Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 15

Miujiza ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?

Miujiza ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?

“Akapita katika inchi akitenda mema na kuponyesha.”​—MDO. 10:38.

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

KIFUPI YA HABARI a

1. Fasiria namna mambo ilikuwa wakati Yesu alifanya muujiza wake wa kwanza.

 WAZIA namna mambo ilikuwa ku mwisho wa mwaka wa 29 K.K.Y., wakati Yesu alianza utumishi wake. Yeye na mama yake Maria, na wanafunzi wake wengine wanaalikwa ku karamu ya ndoa mu Kana, kijiji yenye ilikuwa kaskazini ya Nazareti kwenye Yesu alikuwa anaishi. Maria ni rafiki wa ile familia yenye iko nafanya karamu ya ndoa na pengine iko nasaidia mu kazi ya kukaribisha wageni. Sasa wakati ya karamu ya ndoa, divai inaisha. Ile ilikuwa shida yenye ingeletea haya ile familia na wale wenye walikuwa nafunga ndoa. b Pengine wageni wako wengi sana kuliko vile ilitazamiwa. Palepale Maria anaenda mbio kuambia mutoto wake hivi: “Hawana divai.” (Yoh. 2:1-3) Yesu anafanya nini? Anafanya jambo fulani ya ajabu sana. Anafanya muujiza wa kugeuza maji kuwa “divai ya muzuri.”​—Yoh. 2:9, 10.

2-3. (a) Yesu alifanya miujiza gani? (b) Tutapata faida gani kama tunafikiria miujiza yenye Yesu alifanya?

2 Yesu alifanya miujiza ingine mingi mu utumishi wake. c Alitumia nguvu yake ya ajabu juu ya kusaidia makumi ya maelfu ya watu. Kwa mufano, tuzungumuzie miujiza mbili yenye alifanya. Kwanza, alilisha wanaume 5000 na kisha akalisha wanaume 4000. Inawezekana, mu ile miujiza yote mbili, watu wenye walikula ile chakula walikuwa zaidi ya 27000, kutia ndani wanamuke na watoto wenye walikuwa pia pale. (Mt. 14:15-21; 15:32-38) Mu ileile wakati, Yesu aliponyesha wagonjwa wengi. (Mt. 14:14; 15:30, 31) Wazia namna watu wengi sana walifurahi wakati Yesu aliwaponyesha na kuwalisha kimuujiza!

3 Miujiza ya Yesu inaweza kutufundisha mambo mingi leo. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo yenye ile miujiza inaweza kutufundisha. Ile mambo itatia nguvu imani yetu. Kisha tutazungumuzia namna tunaweza kuiga unyenyekevu na huruma yenye Yesu alionyesha wakati alikuwa nafanya miujiza.

MAMBO YENYE TUNAWEZA KUJIFUNZA JUU YA YEHOVA NA YESU

4. Miujiza ya Yesu inatufundisha mambo fulani juu ya nani?

4 Miujiza ya Yesu inatufundisha mambo fulani yenye kutia nguvu imani yetu, hapana juu yake tu, lakini pia juu ya Baba yake. Kusema kweli, Yehova njo Chanzo ya ile miujiza. Matendo 10:38 inasema hivi: “Mungu alimutia mafuta kwa roho takatifu na nguvu, na akapita katika inchi akitenda mema na kuponyesha wote wenye walikandamizwa na Ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.” Ukumbuke pia kama Yesu aliiga kwa ukamili mawazo na hisia za Baba yake mu mambo yote yenye alisema na kufanya, kutia ndani miujiza yenye alifanya. (Yoh. 14:9) Ona mambo tatu yenye miujiza ya Yesu inaweza kutufundisha.

5. Nini njo ilichochea Yesu afanye miujiza? (Matayo 20:30-34)

5 Kwanza, Yesu na Baba yake wanatupenda sana. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama alipenda sana watu kwa kutumia nguvu yake ya ajabu ili kusaidia wale wenye walikuwa nateseka. Siku moya, vipofu wawili wanaume walimuomba awasaidie. (Soma Matayo 20:30-34.) Yesu “akawasikilia huruma” na kisha akawaponyesha. Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “akawasikilia huruma” yenye inatumiwa hapa, inaonyesha kama Yesu alisikia sana huruma wakati aliona ule mwanaume anateseka. Ile huruma ni namna ya kuonyesha upendo, na njo yenye ilimuchochea pia Yesu alishe watu wenye walikuwa na njala na aponyeshe mutu fulani mwenye alikuwa na ukoma. (Mt. 15:32; Mk. 1:41) Tuko hakika kama Yehova, Mungu wa “huruma nyingi,” na Mwana wake, wanatupenda sana na wanahuzunikaka wakati wanaona tunateseka. (Lu. 1:78; 1 Pe. 5:7) Wanatamani sana kutosha mambo yote ya mubaya yenye iko nahangaisha watu!

6. Mungu amepatia Yesu nguvu ya kufanya nini?

6 Pili, Mungu amepatia Yesu nguvu ya kumaliza magumu yote ya wanadamu. Miujiza yenye Yesu alifanya ilionyesha kama iko na nguvu ya kumaliza magumu yenye hatuwezi kumaliza siye wenyewe. Kwa mufano, iko na nguvu ya kutosha jambo yenye imefanya wanadamu wakuwe mu magumu, ni kusema, zambi yenye waliriti na pia matokeo yake, yenye ni magonjwa na kifo. (Mt. 9:1-6; Ro. 5:12, 18, 19) Kupitia miujiza yake, alionyesha kama iko na nguvu ya kuponyesha “kila namna ya” magonjwa na kama iko na nguvu ya kufufua wafu. (Mt. 4:23; Yoh. 11:43, 44) Tena, iko na nguvu ya kutuliza zoruba yenye upepo mukali na kufukuza pepo wachafu. (Mk. 4:37-39; Lu. 8:2) Inatia moyo kabisa kuona kama Yehova amepatia Mwana wake nguvu ya kufanya ile mambo yote!

7-8. (a) Miujiza ya Yesu inatufundisha nini? (b) Ni muujiza gani wenye uko nachunga kwa hamu kujionea mu dunia mupya?

7 Tatu, tuko hakika kabisa kama ahadi zote za mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utaleta, zitatimia. Miujiza yenye Yesu alifanya wakati alikuwa mwanadamu hapa ku dunia, inatufundisha kama wakati ataanza kutawala dunia, atatufanyia mambo mingi sana ya muzuri. Tufikirie mambo ya muzuri yenye tutajionea hivi karibuni wakati Kristo ataanza kutawala dunia. Tutakuwa na afya kamilifu juu atatosha magonjwa na mateso yote. (Isa. 33:24; 35:5, 6; Ufu. 21:3, 4) Njala ao misiba ya asili haitatusumbua tena. (Isa. 25:6; Mk. 4:41) Tutakuwa na furaha sana ya kukaribisha wapendwa wetu wenye watatoka mu “makaburi ya ukumbusho.” (Yoh. 5:28, 29) Ni muujiza gani wenye uko nachunga kwa hamu kujionea mu dunia mupya?

8 Wakati Yesu alikuwa nafanya miujiza, alikuwa munyenyekevu sana na mwenye huruma. Zile ni sifa zenye tunapaswa kuiga. Tuzungumuzie mifano mbili. tutaanza na habari ya karamu ya ndoa yenye ilifanyika katika Kana.

SOMO YA UNYENYEKEVU

9. Juu ya nini Yesu alifanya muujiza ku karamu ya ndoa mu kijiji ya Kana? (Yohana 2:6-10)

9 Soma Yohana 2:6-10. Yesu alipaswa kufanya jambo fulani wakati divai iliisha ku karamu ya ndoa? Hapana. Hakuna unabii wenye kuonyesha kama Masiya angegeuza maji kuwa divai. Sasa, wazia namna unaweza kujisikia kama vinywaji vyote vinaisha ku karamu yako ya ndoa saa karamu ingali naendelea. Inawezekana Yesu alisikilia huruma ile familia, zaidi sana bibi na bwana-arusi, na alipenda kuwasaidia juu wasipate haya. Njo maana, sawa vile tuliona ku mwanzo wa hii habari, alifanya muujiza. Aligeuza litre ya maji 390 hivi kuwa divai ya muzuri sana. Pengine aligeuza maji kuwa divai mingi vile ili ingine ibakie juu itumiwe wakati ingine ao juu iuzishwe na ile makuta isaidie wale bibi na bwana-arusi. Kusema kweli, wale bibi na bwana-arusi walikuwa wenye shukrani sana!

Umuige Yesu kwa kuepuka kujisifu wakati unafanya mambo fulani ya muzuri (Ona fungu ya 10-11) e

10. Ni mambo gani ya maana yenye inazungumuziwa mu Yohana sura ya 2? (Ona pia picha.)

10 Tuzungumuzie mambo fulani ya maana yenye kuzungumuziwa mu Yohana sura ya 2. Kulingana na ile andiko, Yesu hakujaza maji mu mitungi ya maji yenye ilitengenezwa kwa majiwe. Juu asijikazie uangalifu, aliambia watumishi wenye walikuwa pale wajaze ile mitungi. (Mustari wa 6, 7) Kisha Yesu kugeuza maji kuwa divai, haiko yeye njo mwenye alikamataka sehemu fulani ya divai na kumupatia musimamizi wa karamu. Lakini, aliambiaka watumishi wenye walikuwa pale wafanye vile. (Mustari wa 8) Bila shaka, Yesu hakukamataka kopo moya ya divai na kuenda nayo mbele ya wageni, kuiinua na kuanza kusema hivi kwa kujisifu: ‘Muonje divai ya muzuri yenye nimetoka kufanya!’

11. Muujiza wa Yesu unatufundisha somo gani?

11 Muujiza wa Yesu wa kugeuza maji kuwa divai unatufundisha nini? Tunajifunza somo ya unyenyekevu. Yesu hakujisifu juu ya ule muujiza; na kusema kweli, hakuna hata siku moya yenye alijisifu juu ya mambo yenye alikuwa nafanya. Lakini, juu alikuwa munyenyekevu, kila mara alimupatia Baba yake utukufu na sifa yote. (Yoh. 5:19, 30; 8:28) Kama tunaiga Yesu kwa kuendelea kuwa wanyenyekevu, hatutajisifu wakati tunafanya mambo fulani ya muzuri. Hata kama tunatimiza nini mu utumishi wetu kwa Yehova, tujisifu juu ya pendeleo yenye tuko nayo ya kumutumikia Mungu wetu wa ajabu, hapana kujisifu juu yetu siye wenyewe. (Yer. 9:23, 24) Yeye njo tunapaswa kupatia sifa yote. Zaidi ya ile, kuko jambo fulani yenye tunaweza kutimiza bila musaada wa Yehova?​—1 Ko. 1:26-31.

12. Ni mu njia gani ingine tunaweza kuiga unyenyekevu wa Yesu? Fasiria.

12 Ona ni mu njia gani ingine tunaweza kuiga unyenyekevu wa Yesu. Wazia hii jambo: Muzee fulani anapitisha wakati mingi na iko nasaidia kijana fulani, mwenye ni mutumishi wa huduma, kutayarisha hotuba ya watu wote yenye atatoa kwa mara ya kwanza. Kisha kumusaidia, ule mutumishi wa huduma anatoa hotuba ya kutia moyo sana, yenye watu wote mu kutaniko wanafurahia. Kisha mukutano, mutu fulani anakuya kumuona ule muzee na kumuambia hivi: ‘Ndugu Fulani wa fulani alitoa hotuba ya muzuri sana, na weye uliona vile?’ Je, itaomba ule muzee aseme hivi: ‘Ndiyo, lakini nilipitisha wakati mingi na niko namusaidia?’ Ao anaweza kusema hivi kwa unyenyekevu: ‘Ndiyo, alitoa hotuba ya muzuri sana, niliifurahia kabisa?’ Kama tuko wanyenyekevu, hatutajisifu juu ya mambo ya muzuri yenye tunafanyia wengine. Tutafurahi kujua kama Yehova anaona na anasamini mambo yenye tunafanya. (Linganisha na Matayo 6:2-4; Ebr. 13:16) Kusema kweli, tutamufurahisha Yehova kama tunamuiga Yesu kwa kuwa wanyenyekevu.​—1 Pe. 5:6.

SOMO YA HURUMA

13. Yesu anaona nini wakati anakaribia muji wa Naini, na anafanya nini? (Luka 7:11-15)

13 Soma Luka 7:11-15. Wazia jambo yenye ilitokea mu mwaka wa 31 K.K.Y. wakati Yesu alikuwa mu safari ya kuenda Naini, muji wenye ulikuwa mu Galilaya, karibu na Shunemu kwenye nabii Elisha alifufua mutoto mwanaume wa mwanamuke fulani. (2 Fa. 4:32-37) Wakati Yesu anakaribia mulango mukubwa wa muji, anaona watu wako natoka inje ya ule muji ili kuenda ku mazishi. Ile tukio ilikuwa ya mubaya sana juu ule mujane alikuwa tu na ule mutoto moya mwenye alikufa. Lakini, ule mujane hakukuwa yeye peke; alikuwa pamoya na watu wengi wa mu ule muji. Yesu akasimamisha wale watu na akafanyia ule mama mujane, mwenye alifiwa, jambo fulani ya muzuri sana. Akafufua mutoto wake! Njo muujiza wa kwanza wa ufufuo kati ya miujiza tatu ya ufufuo yenye Yesu alifanya, yenye inazungumuziwa mu Injili.

Umuige Yesu kwa kuonyesha huruma wale wenye wanafiwa (Ona fungu ya 14-16)

14. Ni mambo gani ya maana yenye inazungumuziwa mu habari yenye kuwa mu Luka sura ya 7? (Ona pia picha.)

14 Fikiria mambo fulani ya maana yenye kuzungumuziwa mu habari yenye kuwa mu Luka sura ya 7. Yesu “alimuona” ule mama mwenye alikuwa na huzuni na kisha “akamusikilia huruma.” (Mustari wa 13) Nini njo ilifanya Yesu asikilie ule mama huruma? Pengine alimuona iko nalia wakati alikuwa natembea-tembea karibu na mwili wa mutoto wake. Yesu hakumusikilia tu huruma; lakini alimuonyesha huruma. Yesu aliongea naye, bila shaka alifanya vile kwa sauti ya kufariji, alimuambia hivi: “Acha kulia.” Kisha alifanya jambo fulani. Alifufua ule mutoto na “akamupatia mama yake.”​—Mustari wa 14, 15.

15. Muujiza wenye Yesu alifanya unatufundisha nini?

15 Muujiza wenye Yesu alifanya wa kufufua mutoto wa mujane unatufundisha nini? Tunajifunza somo ya kuonyesha huruma wale wenye wanafiwa. Kusema kweli, hatuna uwezo wa kufufua wafu, sawa vile Yesu. Lakini, sawa vile Yesu, tunaweza kuonyesha huruma wale wenye wanafiwa na wapendwa kwa kuenda ku kilio. Tena, tunaweza kuonyesha huruma kwa kusema ao kufanya jambo fulani yenye inaweza kuwasaidia na kuwafariji. d (Mez. 17:17; 2 Ko. 1:3, 4; 1 Pet. 3:8) Hata maneno kidogo ao ishara kidogo inaweza kuwafariji sana.

16. Sawa vile picha inaonyesha, habari ya mama fulani mwenye alitoka kufiwa na mutoto inakufundisha nini?

16 Fikiria hii jambo. Kulishapita miaka fulani tangu dada fulani aone mama moya mwenye alikuwa karibu yake iko nalia wakati walikuwa naimba wimbo ku mukutano. Ule wimbo ulikuwa nazungumuzia tumaini ya ufufuo. Mu ile kipindi njo ule mama alitoka tu kufiwa na mutoto wake mwanamuke. Wakati ule dada aliona vile, palepale akamukaribia, akamukumbatia, na wakaendelea kuimba pamoya. Kisha wakati kupita, ule mama alifikia kusema hivi: “Niliona kama ndugu na dada walinipenda sana.” Alifurahi sana juu aliendaka ku mukutano ile siku. Alisema tena hivi: “Kule, ni kusema, ku Jumba ya Ufalme, njo tunapataka musaada.” Tuko hakika kama Yehova anaonaka na kusamini hata mambo ya kidogo yenye tunafanyaka juu ya kuonyesha huruma wale wenye wanafiwa na wapendwa na wenye “kupondwa roho.”​—Zb. 34:18.

UJIFUNZE MAMBO YENYE ITATIA NGUVU IMANI YAKO

17. Tunajifunza nini mu hii habari?

17 Imani yetu itakuwa nguvu kama tunajifunza habari juu ya miujiza ya Yesu yenye kuwa mu Injili. Zile habari zinatufundisha kama Yehova na Yesu wanatupendaka sana na kama Yesu iko na nguvu ya kumaliza magumu yote ya wanadamu. Tena, zinatufundisha kama tunapaswa kuwa hakika kama ahadi za muzuri za Mungu juu ya wakati yenye kuya zitatimia hivi karibuni wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia. Wakati tuko nachunguza zile habari, tunaweza kufikiri sana juu ya namna tunaweza kuiga sifa za Yesu. Mu funzo yako ya pekee ao mu ibada ya familia, munaweza kujiwekea programu ya kujifunza habari juu ya miujiza ingine ya Yesu. Tafuta mambo yenye unaweza kujifunza na kisha uambie wengine ile mambo. Wazia namna ile mazungumuzo itakuwa yenye kujenga!​—Ro. 1:11, 12.

18. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

18 Ku mwisho wa utumishi wake hapa ku dunia, Yesu alifanya muujiza wa tatu wa ufufuo. Na njo muujiza wake wa mwisho wa ufufuo wenye Biblia inazungumuzia. Lakini ule muujiza ulikuwa tofauti. Alifufua rafiki yake mupendwa hata kama alikuwa alishafanya siku ine mu kaburi. Habari yenye kuwa mu Injili, yenye inazungumuzia ule muujiza, inaweza kutufundisha nini? Na namna gani tunaweza kuamini kabisa kama Mungu atatimiza ahadi yake ya kufufua wafu? Habari yenye kufuata itajibia ile maulizo.

WIMBO 20 Ulimutoa Mwana Wako Mupendwa

a Yesu alituliza zoruba yenye upepo mukali, aliponyesha wagonjwa, na alifufua wafu. Inagusaka moyo kusoma habari juu ya miujiza yenye alifanya! Habari juu ya miujiza ya Yesu iko mu Biblia, hapana juu ya kutufurahisha, lakini juu ya kutufundisha. Tutazungumuzia miujiza yenye itatusaidia tujifunze mambo fulani juu ya Yehova na Yesu, yenye inaweza kutia nguvu imani yetu na yenye itatusaidia kujua sifa za Mungu zenye tunaweza kuonyesha.

b Musomi moya wa Biblia anafasiria hivi: “Zamani mu mashariki, watu waliwaza kama walikuwa na daraka ya kuwa wakarimu na waliwaza kama mwenye alialika watu alipaswa kuhakikisha kuwa kuko mambo mingi yenye imetayarishwa zaidi tu ya ile yenye wageni wako nayo lazima. Juu ule mwenye alialika watu aonekane kama alipanga mambo muzuri, zaidi sana ku karamu ya ndoa, alipaswa kutayarisha vinywaji na chakula mingi sana.”

c Mu Injili muko miujiza zaidi ya 30 yenye Yesu alifanya. Yesu alifanya miujiza ingine mingi. Lakini mu Biblia, ile miujiza inazungumuziwa pamoya. Siku moya, “muji wote” ulikuya kumuona na “akaponyesha watu wengi wenye walikuwa na magonjwa.”​—Mk. 1:32-34.

d Juu ya kupata mapendekezo kuhusu mambo yenye unaweza kusema ao kufanya ili kufariji wale wenye walifiwa, soma habari “Wafariji Waliofiwa kama Yesu Alivyofanya” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 11, 2010.

e MAFASIRIO YA PICHA: Wakati bibi na bwana-arusi na wageni wao wako nakunywa divai, Yesu anasimama nyuma yao.