Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 14

WIMBO 56 Acha Kweli Ikuongoze

“Tusonge Mbele Kuelekea Ukomavu”

“Tusonge Mbele Kuelekea Ukomavu”

“Tusonge mbele kuelekea ukomavu.”EBR. 6:1.

WAZO KUBWA

Ona namna Mukristo mwenye kukomaa kiroho anawaza na kutenda kupatana na mapenzi ya Mungu, na anakamata maamuzi ya hekima.

1. Yehova anatuomba nini?

 WAZAZI wanakuwaka na furaha sana wakati mutoto wao anazaliwa na afya ya muzuri. Hata kama wazazi wanapendaka mutoto wao mudogo, hawawezi kufurahia abakie mutoto maisha yote. Na wakiona mutoto wao hakomale, ile inaweza kuwaletea wasiwasi sana. Vilevile, Yehova anafurahi wakati tunaanza kutembea, ni kusema wakati tunakamata hatua ya kufuata Yesu. Lakini hapendi tubakie watoto kiroho. (1 Ko. 3:1) Anatuomba tukuwe “watu wazima” kiroho.—1 Ko. 14:20.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Kuwa watu wazima kiroho maana yake nini? Namna gani tunafikia kuwa Wakristo wenye kukomaa kiroho? Namna gani chakula kigumu kinatusaidia kukomaa kiroho? Juu ya nini hatupaswe kujitumainia kupita kiasi? Mu hii habari, tutazungumuzia majibu ya ile maulizo.

KUWA MUKRISTO MUKOMAVU MAANA YAKE NINI?

3. Kuwa mutu muzima kiroho maana yake nini?

3 Mu Biblia, neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “mutu muzima” inaweza pia kumaanisha “mukomavu,” “kamili,” ao “mwenye kuenea.” a (1 Ko. 2:6) Tunakuwa Wakristo wakomavu, ao watu wazima kiroho, wakati tunaacha kuwa watoto kiroho na tunakuwa wanaume na wanamuke wenye kukomaa kiroho. Lakini, hata kisha kufikia kukomaa kiroho hatupaswe kuacha kufanya maendeleo. (1 Ti. 4:15) Siye wote, kutia ndani vijana, tunaweza kuwa watu wakomavu kiroho. Lakini nini njo inaonyesha kama Mukristo amekomaa kiroho?

4. Nini njo inaonyesha kama Mukristo amekomaa kiroho?

4 Mukristo mukomavu kiroho ni mutu mwenye anafuata mambo yote yenye Mungu anaomba, hachague tu ile yenye kumufurahisha. Wakati fulani anaweza kufanya makosa juu hakamilike. Lakini, anaonyesha mu maisha yake ya kila siku kama mawazo yake na matendo yake inapatana na mapenzi ya Mungu. Anavaa utu mupya na anajikaza sikuzote ili namna yake ya kuwaza ikaribie zaidi na zaidi mawazo ya Mungu. (Efe. 4:22-24) Amejizoeza kukamata maamuzi yenye hekima yenye inategemea sheria na kanuni za Yehova. Kwa hiyo hana lazima ya liste murefu ya sheria za kumuongoza. Wakati anakamata uamuzi, anajinyima ili atende kulingana na mambo yenye aliamua.—1 Ko. 9:26, 27.

5. Mukristo mwenye hakomae kiroho iko mu hatari gani? (Waefeso 4:14, 15)

5 Lakini, ni mwepesi kwa Mukristo mwenye anabakia mutoto kiroho aamini “udanganyifu” na “ujanja wa watu.” Pia ni mwepesi aamini waasi-imani na habari za uongo zenye kuenezwa, ao habari zenye hazina musingi zenye kutolewa ku vyombo vya habari. b (Soma Waefeso 4:14, 15.) Anaweza kuwa na muelekeo wa kusikilia wengine wivu, wa kukosa kuelewana na wengine, kukasirika haraka, ao kuangukia mu jaribu.—1 Ko. 3:3.

6. Ni mufano gani unaweza kutusaidia kuelewa namna mutu anafikia kukomaa kiroho? (Ona pia picha.)

6 Sawa vile tumeona, Maandiko inalinganisha kukomaa kiroho na kukomaa kimwili. Mutoto mudogo hakuwake na utambuzi, kwa hiyo iko na lazima mutu muzima amulinde na amuongoze. Kwa mufano, mama anaweza kukamata mukono wa mutoto wake mbele wavuke barabara. Wakati anaanza kukomaa, mama yake anaweza kumuruhusu avuke barabara yeye peke, lakini atamukumbusha aangalie pande zote mbele ya kuvuka. Wakati ule mutoto anakuwa mutu muzima, yeye mwenyewe atajua namna ya kuepuka hatari za mu barabara. Mutoto mudogo iko na lazima ya musaada wa mutu muzima ili aepuke hatari. Vilevile, mara mingi Mukristo mwenye angali mutoto kiroho anakuwaka na lazima ya musaada wa Wakristo wakomavu ili aweze kuepuka hatari za kiroho, na aweze kukamata maamuzi yenye hekima. Lakini wakati Mukristo mukomavu iko na lazima ya kukamata uamuzi, anachunguza kanuni za Biblia juu ajue mawazo ya Yehova kuhusu ile jambo na kisha anatenda kulingana na mambo yenye amejifunza.

Mukristo mwenye angali mutoto kiroho anapaswa kujifunza kukamata maamuzi yenye hekima kwa kutumia kanuni za Biblia (Ona fungu ya 6)


7. Wakristo wakomavu wako na lazima ya musaada wa wengine?

7 Ni kusema kama Mukristo mukomavu hawezi kuwa na lazima ya musaada wa mutu mwingine? Hapana, haiko vile. Wakati fulani Mukristo mukomavu anaweza kuwa na lazima ya kuomba musaada. Lakini iko tofauti na mutu mwenye hakomae kiroho mwenye anaweza kutazamia wengine wamuambie mambo ya kufanya ao wamukamatie uamuzi. Mukristo mukomavu yeye anaweza kufaidika na hekima na uzoefu wa wengine, lakini wakati uleule anatambua kama Yehova anapenda kila mutu ‘abebe muzigo wake mwenyewe.’—Gal. 6:5.

8. Ni mu njia gani Wakristo wakomavu kiroho wako tofauti?

8 Sawa vile watu wazima hawafanane kimwili, Wakristo wakomavu wanaweza kuonyesha mu njia tofauti sifa mbalimbali za Kikristo sawa vile hekima, uhodari, ukarimu, na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Zaidi ya ile, mu hali ileile, Wakristo wawili wenye kukomaa kiroho wanaweza kukamata maamuzi yenye haifanane. Lakini, hata kama ile maamuzi iko tofauti, yote inategemea Biblia. Inakuwaka vile zaidi sana mu mambo yenye kuhusu zamiri. Njo maana Wakristo wakomavu wanaepuka kuhukumu maamuzi ya wengine juu tu iko tofauti na yao. Lakini, wanajikaza kuendeleza umoja.—Ro. 14:10; 1 Ko. 1:10.

NAMNA GANI MUTU ANAFIKIA KUKOMAA KIROHO?

9. Mutu anakomaa kiroho bila kufanya kitu? Fasiria.

9 Bila kufanya jambo yoyote, mutoto anaweza kukomaa na kufikia kuwa mutu muzima kisha wakati. Lakini hakuna mutu mwenye anaweza kukomaa kiroho bila kufanya jambo yoyote. Kwa mufano, ndugu na dada katika Korinto walikubali habari njema, wakabatizwa, wakapokea roho takatifu, na kufaidika na mafundisho ya mutume Paulo. (Mdo. 18:8-11) Lakini, miaka fulani kisha kubatizwa, wengi wao walikuwa wangali watoto kiroho. (1 Ko. 3:2) Nini njo itatusaidia juu tusijikute mu hali sawa ya wale Wakristo wa Korinto?

10. Tunapaswa kufanya nini ili tukomae kiroho? (Yuda 20)

10 Ili tukomae kiroho, tunapaswa kwanza kuwa na nia ya kukomaa. Wale wenye “kupenda kukosa uzoefu,” wenye wanafurahia kubakia watoto kiroho, hawatafanya maendeleo. (Mez. 1:22) Hatupendi kuwa sawa watu wazima wenye wazazi wao wangali nakamatia maamuzi. Lakini, tunapenda kukamata mambo na mikono mbili na kuhangaikia siye wenyewe hali yetu ya kiroho. (Soma Yuda 20.) Kama ungali najikaza ili ufikie kukomaa kiroho, umuombe Yehova akupatie “hamu na pia nguvu za kutenda.”—Flp. 2:13.

11. Yehova anatutolea musaada gani ili tukomae kiroho? (Waefeso 4:11-13)

11 Yehova anatutolea musaada ili tufikie kukomaa kiroho. Wachungaji na walimu katika kutaniko ya Kikristo wamezoezwa ili kusaidia Wakristo wakuwe ‘wenye kukomaa kabisa’ kiroho, “na kufikia kipimo cha ukomavu kamili cha Kristo.” (Soma Waefeso 4:11-13.) Yehova anatutolea pia roho yake takatifu ili itusaidie kuwa na “akili ya Kristo.” (1 Ko. 2:14-16) Zaidi ya ile, Mungu ametupatia vitabu ine vya Injili vyenye kuzungumuzia utumishi wake ku dunia. Vinatusaidia kujua namna ya Yesu ya kufikiri, kusema, na kutenda. Kama unaiga namna ya Yesu ya kufikiri na kutenda, unaweza kufikia muradi wako wa kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho.

NAMNA CHAKULA KIGUMU KINATUSAIDIA

12. “Fundisho la musingi juu ya Kristo” ni nini?

12 Ili tufikie kukomaa kiroho, tunapaswa pia kuacha “nyuma fundisho la musingi juu ya Kristo,” ni kusema mafundisho ya musingi ya Kikristo. Ile mafundisho inatia ndani fundisho kuhusu kutubu, imani, ubatizo, na ufufuo. (Ebr. 6:1, 2) Ile mafundisho ni musingi wa Ukristo. Njo maana mutume Petro aliizungumuzia wakati alikuwa nahubiria watu wengi siku ya Pentekoste. (Mdo. 2:32-35, 38) Ili tukuwe wanafunzi wa Kristo, tunapaswa kukubali ile mafundisho ya musingi. Kwa mufano, mutume Paulo alionya kama mutu yeyote mwenye anakataa fundisho ya ufufuo, anakana imani yote ya Ukristo. (1 Ko. 15:12-14) Lakini, hatupaswe tu kuishia ku kweli za musingi za Biblia.

13. Tunapaswa kufanya nini ili tufaidike na chakula kigumu chenye kuzungumuziwa mu Waebrania 5:14? (Ona pia picha.)

13 Tofauti na mafundisho ya musingi, chakula kigumu kinatia ndani kanuni za Yehova, hapana tu sheria zake. Zile kanuni zinatusaidia kuelewa mawazo ya Yehova. Juu tufaidike na ile chakula ya kiroho, tunapaswa kujifunza, kutafakari, na kutumikisha kwa uangalifu mambo yenye tunajifunza mu Neno ya Mungu. Wakati tunafanya vile, tunajizoeza kukamata maamuzi yenye inamufurahisha Yehova. cSoma Waebrania 5:14.

Chakula kigumu cha kiroho kinatusaidia tujue namna ya kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova (Ona fungu ya 13) d


14. Namna gani Paulo alisaidia Wakorinto wakomae kiroho?

14 Mara mingi Wakristo wenye wangali watoto kiroho hawajuake wafanye nini wakati wanakutana na hali zenye zinaomba kufikiria kanuni za Biblia na kuzitumikisha. Kama mu Biblia hamuna sheria yenye inahusu hali yao, wamoja wanaweza kuona kama wako huru kufanya jambo yoyote yenye wanapenda. Wengine wanaweza kuomba sheria iwekwe kwenye haiko lazima kufanya vile. Kwa mufano, inawezekana Wakristo katika Korinto waliomba Paulo awapatie sheria kuhusu kula ao kutokula chakula yenye ilitolewa kwa sanamu. Kuliko kuwaambia mambo ya kufanya, Paulo aliwaambia kama kila mumoja wao alikuwa na “haki ya kuchagua” kwa kutegemea mambo yenye zamiri yake inamuruhusu kufanya. Alitumia kanuni zenye zingesaidia kila mutu aendelee kuwa na zamiri safi na wakati uleule asikwaze wengine. (1 Ko. 8:4, 7-9) Kwa kufanya vile, Paulo alikuwa nasaidia Wakorinto wakomae kiroho ili waweze kutumia nguvu zao za utambuzi kuliko kutegemea watu wengine ao kutafuta tu sheria.

15. Namna gani Paulo alisaidia Wakristo Waebrania wakomae kiroho?

15 Mambo yenye Paulo aliandikia Wakristo Waebrania inaweza kutufundisha mambo mingi ya maana. Wakristo fulani Waebrania hawakuendelea kukomaa kiroho; walikuwa ‘wamerudia nyuma na kuwa tena na lazima ya maziwa, hapana ya chakula kigumu [cha kiroho].’ (Ebr. 5:12) Walishindwa kujipatanisha na kweli za mupya, zenye zilikuwa zinafunuliwa kupitia kutaniko. (Mez. 4:18) Kwa mufano, Wakristo fulani Wayahudi walikuwa wangali wanatetea Sheria ya Musa hata kama kulikuwa kumepita miaka 30 tangu ile sheria iondolewe kwa musingi wa zabihu ya Kristo. (Ro. 10:4; Tit. 1:10) Kusema kweli, miaka 30 ilikuwa ya kutosha ili Wakristo Wayahudi wabadilishe mawazo yao! Mutu yeyote mwenye amesoma barua yenye kuongozwa na roho ya Mungu yenye Paulo aliandikia Waebrania, anaweza kukubali kama ile kitabu iko na chakula kigumu cha kiroho. Mambo yenye kuwa mu ile kitabu njo yenye wale Wakristo walikuwa nayo lazima ili waamini kama mupango wa ibada ya Kikristo ni wa hali ya juu zaidi, na ili wakuwe na uhodari wa kuendelea kuhubiri hata kama Wayahudi wenzao walikuwa wanawapinga.—Ebr. 10:19-23.

EPUKA KUJITUMAINIA KUPITA KIASI

16. Zaidi ya kufanya maendeleo ili kukomaa kiroho, tunapaswa kufanya nini ingine?

16 Tunapaswa kujikaza kufikia kuwa watu wakomavu kiroho, lakini pia tunapaswa kuendelea kuwa wakomavu. Ili kufanya vile hatupaswe kujitumainia kupita kiasi. (1 Ko. 10:12) Tunapaswa ‘kuendelea kujijaribu’ ili kuhakikisha kama tunaendelea kufanya maendeleo.—2 Ko. 13:5.

17. Namna gani barua yenye Paulo aliandikia Wakolosai inaonyesha kama ni jambo ya lazima tuendelee kuwa wakomavu?

17 Mu barua yake kwa Wakolosai, Paulo anakazia tena kama ni jambo ya maana kuendelea kuwa wakomavu kiroho. Hata kama Wakolosai walikuwa watu wazima kiroho, Paulo aliwaambia wakuwe waangalifu ili wasidanganywe na mawazo ya ulimwengu. (Kol. 2:6-10) Epafra pia, mwenye inaonekana alijua muzuri Wakristo wa ile kutaniko, alisali siku zote ili ‘mwishowe wasimame wakiwa kamili,’ ni kusema wenye kukomaa kiroho. (Kol. 4:12) Ile inatufundisha nini? Paulo na Epafra walielewa kama ili tuendelee kuwa wakomavu kiroho, tuko na lazima ya musaada wa Mungu na tunapaswa kujikaza sana. Walipenda Wakolosai waendelee kuwa wakomavu ao watu wazima kiroho, hata wapambane na magumu gani.

18. Ni nini inaweza kufikia Mukristo mwenye kukomaa kiroho? (Ona pia picha.)

18 Paulo alionya Waebrania kama ingewezekana Mukristo mukomavu afanye mambo yenye itafanya Yehova asimukubali tena. Moyo wa Mukristo unaweza kufikia kuwa mugumu sana mupaka anafikia hatua yenye hawezi tena kutubu na kusamehewa na Mungu. Jambo ya kufurahisha ni kwamba Waebrania walikuwa hawayafikia ile hatua. (Ebr. 6:4-9) Tuseme nini leo kuhusu Wakristo wenye hawakukuwa natenda tena ao walikuwa wametengwa na kutaniko kisha wakafikia kutubu? Juu walitubu kwa unyenyekevu, ile inaonyesha kama wako tofauti na wale wenye Paulo alizungumuzia. Lakini, wakati wanamurudilia Yehova, wako na lazima ya musaada wenye anawatolea. (Eze. 34:15, 16) Wazee wa kutaniko wanaweza kukamata mipango ili Shahidi mwenye kuwa na uzoefu awasaidie wakuwe tena nguvu kiroho.

Yehova anatolea musaada wale wenye wako na lazima ya kutia tena nguvu hali yao ya kiroho (Ona fungu ya 18)


19. Tunapaswa kuwa na muradi gani?

19 Kama uko najikaza ili kuwa Mukristo mukomavu, unaweza kufikia ule muradi! Endelea kutumia chakula kigumu cha kiroho na kujikaza ili namna yako ya kuwaza ikaribie zaidi mawazo ya Yehova. Na kama tayari uko Mukristo mukomavu, usirudie nyuma, endelea vile.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho maana yake nini?

  • Namna gani tunaweza kukomaa kiroho?

  • Juu ya nini tunapaswa kuepuka kujitumainia kupita kiasi?

WIMBO 65 Fanya Maendeleo!

a Hata kama Maandiko ya Kiebrania haitumie maneno “wakomavu,” na “wenye hawako wakomavu,” inatumia maneno ingine yenye iko na ileile wazo. Kwa mufano, kitabu ya Mezali, inaonyesha tofauti kati ya mutu mwenye kuwa kijana na bila uzoefu na mutu mwenye kuwa na hekima na uelewaji.—Mez. 1:4, 5.

b Ona “Ukuwe Muangalifu juu Wasikudanganye” mu sehemu “Habari Zingine” ku jw.org na ku JW Library.®

c Ona habari “Pendekezo juu ya Mambo ya Kujifunza” mu hii gazeti.

d MAELEZO YA PICHA: Wakati ndugu iko nachagua mambo ya kujifurahisha nayo, anatumia kanuni zenye alijifunza mu Neno ya Mungu.