Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Juu ya nini mwanaume mwenye kuitwa “Fulani wa fulani” alisema kama ikiwa anamuoa Rutu ‘angeharibu’ uriti wake mwenyewe? (Rut. 4:1, 6)

Zamani, kama mwanaume anaoa na anakufa bila kuacha watoto, kulikuwa maulizo fulani yenye ilipaswa kujibiwa: Shamba yake ingekuwa ya nani? Jina ya familia yake ingepotea milele? Sheria ya Musa ilisaidia kupata majibu ya ile maulizo.

Ikiwa mutu fulani mwenye alikuwa na shamba anakufa, ndugu yake ao mutu fulani wa jamaa yake ya karibu angeiriti. Ao kama mutu fulani anakuwa maskini na anauzisha shamba yake, ndugu yake ao mutu fulani wa jamaa yake ya karibu angeikomboa. Ile njo ingesaidia familia iendelee kubakia na ile shamba.​—Law. 25:23-28; Hes. 27:8-11.

Walikuwa nafanya nini juu jina ya familia ya mutu mwenye alikufa isipotee? Ndugu ya ule mwenye alikufa alipaswa kuoa ule mujane mwenye angebakia; na ni vile njo ilikuwa mu hali ya Rutu. Kwa kawaida ndugu ya ule mwenye alikufa, alipaswa kuoa mujane mwenye alibakia juu azale naye mutoto mwenye angekamata jina ya ule mwenye alikufa na kuriti mali yake. Ule mupango wa upendo ulikuwa pia namna ya kuhangaikia wajane.​—Kum. 25:5-7; Mt. 22:23-28.

Fikiria mufano wa Naomi. Aliolewa na mwanaume mwenye kuitwa Elimeleki. Wakati Elimeleki na watoto wao wawili wanaume walikufa, Naomi alibakia bila mukombozi wa kumuhangaikia. (Rut. 1:1-5) Kisha kurudia Yuda, Naomi aliambia Rutu, binti-mukwe wake, aambie Boazi akomboe shamba yao. Boazi alikuwa mutu wa karibu wa jamaa ya Elimeleki. (Rut. 2:1, 19, 20; 3:1-4) Lakini, Boazi alijua kama kulikuwa mutu mwingine mwenye alikuwa wa karibu sana, mwenye Biblia inaita “Fulani wa fulani.” Ule mutu njo alikuwa na haki ya kwanza ya kuamua kama atapenda kuwa mukombozi ao hapana.​—Rut. 3:9, 12, 13.

Ku mwanzo, “Fulani wa fulani” alikuwa tayari kuwa mukombozi. (Rut. 4:1-4) Allijua kama alipaswa kutumia makuta yake juu ya kuuza ile shamba; na alijua pia kama Naomi alikuwa alishazeeka. Kwa hiyo, hangezala mutoto mwenye angeriti shamba ya Elimeleki. Kusema kweli, ile shamba ingefikia kuwa ya Fulani wa fulani na ingekuwa sehemu ya uriti wake. Pengine ile ingemuleteaka utajiri.

Lakini, Fulani wa fulani hakupenda tena kukomboa ile shamba juu aliona kama ingeomba amuoe Rutu. Alisema hivi: “Sitaweza kulikomboa, kusudi nisiharibu uriti wangu mwenyewe.” (Rut. 4:5, 6) Juu ya nini alibadilisha mawazo yake?

Kama Fulani wa fulani ao mtu mwingine angemuoa Rutu na kuzala naye mutoto mwanaume, ule mutoto njo angeriti shamba ya Elimeleki. Namna gani ile ‘ingeharibu’ “uriti” wa Fulani wa fulani? Biblia haiseme jambo fulani juu ya ile; lakini, pengine ni juu ya hii mambo.

  • Kwanza, inaonekana angepoteza makuta yake bure kwa kuuza shamba ya Elimeleki, juu haingekuwa yake; ingekuwa ya mutoto wa Rutu.

  • Pili, angekuwa na daraka ya kulisha na kuhangaikia Naomi na Rutu.

  • Tatu, kama Rutu angezala watoto wengine na Fulani wa fulani, wale watoto wangegawanyana ule uriti na watoto wowote wenye ule Fulani wa fulani angekuwa nao.

  • Ine, kama Fulani wa fulani hakukuwa na watoto wengine, mutoto mwenye Rutu angezala njo mwenye angekuwa na haki ya kuriti shamba ya Elimeleki na shamba ya Fulani wa fulani. Kwa hiyo, kisha Fulani wa fulani kufa, shamba yake ingekuwa ya mutoto mwenye angekuwa na jina ya Elimeleki, hapana ya ule mwenye angekuwa na jina yake. Fulani wa fulani hakukuwa tayari kuharibu uriti wake juu ya kusaidia Naomi. Aliona kama ni muzuri aachie mukombozi mwenye alikuwa na haki ya pili, ni kusema Boazi, akamate ile daraka. Boazi alikubali kufanya vile juu alipenda “kurudisha jina la ule mwanaume mwenye amekwisha kufa katika uriti wake.”​—Rut. 4:10.

Inawezekana Fulani wa fulani alipenda sana kufanya jina na uriti wake visipotee. Alijipenda sana yeye mwenyewe. Hata kama alifanya yake yote juu ya kufanya jina yake isipotee, mupaka leo jina yake haijulikane. Hakupata pia pendeleo ya pekee yenye Boazi alipata, ni kusema, kuwa kati ya mababu wa Masiya, Yesu Kristo. Ni jambo ya kuhuzunisha kuona kama Fulani wa fulani alipata matokeo ya mubaya juu, kwa kujipenda yeye mwenyewe, alikatala kusaidia mutu mwenye alikuwa mu uhitaji!​—Mt. 1:5; Lu. 3:23, 32.