Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 14

“Kwa Jambo Hili Wote Watajua Kama Ninyi Ni Wanafunzi Wangu”

“Kwa Jambo Hili Wote Watajua Kama Ninyi Ni Wanafunzi Wangu”

“Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.”​—YOH. 13:35.

WIMBO 106 Tukuwe na Upendo

KIFUPI YA HABARI a

Kisha kuona upendo wenye kuwa kati ya Mashahidi wa Yehova, watu wengi wenye hawako Mashahidi wa Yehova walisema nini? (Ona fungu ya 1)

1. Nini njo inafurahishaka watu wengi wakati wanakusanyika na siye kwa mara ya kwanza? (Ona pia picha.)

 WAZIA bibi na bwana wanakusanyika kwa mara ya kwanza ku Jumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova. Wanafurahi juu wanakaribishwa muzuri na juu wanaona vile ndugu na dada wanapendana. Wakati wako narudia ku nyumba, bibi anaambia hivi bwana yake: ‘Nafurahi kuwa pamoya na Mashahidi wa Yehova juu wako tofauti sana na wengine.’

2. Juu ya nini watu fulani wameacha kumutumikia Yehova?

2 Bila shaka, upendo wenye kuwa kati ya watu wa Yehova ni wa pekee sana. Kusema kweli, Mashahidi wa Yehova hawakamilike (1 Yo. 1:8) Kwa hiyo, kadiri tunaendelea kuwajua muzuri, ni vile tutaanza kuona makosa ao uzaifu fulani wenye wako nao. (Ro. 3:23) Jambo ya kuhuzunisha, watu fulani wameacha kumutumikia Yehova juu ya makosa ao uzaifu wa wengine.

3. Nini njo inatambulisha wanafunzi wa kweli wa Yesu? (Yohana 13:34, 35)

3 Fikiria tena andiko ya musingi ya hii habari. (Soma Yohana 13:34, 35.) Nini njo inatambulisha wanafunzi wa kweli wa Kristo? Ni upendo, Biblia haionyeshe kama ni ukamilifu. Ona pia kama, Yesu hakusema hivi: ‘Kwa jambo hili mutajua kama ninyi ni wanafunzi wangu.’ Lakini alisema hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu.” Kwa kusema vile, Yesu alionyesha kama wanafunzi wake na pia watu wengine wenye hawako Wakristo wangetambua wanafunzi wake wa kweli kupitia upendo wa kweli wenye wanaonyeshana.

4. Watu fulani wanaweza kujiuliza maulizo gani juu ya Wakristo wa kweli?

4 Watu fulani wenye hawako Mashahidi wa Yehova wanaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani upendo unatambulisha wanafunzi wa kweli wa Yesu? Yesu alifanya nini ili kuonyesha kama alipenda mitume wake? Na namna gani tunaweza kuiga mufano wake leo? Siye Mashahidi wa Yehova tunapaswa kufikiria majibu ya ile maulizo. Kufanya vile kunaweza kutusaidia tupende sana ndugu na dada zetu, zaidi sana wakati tunaona makosa ao uzaifu wao.​—Efe. 5:2.

NI AINA GANI YA UPENDO WENYE UNATAMBULISHA WANAFUNZI WA KWELI WA YESU?

5. Fasiria maana ya maneno ya Yesu yenye kuwa mu Yohana 15:12, 13.

5 Yesu alifasiria kama wanafunzi wake wangependana mu njia ya pekee. (Soma Yohana 15:12, 13.) Ona vile aliwaambia: “Mupendane kama vile niliwapenda ninyi.” Ile inamaanisha nini? Sawa vile Yesu alifasiria, ile inamaanisha kupenda wengine zaidi kuliko vile tunajipenda ao ni aina ya upendo wenye unaweza kufanya Mukristo akuwe tayari kufa kwa ajili ya Mukristo mwenzake kama ni lazima. b

6. Ni mambo gani yenye Neno ya Mungu inafundisha yenye inaonyesha kama upendo ni sifa ya maana sana?

6 Neno ya Mungu inatufundisha kama upendo ni sifa ya maana sana. Kati ya Maandiko yenye watu wanapendaka sana, kuko pia hii: “Mungu ni upendo.” (1 Yo. 4:8) “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mt. 22:39) “Upendo unafunika zambi nyingi.” (1 Pe. 4:8) “Upendo haushindwe hata kidogo.” (1 Ko. 13:8) Ile Maandiko pamoya na ingine, inaonyesha wazi kama upendo ni sifa ya maana sana, kwa hiyo, tunapaswa kupendana.

7. Juu ya nini Shetani hana uwezo hata kidogo wa kuunganisha watu na kuwafanya waonyeshane upendo wa kweli?

7 Watu wengi wanajiulizaka hivi: ‘Naweza kutambua namna gani dini ya kweli? Dini zote zinasema kama zinafundishaka kweli, lakini, mambo yenye wanafundishaka juu ya Mungu iko tofauti.’ Juu Shetani amefanya kukuwe dini mingi za uongo, inakuwa nguvu kwa watu wengi kutambua dini ya kweli. Lakini, hana uwezo hata kidogo wa kuunganisha watu mu dunia yote ili wakuwe familia ya ndugu na dada wenye wanaonyeshana upendo wa kweli. Ni Yehova tu njo iko na uwezo wa kufanya vile. Ile inaeleweka juu upendo wa kweli unatoka kwake. Zaidi ya ile, ni wale tu wenye Yehova anabariki na kupatia roho yake njo wanaweza kuonyeshana upendo wa kweli. (1 Yo. 4:7) Njo maana, Yesu alisema kama upendo wa kweli njo alama yenye ingetambulisha wanafunzi wake wa kweli.

8-9. Kuona upendo wa kweli wenye kuwa kati ya Mashahidi wa Yehova, kulifanya watu wengi waseme nini?

8 Sawa vile Yesu alisemaka, watu wengi wamefikia kutambua wanafunzi wake wa kweli kupitia upendo wa kweli wenye kuwa kati yao. Kwa mufano, ndugu mwenye kuitwa Ian anakumbuka mara ya kwanza yenye aliendaka ku mukusanyiko wenye ulifanyika mu uwanja wa kabumbu wenye ulikuwa karibu na kwake. Miezi fulani ilikuwa ilishapita tangu Ian aliendaka ku ule uwanja juu ya kuangalia muchezo wa kabumbu. Anasema hivi: “Kulikuwa tofauti kubwa kati ya watu wenye waliendaka kuangalia muchezo wa kabumbu na watu wenye waliendaka ku mukusanyiko. Mashahidi wa Yehova walikuwa na heshima, walivala muzuri, na watoto wao walijiendesha muzuri.” Anasema tena hivi: “Zaidi ya ile, wale Mashahidi walionekana kuwa wenye kutosheka na wenye amani. Na ile ni jambo yenye nilipenda sana mu maisha yangu. Sikumbuke hata hotuba moya yenye ilitolewaka ile siku, lakini, naendelea kukumbuka namna Mashahidi wa Yehova walijiendesha muzuri.” c Bila shaka, walijiendesha vile juu walikuwa na upendo wa kweli kati yao. Juu tunapenda ndugu na dada zetu, tunawatendea kwa fazili na heshima.

9 Ndugu mwenye kuitwa John alijionea pia ile wakati alianza kukusanyika. Anasema hivi: “Kule watu walikuwa wenye urafiki na walionekana sawa vile ni wakamilifu; ile ilinifurahisha sana. Upendo wa kweli wenye ulikuwa kati yao ulinihakikishia kama nilipata dini ya kweli.” d Mambo yenye wale ndugu walijionea na mambo ingine, inaonyesha kama Mashahidi wa Yehova njo Wakristo kweli.

10. Ni wakati gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda kabisa ndugu na dada zetu? (Ona pia maelezo ya chini.)

10 Sawa vile tuliona ku mwanzo wa hii habari, siye wote hatukamilike. Wakati fulani, ndugu na dada zetu wanaweza kufanya makosa.  e (Yak. 3:2) Wakati ile inatokea, namna yetu ya kutenda itaonyesha kama tunawapenda kabisa ao hapana. Kwa hiyo, mufano wa Yesu unaweza kutufundisha nini?​—Yoh. 13:15.

YESU ALIFANYA NINI ILI KUONYESHA KAMA ALIPENDA MITUME WAKE?

Yesu alitendea mitume wake kwa upendo wakati walionyesha tabia za mubaya (Ona fungu ya 11-13)

11. Yakobo na Yohana walionyesha tabia gani za mubaya? (Ona pia picha.)

11 Yesu hakutazamia mitume wake wakuwe wakamilifu. Lakini, aliwasaidia kwa upendo kurekebisha tabia zao juu wamufurahishe Yehova. Wakati fulani, mitume wawili, Yakobo na Yohana, walimuambia mama yao awaombee kwa Yesu madaraka ya maana mu Ufalme. (Mt. 20:20, 21) Ile ilionyesha kama Yakobo na Yohana walikuwa na kiburi na kama walipenda waonekane kuwa wa maana sana kuliko wengine.​—Mez. 16:18.

12. Ni Yakobo na Yohana tu njo walionyesha tabia za mubaya? Fasiria.

12 Haiko tu Yakobo na Yohana njo walionyesha tabia za mubaya ile wakati. Ona namna mitume wengine walitenda. “Wakati wale wengine kumi walisikia jambo hilo, wakakasirikia wale ndugu wawili.” (Mt. 20:24) Tunaweza kuwazia maneno ya makali yenye Yakobo, Yohana na wale mitume wengine walisema. Pengine wale mitume wengine walisema hivi: ‘Muliomba madaraka ya maana katika Ufalme juu muliwaza kama muko wa maana kuliko siye? Haiko nyiye tu njo mulitumika sana na Yesu. Kama nyiye munastahili kupewa ile madaraka, ni kusema, na siye pia tunastahili.’ Ikuwe walisema vile ao hapana, ile wakati walisahau kama walipaswa kuendelea kutendeana kwa fazili na upendo.

13. Yesu alifanya nini wakati mitume wake walikosana? (Matayo 20:25-28)

13 Wakati ile jambo ilitokea, Yesu alifanya nini? Hakukasirika. Hakusema kama atatafuta mitume wengine wenye kuwa na matendo ya muzuri zaidi, ni kusema, wanyenyekevu sana na wenye kila mara wangetendeana kwa upendo. Kuliko kufanya vile, alizungumuza nao kwa uvumilivu juu alijua kama walipenda kufanya mambo yenye kuwa sawa. (Soma Matayo 20:25-28.) Mitume walikuwa nakosana mara mingi juu ya kujua nani alikuwa mukubwa zaidi kati yao. Hata vile, Yesu aliendelea kuwatendea kwa upendo.​—Mk. 9:34; Lu. 22:24.

14. Mitume wa Yesu walikomalia mu hali gani?

14 Bila shaka Yesu alijua kama mitume wake walikomalia mu hali na fasi tofauti. (Yoh. 2:24, 25) Walikomalia fasi kwenye viongozi wa dini walikuwa nafundisha kama ili mutu akuwe wa maana iliomba akuwe na madaraka makubwa. (Mt. 23:6) Viongozi wa dini walijiona pia kuwa wa maana sana kupita wengine. f (Lu. 18:9-12) Yesu alielewa kama juu mitume wake walikomalia mu hali za vile ile ingefanya wajione kuwa wa maana sana kuliko wengine. (Mez. 19:11) Hakutazamia kama wanafunzi wake hawatafanyaka makosa; njo maana aliwavumilia. Alijua kama walipenda kufanya mambo ya muzuri. Kwa hiyo, aliwasaidia ili wakuwe wanyenyekevu na wapende wengine kuliko kujiona kuwa wa maana zaidi.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUIGA MUFANO WA YESU?

15. Mambo yenye ilitokea kuhusu Yakobo na Yohana, inaweza kutufundisha nini?

15 Mambo yenye ilitokea kuhusu Yakobo na Yohana, inaweza kutufundisha mambo fulani. Hawakufanya muzuri kumuomba Yesu awapatie madaraka ya maana mu Ufalme. Na mitume wengine pia hawakufanya muzuri kuacha ile hali iharibishe umoja wao. Lakini, Yesu alitendea mitume wote 12 kwa upendo na fazili. Ile inatufundisha nini? Tumejifunza kama shida haiko tu juu wengine wanatukosea, lakini pia namna yetu ya kutenda wakati wanatukosea. Nini njo inaweza kutusaidia? Wakati Mukristo mwenzetu anatukosea, ni muzuri kujiuliza hivi: ‘Juu ya nini jambo yenye alifanya ilinikasirisha sana? Ile inaonyesha kama niko na tabia fulani ya mubaya yenye napaswa kufanyia mabadiliko? Inawezekana ule mwenye ananikosea iko na magumu fulani? Hata kama naona kuwa niko na sababu ya kukasirika, naweza kuonyesha kama namupenda kabisa kwa kuwa tayari kumusamehe?’ Wakati tunapendana, tunaonyesha kama tuko wanafunzi wa kweli wa Yesu.

16. Mufano wa Yesu unaweza kutufundisha jambo gani ingine?

16 Mufano wa Yesu unatufundisha pia kama tunapaswa kujikaza kuelewa waamini wenzetu. (Mez. 20:5) Bila shaka, Yesu iko na uwezo wa kujua mambo yenye kuwa mu mioyo ya watu; siye hatuna ule uwezo. Lakini, tunaweza kuvumilia ndugu na dada zetu wakati wanatukosea. (Efe. 4:1, 2; 1 Pe. 3:8) Ni mwepesi kufanya vile kama tunajua muzuri hali yao na fasi kwenye walikomalia. Tufikirie mufano fulani.

17. Mwangalizi fulani wa muzunguko alipata faida gani juu alipenda kujua muzuri zaidi muamini mwenzake?

17 Mwangalizi fulani wa muzunguko mwenye alikuwa natumikia mu Afrika ya Mashariki anakumbuka ndugu fulani. Ku mwanzo, ule mwangalizi alikuwa nawaza kama ule ndugu hakukuwa mwenye fazili. Ule mwangalizi wa muzunguko alifanya nini? Anasema hivi: “Kuliko kumuepuka, nilipenda kumujua muzuri zaidi.” Kwa kufanya vile, ule mwangalizi alifikia kujua namna ule ndugu alikomala na namna ile ilikuwa na matokeo fulani mu namna yake ya kutendea wengine. Ule mwangalizi anasema tena hivi: “Wakati nilifikia kutambua namna ilikuwa nguvu kwa ule ndugu kufanya mabadiliko yenye alipenda kufanya, ni kusema, kuachana na namna ya kutenda ya watu wa fasi kwenye alikomalia, na wakati nilitambua kama tayari alikuwa alishabadilika, nilimufurahia sana. Tulifikia kuwa marafiki wa karibu.” Kusema kweli, wakati tunajikaza kuelewa ndugu na dada zetu, kila mara inakuwaka mwepesi kuwapenda.

18. Tunaweza kujiuliza maulizo gani wakati muamini mwenzetu anatukosea? (Mezali 26:20)

18 Wakati fulani, inaweza kuwa muzuri kuongea na muamini mwenzetu mwenye alitukosea. Kwanza, ni muzuri tujiulize hii maulizo: ‘Niko na habari zote?’ (Mez. 18:13) ‘Inawezekana hakunikosea kimakusudi?’ (Muh. 7:20) ‘Na miye siyakoseaka mutu fulani vile?’ (Muh. 7:21, 22) ‘Kama nazungumuza na ule mutu mwenye alinikosea, ile itafanya mambo iharibike tena zaidi?’ (Soma Mezali 26:20.) Kama tunakamata wakati ya kujiuliza ile maulizo, upendo unaweza kutuchochea kusamehe wengine wakati wanatukosea.

19. Unaazimia kufanya nini?

19 Wakiwa kikundi, Mashahidi wa Yehova wanaonyesha kama ni wanafunzi wa kweli wa Yesu kupitia upendo wenye kuwa kati yao. Kila mumoja wetu anaonyesha kama ni mwanafunzi wa kweli wa Yesu kwa kuonyesha ndugu na dada zake upendo wa kweli ijapokuwa makosa ao uzaifu wao. Kama tunafanya vile, tunaweza kusaidia wengine watambue dini ya kweli na wajiunge na siye ili kumuabudu Yehova, Mungu wa upendo. Kwa hiyo basi, tuazimie kuendelea kupendana juu upendo ni alama yenye kutambulisha Wakristo wa kweli.

WIMBO 17 “Ninataka”

a Upendo wenye kuwa kati yetu unafanyaka watu wengi wapende kujifunza kweli. Lakini, juu hatukamilike, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kwetu kupenda waamini wenzetu. Tuzungumuzie basi, juu ya nini upendo ni sifa ya maana sana na namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yesu wakati ndugu na dada zetu wanafanya makosa.

c Ona habari “Mwishowe, maisha yangu yana kusudi,” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 11, 2012, uku. 13-14.

d Ona habari “Maisha yangu ilionekana kuwa ya muzuri,” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2012, uku. 18-19.

e Mu hii habari hatuzungumuzie zambi nzito zenye zinapaswa kushugulikiwa na wazee, sawa zile zenye kutajwa mu 1 Wakorinto 6:9, 10.

f Imeripotiwa kama, kisha wakati murefu kupita, kiongozi fulani Muyahudi alisema hivi: “Mu dunia muko wanaume makumi tatu ao zaidi wenye haki sawa vile Abrahamu. Kama wako makumi tatu, miye na mutoto wangu mwanaume tuko kati yao; kama wako kumi, miye na mutoto wangu mwanaume tuko kati yao; kama wako tano, miye na mutoto wangu mwanaume tuko kati yao; kama ni wawili, ni miye na mutoto wangu mwanaume; lakini kama muko tu moya, ni miye.”