Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSEMWA WA BIBLIA

Musamaha Mbele Bei ya Ukombozi Itolewe

Musamaha Mbele Bei ya Ukombozi Itolewe

Tunaweza kusamehewa zambi zetu kupitia tu zabihu ya ukombozi yenye Yesu alilipa kupitia damu yake. (Efe. 1:7) Lakini, Biblia inasema hivi: “Mungu kwa uvumilivu wake alikuwa anasamehe zambi zenye zilifanywa wakati wenye ulipita,” ni kusema mbele Yesu alipe bei ya ukombozi. (Ro. 3:25) Namna gani iliwezekana Yehova afanye vile na wakati uleule aendelee kuheshimia kanuni zake za haki zenye kuwa kamilifu?

Wakati tu Yehova aliamua kama atatoa “uzao” wenye utakomboa wanadamu wenye kuwa na imani, kwake ilikuwa sawa vile bei ya ukombozi ilikuwa tayari imelipwa. (Mwa. 3:15; 22:18) Mungu alikuwa hakika kabisa kama kwa wakati wenye aliweka, Mwana wake muzaliwa-pekee atalipa bei ya ukombozi kwa kupenda. (Gal. 4:4; Ebr. 10:​7-10) Wakati Yesu, muwakilishi wa Mungu, alikuwa ku dunia, alikuwa na mamlaka ya kusamehe zambi mbele bei ya ukombozi itolewe. Alifanya vile juu alijua kama zabihu yenye angetoa ingeweza kufunika zambi za wale wenye walikuwa na imani.—Mt. 9:​2-6.