Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

Tutiane Moyo ku Mikutano

Tutiane Moyo ku Mikutano

“Tufikiriane . . . , tutiane moyo.”​—EBR. 10:24, 25.

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini tunatoaka maelezo ku mikutano?

 JUU ya nini tunaendaka ku mikutano? Kwanza, ni juu ya kumutukuza Yehova. (Zb. 26:12; 111:1) Tunaendaka pia ku mikutano juu ya kutiana moyo mu hii wakati ya magumu. (1 Te. 5:11) Wakati tunatoa maelezo ku mikutano tutakuwa tumetimiza ile mambo mbili.

2. Ni nafasi gani zenye tunakuwaka nazo za kutoa maelezo ku mikutano?

2 Kila juma, tunakuwaka na nafasi za kutoa maelezo ku mikutano yetu. Kwa mufano, ku mwisho wa juma, tunaweza kutoa maelezo wakati ya Funzo ya Munara wa Mulinzi. Ku mikutano yetu ya katikati ya juma, tunaweza kutoa maelezo mu sehemu Mali ya Kiroho, Funzo ya Biblia ya Kutaniko, na mu sehemu zingine za mazungumuzo.

3. Nini njo inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kutoa maelezo, na namna gani Waebrania 10:24, 25 inaweza kutusaidia?

3 Siye wote tunapendaka kumutukuza Yehova na kutia moyo waabudu wenzetu. Lakini, kuko mambo yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kutoa maelezo. Tunaweza kuogopa kutoa maelezo, ao pengine tunaweza kupenda kutoa maelezo mara mingi, lakini wakati fulani kiongozi hatupatie nafasi ya kufanya vile. Mu ile hali, nini njo inaweza kutusaidia? Barua yenye Mutume Paulo aliandikia Waebrania itatusaidia kupata jibu. Wakati alikuwa nazungumuzia ulazima wa kukusanyika, alisema kama tunapaswa kujikaza ‘kutiana moyo.’ (Soma Waebrania 10:24, 25.) Kukumbuka kama wengine watatiwa moyo hata kupitia maelezo yetu ya mwepesi, yenye kuonyesha imani yetu, kutatutia moyo tukuwe natoa maelezo. Na kama kiongozi hatupatie nafasi ya kufanya vile, tunaweza kufurahi juu ile itasaidia wengine wapate nafasi ya kutoa maelezo.​—1 Pe. 3:8.

4. Ni mambo gani tatu yenye tutazungumuzia mu hii habari?

4 Mu hii habari, tutazungumuzia kwanza mambo yenye tunaweza kufanya ili kutiana moyo mu kutaniko yenye kuwa na watu kidogo mwenye hesabu ya wenye kutoa maelezo ni ya kidogo. Pili, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili kutiana moyo mu kutaniko yenye kuwa na watu wengi mwenye wengi wanatoaka maelezo. Na tatu, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili kutia wengine moyo kupitia mambo yenye tunasema wakati tunatoa maelezo.

TUTIANE MOYO MU KUTANIKO YENYE KUWA NA WATU KIDOGO

5. Tunaweza kufanya nini ili kutiana moyo mu kutaniko yenye kuwa na watu kidogo?

5 Mu Kutaniko yenye kuwa na watu kidogo ao mu kikundi fulani hamukuwake watu wengi wenye kiongozi anaweza kutaya ili watoe maelezo. Wakati fulani, inaweza kuomba angoye kidogo mbele mutu fulani anyangule mukono juu ya kujibia. Na ile inaweza kuonekana sawa vile mukutano unachokesha na hautie moyo. Unaweza kufanya nini mu ile hali? Ukuwe tayari kunyangula mukono wako kila mara. Kama unafanya vile, utachochea pia wengine wakuwe najibia mara mingi.

6-7. Tunaweza kufanya nini juu tusiogope sana wakati tuko natoa maelezo?

6 Tuseme nini kama unaogopaka kutoa maelezo? Watu wengi wanajisikiaka vile. Kwa hiyo, juu uweze kabisa kutia moyo ndugu na dada zako inaweza kuwa muzuri kufikiria mambo yenye unaweza kufanya juu usikuwe naogopa sana kutoa maelezo. Unaweza kufanya vile namna gani?

7 Inaweza kuwa muzuri kujikumbusha mapendekezo fulani yenye kuwa mu habari za Munara wa Mulinzi zenye tulishajifunza. b Kwa mufano, ujitayarishe muzuri. (Mez. 21:5) Kama unaelewa muzuri habari, itakuwa mwepesi kwako kutoa maelezo. Tena, utayarishe maelezo ya mufupi. (Mez. 15:23; 17:27) Maelezo ya mufupi itakusaidia usiogope sana wakati uko naitoa. Maelezo ya mufupi, pengine yenye kuwa na musemwa moya ao mbili inaweza kuwa hata mwepesi kwa ndugu na dada zako kuelewa kuliko maelezo ya murefu yenye kuwa na mawazo mingi. Wakati unatoa maelezo ya mufupi mu maneno yako, utaonyesha kama ulijitayarisha muzuri na kama ulielewa habari muzuri.

8. Yehova anaona namna gani bidii yetu ya kutoa maelezo?

8 Tuseme nini kama ungali naogopa kutoa maelezo mara mingi kisha kutumikisha mapendekezo fulani kati ya ile mapendekezo? Ukuwe hakika kama Yehova atasamini bidii yako ya kutoa maelezo. (Lu. 21:1-4) Yehova hatuombe kufanya mambo yenye kupita uwezo wetu. (Flp. 4:5) Ujue mambo yenye unaweza kufanya, ujiwekee muradi wa kuifanya, na usali juu ya kuwa na moyo wenye kutulia. Ku mwanzo, unaweza kujiwekea muradi wa kutoa tu jibu moya ya mufupi.

TUTIANE MOYO MU KUTANIKO YENYE KUWA NA WATU WENGI

9. Ni magumu gani yenye inakuwaka mu kutaniko yenye kuwa na watu wengi?

9 Kama kutaniko yenu iko na wahubiri wengi, unaweza kuwa na magumu ingine. Pengine, ndugu na dada wengi wananyangulaka mikono ili kutoa maelezo na ile inafanyaka kiongozi asikutaye. Kwa mufano, Danielle anapendaka sana kutoa maelezo ku mikutano. c Anaonaka ile kuwa sehemu ya ibada yake, njia ya kutia moyo wengine, na njia ya kutia imani yake nguvu mu mambo yenye Biblia inafundisha. Lakini, wakati ule dada alihamia mu kutaniko yenye kuwa na watu wengi, kiongozi hakukuwa namutaya mara mingi. Na wakati fulani hakumutaya hata mara moya mwanzo mupaka mwisho wa mukutano. Alisema hivi: “Nilikasirika. Niliona sawa vile nakosa pendeleo fulani. Wakati ile inafika tena na tena, mutu anaweza kuanza kujiuliza kama kiongozi iko nakatala kumutaya kimakusudi.”

10. Tunaweza kufanya nini juu tupate nafasi ya kutoa maelezo?

10 Ulishakajisikia sawa vile Danielle? Kama ni vile, unaweza kuvunjika moyo na kuanza tu kusikiliza mukutano. Lakini, usiache kutoa maelezo. Unaweza kufanya nini? Inaweza kuwa muzuri kama unatayarisha maelezo mingi ku kila mukutano. Na kama haupate nafasi ya kutoa maelezo ku mwanzo wa funzo, utakuwa na nafasi ingine ya kutoa maelezo wakati mukutano uko naendelea. Wakati uko natayarisha Funzo ya Munara wa Mulinzi fikiria namna kila fungu inapatana na kichwa ya ile habari. Kama unafanya vile, pengine utapata maelezo ya muzuri yenye unaweza kutoa. Zaidi ya ile, unaweza kutayarisha maelezo yenye kuwa mu mafungu yenye kuzungumuzia mafundisho mazito yenye iko nguvu kufasiria. (1 Ko. 2:10) Juu ya nini? Juu kutakuwa watu kidogo wenye watapenda kutoa maelezo mu ile sehemu. Sasa utafanya nini kama unatumikisha ile mapendekezo yote lakini kisha mikutano mingi haupewe tu nafasi ya kutoa maelezo? Mbele mukutano uanze, unaweza kuambia kiongozi kama unapenda kuleta jibu ya ulizo fulani.

11. Wafilipi 2:4 inatutia moyo kufanya nini?

11 Soma Wafilipi 2:4. Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuonyesha kama Wakristo wanapaswa kutafuta faida za wengine. Tunaweza kufanya nini ili kutumikisha ile shauri ku mikutano? Kwa kukumbuka kama wengine pia wanapenda kutoa maelezo.

Sawa vile tu unaachiaka wengine nafasi ya kusema wakati muko munazungumuza, uachie pia wengine nafasi ya kutoa maelezo ku mikutano (Ona fungu ya 12)

12. Ni mu njia gani moya tunaweza kutia wengine moyo ku mikutano? (Ona pia picha.)

12 Fikiria ile jambo mu hii njia. Wakati uko naongea na marafiki wako, utasema mingi sana mupaka wakose nafasi ya kusema? Hapana, juu unapenda nao pia waseme. Vilevile, tunapenda kuachia wengine nafasi ya kutoa maelezo ku mikutano kadiri inawezekana. Kusema kweli, njia moya kati ya njia za muzuri za kutia moyo ndugu na dada zetu ni kuwapatia nafasi ya kutoa maelezo yenye kuonyesha imani yao. (1 Ko. 10:24) Tuone namna tunaweza kufanya vile.

13. Tunaweza kufanya nini juu tuachie wengine nafasi ya kujibia?

13 Moya kati ya mambo yenye inafanya tutoe maelezo ya mufupi ni juu tupatie watu wengi zaidi nafasi ya kutoa pia maelezo. Wazee na wahubiri wenye uzoefu wanaweza kuonyesha mufano. Hata wakati unatoa maelezo ya mufupi, epuka kuzungumuzia mawazo mingi sana. Kama unazungumuzia mawazo mingi sana yenye kuwa mu fungu, hakutabakia mambo mingi yenye wengine watasema. Kwa mufano, mu hii fungu muko hii mapendekezo mbili: Kutoa maelezo ya mufupi na kuepuka kuzungumuzia mawazo mingi sana. Kama weye njo utakuwa wa kwanza kutoa maelezo mu hii fungu, hauone kama itakuwa muzuri kujibia pendekezo moya kati ya ile mapendekezo?

Ni wakati gani inaweza kuwa muzuri usinyangule mukono ku mukutano? (Ona fungu ya 14) f

14. Nini njo inaweza kukusaidia kuamua ni mara ngapi utanyangula mukono? (Ona pia picha.)

14 Utumie busara wakati unaamua ni mara ngapi utatoa maelezo. Kama tunanyangula mukono mara mingi itakuwa sawa vile tunalazimisha kiongozi atutaye mara mingi hata kama wengine hawayatoa maelezo. Ile itafanya wengine wasinyangule tena mikono.​—Muh. 3:7.

15. (a) Hatupaswe kufanya nini kama kiongozi hatupatie nafasi ya kutoa maelezo? (b) Viongozi wanaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama wanafikiria kila mutu? (Ona kisanduku “ Kama Uko Naongoza”)

15 Kama wahubiri wengi wananyangula mukono wakati ya funzo, ile inaweza kufanya tusijibie mara mingi sawa vile tunapenda. Wakati fulani, pengine kiongozi hatatutaya hata mara moya. Ile inaweza kutuvunja moyo. Lakini, hatupaswe kukasirika.​—Muh. 7:9.

16. Tunaweza kufanya nini juu ya kutia wengine moyo wakati wanatoa maelezo?

16 Kama haitawezekana utoe maelezo mara mingi vile unapenda, inaweza kuwa muzuri usikilize kwa uangalifu wakati wengine wako natoa maelezo na kisha mukutano uwapongeze. Pengine ndugu na dada zako watatiwa moyo sana wakati unawapongeza sawa vile tu wangetiwa moyo wakati unatoa maelezo. (Mez. 10:21) Pongezi ni njia ingine ya kutiana moyo.

MAMBO INGINE YA KUFANYA ILI KUTIANA MOYO

17. (a) Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao watayarishe maelezo yenye kufaa? (b) Sawa vile uliona mu video, inaomba kufanya mambo gani ine juu ya kutayarisha maelezo? (Ona pia maelezo ya chini.)

17 Ni mambo gani ingine yenye tunaweza kufanya juu ya kutiana moyo ku mikutano? Kama uko muzazi, usaidie watoto wako watayarishe maelezo yenye kufaa kulingana na miaka yao. (Mt. 21:16) Wakati fulani, mambo mazito sawa vile magumu ya ndoa ao namna ya kuwa na mwenendo safi inazungumuziwaka wakati ya funzo. Hata vile, kunaweza kuwa fungu moya ao mbili kwenye mutoto anaweza kutoa maelezo. Tena, usaidie watoto wako waelewe juu ya nini kiongozi hatawataya kila mara wakati wananyangula mikono. Kufanya vile, kunaweza kuwasaidia wasikasirike wakati kiongozi anataya wengine.​—1 Ti. 6:18. d

18. Tunaweza kufanya nini ili kuepuka kukaza akili juu yetu wakati tuko natoa maelezo? (Mezali 27:2)

18 Siye wote tunaweza kutayarisha maelezo yenye itamutukuza Yehova na yenye itajenga Wakristo wenzetu. (Mez. 25:11) Kama tunazungumuzia jambo yenye inatuhusu, tunapaswa kuepuka kusema mambo mingi juu yetu. (Soma Mezali 27:2; 2 Ko. 10:18) Kuliko kufanya vile, tutakaza akili juu ya Yehova, Neno yake, na watu wake. (Ufu. 4:11) Lakini, kama fungu iko na ulizo yenye inaomba mutu azungumuzie mawazo yake juu ya jambo fulani, ni muzuri kufanya vile. Kwa mufano, fungu yenye kufuata ya hii habari iko na ulizo ya vile.

19. (a) Juu ya nini ni muzuri kufikiria wote wenye wanakuya kukusanyika? (Waroma 1:11, 12) (b) Weye kipekee unafurahiaka nini kuhusu kutoa maelezo ku mikutano?

19 Juu hakuna sheria zenye kuonyesha namna ya kutoa maelezo, siye wote tunapaswa kujikaza kutoa maelezo yenye kutia moyo. Ile inaweza kumaanisha kuepuka kutoa maelezo mara mingi sana. Ao inaweza kumaanisha kutosheka na nafasi zenye tuko nazo za kutoa maelezo na kufurahi wakati wengine wanapata nafasi ya kufanya vile. Kama tunajikaza kutafuta faida ya wengine ku mikutano, siye wote tunaweza kufurahia “ubadilishanaji wa kitia-moyo.”​—Soma Waroma 1:11, 12.

WIMBO 93 Bariki Mikutano Yetu

a Tunatiana moyo wakati tunatoa maelezo ku mikutano. Lakini watu fulani wanasikiaka woga wa kutoa maelezo. Na wengine wanapendaka kiongozi awataye mara mingi ili kutoa maelezo. Ikuwe hali ni gani, tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunafikiriana juu siye wote tuweze kutiwa moyo? Tunaweza kufanya nini juu tutoe maelezo yenye itachochea ndugu na dada zetu katika upendo na matendo ya muzuri? Hii habari itafasiria ile jambo.

b Juu ya kupata mapendekezo zaidi, usome tena habari yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 1, 2019, uku. 8-13, na Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 9, 2003, uku. 19-22.

c Jina imebadilishwa.

e Ona habari yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, uku. 32, na habari yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 9, 2003, uku. 21-22.

f MAFASIRIO YA PICHA: Mu kutaniko yenye kuwa na watu wengi, ndugu mwenye alishatoa maelezo anaachia wengine nafasi ya kufanya vile.