Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 10

Juu ya Nini Unapaswa Kubatizwa?

Juu ya Nini Unapaswa Kubatizwa?

“Kila mumoja wenu abatizwe.”​—MDO. 2:38.

WIMBO 34 Nitatembea kwa Uaminifu-Mushikamanifu

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Mara mingi inakuwaka namna gani wakati watu wanabatizwa, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

 WAZIA uko naangalia kikundi ya watu wenye wanataka kubatizwa. Mbele wabatizwe, unasikia wanajibia maulizo mbili bila kusita. Unaona vile watu wa familia yao na marafiki wao wanawafurahia kabisa. Wakati wale wenye kubatizwa wanatoka mu maji, unasikia watu wanapiga mikono na unaona namna wale wenye wanabatizwa wako na furaha. Kwa kukadiria, maelfu ya watu wako najitoa kwa Mungu kila juma na kuwa Mashahidi wa Yehova Mungu wenye kubatizwa.

2 Na weye unawaza nini? Kama unafikiria kubatizwa, uko mutu wa maana sana mu hii dunia ya Shetani juu uko “namutafuta Yehova.” (Zb. 14:1, 2) Hii habari iliandikwa kwa ajili yako, ikuwe uko kijana ao muzee. Lakini, hata wale wenye walishabatizwa, wako pia na lazima ya kutia nguvu imani yao ili waendelee kumutumikia Yehova milele. Kwa hiyo, tuzungumuzie mambo tatu yenye inaweza kumuchochea mutu amutumikie Yehova.

UNAPENDA KWELI NA HAKI

Shetani amesema uongo juu ya jina ya muzuri ya Yehova kwa maelfu ya miaka na anaendelea kufanya vile (Ona fungu ya 3-4)

3. Juu ya nini watumishi wa Yehova wanapendaka kweli na haki? (Zaburi 19:8; 119:163)

3 Yehova aliambia hivi watu wake: “Mupende kweli.” (Zek. 8:19) Yesu aliambia wanafunzi wake wafuatilie haki. (Mt. 5:6) Ile inamaanisha kama inaomba mutu apende kabisa kufanya mambo yenye kuwa sawa, ya muzuri, na yenye kuwa safi mbele ya Mungu. Unapendaka kweli na haki? Tuko hakika kama unapendaka. Unachukia uongo na mambo yote yenye haifae na ya mubaya sana. (Soma Zaburi 19:8; 119:163.) Uongo unaonyesha utu wa Shetani, mutawala wa hii ulimwengu. (Yoh. 8:44; 12:31) Shetani iko na kusudi moya: Kusema uongo juu ya jina takatifu ya Yehova Mungu. Shetani ameeneza uongo juu ya Mungu tangu uasi mu Edeni. Amejaribu kufanya watu wawaze kama Yehova ni Mungu mwenye hahangaikiake watu, ni Mutawala mwenye kusema uongo, na mwenye kuima watu mambo ya muzuri. (Mwa. 3:1, 4, 5) Uongo wenye Shetani ameeneza juu ya Yehova unaendelea kufanya watu wakuwe na mawazo ya mubaya juu ya Yehova. Wakati watu ‘hawapende kweli,’ Shetani anaweza kuwachochea wafanye mambo yenye haiko ya haki na ya mubaya sana.​—Ro. 1:25-31.

4. Yehova amefanya nini ili kuonyesha kama ni “Mungu wa ukweli”? (Ona pia picha.)

4 Yehova ni “Mungu wa ukweli,” na anafundisha kweli wale wenye wanamupenda. (Zb. 31:5) Kwa kufanya vile, anawasaidia wasidanganywe na uongo wa Shetani. Tena, Yehova anafundisha watumishi wake wakuwe nasema kweli na wakuwe wenye haki. Ile inawasaidia wajiheshimishe na wakuwe na amani ya moyo. (Mez. 13:5, 6) Yehova alikufundishaka vile wakati ulikuwa najifunza Biblia? Ulijifunza kama njia za Yehova njo za muzuri sana kwa wanadamu wote na kwako kipekee. (Zb. 77:13) Kwa hiyo, unapenda kufanya mambo yenye Mungu anasema kama ni ya muzuri. (Mt. 6:33) Njo maana unapenda kutetea kweli na kuonyesha kama mambo yenye Shetani alisemaka juu ya Mungu wetu Yehova ni ya uongo. Unaweza kufanya vile namna gani?

5. Namna gani unaweza kutetea kweli na haki?

5 Unaweza kujiambia hivi mu maisha yako: “Nakatala uongo wa Shetani na niko natetea kweli. Napenda Yehova akuwe Mutawala wangu na napenda kufanya mambo yenye anasema kama ni ya muzuri.” Unaweza kufanya vile namna gani? Umukaribie Yehova katika sala na kujitoa kwake. Kisha, unaweza kuonyesha mbele ya watu kama ulishajitoa kwake kwa kubatizwa. Kupenda kweli na haki ni kati ya mambo yenye inaweza kukuchochea kabisa ufikie kubatizwa.

UNAMUPENDA YESU KRISTO

6. Ni mambo gani yenye kuwa mu Zaburi 45:4 yenye inafanya umupende Yesu Kristo?

6 Juu ya nini unamupenda Yesu Kristo? Ona sababu fulani mu Zaburi 45:4. (Soma.) Yesu anapenda kweli, unyenyekevu, na haki. Kama unapenda kweli na haki, ni kusema, unamupenda pia Yesu Kristo. Fikiria namna Yesu alitetea kweli na haki kwa uhodari. (Yoh. 18:37) Sasa, ni mu njia gani Yesu anapenda unyenyekevu?

7. Juu ya nini unafurahia unyenyekevu wa Yesu?

7 Matendo ya Yesu inaonyesha kama anapendaka unyenyekevu. Kwa mufano, hajitukuzake hata kidogo. Anapatiaka Baba yake utukufu wote. (Mk. 10:17, 18; Yoh. 5:19) Unyenyekevu wa Yesu unafanyaka ujisikie namna gani? Ile haikuchochee kumupenda na kumufuata? Bila shaka inakuchochea. Juu ya nini Yesu ni munyenyekevu? Juu anapenda Baba yake mwenye ni munyenyekevu na juu anapenda kumuiga. (Zb. 18:35; Ebr. 1:3) Ile inakuvuta kwa Yesu, mwenye aliiga kwa ukamili sifa za Yehova, hauone vile?

8. Juu ya nini tunamupenda Yesu Mufalme wetu?

8 Tunamupenda Yesu Mufalme wetu juu ni Mutawala muzuri sana. Yehova yeye peke njo alimuzoeza na kumuweka kuwa Mufalme. (Isa. 50:4, 5) Tena, fikiria upendo mukubwa wenye Yesu alituonyesha. (Yoh. 13:1) Juu Yesu ni Mufalme wako, unapaswa kumupenda kabisa. Alionyesha kama wale wenye wanamupenda, ni kusema, wale wenye anaita marafiki wake, wanaonyesha kama wanamupenda kwa kutii amri zake. (Yoh. 14:15; 15:14, 15) Ni pendeleo kubwa sana kuwa rafiki ya Mwana wa Yehova!

9. Ni mu njia gani ubatizo wa Wakristo unafanana na ubatizo wa Kristo?

9 Ubatizo ni moya kati ya amri zenye Yesu alipatia wanafunzi wake. (Mt. 28:19, 20) Alituwekea mufano kwa kubatizwa. Mu njia fulani, ubatizo wake ulikuwa tofauti na ubatizo wa wanafunzi wake. (Ona kisanduku “ Tofauti Kati ya Ubatizo wa Yesu na Ubatizo wa Wanafunzi Wake.”) Lakini mu njia zingine, unafanana. Wakati Yesu alibatizwa, alionyesha wazi kama alikuwa tayari kufanya mapenzi ya Baba yake. (Ebr. 10:7) Wakati wanafunzi wa Kristo wanabatizwa wanaonyesha waziwazi kama walishajitoa kwa Yehova Mungu. Lakini sawa vile Yesu, ubatizo wao unaonyesha kama wako sasa tayari kufanya mapenzi ya Mungu mu maisha yao yote, hapana mapenzi yao. Kwa hiyo, wanafuata mufano wa Bwana wao.

10. Juu ya nini unamupenda Yesu, na ule upendo unapaswa kukuchochea kufanya nini?

10 Unajua kama Yesu ni Mwana muzaliwa pekee wa Yehova na kama ni Mufalme mwenye Yehova aliweka ili atutawale. Unajua kama Yesu ni munyenyekevu na anamuiga Baba yake kwa ukamili. Umejifunza kama alipatia chakula wenye njaa, alifariji wenye kuvunjika moyo, na hata aliponyesha wagonjwa. (Mt. 14:14-21) Umeona kama iko naongoza kutaniko yake leo. (Mt. 23:10) Na unajua kama juu yeye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu, atafanya mambo mingi zaidi wakati yenye kuya. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unamupenda Yesu? Unaweza kufuata mufano wake. (Yoh. 14:21) Jambo ya kwanza yenye unaweza kufanya ni kujitoa kwa Yehova na kubatizwa.

UNAMUPENDA YEHOVA MUNGU

11. Ni sababu gani ya maana sana yenye inapaswa kukuchochea ubatizwe?

11 Ni sababu gani ya maana sana yenye inapaswa kukuchochea ubatizwe? Yesu alionyesha amri kubwa sana kati ya amri za Mungu, kwa kusema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Mk. 12:30) Ile maneno inaonyesha ni kwa kiasi gani unamupenda Mungu?

Yehova ni Mupaji wa kila zawadi ya muzuri sana (Ona fungu ya 12-13)

12. Juu ya nini unamupenda Yehova? (Ona pia picha.)

12 Kuko sababu mingi zenye zinapaswa kuchochea mutu amupende Yehova. Kwa mufano, umefikia kuelewa kama yeye ni “chemchemi ya uzima” na kama ni Mupaji wa “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.” (Zb. 36:9; Yak. 1:17) Mambo yote yenye tuko nafurahia inatoka kwa Mungu wetu mukarimu na mwenye upendo.

13. Juu ya nini bei ya ukombozi ni zawadi ya muzuri sana?

13 Bei ya ukombozi ni zawadi ya muzuri sana yenye Yehova ametupatia. Juu ya nini tunasema vile? Fikiria uhusiano wenye kuwa kati ya Yehova na Mwana wake. Yesu alisema hivi: “Baba ananipenda” na alisema pia hivi: “Ninamupenda Baba.” (Yoh. 10:17; 14:31) Uhusiano kati ya Yehova na Yesu ulikuwa wa nguvu sana juu waliishi pamoya kwa mamiliare ya miaka. (Mez. 8:22, 23, 30) Sasa fikiria namna Mungu angehuzunika kwa kuacha Mwana wake ateseke na kufa. Yehova anapenda sana wanadamu, kutia ndani na weye. Njo maana alitoa Mwana wake mupendwa akuwe zabihu ili weye na watu wengine mukuwe na tumaini ya kuishi milele. (Yoh. 3:16; Gal. 2:20) Ile njo sababu kubwa sana yenye inafanya tumupende Mungu.

14. Ni muradi gani wa muzuri sana wenye unaweza kujiwekea mu maisha?

14 Upendo wako kwa Yehova uliongezeka wakati ulijifunza mambo mingi zaidi juu yake. Bila shaka unapenda kumukaribia sana, kuanzia sasa na milele. Na unaweza kufikia kufanya vile. Anakuomba ufurahishe moyo wake. (Mez. 23:15, 16) Unaweza kufanya vile, hapana tu kwa maneno, lakini pia kupitia matendo. Namna yako ya kuishi itaonyesha kama unamupenda kabisa Yehova. (1 Yo. 5:3) Kuchagua kuishi maisha yenye itamufurahisha Yehova, njo muradi ya muzuri yenye unaweza kujiwekea.

15. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unamupenda Yehova?

15 Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unamupenda Yehova? Kwanza, unaweza kutoa sala ya pekee ya kujitoa kwake. (Zb. 40:8) Kisha, unapaswa kubatizwa ili kuonyesha mbele ya watu wote kama ulijitoa kwake. Sawa vile tulizungumuzia ku mwanzo wa hii habari, ubatizo ni hatua ya maana sana na yenye kufurahisha mu maisha yako. Wakati unabatizwa unaanza kuishi maisha ya mupya, ni kusema, hauishi tena kwa ajili yako, lakini kwa ajili ya Yehova. (Ro. 14:8; 1 Pe. 4:1, 2) Kusema kweli, ile ni hatua ya maana sana. Inakupatia nafasi ya kuishi maisha ya muzuri sana. Namna gani?

16. Sawa vile Zaburi ya 41:12 inaonyesha, Yehova atapatia nini wale wenye wanatoa maisha yao ili kumutumikia?

16 Hakuna mutu mukarimu sawa vile Yehova. Hata umupatie nini, yeye atakupatia zaidi ya ile yenye unamupatia. (Mk. 10:29, 30) Atakupatia maisha ya muzuri, yenye kufurahisha, na yenye kuwa na kusudi hata mu hii dunia ya Shetani; na ile ni mwanzo tu. Wakati unabatizwa, unaanza maisha yenye haina mwisho. Unaweza kuendelea kumutumikia Yehova Baba yako mupendwa milele. Na upendo wenye kuwa kati yako na Yehova, utaendelea kuongezeka. Tena, juu Yehova ni wa milele, na weye utaishi milele sawa vile yeye.​—Soma Zaburi 41:12.

17. Unaweza kumupatia Yehova nini yenye bado hauyamupatiaka?

17 Wakati unakamata hatua ya kujitoa kwa Yehova na kubatizwa, unakuwa sasa na pendeleo ya kumupatia Baba yako wa mbinguni jambo fulani ya maana sana. Amekupatia kila kitu ya muzuri na wakati ya kufurahisha. Ile ni mambo yenye ulikuwa hauyapataka. Na weye unaweza kumupatia Muumbaji wa mbingu na dunia jambo fulani yenye bado hauyamupatiaka, ni kusema, utumishi wako mushikamanifu. (Yob. 1:8; 41:11; Mez. 27:11) Bila shaka, ile itafanya ukuwe na maisha ya muzuri sana! Kusema kweli, kumupenda Yehova njo jambo ya maana sana yenye inapaswa kukuchochea ubatizwe.

UKO NACHUNGA NINI?

18. Unaweza kujiuliza maulizo gani?

18 Utabatizwa? Unaweza kujibia namna gani ile ulizo? Ni weye tu njo unaweza kuijibia. Lakini ni muzuri ujiulize hivi: ‘Niko nachunga nini?’ (Mdo. 8:36) Kumbuka mambo tatu yenye tumezungumuzia. Ya kwanza, unapenda kweli na haki. Ujiulize hivi: ‘Na miye napendaka kuishi mu dunia mwenye kila mutu atakuwa nasema kweli na kufanya mambo yenye kuwa sawa?’ Ya pili, unamupenda Yesu Kristo. Ujiulize hivi: ‘Napenda Mwana wa Mungu akuwe Mufalme wangu na napenda kufuata mufano wake?’ Na ya tatu, yenye ni ya maana sana, unamupenda Yehova. Ujiulize hivi: ‘Napendaka kufurahisha moyo wa Yehova kwa kumutumikia?’ Kama unajibia ndiyo ku ile maulizo, sasa juu ya nini haubatizwe? Uko nachunga nini?​—Mdo. 16:33.

19. Juu ya nini haupaswe kuogopa kubatizwa? Fasiria. (Yohana 4:34)

19 Kama uko naogopa kubatizwa, fikiria mambo yenye Yesu alisema. (Soma Yohana 4:34.) Yesu alilinganisha kufanya mapenzi ya Baba yake na chakula. Juu ya nini? Juu chakula inajengaka mwili wetu. Yesu alijua kama kila kitu yenye Yehova anatuomba tufanye inakuwaka na faida kwetu. Yehova hapende tufanye jambo yoyote yenye inaweza kutuumiza. Anapenda ubatizwe? Ndiyo. (Mdo. 2:38) Kwa hiyo, ukuwe hakika kama utapata faida kama unatii ile amri ya kubatizwa. Kama unafurahiaka kula chakula ya muzuri sana, sasa juu ya nini unaogopa kubatizwa?

20. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

20 Uko nachunga nini? Wengi wanaweza kujibia hivi: “Siyakuwa tayari.” Kusema kweli, uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kubatizwa njo uamuzi wa maana sana wenye unapaswa kukamata mu maisha yako. Kwa hiyo, inaomba wakati, kufikiri sana, na kujikaza sana ili ukuwe tayari kwa ajili ya ubatizo. Lakini, kama unapenda sana kukamata ile hatua, unaweza kufanya nini sasa ili kujitayarisha? Tutapata jibu ya ile ulizo mu habari yenye kufuata.

WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?

a Ubatizo ni hatua ya maana yenye kila mwanafunzi wa Biblia anapaswa kukamata. Nini njo inaweza kuchochea mwanafunzi akamate ile hatua? Kwa kifupi, ni upendo. Sasa, ni kupenda nini na nani? Mu hii habari, tutapata majibu ya ile maulizo na tutazungumuzia namna maisha yetu inaweza kuwa wakati tunabatizwa.