Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

Mufundishe Watoto Wenu juu ya Yehova Kupitia Uumbaji

Mufundishe Watoto Wenu juu ya Yehova Kupitia Uumbaji

“Ni nani ameumba vitu hivi?”​—ISA. 40:26.

WIMBO 11 Uumbaji Unamusifu Mungu

KIFUPI YA HABARI a

1. Wazazi wanapendaka kabisa kufanyia watoto wao nini?

 WAZAZI, tunajua kama munapendaka kabisa kusaidia watoto wenu wafikie kumujua Yehova na kumupenda. Sasa, vile Yehova haonekanake, namna gani munaweza kusaidia watoto wenu waone kama Yehova ni mutu mwenye iko kabisa? Na namna gani munaweza kuwasaidia wamukaribie?​—Yak. 4:8.

2. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kufundisha watoto wao juu ya sifa za Yehova?

2 Kujifunza Biblia na watoto njo njia ya muzuri ya kuwasaidia wamukaribie Yehova. (2 Ti. 3:14-17) Lakini, Biblia inaonyesha njia ingine yenye inaweza kusaidia vijana wajifunze juu ya Yehova. Mu kitabu ya Mezali, baba fulani anakumbusha mutoto wake mwanaume asisahau sifa za Yehova zenye zinaonekana kupitia uumbaji. (Mez. 3:19-21) Tutazungumuzia mambo mbalimbali yenye wazazi wanaweza kufanya ili kufundisha watoto wao juu ya sifa za Yehova kupitia uumbaji.

NAMNA GANI UNAWEZA KUFUNDISHA WATOTO WAKO KUPITIA UUMBAJI?

3. Wazazi wanaweza kusaidia namna gani watoto wao?

3 Biblia inasema kama “Sifa zake [Mungu] zenye hazionekane zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaonekana kupitia vitu vyenye vilifanywa.” (Ro. 1:20) Wazazi, pengine munapendaka kuenda na watoto wenu fasi ingine juu ya kupitisha nao wakati. Mutumie ile nafasi ili kuwasaidia waone uhusiano wenye uko kati ya “vitu vyenye vilifanywa” na sifa za muzuri za Yehova. Kwa hiyo, tuone basi mambo yenye wazazi wanaweza kujifunza kupitia njia ya Yesu ya kufundisha.

4. Yesu alifanya nini ili kufundisha wanafunzi wake kupitia uumbaji? (Luka 12:24, 27-30)

4 Ona namna Yesu alifundisha kupitia uumbaji. Siku moya, aliambia wanafunzi wake waangalie kunguru na maua ya mayungiyungi. (Soma Luka 12:24, 27-30.) Yesu angetumiaka munyama ao mumea wowote, lakini, alichagua kutumia mufano wa ndege na maua yenye wanafunzi wake walijua muzuri. Inawezekana wanafunzi wake walikuwa naona kunguru wanaruka na pia maua ya shamba yenye kupendeza. Wazia Yesu iko nawaonyesha vile vitu wakati iko nasema. Alifanya nini kisha kuzungumuzia ile mifano? Alifundisha wanafunzi wake hii somo ya maana kuhusu ukarimu na fazili ya Baba yao wa mbinguni: Yehova atalisha na kuvalisha watumishi wake waaminifu sawa vile anafanyaka kuhusu kunguru na maua ya shamba.

5. Ni vitu gani vyenye Mungu aliumba vyenye muzazi anaweza kutumia ili kufundisha mutoto wake juu ya Yehova?

5 Wazazi, mutafanya nini juu ya kuiga njia ya Yesu ya kufundusha? Unaweza kumuambia mutoto wako kuhusu kitu moya yenye Mungu aliumba yenye unapendaka sana, sawa vile munyama ao mumea fulani. Wakati uko nafanya vile, umufasirie mambo yenye ule mufano unatufundisha juu ya Yehova. Kisha, unaweza kumuuliza mutoto wako akuambie pia ni munyama ao mumea gani wenye anapendaka sana. Pengine atakusikiliza kwa uangalifu zaidi wakati uko nazungumuzia sifa za Yehova kwa kutumia kitu fulani yenye anapendaka sana yenye Yehova aliumba.

6. Mambo yenye mama ya Christopher alifanya inaweza kutufundisha nini?

6 Inaomba muzazi atumie wakati mingi juu ya kutafuta munyama ao mumea fulani mbele aonyeshe mutoto wake mambo yenye ile inafundisha juu ya Yehova? Haiko lazima kabisa. Yesu hakuleta mafasirio ya murefu juu ya namna kunguru wanakulaka na namna maua ya mayunginyungi inakomalaka. Kusema kweli, wakati fulani mutoto wako anaweza kufurahia kujifunza mambo mbalimbali juu ya uumbaji, lakini wakati fulani inaomba tu mafasirio ya mufupi ao ulizo fulani juu aelewe jambo yenye unapenda kumufundisha. Ndugu mwenye kuitwa Christopher anakumbuka mambo yenye alijioneaka wakati alikuwa mutoto. Anasema hivi: “Mama yangu alikuwa naleta tu mafasirio ya mufupi juu ya kutusaidia tufurahie uumbaji. Kwa mufano, wakati tulikuwa karibu na milima alikuwa nasema hivi: ‘Muone ukubwa na uzuri wa ile milima! Hamuone kama Yehova ni wa ajabu sana?’ Ao wakati tulikuwa karibu na bahari, alikuwa nasema hivi: ‘Muone nguvu ya ile mawimbi ya bahari! Hamuone kama Mungu iko na nguvu?’” Christopher anasema hivi: “Ile mafasirio ya mwepesi tena ya maana ilikuwa natusaidia tufikiri.”

7. Unaweza kufanya nini ili kuzoeza watoto wako wakuwe nafikiri juu ya uumbaji?

7 Wakati watoto wako wako nakomala unaweza kuwazoeza waanze kufikiri sana juu ya uumbaji na kujifunza juu ya Yehova. Unaweza tu kuzungumuzia kitu fulani yenye Mungu aliumba na kuwauliza hivi: “Ile inawafundisha nini juu ya Yehova?” Wanaweza kukutolea majibu yenye pengine inaweza kukushangaza na kukufurahisha.​—Mt. 21:16.

NI WAKATI GANI UNAWEZA KUFUNDISHA WATOTO WAKO KUPITIA UUMBAJI?

8. Wakati wazazi Waisraeli walikuwa natembea “katika barabara,” walikuwa na nafasi ya kufanya nini?

8 Yehova aliambia wazazi Waisraeli wafundishe watoto wao amri zake wakati wako natembea “katika barabara.” (Kum. 11:19) Mu vijiji vya Israeli mulikuwa barabara mingi. Ilikuwa mwepesi kuona wanyama, ndege, na maua mbalimbali. Wakati Waisraeli walikuwa natembea katika barabara, wazazi walikuwa na nafasi ya kufundisha watoto wao juu ya vitu vyenye Yehova aliumba. Wazazi, muko pia na nafasi ya kufundisha watoto wenu kupitia uumbaji. Tuzungumuzie namna wazazi fulani walifanya vile.

9. Mufano wa Punitha na Katya unakufundisha nini?

9 Mama fulani mwenye kuitwa Punitha, mwenye anaishi mu muji mukubwa wa India, ansema hivi: “Wakati tunaendaka kuangalia familia mu vijiji, tunatumiaka ile nafasi ili kusaidia watoto wetu wajifunze juu ya vitu vya muzuri vyenye Yehova aliumba. Naona kama watoto wangu wanaelewaka muzuri zaidi uumbaji wakati hawako mu muji mwenye muko watu wengi na magari mingi.” Wazazi, pengine watoto wenu hawawezi kusahau hata kidogo wakati ya muzuri yenye munapitisha nao fasi ya muzuri. Katya, dada fulani wa mu Moldova, anasema hivi: “Mambo ya muzuri yenye niko nakumbuka, ni kupitisha wakati pamoya na wazazi wangu mu kijiji wakati nilikuwa mutoto. Nawashukuru sana juu walinifundishaka tangu utoto kutua na kuchunguza kwa uangalifu vitu vyenye Yehova aliumba na kujifunza juu yake kupitia uumbaji.”

Hata kama unaishi mu muji, unaweza kupata vitu vyenye Yehova aliumba, vyenye unaweza kutumia ili kufundisha watoto wako juu yake (Ona fungu ya 10)

10. Wazazi wanaweza kufanya nini kama ni nguvu kwao kuenda mu kijiji? (Ona kisanduku “ Musaada kwa Ajili ya Wazazi.”)

10 Tuseme nini kama ni nguvu kwako kuenda mu kijiji? Amol, mwenye anaishi pia mu India, anasema hivi: “Kwenye naishi, wazazi wanatumikaka saa mingi, na inaomba makuta mingi juu mutu aende mu kijiji. Lakini, unaweza kuona uumbaji wa Yehova na kuzungumuzia sifa zake hata wakati uko mu bustani ya kidogo ao wakati uko inje ya jengo fulani.” Kama unaangalia kwa uangalifu, unaweza pia kuona karibu na kwako vitu mingi vyenye Yehova aliumba vyenye unaweza kuonyesha watoto wako. (Zb. 104:24) Pengine unaweza kuona ndege, vidudu, mimea, na vitu vingine. Karina wa Alemanye anasema hivi: “Mama yangu anapendaka maua, kwa hiyo, wakati nilikuwa mutoto alikuwa nanionyesha maua ya muzuri kila mara wakati nilikuwa natembea naye.” Wazazi, munaweza pia kufundisha watoto wenu kupitia video na vichapo mingi vyenye vinazungumuzia uumbaji vyenye tengenezo yetu imetutolea. Hata kama munaishi wapi, munaweza kusaidia watoto wenu wachunguze kwa uangalifu vitu vyenye Mungu aliumba. Sasa, tuzungumuzie sifa fulani za Yehova zenye munaweza kufundisha watoto wenu.

‘SIFA ZA YEHOVA ZENYE HAZIONEKANE ZINAONEKANA WAZIWAZI’

11. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao wajue kama Yehova iko na upendo?

11 Juu ya kusaidia watoto wako wajue kama Yehova iko na upendo, unaweza kuzungumuzia namna wanyama wengi wanafanyaka ili kuhangaikia watoto wao kwa upendo. (Mt. 23:37) Unaweza kuzungumuzia pia vitu mbalimbali vya muzuri vyenye Yehova aliumba vyenye tunafurahiaka. Karina mwenye tulishataya, anasema hivi: “Wakati tulikuwa naenda kutembea na mama yangu, alikuwa naniambia nitue na nichunguze kwa uangalifu namna kila liua ilikuwa tofauti na ingine na namna uzuri wake ulionyesha kama Yehova iko na upendo. Kisha miaka fulani, niliendelea kuchunguza kwa uangalifu maua na niliona kama kila liua ilikuwa na rangi yake na ilikuwa tofauti na ingine. Ile yote inanikumbusha kama Yehova anatupendaka sana.”

Unaweza kuzungumuzia namna Yehova aliumba mwili wetu mu njia ya ajabu ili kufundisha watoto wako wajue kama iko na hekima (Ona fungu ya 12)

12. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao wajue kama Mungu iko na hekima? (Zaburi 139:14) (Ona pia picha.)

12 Usaidie watoto wako wajue kama Mungu iko na hekima. Yehova iko na hekima mingi sana kuliko siye. (Ro. 11:33) Kwa mufano, unaweza kuambia mutoto wako namna maji inapandaka na kufanya mawingu na namna ile mawingu inafanyaka maji iende huku na huku kwa wepesi. (Yob. 38:36, 37) Unaweza pia kumuonyesha namna Mungu aliumbaka mwili wa mwanadamu mu njia ya ajabu. (Soma Zaburi 139:14.) Ona namna baba mwenye kuitwa Vladimir alifanya vile. Anasema hivi: “Siku moya mutoto wetu mwanaume alianguka na kinga yake na kujiumiza. Kisha siku kidogo ile kidonda ilipona. Miye na bibi yangu tulimufasiria kama Yehova aliumba mwili wetu na uwezo wa kujitunza. Tulimuonyesha kama kati ya vitu vyote vyenye mwanadamu alifanya hakuna kitu yenye kuwa sawa vile mwili wa mwanadamu. Kwa mufano, kisha kufanya aksida gari haiwezi kujitengeneza. Ile ilisaidia mutoto wetu aelewe kama Yehova iko na hekima.”

13. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao wajue kama Mungu iko na nguvu? (Isaya 40:26)

13 Yehova anatuomba tuinue macho yetu mbinguni na kufikiria namna nguvu yake ya ajabu imefanya nyota zote zikuwe fasi moya. (Soma Isaya 40:26.) Unaweza kuambia mutoto wako aangalie mu anga na afikiri juu ya mambo yenye anaona. Tingting, dada wa Taiwan, anakumbuka jambo fulani yenye ilitokeaka wakati alikuwa mutoto. Anasema hivi: “Siku moya tuliendaka na mama yangu mu kijiji, na kule tuliona nyota mingi mu anga juu mwangaza haikukuwa mingi, sawa vile mu muji. Na ni mu ile kipindi njo nilikuwa najiuliza kama ningefanya nini ili niendelee kuwa muaminifu kwa Yehova juu wanafunzi wenzangu walijaribu kunikaza niache kumutumikia. Mama yangu aliniambia nifikiri kuhusu nguvu yenye Yehova alitumia juu ya kuumba zile nyota zote, na alinikumbusha kama Mungu atatumia nguvu ileile juu ya kunisaidia nipambane na jaribu yoyote. Kuchunguza kwa uangalifu uumbaji, fasi kwenye tulienda, kulinichochea kumujua Yehova muzuri zaidi na kuazimia kuendelea kumutumikia.”

14. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kufundisha watoto wao kupitia uumbaji juu waone kama Yehova ni Mungu mwenye furaha?

14 Vitu vyenye Yehova aliumba vinaonyesha kama iko na furaha na anapenda na siye pia tukuwe na furaha. Kisha kufanya uchunguzi, wanasayansi wamevumbula kama wanyama wengi wanachezaka. Ndege na samaki pia wanachezaka. (Yob. 40:20) Watoto wako walishakacheka wakati waliona munyama fulani iko nacheza? Pengine walishakaona pusi iko nacheza na kabumbu ya uzi, imbwa wako nacheza kwa kurukiana juu waangushane. Siku ingine yenye utaona watoto wako wako nacheka juu wako naangalia mambo ya kuchekesha yenye munyama fulani iko nafanya, hauone kama ni nafasi ya muzuri ya kuwakumbusha kama tuko natumikia Mungu mwenye furaha?​—1 Ti. 1:11.

MUFURAHIE UUMBAJI WA YEHOVA MU FAMILIA

Muzazi, mutoto wako anaweza kuona kama ni mwepesi kukuambia mambo yenye iko namuhangaisha kama muko naangalia uumbaji pamoya naye (Ona fungu ya 15)

15. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kujua mawazo ya watoto wao? (Mezali 20:5) (Ona pia picha.)

15 Wakati fulani, inaweza kuwa nguvu kwa wazazi kujua magumu yenye watoto wako nayo. Kama ile njo hali yako, ni muzuri ujikaze sana ili kujua mawazo yao. (Soma Mezali 20:5.) Wazazi fulani wanaona kama ni mwepesi kufanya vile wakati wako naangalia uumbaji pamoya na watoto wao. Juu ya nini? Kwanza, ni juu ile wakati hakukuwake mambo mingi ya kukengeusha wazazi na watoto. Masahiko, baba fulani wa mu Taiwan, anaonyesha sababu ya pili. Anasema hivi: “Kupitisha wakati pamoya na watoto wetu fasi ingine, kupanda milima ao kutembea pembeni ya plage ni mambo yenye inawafurahishaka sana. Tunaonaka kama inakuwaka mwepesi zaidi kujua mawazo yao ile wakati.” Katya, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Mara mingi mama yangu alikuwa nanipeleka ku bustani ya muzuri kisha masomo. Ku ile fasi ya kimya, ilikuwa mwepesi kuambia mama yangu mambo yenye ilitokea ku masomo ao mambo yenye ilikuwa nanihangaisha.”

16. Familia zinaweza kufanya nini juu ya kujifurahisha kupitia uumbaji?

16 Kuangalia vitu vyenye Yehova aliumba kunaweza kusaidia pia watu wa familia wajifurahishe. Ile itawasaidia wapendane zaidi. Biblia inasema kama kuko “wakati wa kucheka” na “wakati wa kuruka-ruka.” (Muh. 3:1, 4, maelezo ya chini) Kati ya mambo yote yenye Yehova aliumba, aliumba pia fasi mbalimbali za muzuri hapa ku dunia kwenye tunaweza kufanya mambo yenye tunapendaka. Familia mingi zinapendaka kuenda pamoya fasi fulani juu ya kuangalia uumbaji, sawa vile mu vijiji, ku milima ao ku plage. Watoto fulani wanapendaka kukimbia na kucheza mu bustani, kuangalia wanyama ao kuogelea mu muto, mu ziwa, ao mu bahari. Tuko na nafasi mingi za kufurahia vitu vyenye Yehova aliumba.

17. Juu ya nini wazazi wanapaswa kusaidia watoto wao wafurahie uumbaji?

17 Mu dunia mupya, wazazi na watoto watafurahia uumbaji kupita vile wanaufurahiaka leo. Tofauti na leo, hatutaogopa wanyama; nao pia hawatatuogopa. (Isa. 11:6-9) Tutafurahia milele mambo yenye Yehova aliumba. (Zb. 22:26) Lakini wazazi, musingoye dunia mupya ifike njo muanze kusaidia watoto wenu wafurahie uumbaji. Wakati munafundisha watoto wenu juu ya Yehova kupitia uumbaji, pengine watakubaliana na maneno ya Mufalme Daudi mwenye alisema hivi: “Ee Yehova, hakuna kazi zenye kuwa kama kazi zako.”​—Zb. 86:8.

WIMBO 134 Watoto Ni Zawadi Yenye Mungu Anatupatia

a Ndugu na dada wengi wanakumbukaka wakati ya muzuri yenye walipitisha pamoya na wazazi wao Wakristo na wako nafurahia uumbaji. Wanaendelea kukumbuka namna wazazi wao walitumia ile nafasi ili kuwafundisha juu ya sifa za Yehova. Kama uko na watoto, namna gani unaweza kuwafundisha juu ya sifa za Mungu kupitia uumbaji? Hii habari itajibia ile ulizo.