Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kujifunza

Namna ya Kujifunza

Uko nafaidika na mafasirio ya maandiko ya Biblia yenye kuwa mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari Kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova?

Ile Mafasirio inaweza kukusaidia uchimbe kabisa Neno ya Mungu. Inaweza kuwa na habari mbalimbali juu ya namna mambo ilikuwa wakati matukio fulani yenye Biblia inazungumuzia ilitokea, juu ya nini iliandikwa, ilihusu nani, ao maana ya maneno fulani ao misemwa fulani.

Watchtower MAKTABA KU ENTERNETE na JW Library® itakusaidia ufike mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari na upate referanse za andiko fulani ya Biblia. Unaweza kupata zile referanse ku sehemu ya funzo ya kila tafsiri ya Biblia.

Wakati uko natumia zile referanse, ukuwe muangalifu kuhusu tarehe. Referanse zenye kuwa na habari za mupya zinakuwaka ku mwanzo wa liste. Ku mwisho wa liste, kunaweza kuwa referanse za zamani zenye kuwa na mafasirio yenye ilishakuwa na mwangaza mupya.

  • Referanse za andiko yenye kuwa mu Musaada wa Kutafuta Habari inapatikana mu Watchtower MAKTABA KU ENTERNETE.

  • Juu ukuwe napata referanse za andiko ku JW Library, uchukue kitabu Musaada wa Kutafuta Habari na ufanye upya mambo yenye kuwa ndani wakati inaomba kufanya vile. Unaweza kufanya vile kwa kufinyanga button yenye kuwa yulu ya sehemu ya funzo ya kila sura ya andiko.