Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani?

Ukuwe Hakika Kama Yehova Anakukubali

Ukuwe Hakika Kama Yehova Anakukubali

“Nimekukubali.”LU. 3:22.

WAZO KUBWA

Namna unaweza kuwa hakika kama Yehova anakukubali.

1. Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wanaweza kujiuliza nini?

 INATIA moyo sana kujua kama Yehova anakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema: “Yehova anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Lakini, wakati fulani kuko Wakristo wenye wanaweza kuvunjika moyo na kujiuliza hivi: ‘Yehova ananikubali na miye?’ Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wa zamani walijiuliza pia vile wakati fulani.—1 Sa. 1:​6-10; Yob. 29:​2, 4; Zb. 51:11.

2. Ni nani mwenye Yehova anakubali?

2 Biblia inaonyesha wazi kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kukubaliwa na Yehova. Namna gani? Tunapaswa kukubali Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Kwa kufanya vile tunaonyesha waziwazi kama tumetubu zambi zetu na tumemuahidi Mungu kama tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi sana wakati tunafanya ile mambo ili kuwa marafiki wake wa karibu. Wakati tunaendelea kufanya yetu yote ili kuheshimia naziri yetu ya kujitoa kwake, Yehova anatukubali na kutuona kuwa marafiki wake.—Zb. 25:14.

3. Tutazungumuzia sasa nini?

3 Sasa, juu ya nini Wakristo fulani wanawaza kama Yehova hawakubali? Yehova anaonyesha namna gani kuwa anatukubali? Na namna gani Mukristo anaweza kuwa hakika zaidi kama Mungu anamukubali?

JUU YA NINI WAKRISTO FULANI WANAWAZA KAMA YEHOVA HAWAKUBALI?

4-5. Hata kama tunajisikia kuwa watu wa bure, tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

4 Tangu utoto, wengi kati yetu wanajisikia kuwa watu wa bure. (Zb. 88:15) Ndugu mwenye kuitwa Adrián anasema hivi: “Tangu zamani najiona kuwa mutu wa bure. Tangu wakati nilikuwa mudogo nilisali juu familia yangu iingie mu Paradiso, hata kama nilikuwa hakika kama miye sikustahili kuingia.” Tony, mwenye hakukomalia mu familia ya Kikristo, anasema hivi: “Wazazi wangu hawakuniambia hata siku moya kama wananipenda ao wanafurahia mambo yenye niko nafanya. Walionyesha tu kama ninaweza kufanya muzuri zaidi.”

5 Ikiwa wakati fulani tunajiona kuwa watu wa bure, tukumbuke kama ni Yehova njo alituvuta kwake. (Yoh. 6:44) Anaona jambo fulani ya muzuri ndani yetu, jambo fulani yenye pengine siye wenyewe hatuone, na anajua moyo wetu. (1 Sa. 16:7; 2 Ny. 6:30) Kwa hiyo tunaweza kumuamini wakati anasema kama tuko wa maana.—1 Yo. 3:​19, 20.

6. Mutume Paulo alisema kama alijisikia namna gani kwa sababu ya zambi zake za zamani?

6 Mbele ya kujifunza kweli, wamoja kati yetu walifanya mambo yenye pengine wanaendelea kuhuzunikia mupaka leo. (1 Pe. 4:3) Hata Wakristo waaminifu wanapiganisha muelekeo wa kufanya zambi. Moyo wako uko nakuhukumu? Kama ni vile, usivunjike moyo. Ujue kama hata watumishi fulani wa Yehova walijisikia vile. Kwa mufano, mutume Paulo alijiona kuwa wa bure wakati alifikiria uzaifu wake. (Ro. 7:24) Kwa kweli, Paulo alikuwa ametubu zambi zake na kubatizwa. Lakini, aliendelea kujiona kuwa “mudogo zaidi kati ya mitume” na mutenda-zambi “wa kwanza kabisa.”—1 Ko. 15:9; 1 Ti. 1:15.

7. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu zambi zetu za zamani?

7 Baba yetu wa mbinguni anaahidi kama atatusamehe ikiwa tunatubu. (Zb. 86:5) Kwa hiyo kama tumehuzunika kabisa kwa sababu ya zambi zenye tulifanya, tunaweza kumuamini Yehova wakati anasema kuwa ametusamehe.—Kol. 2:13.

8-9. Namna gani tunaweza kuacha kuwaza kama mambo yenye tunafanya ni ya kidogo sana na haiwezi kumufurahisha Yehova?

8 Siye wote tunapenda kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote. Lakini, Wakristo fulani wanaona kama mambo yenye wanafanya ni ya kidogo sana na Yehova hawezi kuwakubali. Dada mwenye kuitwa Amanda anasema hivi: “Ninawazaka kama ili nimutumikie Yehova kwa nguvu yangu yote inaomba kufanya mengi zaidi. Mara mingi ninapendaka kufanya mambo mingi kuliko yenye niko na uweza wa kufanya. Na wakati ninashindwa kufanya vile, ninaona kama Yehova hanifurahie sawa vile tu miye peke sijifurahie.”

9 Namna gani tunaweza kuacha kuona kama mambo yenye tunamutolea Yehova ni ya kidogo sana na haiwezi kumufurahisha? Kumbuka kama Yehova iko na usawaziko, hatuombe mambo mingi zaidi ya ile yenye tunaweza kufanya. Anafurahia mambo yote yenye tunamufanyia kama tu tunaifanya kwa moyo wote. Pia, fikiria mifano ya watumishi wa Yehova wenye kuzungumuziwa mu Biblia wenye walimutumikia kwa moyo wote. Fikiria mufano wa Paulo. Alitumika kwa bidii kwa miaka mingi, alifanya safari za murefu na kuanzisha makutaniko mingi. Lakini, wakati hali yake ilifanya asihubiri sana sawa zamani, je, Mungu aliacha kumukubali? Hapana. Paulo aliendelea kufanya yote yenye aliweza na Yehova alimubariki. (Mdo. 28:​30, 31) Vilevile, namna yetu ya kumutumikia Yehova inaweza kubadilika kulingana na hali. Lakini jambo ya maana zaidi kwa Yehova ni nia yenye inatuchochea tumutumikie. Tuone sasa njia mbalimbali zenye Yehova anatumia ili kuonyesha kama anatukubali.

NAMNA YEHOVA ANAONYESHA KAMA ANATUKUBALI

10. Namna gani tunaweza “kusikia” Yehova anasema kama anatukubali? (Yohana 16:27)

10 Kupitia Biblia. Yehova anapenda kuonyesha kama anakubali wale wenye anapenda. Maandiko inazungumuzia mara mbili zenye Yehova aliambia Yesu kama alikuwa Mwana wake mupendwa mwenye alikubali. (Mt. 3:17; 17:5) Unapenda kumusikia Yehova anasema kama anakukubali? Hatuwezi kusikia sauti ya Yehova, lakini anazungumuza na siye kupitia Neno yake. Tunaweza “kumusikia” Yehova anasema kuwa anatukubali wakati tunasoma maneno ya Yesu yenye kuwa mu Injili. (Soma Yohana 16:27.) Yesu alionyesha kwa ukamili utu wa Baba yake. Wakati tunasoma namna Yesu aliambia wafuasi wake waaminifu kama anawakubali hata kama hawakukuwa wakamilifu, tunaweza kuwazia kama ni Yehova njo iko natuambia ile maneno.—Yoh. 15:​9, 15.

Yehova anaonyesha mu njia mbalimbali kama anatukubali (Ona fungu ya 10)


11. Juu ya nini hatupaswe kuwaza kama Yehova hatukubali tena wakati tunapata magumu? (Yakobo 1:12)

11 Kupitia matendo yake. Yehova anapenda sana kutusaidia. Kwa mufano, anatupatia mambo ya kimwili yenye tuko nayo lazima. Lakini wakati fulani anaweza kuruhusu tupate magumu, sawa vile aliruhusu mwanaume muaminifu Yobu apate magumu. (Yob. 1:​8-11) Magumu haimaanishe kama Yehova hatukubali tena. Lakini inatupatia nafasi ya kuonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda na kumutumainia. (Soma Yakobo 1:12.) Tunaona kama Yehova anatupenda na kututegemeza wakati anatusaidia kuvumilia magumu.

12. Mufano wa Dmitrii unatufundisha nini?

12 Fikiria ndugu mwenye kuitwa Dmitrii wa mu Asia. Alipoteza kazi yake na kwa miezi mingi hakuweza kupata kazi ingine. Kwa hiyo aliamua kufanya mengi zaidi mu kazi ya kuhubiri na kuonyesha kama alimutumainia Yehova. Miezi mingi ilipita na hakupata tu kazi. Kisha akagonjwa sana na hakukuwa natoka tena ku kitanda. Alianza kuona kama hakukuwa tena bwana na baba muzuri, na alianza jiuliza ikiwa Yehova angali anamukubali. Kisha, mangaribi moya mutoto wake mwanamuke alimuandikia ku karatasi maneno yenye kuwa mu Isaya 30:15: “Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.” Alimuletea ile karatasi ku kitanda na kumuambia, “Papa, wakati unajisikia mubaya unaweza kukumbuka hii andiko.” Dmitrii aliona kama kwa musaada wa Yehova, familia yake iliendelea kupata chakula, manguo, na fasi ya kuishi. Anasema hivi: “Jambo yenye nilipaswa kufanya ni kuendelea kumutumainia Yehova.” Kama uko napambana na magumu ya vile, unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuhangaikia na ataendelea kukusaidia ili uvumilie.

Yehova anaonyesha mu njia mbalimbali kama anatukubali (Ona fungu ya 12) a


13. Yehova anatumia nani ili kuonyesha kama anatukubali, na namna gani?

13 Kupitia waabudu wenzetu. Yehova anatumia ndugu na dada zetu ili kuonyesha kama anatukubali. Kwa mufano, anaweza kuchochea wengine watuambie maneno yenye kutia moyo wakati tuko nayo lazima. Dada fulani wa Asia alijionea ile wakati alikuwa na mahangaiko ya mingi. Alipoteza kazi na aligonjwa sana. Kisha bwana yake alifanya zambi nzito na kupoteza pendeleo ya kuwa muzee. Anasema hivi: “Sikuelewa juu ya nini ile mambo yote ilikuwa nanifikia. Niliwaza kama pengine nilifanya jambo fulani ya mubaya na Yehova hakunikubali tena.” Dada yetu alimulilia Yehova amusaidie kuona kama angali anamukubali. Namna gani Yehova alifanya vile? Ule dada anasema tena hivi: “Wazee wa kutaniko walizungumuza na miye na wakanihakikishia kama Yehova ananipenda.” Kisha alimuomba tena Yehova amusaidie. Ileile siku alipata barua kutoka kwa ndugu na dada fulani wa mu kutaniko. Anasema: “Wakati nilikuwa nasoma maneno yao yenye kufariji niliona kama Yehova alinisikia.” Kwa kweli, mara kwa mara Yehova anaonyesha kama anatukubali kupitia maneno yenye kutia moyo ya wengine.—Zb. 10:17.

Yehova anaonyesha mu njia mbalimbali kama anatukubali (Ona fungu ya 13) b


14. Ni mu njia gani ingine Yehova anaonyesha kama anatukubali?

14 Yehova anaonyesha pia kama anatukubali wakati anatumia waabudu wenzetu ili watupatie mashauri yenye tuko nayo lazima. Kwa mufano, mu karne ya kwanza Yehova alitumia mutume Paulo ili kuandikia waabudu wenzake barua 14 zenye kuongozwa na roho. Mu zile barua mulikuwa pia mashauri mazito lakini yenye upendo. Juu ya nini Yehova alimuongoza Paulo ili aandike ile mashauri? Yehova ni Baba muzuri na anapatia nizamu watoto wake ‘wenye anafurahia sana.’ (Mez. 3:​11, 12) Kwa hiyo, wakati tunapewa mashauri yenye kutegemea Biblia, tunaweza kuiona kuwa njia yenye Yehova anatumia ili kuonyesha kama anatukubali, hapana alama yenye kuonyesha kama hatukubali tena. (Ebr. 12:6) Yehova anatumia njia gani zingine ili kuonyesha kama anatukubali?

MAMBO INGINE YENYE KUONYESHA KAMA YEHOVA ANATUKUBALI

15. Yehova anapatia nani roho takatifu, na juu ya nini ile inapaswa kutuhakikishia kama anatukubali?

15 Yehova anapatia roho takatifu wale wenye anakubali. (Mt. 12:18) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nimeweza kuonyesha sehemu fulani ya tunda la roho ya Mungu mu maisha yangu?’ Umetambua kama unavumilia wengine zaidi kuliko vile ulikuwa mbele umujue Yehova? Kwa kweli, kadiri unajifunza kuonyesha zaidi sifa za tunda la roho ya Mungu, ni vile inaonekana wazi zaidi kama Yehova anakukubali!—Ona kisanduku “ Tunda la Roho Ni . . . ”

Ni mambo gani inaweza kukuhakikishia kama Yehova anakukubali? (Ona fungu ya 15)


16. Yehova anatumia nani ili kuhubiri habari njema, na ile inakufanya ujisikie namna gani? (1 Watesalonike 2:4)

16 Yehova anafurahi kupatia kazi ya kuhubiri habari njema wale wenye anakubali. (Soma 1 Watesalonike 2:4.) Ona namna kazi ya kuhubiri habari njema ilisaidia sana dada mwenye kuitwa Jocelyn. Siku moya, Jocelyn aliamuka na iko najisikia kuwa mwenye kushuka moyo. Anasema hivi: “Nilijisikia kuwa sina nguvu na siko wa maana. Lakini nilikuwa painia na ile ilikuwa siku yangu ya kuhubiri. Kwa hiyo nilisali, kisha nikaenda mu mahubiri.” Ile asubui Jocelyn alikutana na Mary, mwanamuke mwenye moyo muzuri mwenye alikubali funzo ya Biblia. Kisha miezi fulani ule mwanamuke alisema kama alikuwa nasali kwa Mungu amusaidie wakati Jocelyn aligonga ku mulango wake. Wakati Jocelyn anafikiria ile jambo, anasema hivi: “Ni sawa vile Yehova alikuwa naniambia, ‘Ninakukubali.’” Kusema kweli, haiko kila mutu njo atakubali habari njema. Lakini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anafurahi wakati tunafanya yetu yote ili kutangazia wengine habari njema.

Ni mambo gani inaweza kukuhakikishia kama Yehova anakukubali? (Ona fungu ya 16) c


17. Maneno ya Vicky inakufundisha nini kuhusu bei ya ukombozi? (Zaburi 5:12)

17 Yehova anatumia samani ya bei ya ukombozi kwa wale wenye anakubali. (1 Ti. 2:​5, 6) Lakini tutafanya nini ikiwa moyo wetu unakatala kuamini kama Yehova anatukubali, hata kama tuko na imani katika bei ya ukombozi na tumebatizwa? Kumbuka kama wakati fulani hatupaswe kutumainia moyo wetu, lakini tunapaswa kumutumainia Yehova. Anaona wale wenye kuamini bei ya ukombozi kuwa wenye haki na anaahidi kuwabariki. (Soma Zaburi 5:12; Ro. 3:26) Kutafakari kuhusu bei ya ukombozi kulisaidia Vicky. Siku moya kisha kufikiri sana juu ya bei ya ukombozi alisema: “Yehova amekuwa akinivumilia kwa muda murefu. . . . Hata hivyo, ni kama vile nilikuwa ninamuambia hivi: ‘Upendo wako hautoshe ili kunifikia. Zabihu ya Mwana wako haiwezi kufunika zambi zangu.’” Wakati alifikiri sana juu ya zawadi ya bei ya ukombozi alianza kuona kama Yehova anamupenda. Siye pia tunaweza kuona kama Yehova anatupenda na anatukubali ikiwa tunafikiri juu ya bei ya ukombozi.

Ni mambo gani inaweza kukuhakikishia kama Yehova anakukubali? (Ona fungu ya 17)


18. Tunaweza kuwa hakika na jambo gani kama tunaendelea kumupenda Baba yetu wa mbinguni?

18 Hata kama tunaweza kujikaza sana kutumikisha mapendekezo yenye tumejifunza, wakati fulani tunaweza kuvunjika moyo na kujiuliza ikiwa Yehova anatukubali. Kama ile inatokea, kumbuka kama Yehova anakubali “wenye wanaendelea kumupenda.” (Yak. 1:12) Kwa hiyo, endelea kumukaribia Yehova na kutambua mambo yenye inaonyesha kama anakukubali. Sikuzote ukumbuke kama Yehova “haiko mbali sana na kila mumoja wetu.”—Mdo. 17:27.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Juu ya nini Wakristo fulani wanawaza kama Yehova hawakubali?

  • Ni mu njia gani mbalimbali Yehova anaonyesha kama anatukubali?

  • Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anatukubali?

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

a MAFASIRIO YA PICHA: Picha

b MAFASIRIO YA PICHA: Picha

c MAFASIRIO YA PICHA: Picha