani tunaweza kupata faraja kutoka kwa Yehova?

Acha Baba yako wa mbinguni akufariji kupitia Maandiko (Ona fungu ya 15-16)


16. Tunaweza kufanya nini ili Yehova atufariji? (Ona pia picha.)

16 Mambo yenye tunapaswa kufanya. Uzoee kupitisha wakati pamoja na Yehova kwa kusali na kusoma Neno yake. (Zb. 77:1, 12-14) Kisha wakati utakuwa na mahangaiko, jambo ya kwanza yenye utafikiria ni kutafuta musaada wake. Umuambie Yehova mambo yenye inakuogopesha na mahangaiko yako. Acha azungumuze na weye na akufariji kupitia Maandiko. (Zb. 119:28) Unaweza kupata maandiko fulani ye Biblia yenye inaweza kukufariji kabisa wakati unaogopa. Kwa mufano, unaweza kutiwa moyo sana wakati unasoma kitabu ya Yobu, Zaburi, Mezali, na maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo sura ya 6. Wakati unasali kwa Yehova na kusoma Neno yake, utasikia vile atakufariji.

17. Tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

17 Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atakuwa pamoya na siye wakati tunapambana na hali za nguvu sana mu maisha. Hatutakuwa peke yetu hata siku moja. (Zb. 23:4; 94:14) Yehova anaahidi kama atatulinda, atatutegemeza, na atatufariji. Andiko ya Isaya 26:3 inasema hivi: “Utalinda wale wenye kukutegemea kabisa; utawapatia amani ya kudumu, kwa sababu wanakutegemea wewe.” Kwa hiyo, umutegemee Yehova na ufaidike na njia zenye anatumia ili kukusaidia. Kama unafanya vile, utapata nguvu hata wakati wa magumu.

UTAJIBIA NAMNA GANI?

  • Tunaweza kuwa na lazima ya musaada wa Yehova zaidi sana mu hali gani?

  • Yehova anafanya mambo gani ine ili kutusaidia wakati wa magumu?

  • Tunaweza kufanya nini ili tufaidike na musaada wa Yehova?

WIMBO 12 Yehova Ni Mungu Mukubwa

a Majina fulani imebadilishwa.