Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 10

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

‘Endelea Kufuata’ Yesu Kisha Ubatizo

‘Endelea Kufuata’ Yesu Kisha Ubatizo

“Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue muti wake wa mateso kila siku na aendelee kunifuata.”LU. 9:23.

WAZO KUBWA

Hii habari inaweza kutusaidia siye wote tufikirie maana ya ahadi yetu ya kujitoa kwa Yehova. Zaidi sana, inaweza kusaidia wale wenye walibatizwa karibuni ili waendelee kuwa waaminifu.

1-2. Namna gani maisha inakuwa muzuri zaidi kisha kubatizwa?

 NI FURAHA sana kubatizwa na kuingia mu familia ya Yehova. Wale wenye wanafikia ile pendeleo wanakubaliana na hii maneno ya Daudi: “Mwenye furaha ni ule mwenye unachagua na kumuleta karibu ili akae katika viwanja vyako.”—Zb. 65:4.

2 Haiko kila mutu njo Yehova anaalika mu uwanja wake. Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, anavuta kwake wale wenye wanaonyesha kama wanapenda kuwa na uhusiano wa karibu pamoya naye. (Yak. 4:8) Wakati unajitoa kwa Yehova na kubatizwa, unamukaribia mu njia ya pekee. Unaweza kuwa hakika kama kisha pale ‘atakumwangia baraka mupaka kusikuwe kitu chenye kitakosa.’—Mal. 3:10; Yer. 17:​7, 8.

3. Wakristo wenye wamejitoa kwa Yehova na kubatizwa wako na daraka gani nzito? (Muhubiri 5:​4, 5)

3 Kusema kweli, kubatizwa ni mwanzo tu. Kisha kukamata ile hatua, utapenda kufanya yako yote ili kuheshimia naziri yako ya kujitoa kwa Yehova, hata kama unapambana na magumu ao majaribu ya imani. (Soma Muhubiri 5:​4, 5.) Juu sasa uko mwanafunzi wa Yesu, utajikaza kabisa kufuata mufano wake na amri zake. (Mt. 28:​19, 20; 1 Pe. 2:21) Hii habari itakusaidia kufanya vile.

‘ENDELEA KUFUATA’ YESU HATA KAMA UNAPAMBANA NA MAGUMU NA MAJARIBU

4. Ni mu maana gani wanafunzi wa Yesu wanabeba ‘muti wa mateso’? (Luka 9:23)

4 Kisha kubatizwa, usiwaze kama hautapata tena magumu mu maisha yako. Kwa kweli, Yesu alisema wazi kama wanafunzi wake watabeba ‘muti wa mateso,’ na watafanya vile “kila siku.” (Soma Luka 9:23.) Yesu alimaanisha kama wafuasi wake watakuwa tu nateseka sikuzote? Hapana. Alipenda tu kukazia kama zaidi ya baraka zenye watapata, watapata pia magumu. Na magumu fulani kati ya ile inaweza kuwa yenye kuumiza sana.—2 Ti. 3:12.

5. Yesu alisema kama wale wenye wanajiima juu yake watapata baraka gani?

5 Pengine tayari umepambana na upinzani wa watu wa familia, ao pengine umeacha vitu fulani vya kimwili ili kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Kama ni vile, unaweza kuwa hakika kama Yehova anaona matendo yako ya uaminifu. (Ebr. 6:10) Na inawezekana kabisa umejionea utimizo wa hii maneno ya Yesu: “Hakuna mutu mwenye ameacha nyumba ao ndugu ao dada ao mama ao baba ao watoto ao mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema mwenye hatapata mara mia moja (100) sasa katika kipindi hiki—nyumba, ndugu, dada, mama, watoto, mashamba, pamoja na mateso—na katika mupangilio wa mambo wenye unakuja, uzima wa milele.” (Mk. 10:​29, 30) Baraka zenye umepata ni za mingi sana kupita jambo yoyote yenye umejiima.—Zb. 37:4.

6. Juu ya nini unapaswa kuendelea kupiganisha “tamaa ya mwili” kisha ubatizo?

6 Unapaswa kuendelea kupiganisha “tamaa ya mwili” kisha ubatizo. (1 Yo. 2:16) Kwa kweli, juu uko muzao wa Adamu ungali tu mutenda-zambi. Wakati fulani unaweza kujisikia sawa vile mutume Paulo. Aliandika hivi: “Kwa kweli ninapenda sheria ya Mungu kulingana na mutu mwenye niko kwa ndani, lakini ninaona ndani ya mwili wangu sheria ingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunipeleka nikiwa nimetekwa kwa sheria ya zambi yenye kuwa ndani ya mwili wangu.” (Ro. 7:​22, 23) Unaweza kuvunjika moyo kwa sababu ya muelekeo wako wa kufanya zambi. Lakini, kufikiria ahadi yenye ulimutolea Yehova kunaweza kukusaidia upambane na majaribu. Kusema kweli, kufikiria naziri yako ya kujitoa kwa Yehova kutafanya mambo ikuwe mwepesi zaidi wakati unapambana na majaribu. Namna gani?

7. Namna gani kujitoa kwa Yehova kutakusaidia kubakia muaminifu?

7 Wakati unajitoa kwa Yehova, unajikana mwenyewe. Ile inamaanisha kama unatia pembeni tamaa na miradi yenye haimufurahishe Yehova. (Mt. 16:24) Kwa hiyo wakati unapambana na majaribu, hautapitisha wakati mingi na uko najiuliza utafanya nini. Kati ya njia zote utakuwa ulishachagua njia moya tu ya kufuata: kubakia muaminifu kwa Yehova. Utaazimia kabisa kuendelea kumufurahisha Yehova. Mu njia fulani utakuwa sawa vile Yobu. Hata kama alipambana na magumu ya nguvu sana, alisema hivi kwa uhakika: “Sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”—Yob. 27:5.

8. Namna gani kufikiria sala yako ya kujitoa kwa Yehova kunaweza kukusaidia ushinde majaribu?

8 Kama unafikiria naziri yenye ulifanya wakati ulijitoa kwa Yehova katika sala, utapata nguvu ya kushinda jaribu yoyote. Kwa mufano, hautaanza kupendezwa na bibi ao bwana ya mutu mwingine juu utakuwa ulishaamua kama hauwezi kufanya vile. Na ile itafanya uepuke mahangaiko yenye inatokana na hisia zenye hazifae, kisha zile hisia kuota mizizi mu moyo. ‘Utajiepusha’ na “njia ya waovu.”—Mez. 4:​14, 15.

9. Namna gani kufikiria sala yako ya kujitoa kwa Yehova kunakusaidia pia uendelee kuweka mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza?

9 Utafanya nini kama unapata kazi yenye itakuzuia kukusanyika kwa ukawaida? Jibu yako itakuwa wazi. Utakuwa ulishaamua mbele ya wakati kama hautaitika kazi ya vile. Hauwezi kujiambia kama utakamata uamuzi mubaya na kisha utajikaza juu ya kuufanya ukuwe na matokeo ya muzuri. Kukumbuka namna Yesu aliazimia kabisa kumufurahisha Baba yake, kutakusaidia ukatae mara moya na kwa uhodari jambo yoyote yenye inaweza kumuhuzunisha Yehova mwenye ulijitoa kwake.—Mt. 4:10; Yoh. 8:29.

10. Yehova atakusaidia namna gani kisha kubatizwa ili ‘uendelee kufuata’ Yesu?

10 Kusema kweli magumu na majaribu inakupatia nafasi ya kuonyesha kama umeazimia ‘kuendelea kufuata’ Yesu. Wakati unaazimia kufanya vile, unaweza kuwa hakika kama Yehova atakusaidia. Biblia inasema hivi: “Mungu ni muaminifu, na hatawaacha ninyi mujaribiwe kupita vile munaweza kuvumilia, lakini pamoja na jaribu hilo atafanya pia njia ya kutokea ili muweze kulivumilia.”—1 Ko. 10:13.

NAMNA YA KUENDELEA KUMUFUATA YESU

11. Moya kati ya njia za muzuri zaidi za kumufuata Yesu ni gani? (Ona pia picha.)

11 Yesu alikuwa na bidii, na sala ilimusaidia aendelee kumukaribia Yehova. (Lu. 6:12) Kwa hiyo, moya kati ya njia za muzuri za kuendelea kumufuata Yesu kisha ubatizo ni kuwa na zoea ya kufanya mambo yenye itakusaidia umukaribie Yehova zaidi. Biblia inasema: “Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.” (Flp. 3:16) Mara kwa mara, utasikia kuhusu ndugu na dada wenye wamejitoa ili kupanua utumishi wao mutakatifu. Pengine walisoma masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme ao walihamia fasi kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kama inawezekana, ujitilie muradi wa vile. Watu wa Yehova wanapenda sana kupanua utumishi wao. (Mdo. 16:9) Lakini, utafanya nini kama kwa sasa haiwezekane ufanye vile? Usiwaze kama wale wenye wanafanya vile ni wa maana zaidi kuliko weye. Jambo ya maana kwa siye Wakristo ni kuendelea kuvumilia. (Mt. 10:22) Usisahau kama unamufurahisha sana Yehova wakati unamutumikia kulingana na uwezo na hali yako. Ile ni njia ya muzuri sana ya kuendelea kumufuata Yesu kisha kubatizwa.—Zb. 26:1.

Kisha kubatizwa, ujitilie muradi wa kufanya mambo yenye itakusaidia umukaribie Yehova zaidi (Ona fungu ya 11)


12-13. Utafanya nini kama bidii yako inaanza kupunguka? (1 Wakorinto 9:​16, 17) (Ona pia kisanduku “ Bakia Katika Mbio.”)

12 Utafanya nini ikiwa unaona kama sala zako hazitoke tena ku moyo ao haufurahie tena mahubiri sawa zamani? Halafu kama haufurahie tena kusoma Biblia sawa zamani? Kama hali za vile zinakufikia kisha kubatizwa, usiwaze kama umepoteza roho ya Yehova. Juu haukamilike, hisia zako zinaweza kubadilika-badilika. Kama bidii yako inaanza kupunguka, fikiria mufano wa mutume Paulo. Hata kama alijikaza kumuiga Yesu, alijua kama wakati fulani hatajisikia kuwa mwenye bidii. (Soma 1 Wakorinto 9:​16, 17.) Anasema hivi: “Hata kama ninafanya vile bila kupenda, bado nimepewa usimamizi-nyumba.” Mu maneno ingine, Paulo aliazimia kutimiza utumishi wake hata ajisikie namna gani.

13 Vilevile, usiache hisia zikamate uamuzi pa nafasi yako. Azimia kufanya mambo ya muzuri hata kama unajisikia namna gani. Kama unaendelea kufanya mambo ya muzuri, kisha wakati fulani hisia zako zinaweza kubadilika. Mu hali yoyote, kuendelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho kutakusaidia uendelee kumufuata Yesu kisha kubatizwa. Pia, wakati unajikaza kuendelea kumutumikia Yehova, ile itatia moyo waamini wenzako.—1 Te. 5:11.

“MUENDELEE KUJIJARIBU . . . MUENDELEE KUHAKIKISHA”

14. Unapaswa kufanya nini kwa ukawaida, na juu ya nini? (2 Wakorinto 13:5)

14 Kujichunguza kwa ukawaida kisha kubatizwa kunaweza pia kukusaidia. (Soma 2 Wakorinto 13:5.) Mara kwa mara, chunguza maisha yako na mambo yenye unazoea kufanya ili kuona kama uko nasali kila siku, uko nasoma na kujifunza Biblia, uko na kusanyika, na uko nahubiri. Utafute njia za kufanya ile mambo muzuri zaidi juu ikuletee faida. Kwa mufano, ujiulize maulizo sawa vile: ‘Naweza kufasiria wengine mafundisho ya musingi ya Biblia? Kuko njia zingine zenye ninaweza kutumia ili nifurahie zaidi kazi ya kuhubiri? Ninazungumuza na Yehova waziwazi katika sala, na sala zangu zinaonyesha kama ninamutegemea? Ninakusanyika kwa ukawaida? Ninaweza kufanya nini juu nifuate kwa uangalifu zaidi mikutano na nishiriki?’

15-16. Jambo yenye ilimufikia ndugu Robert inatufundisha nini kuhusu kushinda jaribu?

15 Pia ni muzuri ujichunguze ili ujue ikiwa uko na uzaifu gani. Ndugu mwenye anaitwa Robert anaeleza jambo fulani yenye ilimufikia yenye inaonyesha faida ya kufanya vile: “Wakati nilikuwa na miaka 20 nilianza kutumika kazi fulani yenye haikunikamata wakati wote. Siku fulani kisha kazi, mufanyakazi mwenzangu mwanamuke alinialika kwake. Alisema tutakuwa tu siye wawili na tutapitisha wakati wa muzuri pamoya. Ku mwanzo sikuonyesha musimamo wangu, nilitoa tu visababu fulani. Lakini ku mwisho nilikatala na nikamufasiria juu ya nini.” Robert alishinda ile jaribu, na ile ni jambo ya muzuri. Lakini, wakati anafikiria ile jambo, anaona kama angeishugulikia muzuri zaidi. Anasema hivi: “Sikukatala mwaliko wake kwa uhodari ao haraka sawa vile Yosefu alikatala bibi ya Potifa. (Mwa. 39:​7-9) Na hata, nilishangala kuona vile ilikuwa nguvu sana kwangu kukatala. Ile jambo ilinisaidia kuona kama nilipaswa kutia nguvu urafiki wangu pamoja na Yehova.”

16 Ukijichunguza sawa vile Robert alifanya unaweza pia kupata faida. Hata kama uliweza kushinda jaribu fulani, ujiulize: ‘Ilinikamata muda gani juu ya kusema hapana?’ Ikiwa unaona kama inaomba utumikie jambo fulani, usijilaumu. Ukuwe na furaha kwa sababu sasa unajua ule uzaifu. Sali juu ya ule uzaifu, na ukamate hatua za kutia nguvu azimio yako ya kuishi kulingana na kanuni za mwenendo za Yehova.—Zb. 139:​23, 24.

17. Namna gani uamuzi wa Robert ulisaidia kutukuza jina ya Yehova?

17 Habari ya Robert haikuishia pale. Anasema hivi: “Kisha kukatala mwaliko wa ule mwanamuke, aliniambia hivi: ‘Umeshinda jaribu!’ Nilimuuliza anapenda kusema nini. Aliniambia kama rafiki yake fulani mwenye alikuwa Shahidi zamani, alimuambia kama Mashahidi wote vijana wanaishi maisha ya unafiki, na wako tayari kufanya mambo ya mubaya kama tu wanapata nafasi. Kwa hiyo aliambia rafiki yake kama atanijaribu ili aone kama ni kweli. Nilifurahi sana kuona vile nilitukuza jina ya Yehova.”

18. Unaazimia kufanya nini kisha kubatizwa? (Ona pia kisanduku “ Habari Zenye Utafurahia.”)

18 Wakati unajitoa kwa Yehova na kubatizwa, unaonyesha kama unapenda kutakasa jina yake hata kutokee nini. Unaweza kuwa hakika kama Yehova anajua magumu yenye uko napambana nayo na majaribu yenye uko nashinda. Atakubariki juu uko najikaza kubakia muaminifu. Ukuwe hakika kama kupitia roho yake takatifu, atakupatia nguvu ya kufanya vile. (Lu. 11:​11-13) Kwa musaada wa Yehova utaweza kuendelea kumufuata Yesu kisha kubatizwa.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni mu maana gani Wakristo wanabeba ‘muti wa mateso kila siku’?

  • Tunapaswa kufanya nini ili ‘tuendelee kufuata’ Yesu kisha kubatizwa?

  • Namna gani kufikiria sala yetu ya kujitoa kwa Yehova kunatusaidia kuendelea kuwa waaminifu?

WIMBO 89 Tii juu Ubarikiwe