Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

Namna ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Ubatizo

Namna ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Ubatizo

“Ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?”​—MDO. 8:36.

WIMBO 50 Sala Yangu ya Kujitoa kwa Mungu

KIFUPI YA HABARI a

Mu dunia yote, vijana na wazee wako nafanya maendeleo na wanafikia kubatizwa (Ona fungu ya 1-2)

1-2. Kama hauyakuwa tayari kwa ajili ya ubatizo, juu ya nini haupaswe kuvunjika moyo? (Ona picha ku jalada.)

 KAMA unapenda kubatizwa, ni kusema, ulishajiwekea muradi wa muzuri sana. Uko tayari kubatizwa sasa hivi? Ikiwa unawaza kama uko tayari na kama wazee pia wanakubali, basi usiogope kubatizwa ku mukusanyiko wenye utafuata. Kama unafanya vile, Yehova atakubariki wakati uko namutumikia.

2 Kwa upande mwingine, kuko mutu alishakakuambia kama inaomba ubadilishe mambo fulani mbele ufikie kubatizwa? Ao ulijionea vile weye mwenyewe? Kama ni vile, usivunjike moyo juu unaweza kufanya maendeleo ili kufikia kubatizwa, ikuwe uko kijana ao muzee.

“NI KITU GANI KINANIZUIA?”

3. Ofisa fulani Mwetiopia alimuuliza Filipo nini, na ile inatokeza ulizo gani? (Matendo 8:36, 38)

3 Soma Matendo 8:36, 38. Ofisa fulani Mwetiopia alimuuliza hivi Filipo mweneza-injili: “Ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?” Ule mwanaume Mwetiopia alipenda kubatizwa, lakini alikuwa tayari kabisa?

Ule ofisa Mwetiopia alipenda kuendelea kujifunza juu ya Yehova (Ona fungu ya 4)

4. Nini njo inaonyesha kama ule mwanaume Mwetiopia alipenda kuendelea kujifunza?

4 Ule mwanaume Mwetiopia “alikuwa ameenda Yerusalemu kuabudu.” (Mdo. 8:27) Kwa hiyo, inawezekana alikuwa Muyahudi mugeuzwa-imani na alikuwa mu dini ya Kiyahudi. Bila shaka, maandishi matakatifu ya Maandiko ya Kiebrania njo ilimusaidiaka ajifunze juu ya Yehova. Lakini alikuwa napenda kujifunza mambo mingi zaidi. Sasa wakati Filipo alikutana naye mu barabara, alimukuta iko nafanya nini? Alikuwa nasoma maandishi yenye ilikuwa mu kitabu ya kukunjwa ya nabii Isaya. (Mdo. 8:28) Ile ilikuwa mafundisho mazito ya Biblia. Ule ofisa hakutosheka tu na kujifunza mafundisho fulani ya musingi, alipenda pia kuendelea kujifunza.

5. Ule Mwetiopia alifanya nini na mambo yenye alijifunza?

5 Ule mwanaume alikuwa ofisa mukubwa mwenye alikuwa na mamlaka chini ya Kandake Malkia wa Waetiopia; “alikuwa anasimamia hazina yote ya malkia.” (Mdo. 8:27) Inawezekana alikuwa na madaraka mingi na mambo mingi ya kufanya. Lakini alipanga wakati ya kumuabudu Yehova. Hakutosheka tu na kujifunza kweli, alikuwa pia natumikisha mambo yenye alijifunza. Kwa hiyo, alitoka Etiopia na kuenda Yerusalemu ili kumuabudu Yehova ku hekalu. Inawezekana ile safari iliomba wakati na makuta mingi, hata vile alienda tu juu alipenda kumuabudu Yehova.

6-7. Ule Mwetiopia alifanya nini ili kuonyesha kama alimupenda sana Yehova?

6 Filipo njo alifundisha ule Mwetiopia kweli fulani za maana za mupya na alimufundisha pia kama Yesu njo Masiya. (Mdo. 8:34, 35) Ule ofisa mukubwa alifurahi sana wakati alijifunza kuhusu mambo yenye Yesu alimufanyia. Alitenda namna gani? Pengine angebakia tu vile alikuwaka, ni kusema, Muyahudi mugeuzwa-imani mwenye kuheshimiwa. Lakini, alifikia kupenda sana Yehova na Mwana wake. Kwa hiyo, alikamata uamuzi wa maana wa kubatizwa na kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo. Filipo aliona kama ule mwanaume alikuwa tayari kwa ajili ya ubatizo, njo maana alimubatiza.

7 Kama unafuata mufano wa ule Mwetiopia unaweza kujua namna ya kujitayarisha kwa ajili ya ubatizo. Weye pia utasema hivi kwa uhakika: “Ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?” Tuzungumuzie sasa namna unaweza kufuata mufano wa ule Mwetiopia mwenye alifanya mambo yenye kufuata: Aliendelea kujifunza, alitumikisha mambo yenye alijifunza, na alifikia kumupenda sana Yehova.

UENDELEE KUJIFUNZA

8. Kulingana na Yohana 17:3, unapaswa kufanya nini?

8 Soma Yohana 17:3. Maneno yenye Yesu alisema mu hii andiko ilikusaidia uamue kuanza kujifunza Biblia? Ile maneno ilisaidia wengi kati yetu. Lakini, ni lazima tuendelee kujifunza? Ndiyo. Hatutaacha hata kidogo ‘kufikia kumujua . . . Mungu wa pekee wa kweli.’ (Muh. 3:11; Yoh. 17:3, maelezo ya chini) Tutaendelea kujifunza milele na milele. Kadiri tunajifunza, ni vile tutamukaribia Yehova zaidi.​—Zb. 73:28.

9. Tunapaswa kufanya nini kisha kujifunza mafundisho ya musingi ya Biblia?

9 Bila shaka, kujifunza juu ya Yehova kunaanzaka na mafundisho ya musingi. Mu barua yenye aliandikia Waebrania, mutume Paulo aliita ile mafundisho “mambo ya musingi.” Hakuzarau “fundisho la musingi;” alikuwa nailinganisha na maziwa yenye mutoto ananyonyaka. (Ebr. 5:12; 6:1) Kwa hiyo, aliambia pia Wakristo wasisimamie tu ku mafundisho ya musingi, lakini wajifunze pia mafundisho mazito ya Neno ya Mungu. Unapenda kujifunza mafundisho mazito ya Biblia? Unapenda kufanya maendeleo na kuendelea kujifunza juu ya Yehova na makusudi yake?

10. Juu ya nini watu fulani wanaona kama ni nguvu kujifunza?

10 Watu wengi wanaona kama ni nguvu kujifunza. Inakuwaka pia vile kwako? Wakati ulikuwaka ku masomo ulijuaka kusoma na kujifunza muzuri? Ulikuwaka nafurahia kujifunza mambo mingi? Ao ulifikiaka kuona kama haujue kujifunza muzuri mambo fulani yenye kuwa mu vitabu? Kama ni vile, hauko weye peke. Lakini ujue kama Yehova anaweza kukusaidia. Yeye ni Mwalimu mwenye kukamilika na muzuri sana, hakuna mwenye anamupita.

11. Yehova anafanyaka nini ili kuonyesha kama ni ‘Mufundishaji Mukubwa’?

11 Yehova anajiita “Mufundishaji wako Mukubwa.” (Isa. 30:20, 21) Ni Mwalimu mwenye uvumilivu, mwenye fazili, na mwenye anatuelewa. Anatafutaka mambo ya muzuri kwa wanafunzi wake. (Zb. 130:3) Hatazamiake hata kidogo tufanye mambo yenye inapita uwezo wetu. Kumbuka kama aliumba ubongo wako wenye ni zawadi ya muzuri sana. (Zb. 139:14) Kwa kawaida tunapendaka kujifunza. Muumbaji wetu anapenda tuendelee kujifunza milele na tufurahie kufanya vile. Kwa hiyo, ni jambo ya hekima ‘kukomalisha tamaa’ ya kujifunza kweli za Biblia sasa. (1 Pe. 2:2) Ujiwekee miradi yenye unaweza kufikia na ukuwe nasoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida. (Yos. 1:8) Kama unafanya vile, Yehova atakusaidia ufurahie kusoma na kujifunza zaidi juu yake.

12. Juu ya nini tunapaswa kufikiri sana juu ya maisha na utumishi wa Yesu wakati ya funzo yetu ya pekee?

12 Ukuwe nafikiri sana kwa ukawaida juu ya maisha na utumishi wa Yesu. Kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu njo jambo yenye itatusaidia tuendelee kumutumikia Yehova zaidi sana mu hii wakati yenye kuwa nguvu. (1 Pe. 2:21) Yesu aliambia wanafunzi wake waziwazi magumu yenye wangepata. (Lu. 14:27, 28) Hata vile, alikuwa hakika kama wanafunzi wake wa kweli wataendelea kuwa waaminifu kama vile yeye. (Yoh. 16:33) Ujifunze mambo mbalimbali juu ya maisha ya Yesu na ujiwekee muradi wa kumuiga mu maisha yako ya kila siku.

13. Unapaswa kuendelea kumuomba Yehova nini, na juu ya nini?

13 Kuwa na ujuzi haitoshe. Lakini, jambo yenye inafanya tukuwe na lazima ya ujuzi ni juu tujifunze mingi zaidi juu ya Yehova na juu tukomalishe sifa sawa vile upendo na imani. (1 Ko. 8:1-3) Wakati unaendelea kujifunza, uendelee kumuomba Yehova akusaidie ukuwe na imani zaidi. (Lu. 17:5) Anajibiaka sala za vile. Kama uko na imani yenye kutegemea ujuzi wa kweli juu ya Mungu, ile itakusaidia kufanya maendeleo.​—Yak. 2:26.

UENDELEE KUTUMIKISHA MAMBO YENYE UNAJIFUNZA

Mbele garika itokee, Noa na familia yake walitumikisha mambo yenye walijifunza (Ona fungu ya 14)

14. Mutume Petro alizungumuzia habari ya nani ili kuonyesha kama ni jambo ya maana kutumikisha mambo yenye tunajifunza? (Ona pia picha.)

14 Mutume Petro alionyesha kama ni jambo ya maana wanafunzi Wakristo waendelee kutumikisha mambo yenye wanajifunza. Alizungumuzia habari ya Noa. Yehova aliambia Noa kama ataharibu watu waovu wa mu ile wakati kupitia garika. Bila shaka, Noa na familia yake walijua kama garika itakuya, lakini kujua ile haikutosha juu waokoke. Hapa, mutume Petro alikuwa nazungumuzia kipindi ya mbele ya garika “wakati safina ilikuwa inajengwa.” (1 Pe. 3:20) Na Noa na familia yake walitumikisha mambo yenye Mungu aliwafundisha kwa kujenga safina, mashua kubwa. (Ebr. 11:7) Kisha, Petro alilinganisha kazi yenye Noa alifanya na ubatizo wakati aliandika hivi: “Ubatizo wenye unalingana na jambo hilo, unawaokoa ninyi sasa pia.” (1 Pe. 3:21) Mu njia fulani, tunaweza kulinganisha mambo yenye tuko nafanya kwa sasa ili kujitayarisha kwa ajili ya ubatizo na kazi yenye Noa na familia yake walifanya kwa miaka mingi ili kujenga safina. Unapaswa kufanya mambo gani ili ukuwe tayari kwa ajili ya ubatizo?

15. Kutubu kikweli maana yake nini?

15 Jambo ya kwanza yenye tunapaswa kufanya ni kutubu kikweli zambi zetu. (Mdo. 2:37, 38) Kutubu kikweli maana yake kufanya mabadiliko. Ulishaacha kufanya mambo yenye inamuchukiza Yehova, sawa vile mwenendo mubaya, kuvuta tumbako, ao kutumia maneno machafu? (1 Ko. 6:9, 10; 2 Ko. 7:1; Efe. 4:29) Kama hauyafanya vile, ujikaze kufanya mabadiliko. Ambia ule mwenye unajifunzaka naye Biblia ao wazee wa kutaniko wakusaidie na kukupatia muongozo. Kama uko kijana na ungali unaishi kwenu, ambia wazazi wako wakusaidie uachane na mwenendo mubaya wenye unaweza kukuzuia ubatizwe.

16. Kuwa na programu ya muzuri ya kiroho kunatia ndani nini?

16 Ni jambo ya maana pia kuwa na programu ya muzuri ya kiroho. Ile inatia ndani kuenda ku mikutano ya Kikristo na kuishiriki. (Ebr. 10:24, 25) Na kama unakuwa muhubiri, ukuwe nahubiri kwa ukawaida. Kama unafanya vile, utafurahia mahubiri. (2 Ti. 4:5) Ujiulize hivi: ‘Juu niende ku mikutano ao mu mahubiri inaombaka wazazi wangu wanikumbushe? Ao naendaka tu bila kukumbushwa?’ Kama unaendaka bila kukumbushwa, unaonyesha kama uko na imani na kama unamupenda Yehova Mungu. Tena, unaonyesha kama uko mwenye shukrani juu ya mambo yote yenye Yehova Mungu amekupatia. Ile njo “vitendo vya ushikamanifu kwa Mungu,” ni kusema, zawadi zenye unamupatia Yehova. (2 Pe. 3:11; Ebr. 13:15) Zawadi zote zenye tunamupatia Mungu bila kulazimishwa zinamufurahishaka. (Linganisha na 2 Wakorinto 9:7.) Tunafanyaka vile juu inatufurahishaka wakati tunamupatia Yehova yetu yote.      

UENDELEE KUMUPENDA SANA YEHOVA

17-18. Ni sifa gani njo itakusaidia ufanye maendeleo ili ufikie kubatizwa, na juu ya nini? (Mezali 3:3-6)

17 Wakati uko nafanya maendeleo ili kubatizwa, utapata magumu fulani. Watu fulani wanaweza kukuzarau juu ya mambo yenye unaamini kwa sasa, wanaweza hata kukupinga ao kukutesa. (2 Ti. 3:12) Pengine unajikaza kuachana na jambo fulani yenye unajua kama ni ya mubaya, lakini wakati fulani unaendelea kufanya ileile jambo. Ao pengine unaweza kuvunjika moyo na kuhangaika juu unawaza kama hautabadilikaka. Nini njo itakusaidia kuvumilia? Ni hii sifa ya maana: Upendo wako kwa Yehova.

18 Upendo wako kwa Yehova njo sifa ya maana sana. (Soma Mezali 3:3-6.) Kumupenda sana Yehova njo kutakusaidia usiache kumutumikia Yehova wakati unapata magumu. Mara mingi Biblia inazungumuzia kama Yehova anaonyeshaka watumishi wake upendo mushikamanifu. Ile inamaanisha kama hataacha watumishi wake ao hataacha kuwapenda. (Zb. 100:5) Mungu alikuumba kwa mufano wake. (Mwa. 1:26) Unaweza kufanya nini ili kuonyesha upendo wa vile?

Unaweza kumushukuru Yehova kila siku (Ona fungu ya 19) b

19. Unaweza kufanya nini ili kumushukuru sana Yehova juu ya mambo yote yenye alishakufanyia? (Wagalatia 2:20)

19 Kwanza, umushukuru Yehova. (1 Tes. 5:18) Kila siku ujiulize hivi: ‘Yehova alishanifanyia nini ili kuonyesha kama ananipenda?’ Tena mu sala zako usisahau kumushukuru Yehova kwa kutaya waziwazi mambo yenye alishakufanyia. Uelewe kama Yehova anakufanyia mambo ya muzuri juu anakupenda, sawa vile mutume Paulo alifikia kuelewa ile kumuhusu. (Soma Wagalatia 2:20.) Ujiulize hivi: ‘Napendaka pia kumuonyesha Yehova kama namupenda?’ Kumupenda Yehova kutakusaidia kupinga majaribu na kuvumilia magumu. Na ile itakuchochea uendelee kuheshimia programu yako ya kiroho na kumuonyesha Yehova kama unamupenda kila siku.

20. Kujitoa kwa Yehova kunatia ndani nini, na juu ya nini ule ni uamuzi wa maana sana?

20 Kisha, upendo wako kwa Yehova utakuchochea utoe sala ya pekee ya kujitoa kwake. Usisahau kama wakati unajitoa kwake unakuwa na hii tumaini ya muzuri: Unaweza kuwa mali ya Yehova milele. Wakati unatoa maisha yako kwa Yehova, unamuahidi kama utamutumikia wakati ya furaha na wakati ya magumu. Hautafanyaka tena ile ahadi. Kusema kweli, wakati tunajitoa kwa Yehova tunakamata hatua ya maana sana. Lakini fikiria hii jambo: Utakamata maamuzi mingi mu maisha yako, maamuzi fulani itakuwa ya muzuri sana, lakini, hautakamataka uamuzi wa muzuri sana kupita uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. (Zb. 50:14) Shetani atajaribu kukufanya uache kumupenda Baba yako Yehova na atatazamia kama utaacha kumutumikia. Lakini, usimuache Shetani apate ushindi! (Yob. 27:5) Juu unamupenda sana Yehova, Baba yako wa mbinguni, ile itakusaidia utimize ahadi yako ya kumutumikia na itafanya umukaribie hata zaidi.

21. Juu ya nini tunaweza kusema kama ubatizo haiko mwisho lakini ni mwanzo?

21 Kisha kujitoa kwa Yehova, uambie wazee wa kutaniko yako kama unapenda kukamata hatua ingine ya maana. Lakini, sikuzote ukumbuke kama ubatizo haiko mwisho lakini ni mwanzo. Ni mwanzo wa maisha yenye haina mwisho ya kumutumikia Yehova. Kuanzia sasa, uendelee kumupenda zaidi Baba yako. Ujiwekee miradi yenye itakusaidia uendelee kumupenda Yehova kila siku. Miradi ya vile, itakusaidia ufikie kubatizwa. Ile itakuwa siku ya muzuri sana. Lakini ni mwanzo tu. Uendelee basi kumupenda sana Yehova na Mwana wake milele!

WIMBO 135 Yehova Anakuomba “Ukuwe na Hekima”

a Juu ya kufanya maendeleo ili tufikie kubatizwa, tunapaswa kuwa na sababu za muzuri za kutuchochea kufanya vile. Tunapaswa pia kuwa na matendo ya muzuri. Mu hii habari, tutatumia mufano wa ofisa Mwetiopia juu ya kusaidia mwanafunzi wa Biblia ajue mambo yenye anapaswa kufanya ili afikie kubatizwa.

b MAFASIRIO YA PICHA: Dada fulani kijana anasali kwa Yehova juu ya kumushukuru kwa ajili ya mambo yenye alishamufanyia.