Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 16

“Ndugu Yako Atafufuka”!

“Ndugu Yako Atafufuka”!

“Yesu akamuambia [Marta]: ‘Ndugu yako atafufuka.’”​—YOH. 11:23.

WIMBO 151 Yehova Ataita

KIFUPI YA HABARI a

1. Namna gani kijana moya mwanaume alionyesha kama aliamini kabisa ahadi ya Mungu ya kufufua wafu?

 KIJANA moya mwenye kuitwa Matthew alikuwa na ugonjwa wa nguvu wenye uliomba afanyiwe upasuaji mara mingi. Wakati alikuwa na miaka saba, yeye na familia yake walikuwa naangalia programu ya JW Télédiffusion ya mwezi fulani. Karibu na mwisho wa ile programu, waliona video ya muziki yenye ilionyesha watu wako nakaribisha wale wenye walifufuka. b Kisha kuangalia ile programu, Matthew alikaribia wazazi wake, akawakamata ku mikono na kuwaambia hivi: “Mama na Papa, munaona, hata kama nakufa nitafufuka. Jambo yenye munaweza kufanya ni kuningoya tu; hamupaswe kuhangaika.” Unaweza kuwazia namna wale wazazi walijisikia wakati walifikia kujua kama mutoto wao aliamini kabisa ahadi ya Mungu ya kufufua wafu?

2-3. Juu ya nini ni muzuri kufikiria ahadi ya Mungu ya ufufuo?

2 Mara kwa mara, ni muzuri kufikiria ahadi ya ufufuo yenye kuwa mu Biblia. (Yoh. 5:28, 29) Juu ya nini? Juu hatujue ni wakati gani tunaweza kupatwa na magonjwa ya nguvu ao kufiwa na mupendwa wetu bila kutazamia. (Muh. 9:11; Yak. 4:13, 14) Kuamini ahadi ya Mungu ya ufufuo kunaweza kutusaidia kuvumilia magumu ya vile. (1 Te. 4:13) Maandiko inatuhakikishia kama Baba yetu wa mbinguni anatujua muzuri na anatupenda sana. (Lu. 12:7) Juu Yehova anatujua muzuri sana, atatufufua na utu uleule na kumbukumbu ileile. Na juu anatupenda sana, anatupatia tumaini ya uzima wa milele. Hata kama tunakufa atatufufua.

3 Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tatu. Kwanza, tutaona juu ya nini tunaamini kabisa kama ahadi ya Mungu ya kufufua wafu itatimia. Pili, tutazungumuzia habari fulani ya mu Biblia yenye itatia nguvu imani yetu. Ile habari iko na maneno ya andiko yetu ya musingi: “Ndugu yako atafufuka.” (Yoh. 11:23) Tatu, tutaona mambo ya kufanya ili tuamini kabisa kama ahadi ya Mungu ya ufufuo itatimia.

JUU YA NINI TUNAAMINI KABISA KAMA AHADI YA MUNGU YA KUFUFUA WAFU ITATIMIA

4. Juu tuamini ahadi fulani, tunapaswa kuwa hakika na mambo gani? Fasiria.

4 Juu tuamini ahadi fulani, tunapaswa kuwa hakika kama mwenye anaitoa anapenda na iko na nguvu ao uwezo wa kuitimiza. Kwa mufano, wazia upepo mukali unaharibisha sana nyumba yako. Rafiki yako fulani anakuya na kukuahidi hivi: ‘Nitakusaidia kujenga tena nyumba yako.’ Haseme uongo. Na uko hakika kama anapenda kukusaidia. Kama ni mujenzi mwenye kuwa na ufundi na kama iko na vifaa vyote vya kutumikisha, utakuwa hakika kama iko pia na uwezo wa kukusaidia. Kwa hiyo, utaamini kabisa ahadi yake. Sasa, tuseme nini juu ya ahadi ya Mungu ya kufufua wafu? Anapenda kabisa na iko na nguvu ya kuitimiza?

5-6. Nini njo inatuhakikishia kama Yehova anapenda kabisa kufufua wafu?

5 Yehova anapenda kabisa kufufua wafu? Bila shaka anapenda. Alipatia waandikaji wengi wa Biblia roho yake takatifu ili waandike ahadi yake ya kufufua wafu wakati yenye kuya. (Isa. 26:19; Hos. 13:14; Ufu. 20:11-13) Kila mara, Yehova anatimizaka ahadi zote zenye anatoaka. (Yos. 23:14) Kusema kweli, anapenda kabisa kufufua wafu. Juu ya nini tunasema vile?

6 Fikiria maneno yenye Yobu alisema. Alikuwa hakika kuwa hata kama anakufa Yehova angetamani kumufufua. (Yob. 14:14, 15, maelezo ya chini.) Yehova hayabadilika. Anatamani kufufua waabudu wake wenye walishakufa. Anapenda sana kuwafufua na kuwapatia afya ya muzuri na maisha yenye furaha. Tuseme nini juu ya mamiliare ya watu wenye hawakupata nafasi ya kujifunza kweli juu ya Yehova mbele wakufe? Yehova Mungu wetu wa upendo anapenda kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anapenda kuwapatia nafasi ya kuwa marafiki wake na kuishi milele ku dunia. (Yoh. 3:16) Mambo iko wazi: Yehova anapenda kabisa kufufua wafu.

7-8. Nini njo inatuhakikishia kama Yehova iko na nguvu ya kufufua wafu?

7 Yehova iko pia na nguvu ya kufufua wafu? Bila shaka iko nayo. Ni “Mweza-Yote.” (Ufu. 1:8) Kwa hiyo, iko na nguvu ya kutosha kila adui, hata kifo. (1 Ko. 15:26) Kujua vile kunatupatia nguvu na kunatufariji. Fikiria mufano wa dada Emma Arnold. Imani yake na ya familia yake ilijaribiwa wakati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu. Walifiwa na wapendwa wao mu kambi za mateso za Nazi. Ili kumufariji mutoto wake mwanamuke, Emma anasema hivi: “Kama watu wenye walishakufa hawatafufuliwa, ni kusema, adui yetu kifo iko na nguvu zaidi kuliko Mungu, hauone vile?” Kusema kweli, hakuna kitu yenye kuwa na nguvu kupita Yehova. Juu yeye ni Mungu Mweza-Yote mwenye aliumba uzima, iko na uwezo wa kupatia tena uzima wale wenye walishakufa.

8 Kumbukumbu ya Mungu haina mipaka. Ile njo sababu ingine yenye inatuhakikishia kama iko na uwezo wa kufufua wafu. Anaita kila nyota kwa jina. (Isa. 40:26) Anakumbuka pia wale wote wenye walishakufa. (Yob. 14:13; Lu. 20:37, 38) Anaweza kukumbuka hata mambo ya kidogo sana kuhusu wale wenye atafufua, kutia ndani utu wao na namna yao ya kuonekana, mambo yenye walifanya mbele wakufe, na kumbukumbu zao.

9. Juu ya nini tunaamini kama Yehova atatimiza ahadi yake ya kufufua wafu?

9 Kusema kweli, tunaamini kama Yehova atatimiza ahadi yake ya kufufua wafu wakati yenye kuya juu tunajua kama anapenda sana kufanya vile na iko na nguvu ya kuitimiza. Haitakuwa njo mara yake ya kwanza kufufua wafu. Ile njo sababu ingine yenye inafanya tuamini ahadi ya Mungu ya ufufuo. Zamani, alipatia Yesu na watumishi wake wengine waaminifu nguvu ya kufufua wafu. Tuzungumuzie habari moya ya mutu mwenye Yesu alifufua yenye kuwa mu Yohana sura ya 11.

RAFIKI MUPENDWA WA YESU ANAKUFA

10. Ni mambo gani inatokea Betania wakati Yesu iko nahubiri pembeni ya Yordani, na anafanya nini? (Yohana 11:1-3)

10 Soma Yohana 11:1-3. Wazia mambo yenye inatokea Betania karibu na mwisho wa mwaka wa 32 K.K.Y. Yesu iko na marafiki wake wa karibu mu ile kijiji, Lazaro na dada zake wawili, Maria na Marta. (Lu. 10:38-42) Lazaro anagonjwa na dada zake wawili wanahangaika. Wanamutumia Yesu habari wakati iko karibu na Yordani. Kutoka Betania kufika fasi yenye Yesu alikuwa, iliomba kutembea karibu siku mbili. (Yoh. 10:40) Jambo ya kuhuzunisha, wakati tu mujumbe anamufikia Yesu, Lazaro anakufa. Hata kama Yesu anajua kuwa rafiki yake amekufa, anaendelea kubakia fasi kwenye alikuwa kwa siku ingine mbili. Kisha njo anaenda sasa Betania. Kwa hiyo, wakati Yesu anafika Betania, kulikuwa kulishapita masiku ine tangu Lazaro akufe. Yesu anapenda sasa kufanya jambo fulani yenye italetea marafiki wake faida, na yenye itamuletea Mungu utukufu.​—Yoh. 11:4, 6, 11, 17.

11. Hii habari inatufundisha somo gani kuhusu urafiki?

11 Hii habari inatufundisha somo fulani kuhusu urafiki. Fikiria hii jambo: Wakati Maria na Marta walimutumia Yesu habari, hawakumuambia aende Betania. Walisema tu kama rafiki yake mupendwa alikuwa mugonjwa. (Yoh. 11:3) Wakati Lazaro alikufa, Yesu angemufufua na iko kule mbali. Lakini, aliamua kuenda Betania juu akuwe na marafiki wake Maria na Marta. Uko na rafiki mwenye anaweza kukusaidia bila kumuomba musaada? Bila shaka, unaweza kutegemea rafiki wa vile mu “nyakati za taabu.” (Mez. 17:17) Tumuige Yesu kwa kuwa marafiki wa vile. Sasa tuzungumuzie tena ile habari juu tuone jambo yenye ilitokea kisha.

12. Yesu alipatia Marta ahadi gani, na juu ya nini Marta alipaswa kuamini ile ahadi? (Yohana 11:23-26)

12 Soma Yohana 11:23-26. Marta anajua kama Yesu iko karibu na Betania. Anaenda mbio kukutana naye na kusema hivi: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” (Yoh. 11:21) Kusema kweli, Yesu angemuponyesha Lazaro. Lakini, Yesu anapenda kufanya jambo fulani ya ajabu zaidi. Anamutolea Marta hii ahadi: “Ndugu yako atafufuka.” Kisha anamuambia tena jambo ingine juu aamini kabisa ile ahadi, kwa kusema hivi: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” Kwa kweli, Mungu amemupatia Yesu nguvu ya kufufua wafu. Mbele ya pale, alifufuaka kijana fulani mwanamuke wakati mufupi tu kisha yeye kufa na alifufuaka pia mwanaume fulani mwenye pengine alikufaka ileile siku yenye alimufufuaka. (Lu. 7:11-15; 8:49-55) Sasa, ingewezekana kweli afufue mutu mwenye alikufa kumepita siku ine na mwenye alikuwa alishaanza kuoza?

“LAZARO, KUJA HUKU INJE!”

Yesu alisikilia huruma sana marafiki wake wenye walifiwa (Ona fungu ya 13-14)

13. Sawa vile Yohana 11:32-35 inaonyesha, Yesu alifanya nini wakati aliona Maria na watu wengine wako nalia? (Ona pia picha.)

13 Soma Yohana 11:32-35. Fikiria mambo yenye ilitokea kisha. Maria, dada mwingine wa Lazaro, alienda kukutana na Yesu. Alirudilia hii maneno yenye dada yake alisemaka: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” Yeye na watu wengine wenye walikuwa naye pale walihuzunika sana. Wakati Yesu aliwaona na kusikia namna wako nalia, alihuzunika sana. Juu alisikilia marafiki wake huruma, naye pia alitokwa na machozi. Alielewa namna mutu anahuzunikaka sana wakati anafiwa na mupendwa wake. Bila shaka, alipenda sana kutosha jambo yenye ilifanya walie.

14. Namna Yesu alitenda wakati aliona Maria iko nalia inatufundisha nini juu ya Yehova?

14 Namna Yesu alitenda wakati aliona Maria iko nalia inatufundisha kama Yehova ni Mungu mwenye huruma. Juu ya nini tunasema vile? Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, Yesu aliiga mawazo na hisia ya Baba yake. (Yoh. 12:45) Yesu alilia juu alisikilia huruma sana marafiki wake wenye walifiwa. Kwa hiyo, tunajua kama Yehova pia anatusikiliaka huruma wakati anaona tuko nalia. (Zb. 56:8) Ile haikuchochee kumukaribia zaidi Mungu wetu mwenye huruma?

Yesu alifanya jambo yenye ilionyesha kama iko na nguvu juu ya kifo (Ona fungu ya 15-16)

15. Sawa vile Yohana 11:41-44 inaonyesha, ni mambo gani yenye ilitokea ku kaburi ya Lazaro? (Ona pia picha.)

15 Soma Yohana 11:41-44. Yesu anafika ku kaburi ya Lazaro na anaomba watoshe jiwe yenye ilikuwa nafunika ile kaburi, Marta anakatala na kusema kama mwili wa Lazaro ulikuwa ulishaanza kunuka. Yesu akamuambia hivi: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?” (Yoh. 11:39, 40) Kisha, Yesu akaangalia mbinguni na kutoa sala mbele ya watu. Alipenda kumupatia Yehova utukufu wote juu ya mambo yenye ingetokea kisha. Ku mwisho, Yesu akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro, kuja huku inje!” Na Lazaro akatoka inje ya ile kaburi. Yesu alifanya jambo yenye watu fulani waliwaza kama haingewezekana.

16. Namna gani habari yenye kuwa mu Yohana sura ya 11 inafanya tuamini kabisa kama ahadi ya Mungu ya ufufuo itatimia?

16 Habari yenye kuwa mu Yohana sura ya 11 inafanya tuamini kabisa kama ahadi ya Mungu ya ufufuo itatimia. Namna gani? Kumbuka hii ahadi yenye Yesu alimutolea Marta: “Ndugu yako atafufuka.” (Yoh. 11:23) Sawa vile Baba yake, Yesu anapenda sana na iko na nguvu ya kutimiza ile ahadi. Machozi yake ilionyesha kabisa kama anapenda kutosha kifo yenye inaleteaka watu huzuni. Na juu Lazaro alitoka inje ya kaburi, ile ilionyesha kama Yesu iko pia na nguvu ya kufufua wafu. Ona pia jambo yenye alimukumbusha Marta: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?” (Yoh. 11:40) Tuko kabisa na sababu ya kuamini kama ahadi ya Mungu ya ufufuo itatimia. Sasa, tunaweza kufanya nini ili kuamini kabisa kama ile ahadi itatimia?

MAMBO YA KUFANYA ILI TUAMINI KABISA KAMA AHADI YA MUNGU YA UFUFUO ITATIMIA

17. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tuko nasoma habari zenye kuwa mu Biblia juu ya watu wenye walifufuliwa?

17 Usome na ufikiri sana juu ya habari ya watu wenye walifufuliwaka zamani. Mu Biblia muko habari munane za watu wenye walifufuliwaka ili kuishi ku dunia. c Inaweza kuwa muzuri kama unachunguza kwa uangalifu kila habari. Wakati uko nafanya vile, ukumbuke kama haiko habari ya kuwazia. Wale wanaume, wanamuke, na watoto walifufuliwaka kabisa. Tafuta mambo yenye ile habari inaweza kukufundisha. Fikiria namna kila habari inaonyesha kama Mungu anapenda na iko na nguvu ya kufufua wafu. Zaidi ya yote, fikiria pia ufufuo wa maana sana, ni kusema, ufufuo wa Yesu. Kumbuka kama mamia ya watu waliona wakati alifufuliwa. Na ile inafanya tuamini kabisa kama kutakuwa ufufuo.​—1 Ko. 15:3-6, 20-22.

18. Unaweza kufanya nini juu ya kutumia muzuri zaidi nyimbo zetu zenye kuzungumuzia tumaini ya ufufuo? (Ona pia maelezo ya chini.)

18 Utumie muzuri “nyimbo za kiroho” zenye zinazungumuzia ahadi ya Mungu ya ufufuo. d (Efe. 5:19) Zile nyimbo zitafanya uamini kabisa kama kutakuwa ufufuo. Uzisikilize, ufanye mazoezi juu ujue kuimba muzuri, na uzungumuzie maana ya maneno ya zile nyimbo mu ibada ya familia. Utie maneno ya zile nyimbo mu akili yako na uifikirie sana juu ikusaidie uamini kabisa kama kutakuwa ufufuo na juu iguse moyo wako. Kama unafanya vile wakati unapambana na jaribu fulani ao unafiwa na mupendwa wako, roho ya Yehova itakusaidia ukumbuke zile nyimbo ili zikufariji na kukupatia nguvu.

19. Tunaweza kuwazia mambo gani juu ya ufufuo? (Ona kisanduku “ Utawauliza Maulizo Gani?”)

19 Tumia uwezo wako wa kuwazia. Yehova alituumba na uwezo wa kujiwazia mu dunia mupya. Dada moya alisema hivi: “Nilipitisha wakati mingi niko nawazia maisha mu dunia mupya na nikaona sawa vile niko nasikia harufu ya muzuri ya maua mu Paradiso.” Wazia unaonana na wanaume na wanamuke wenye imani wenye Biblia inazungumuzia. Utapenda kuonana na nani? Utamuuliza maulizo gani? Wazia tena unaonana na wapendwa wako wakati watafufuliwa, fikiria mambo ya kwanza yenye utapenda kuwaambia, namna utawakumbatia kwa uchangamufu, na namna utafurahi wakati utawaona.

20. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

20 Tunamushukuru sana Yehova juu ya ahadi ya ufufuo. Tunapaswa kuwa hakika kabisa kama ile ahadi itatimia juu Yehova Mungu anapenda na iko na nguvu ya kuitimiza. Tuazimie basi kuamini kabisa kama ataitimiza. Kama tunafanya vile, tutamukaribia zaidi. Anaahidi hivi kila mumoja wetu: ‘Wapendwa wako watafufuliwa!

WIMBO 147 Ahadi ya Uzima wa Milele

a Kama mutu fulani mwenye unapenda alishakufa, bila shaka ahadi ya Mungu ya kufufua wafu itakufariji sana. Sasa, namna gani unaweza kufasiria wengine sababu yenye inafanya uamini ile ahadi? Na namna gani unaweza kuamini kama ile ahadi itatimia kabisa? Hii habari itatusaidia tuamini kabisa kama Mungu atatimiza ahadi yake ya kufufua wafu.

b Ile video ya muziki iko na kichwa Iko Karibu Sana. Ilitolewa mu JW Télédiffusion ya Mwezi wa 11, 2016.

c Ona kisanduku “Ufufuo Munane Wenye Kuzungumuziwa Katika Biblia” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, 2015, uku. 4.

d Ona nyimbo zenye kufuata mu kitabu ‘Tumuimbie Yehova Kwa Furaha:Wazia Uko mu Dunia Mupya” (Wimbo 139), “Kaza Macho ku Zawadi!” (Wimbo 144), na “Yehova Ataita” (Wimbo 151). Ona pia ku jw.org nyimbo za pekee zenye kufuata: “Iko Karibu Sana,” “Dunia Mupya Yenye Kuja,” na “Uone.”