Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 16

WIMBO 64 Kufanya Kazi ya Mavuno kwa Furaha

Namna ya Kufurahia Zaidi Mahubiri

Namna ya Kufurahia Zaidi Mahubiri

“Mumutumikie Yehova kwa furaha.”ZB. 100:2.

WAZO KUBWA

Hii habari inazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili tufurahie zaidi kazi ya kuhubiri.

1. Juu ya nini inakuwaka nguvu kwa Wakristo fulani kuzungumuza na watu wengine mu mahubiri? (Ona pia picha.)

 SIYE watu wa Yehova, tunahubiria wengine kwa sababu tunamupenda Baba yetu wa mbinguni na tunapenda kusaidia majirani wetu wafikie kumujua. Wahubiri wengi wanafurahia sana kazi ya kuhubiri. Lakini ni nguvu kwa wengine kuifurahia. Juu ya nini? Wahubiri fulani ni watu wa haya na hawajitumainie. Wengine hawajisikie huru kuenda ku nyumba za watu bila kualikwa. Wengine wanaogopa kama watu watawakasirikia. Wengine walifundishwa kuepuka mambo yenye inaweza kukasirisha watu. Hata kama wanamupenda sana Yehova, inakuwaka nguvu kwa wale ndugu na dada kuhubiria watu wenye hawajue. Lakini, juu wanajua kama hii kazi ni ya maana sana, wanajikaza kuhubiri kwa ukawaida. Bila shaka Yehova anafurahi sana!

Unafurahia kazi ya kuhubiri? (Ona fungu ya 1)


2. Kama ni nguvu kwako kufurahia kazi ya kuhubiri, juu ya nini haupaswe kuvunjika moyo?

2 Ni nguvu kwako kufurahia kazi ya kuhubiri kwa sababu ya mambo kama ile? Kama ni vile, usivunjike moyo. Kukosa kujitumainia kunaonyesha kama uko munyenyekevu na haupendi watu wakukazie uangalifu. Kunaonyesha pia kama unapenda kuepuka mabishano. Tena hakuna mwenye anapendaka wengine wamukasirikie, zaidi sana wakati iko najikaza kuwafanyia mambo ya muzuri. Baba yako wa mbinguni anajua ile matatizo yote yenye uko napambana nayo na anapenda kukupatia musaada wenye uko nao lazima. (Isa. 41:13) Mu hii habari muko mapendekezo tano juu ya namna ya kupambana na hali za vile na mambo yenye unaweza kufanya juu ufurahie zaidi kazi ya kuhubiri.

ACHA NENO YA MUNGU IKUTIE NGUVU

3. Nini ilisaidia nabii Yeremia ahubirie wengine?

3 Wakati watumishi wa Mungu wa zamani walikuwa na mugao wa nguvu, Neno ya Mungu iliwatia nguvu. Kwa mufano, fikiria nabii Yeremia. Alisita wakati Mungu alimupatia mugao wa kuhubiri. Yeremia alisema hivi: “Sijue namna ya kusema, kwa maana niko kijana mudogo tu.” (Yer. 1:6) Ni nini ilimusaidia akuwe na uhodari wa kuhubiri? Neno la Mungu njo lilimutia nguvu. Alisema hivi: “Lilikuwa kama moto wenye kuwaka wenye kufungiwa katika mifupa yangu, na nikachoka kulizuia.” (Yer. 20:8, 9) Hata kama watu wa mu eneo yenye Yeremia alihubiri hawakupendezwa na ujumbe wake, ujumbe wenye alikuwa nahubiri ulimupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kutimiza mugao wake.

4. Matokeo inakuwa nini wakati tunasoma Neno ya Mungu na kutafakari juu ya mambo yenye tunasoma? (Wakolosai 1:9, 10)

4 Ujumbe wenye kuwa mu Neno ya Mungu unatia Wakriso nguvu. Wakati mutume Paulo aliandikia kutaniko yenye ilikuwa Kolosai, alisema kama kuwa na ujuzi wenye hauna makosa kungechochea wale ndugu “watembee kwa namna yenye kumustahili Yehova” wakati walikuwa naendelea “kuzaa matunda katika kila kazi njema.” (Soma Wakolosai 1:9, 10.) Ile kazi njema ilitia ndani kuhubiri habari njema. Kwa hiyo wakati tunasoma Neno ya Mungu na kutafakari juu ya mambo yenye tunajifunza, tunamutumainia Yehova zaidi na tunaona kama ni jambo ya maana sana kuhubiri habari njema ya Ufalme.

5. Tunaweza kufanya nini ili tufaidike zaidi wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia?

5 Ili Neno ya Mungu ituletee faida kabisa, hatupaswe kuenda mbio-mbio wakati tuko nasoma, wakati tuko najifunza, na kutafakari juu ya mambo yenye tumesoma. Enda polepole. Kama unasoma andiko yenye hauelewe muzuri, usiipite tu. Tumia kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova ao vyombo vyetu vingine vya kutafuta habari ili upate mafasirio zaidi juu ya ile andiko. Kama unaenda polepole wakati uko najifunza, utaamini kabisa kama mambo yenye Neno ya Mungu inasema ni ya kweli. (1 Te. 5:21) Kadiri unaamini zaidi mambo yenye uko najifunza, ni vile utafurahia kuielezea wengine.

JITAYARISHE MUZURI KWA AJILI YA MAHUBIRI

6. Juu ya nini tunapaswa kujitayarisha muzuri kwa ajili ya mahubiri?

6 Kama unajitayarisha muzuri kwa ajili ya mahubiri, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuzungumuza na wengine. Mbele ya kuwatuma mu mahubiri, Yesu alisaidia wanafunzi wake wajitayarishe. (Lu. 10:1-11) Juu walitumikisha mambo yenye Yesu aliwafundisha, walifurahi sana kwa sababu ya mambo yenye waliweza kutimiza.—Lu. 10:17.

7. Tunaweza kujitayarisha namna gani kwa ajili ya mahubiri? (Ona pia picha.)

7 Tunaweza kujitayarisha namna gani kwa ajili ya mahubiri? Tufikirie namna tunaweza kufasiria kweli muzuri zaidi mu maneno yetu wenyewe. Pia ni jambo ya maana tufikirie mawazo ao maulizo mbili ao tatu yenye watu wa mu eneo yetu wanazoea kuwa nayo, kisha tufikirie mbele ya wakati namna tunaweza kuwajibu. Na wakati tunakaribia watu, tunaweza kujikaza kutulia, kucheka kidogo, na kuzungumuza nao kwa njia ya urafiki.

Ujitayarishe muzuri kwa ajili ya mahubiri (Ona fungu ya 7)


8. Ni mu njia gani Wakristo wako sawa vyombo vya udongo vyenye Paulo alizungumuzia mu mufano wake?

8 Mutume Paulo alizungumuzia mufano wenye kuonyesha daraka yetu mu kazi ya kuhubiri wakati alisema: “Tuko na hazina hii katika vyombo vya udongo.” (2 Ko. 4:7) Ile hazina ni nini? Ni kazi ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme wenye unaweza kuokoa uzima. (2 Ko. 4:1) Vyombo vya udongo ni nini? Vinafananisha watumishi wa Mungu, wenye wanahubiria wengine habari njema. Mu wakati wa Paulo, wafanyabiashara walizoea kuweka mu mitungi ya udongo vitu vya maana sawa vile chakula, divai, na makuta. Vilevile, Yehova ametupatia ujumbe wa maana, ni kusema habari njema. Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuwa na nguvu yenye tuko nayo lazima ili kutangazia wengine ule ujumbe kwa uaminifu.

UMUOMBE YEHOVA AKUPE UHODARI

9. Namna gani tunaweza kuacha kuogopa watu? (Ona pia picha.)

9 Wakati fulani, tunaweza kuogopa watu. Namna gani tunaweza kupambana na ile hali? Fikiria sala yenye mitume walitoa wakati wapinzani waliwaamuru waache kuhubiri. Kuliko kuogopa, walimuomba Yehova awasaidie “waendelee kutangaza neno [lake] bila woga wowote.” Bila kukawia Yehova alijibia sala yao. (Mdo. 4:18, 29, 31) Kama wakati fulani tunaogopa watu, siye pia tunapaswa kumuomba Yehova atusaidie. Umuombe Yehova akusaidie ili upendo wako kwa watu ukuwe nguvu zaidi kuliko woga wako.

Uombe Yehova akupatie uhodari (Ona fungu ya 9)


10. Namna gani Yehova anatusaidia tutimize daraka yetu ya kuwa Mashahidi? (Isaya 43:10-12)

10 Yehova ametuweka kuwa Mashahidi wake, na anatuahidi kama atatusaidia tukuwe hodari. (Soma Isaya 43:10-12.) Anafanya vile mu njia mbalimbali. Tuzungumuzie tu njia ine. Kwanza, Yesu iko pamoya na siye wakati wote wenye tuko nahubiri habari njema. (Mt. 28:18-20) Pili, Yehova ameweka malaika ili watusaidie. (Ufu. 14:6) Tatu, Yehova ametupatia musaidizi, ni kusema roho takatifu ili itukumbushe mambo yenye tumejifunza. (Yoh. 14:25, 26) Ine, Yehova ametupatia ndugu na dada wa kutusindikiza mu mahubiri. Kwa musaada wa Yehova na wa ndugu na dada zetu wenye upendo, tuko na mambo yote ya lazima ili tutimize muzuri mugao wetu.

UJIPATANISHE NA HALI NA UKUWE NA MAWAZO YENYE KUFAA

11. Unapaswa kufanya nini juu upate watu wengi zaidi mu mahubiri? (Ona pia picha.)

11 Unavunjikaka moyo wakati unapata tu watu kidogo mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba? Kama ni vile, ujiulize hivi: ‘Watu wa mu eneo yangu, wako wapi hii saa?’ (Mdo. 16:13) ‘Wako ku kazi ao wako mu soko?’ Kama ni vile, hauone kama unaweza kupata watu wengi zaidi ukifanya mahubiri ya mu barabara? Ndugu mwenye kuitwa Joshua anasema hivi: “Nimepata nafasi za kuhubiri wakati nilikuwa natembelea fasi zenye kuwa na maduka ao fasi zingine za watu wengi.” Yeye na bibi yake, Bridget, wamepata pia watu wengi zaidi ku nyumba wakati wanawatembelea mangaribi na Siku ya Yenga kisha midi.—Efe. 5:15, 16.

Ubadilishe fasi na saa yako ya kuhubiri (Ona fungu ya 11)


12. Namna gani tunaweza kujua mambo yenye watu wanaamini ao yenye kuwahangaisha?

12 Kama watu wengi hawapendezwe na ujumbe wako, tafuta kujua mambo yenye wanaamini ao yenye kuwahangaisha. Ili kuanzisha mazungumuzo, Joshua na Bridget wanatumiaka ulizo yenye kuwa ku mwanzo wa trakte. Kwa mufano, kwa kutumia trakte Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia? wanasemaka hivi: “Watu fulani wanaona kama Biblia ni kitabu ya Mungu, lakini wengine hawaone vile. Weye unawaza nini?” Mara mingi ile inafanyaka mazungumuzo iendelee.

13. Juu ya nini tunapaswa kuona kama tumetimiza muzuri kazi ya kuhubiri hata kama watu hawakubali ujumbe wetu? (Mezali 27:11)

13 Kama watu wanakataa ujumbe wetu, ile haimaanishe kama hatukutimiza muzuri mugao wetu wa kuhubiri. Juu ya nini? Juu tumefanya mambo yenye Yehova na Mwana wake wanatuomba kufanya, ni kusema tumetoa ushahidi. (Mdo. 10:42) Hata wakati hatupate mutu wa kuzungumuza naye mu mahubiri ao wakati watu wanakataa ujumbe wetu, tunaweza kuwa na furaha kwa sababu tunajua kama tuko namufurahisha Baba yetu wa mbinguni.—Soma Mezali 27:11.

14. Juu ya nini tunapaswa kufurahi wakati muhubiri mwingine anapata mutu mwenye kupendezwa mu eneo?

14 Tunaweza pia kufurahi wakati muhubiri mwingine anapata mutu mwenye kupendezwa mu eneo. Munara wa Mulinzi umefananisha kazi yetu ya kuhubiri na kazi ya kutafuta mutoto mwenye amepotea. Watu wengi wanasaidia kutafuta, wanatafuta mu kila eneo. Wakati mutoto anapatikana, kila mutu anafurahi, hapana ule tu mwenye alimupata. Vilevile, kazi ya kufanya wanafunzi haiko kazi ya mutu mumoja, ni kazi yenye tunafanya siye wote pamoya. Siye wote tunapaswa kutumika pamoya ili kuhubiria eneo yote, na siye wote tunafurahi wakati mutu anaanza kukusanyika.

KAZIA AKILI UPENDO WAKO KWA YEHOVA NA KWA JIRANI

15. Namna gani Matayo 22:37-39 inatusaidia tukuwe na bidii zaidi mu kazi ya kuhubiri? (Ona pia picha)

15 Tunaweza kuongeza bidii yetu mu kazi ya kuhubiri ikiwa tunakazia akili upendo wetu kwa Yehova na kwa jirani. (Soma Matayo 22:37-39.) Fikiria namna Yehova anafurahi sana wakati anatuona tuko nafanya kazi ya kuhubiri, na namna watu watafurahi wakati wataanza kujifunza Biblia! Fikiria pia namna ujumbe wetu utasaidia watu wenye kuukubali waokolewe.—Yoh. 6:40; 1 Ti. 4:16.

Kukazia akili upendo wako kwa Yehova na kwa jirani kutakusaidia ufurahie zaidi kazi ya kuhubiri (Ona fungu ya 15)


16. Namna gani tunaweza kufurahia kazi ya kuhubiri hata kama hatuwezi kutoka ku nyumba? Toa mifano fulani.

16 Kuko sababu zenye zinafanya usiweze kutoka ku nyumba? Kama ni vile, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya juu ya kuonyesha kama unamupenda Yehova na unapenda jirani. Mu kipindi ya Korona, Samuel na Dania hawakuweza kutoka ku nyumba. Hata kama walikuwa na ile magumu, waliendelea kutoa ushahidi kwa ukawaida kupitia telefone, barua, na waliongoza mafunzo ya Biblia kupitia Zoom. Samuel alihubiria wale wenye alikutana nao ku hopitali kwenye alikuwa napata matunzo ya ugonjwa wa kansere. Anasema hivi: “Magumu inafanyaka tuchoke kiakili, kimwili, na kiroho. Tunapaswa kuwa na furaha mu utumishi wetu kwa Yehova.” Mu ile kipindi ya magumu, Dania alianguka na alilazimika kubakia ku kitanda kwa miezi tatu. Kisha alitumia kinga ya vilema kwa miezi sita. Anasema hivi: “Nilijikaza kufanya yote yenye ninaweza kulingana na hali yangu. Niliweza kuhubiria munganga mwenye alikuwa nanitembelea, na kuzungumuza na wale wenye walikuwa natuletea vitu ku nyumba. Pia nilikuwa na mazungumuzo ya muzuri pamoya na mwanamuke fulani mwenye alikuwa natumika mu kompanyi fulani ya mambo ya kinganga.” Hali ya Samuel na Dania iliwazuia kufanya mambo fulani, lakini walifanya yote yenye waliweza na ile iliwaletea furaha.

17. Namna gani unaweza kufaidika na mapendekezo yenye tunazungumuzia mu hii habari?

17 Mapendekezo yenye tunazungumuzia mu hii habari inaweza kutusaidia ikiwa tunaitumikisha yote. Kila pendekezo iko sawa vile kiungo kimoya kati ya viungo mbalimbali vyenye vinatumiwa ili kupika chakula fulani. Wakati viungo vyote vinatiwa pamoja, chakula inakuwa muzuri sana. Vilevile kama tunatumikisha mapendekezo yote yenye tumezungumuzia, tutaweza kupambana na matatizo mbalimbali na tutafurahia zaidi kazi ya kuhubiri.

NAMNA GANI KUFANYA MAMBO YENYE KUFUATA KUNAWEZA KUKUSAIDIA UFURAHIE ZAIDI KAZI YA KUHUBIRI?

  • Kujitayarisha muzuri

  • Kuomba Yehova akupatie uhodari

  • Kukazia akili upendo wako kwa Yehova na kwa jirani

WIMBO 80 “Uonje na Uone Vile Yehova Ni Mwema”