Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Uzaifu Wangu Umetukuza Nguvu za Mungu

Uzaifu Wangu Umetukuza Nguvu za Mungu

WAKATI miye na bibi yangu tulifika Kolombia mu 1985, mu ile inchi mulikuwa jeuri mingi sana. Mu miji, serikali ilikuwa inapiganisha vikundi vya kuuzisha dawa za kulewesha na ku milima ilikuwa napiganisha maaskari waasi. Mu eneo ya Medellín, kwenye tulitumikia wakati fulani, vikundi vya vijana wenye silaha vilikuwa fasi yote. Wale vijana walilazimisha watu wawalipe ili kulindwa, na pia walilipwa ili waue watu.

Namna gani watu wawili wa kawaida wa kutoka Finlandi, moja kati ya inchi zenye kuwa kaskazini zaidi mwa dunia, walijikuta mu Amerika ya Kusini? Na nimejifunza mambo gani kadiri miaka imepita?

WAKATI NILIKUWA KIJANA KATIKA FINLANDI

Nilizaliwa mu mwaka wa 1955. Tulizaliwa watoto wanaume tatu na miye njo nilikuwa wa mwisho. Nilizaliwa karibu na eneo ya pembeni ya bahari kusini mwa Finlandi, mu eneo yenye leo inaitwa muji wa Vantaa.

Mama yangu alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova miaka fulani mbele nizaliwe. Baba yangu alipinga kweli na hakuruhusu mama ajifunze na siye Biblia ao atupeleke ku mikutano. Kwa hiyo mama alikuwa natufundisha mafundisho ya musingi ya Biblia wakati baba hakukuwa.

Niliazimia kumutii Yehova wakati nilikuwa na miaka saba

Tangu utoto niliamua kumutii kabisa Yehova. Kwa mufano, wakati nilikuwa na miaka saba, mwalimu wangu mwanamuke alikasirika sana kwa sababu nilikataa kula verilättyjä (aina fulani ya keki ya watu wa Finlandi yenye kuwa ndani damu). Alinifungula kinywa kinguvu na mukono moya, kisha kwa kutumia kanya, akajaribu kunitia ile keki mu kinywa. Niliweza kuangusha ile kanya kutoka ku mukono wake.

Wakati nilikuwa na miaka 12, baba yangu alikufa. Kisha pale nilianza kuenda ku mikutano. Ndugu mu kutaniko walinihangaikia sana na ile ilinichochea nifanye maendeleo ya kiroho. Nilianza kusoma Biblia kila siku na kujifunza kwa uangalifu vichapo vya Kikristo. Ile ilinisaidia nibatizwe wakati nilikuwa na miaka 14, tarehe 8, Mwezi wa 8, 1969.

Muda mufupi kisha kumaliza masomo nilianza kazi ya upainia. Kisha majuma fulani nilihamia mu eneo yenye ilikuwa na lazima ya wahubiri katika Pielavesi, karibu na eneo ya katikati mwa Finlandi.

Katika Pielavesi, nilikutana na dada mwenye kuitwa Sirkka, mwenye alifikia kuwa bibi yangu. Sifa yake ya kiasi na hali yake ya kiroho vilinivutia. Hakutafuta kujulikana ao kuwa na vitu mingi vya kimwili. Siye wote tulipenda kumutumikia Yehova kwa nguvu yetu yote na tulikuwa tayari kutimiza mugao wowote wenye tungepewa. Tulioana tarehe 23 Mwezi wa 3, 1974. Kuliko kuenda mu mapumuziko kisha ndoa, tulienda Karttula, kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme.

Nyumba yenye tulikuwa nalipia katika Karttula, Finlandi

YEHOVA ALITUHANGAIKIA

Gari yenye kaka yangu alitupatia

Tangu tu kuoana, Yehova alionyesha kama atahangaikia mahitaji yetu ya kimwili kama tunatia Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Kwa mufano, katika Karttula, hatukukuwa na gari. Ku mwanzo tulisafiri kwa kutumia kinga. Lakini mu kipindi ya baridi ilikuwa nguvu kufanya vile juu kulikuwa baridi mingi sana. Ili kuhubiria eneo kubwa ya kutaniko tulikuwa na lazima ya gari, lakini hatukukuwa na makuta ya kuiuza.

Bila kutazamia, mukubwa yangu alitutembelea na alitupatia gari yake. Alikuwa alishalipa assurance. Tulipaswa tu kuuza carburant. Vile njo tulipata gari.

Yehova alionyesha kama ilikuwa daraka yake kuhangaikia mahitaji yetu ya kimwili. Siye tulipaswa tu kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza.

MASOMO YA GILEADI

Darasa yetu ku Masomo ya Mapainia mu 1978

Wakati tulikuwa nasoma Masomo ya Mapainia mu 1978, ndugu Raimo Kuokkanen, a mumoja kati ya walimu wetu, alitutia moya tujaze fomu ya Gileadi. Kwa hiyo tulianza kujifunza Kiingereza ili tuweze kusoma ile masomo. Lakini mu 1980, mbele tujaze fomu, tulialikwa ku biro ya tawi ya Finlandi. Ile wakati Wanabeteli hawakuruhusiwa kujaza fomu ya Gileadi. Lakini tulipenda kumutumikia Yehova fasi kwenye yeye mwenyewe anachagua, hapana kwenye siye tunapenda. Kwa hiyo tulikubali mualiko. Lakini tuliendelea kujifunza Kiingereza juu kama nafasi inajitokeza tuweze kujaza fomu ya Gileadi.

Miaka kidogo kisha pale, Baraza Yenye Kuongoza iliruhusu wanabeteli pia kujaza fomu ya Gileadi. Mara moya tulijaza fomu, haiko juu hatukufurahia Beteli lakini tulipenda kuonyesha kama tuko tayari kutumikia fasi yoyote yenye kuwa na lazima kubwa ikiwa tungekubaliwa. Tulialikwa ku Gileadi na tulipewa diplome ku darasa ya 79 mu Mwezi wa 9, 1985. Kisha tukatumwa Kolombia.

MUGAO WETU WA KWANZA MU KAZI YA UMISIONERE

Katika Kolombia, mugao wetu wa kwanza ulikuwa kutumikia ku biro ya tawi. Nilijikaza sana kutumikia mugao wangu, lakini kisha kufanya mwaka moya ku biro ya tawi niliona kama nilikuwa na lazima ya kubadilishwa mugao. Kwa mara ya kwanza mu maisha yangu, niliomba mugao mwingine, na ile njo ilikuwa ya kwanza na ya mwisho ninafanya vile. Kisha pale, walitupatia mugao wa kuenda kuhubiri mu muji wa Neiva, mu eneo ya Huila.

Ninapendaka sana kazi ya kuhubiri. Wakati nilikuwa siyaoa na niko painia katika Finlandi, wakati fulani nilikuwa nahubiri kuanzia asubui mupaka mangaribi. Kisha kuoana, wakati fulani miye na Sirkka tulikuwa napitisha siku muzima mu mahubiri. Wakati tulikuwa nahubiri mu maeneo ya mbali, wakati fulani tulikuwa nalala mu gari yetu. Ile ilifanya tusipitishe wakati mingi mu safari za kuenda na kurudia na ilisaidia tuanze mahubiri asubui siku ya kufuata.

Juu tulikuwa napitisha tena wakati mingi mu mahubiri, tulisikia tena furaha yenye tulikuwa nasikia zamani mu mahubiri. Watu waliongezeka mu kutaniko yetu na ndugu na dada zetu wa Kolombia walikuwa wenye heshima, wenye upendo na wenye shukrani.

SALA IKO NA NGUVU

Pembeni-pembeni ya muji wa Neiva kulikuwa maeneo yenye haikukuwa na Mashahidi. Nilihangaishwa sana juu ya namna habari njema itafika mu ile maeneo. Lakini kwa sababu ya waasi, haikukuwa salama kwa mutu mwenye haiko wa mu ile eneo kuenda kule. Kwa hiyo nilisali ili mutu wa kutoka mu ile maeneo afikie kuwa Shahidi wa Yehova. Niliwaza kama iliomba ule mutu aishi Neiva ili ajifunze kweli. Kwa hiyo, nilisali pia kama kisha ule mutu kubatizwa, akomae kiroho na arudie mu eneo yake ili kuhubiri. Lakini sikujua kama Yehova alikuwa na mipango ya muzuri zaidi kunipita.

Muda mufupi kisha pale, nilianza kujifunza Biblia na kijana mwanaume mwenye kuitwa Fernando González. Alikuwa anaishi Algeciras, mu eneo moya kati ya ile maeneo yenye haikukuwa na Mashahidi. Fernando alikuwa anasafiri zaidi ya kilometre 50 ili kuja kutumika mu muji wa Neiva. Alikuwa anatayarisha muzuri kila funzo na bila kukawia akaanza kuhuzuria mikutano yote. Kuanzia tu juma ya kwanza yenye alianza kujifunza Biblia, Fernando alikuwa nakusanya watu wa mu eneo yake na kuwafundisha mambo yenye alijifunza mu funzo yake ya Biblia.

Niko na Fernando mu 1993

Fernando alibatizwa Mwezi wa 1, 1990, miezi sita kisha kuanza kujifunza. Kisha pale akakuwa painia wa kawaida. Juu kulikuwa sasa Shahidi mu Algeciras, biro ya tawi iliona kama ilikuwa sasa salama kutuma mapainia wa pekee mu ile eneo. Mu Mwezi wa 2, 1992, kutaniko ilianzishwa mu ile eneo.

Fernando alihubiri tu mu muji wake? Hapana. Kisha kuoa, yeye na bibi yake walihamia San Vicente del Caguán, muji mwingine wenye haukukuwa na Mashahidi. Kule walisaidia kuanzisha kutaniko. Mu 2002, Fernando aliwekwa kuwa mwangalizi wa muzunguko, na yeye na bibi yake Olga wanaendelea kufanya kazi ya muzunguko mupaka leo.

Ile mambo ilinifundisha kama ni jambo ya maana kutaya waziwazi katika sala mambo mbalimbali kuhusu mugao wetu. Yehova anafanyaka mambo yenye siye hatuna uwezo wa kufanya. Ile haitushangaze juu hii kazi ya mavuno ni yake, haiko yetu.—Mt. 9:38.

YEHOVA ALITUPATIA “HAMU NA PIA NGUVU ZA KUTENDA”

Mu 1990 tulitumwa mu kazi ya kusafiri. Muzunguko wetu wa kwanza ulikuwa Bogotá, muji mukubwa wa Kolombia. Ule mugao ulituogopesha. Miye na bibi yangu tulikuwa tu watu wa kawaida wenye hawakukuwa na uwezo fulani wa pekee. Na hatukuzoea kuishi mu muji wenye kuwa na watu wengi sana. Lakini Yehova alitimiza ahadi yake yenye kuwa mu Wafilipi 2:13: “Mungu ndiye kwa ajili ya mapenzi yake mema anawachochea ninyi, na kuwapatia hamu na pia nguvu za kutenda.”

Kisha tulitumwa mu muzunguko wenye ulikuwa mu eneo ya Medellín, muji wenye nilizungumuzia ku mwanzo. Watu wa kule walizoea sana jeuri na haikukuwa tena inawashitua. Kwa mufano, siku fulani wakati nilikuwa naongoza funzo ya Biblia, masasi ilianza kulia inje ya nyumba ya mutu mwenye nilikuwa najifunza naye. Nilikuwa karibu kulala chini, lakini mwanafunzi wa Biblia yeye aliendelea tu kusoma fungu sawa tu vile hakuna kitu. Wakati alimaliza kusoma, akaniomba atoke kidogo kisha akaenda inje. Kisha wakati fulani akarudia na watoto wawili wadogo, na kwa utulivu akaniambia, “unisamehe, nilipaswa kutafuta watoto wangu.”

Kuko wakati ingine yenye tulikuwa mu hatari. Kwa mufano, siku fulani wakati tulikuwa mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba, bibi yangu alikuya na iko nakimbia na mwenye kuogopa sana. Aliniambia kama mutu fulani alitaka kumupiga masasi. Ile ilinitetemesha. Lakini tulifikia kuelewa kama ule mutu hakukuwa napenda kumupiga Sirkka masasi; alikuwa njo napiga masasi mwanaume mwingine mwenye alikuwa napita karibu na Sirkka.

Kisha wakati, ile jeuri haikutuogopesha tena sana. Mufano wa Mashahidi wa ile eneo wenye walipambana na ile hali na hata hali za nguvu zaidi ulitutia moyo. Tuliona kama ikiwa Yehova alikuwa nawasaidia, angetusaidia na siye. Kila mara tulisikiliza mashauri ya wazee, tulikamata mipango juu ya kujilinda na tuliacha mambo ingine mu mikono ya Yehova.

Lakini hali fulani hazikukuwa hatari sawa vile tuliwazia. Siku moya nilisikia sawa vile wanamuke wawili wako wanatukanana inje ya nyumba yenye nilikuwa natembelea. Sikupenda kuenda kuangalia ile mabishano, lakini mwenye-nyumba aliniita mu veranda yake. Nilifikia kutambua kama ile “mabishano” ilikuwa kati ya kasuku wawili wenye walikuwa wanaiga sauti ya majirani.

MAPENDELEO INGINE NA PIA MAGUMU

Mu 1997, niliwekwa kuwa mwalimu ku Masomo ya Huduma ya Ufalme. b Tangu zamani ninafurahiaka sana masomo mbalimbali za kiteokrasi. Lakini sikuwaziaka kama siku fulani nitakuwa na pendeleo ya kufundisha ku masomo fulani ya kiteokrasi.

Kisha wakati, niliwekwa kuwa mwangalizi wa wilaya. Wakati tengenezo iliamua kama hakutakuwa tena waangalizi wa wilaya, nilirudia mu kazi ya muzunguko. Kwa hiyo, kwa zaidi ya miaka 30, nimekuwa na pendeleo ya kuwa mwalimu na mwangalizi mwenye kusafiri. Ile migao imeniletea baraka mingi sana. Lakini mambo haikukuwa mwepesi kila wakati. Juu ya nini?

Ninakuwaka na utu wenye nguvu. Ile imenisaidia kupambana na hali fulani za nguvu. Lakini, wakati fulani nimeonyesha bidii kupita kiasi wakati nilikuwa najaribu kurekebisha mambo mu kutaniko. Kuko wakati wenye nilipatia ndugu mashauri makali kuhusu kuonyeshana upendo na kuwa na usawaziko, lakini jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, ni mu wakati za vile njo miye mwenyewe nilikosa zile sifa.—Ro. 7:21-23.

Wakati fulani nimevunjika moyo sana kwa sababu ya uzaifu wangu. (Ro. 7:24) Na hata niliambia Yehova mu sala kwamba ilikuwa muzuri zaidi niache mugao wangu wa umisionere na nirudie Finlandi. Ile mangaribi nilienda ku mikutano. Mambo yenye nilisikia ku ile mikutano ilinitia moyo sana na ilinihakikishia kama nilipaswa kubakia mu mugao wangu na kujikaza ili kupiganisha uzaifu wangu. Mupaka leo ninaguswa moyo sana wakati ninafikiria namna Yehova alijibia waziwazi ile sala. Zaidi ya ile, niko mwenye shukrani juu ya namna amenisaidia kwa upendo kupiganisha uzaifu wangu.

NIKO HAKIKA KAMA MAMBO ITAENDELEA KUWA MUZURI

Miye na Sirkka tuko wenye shukrani sana kwa Yehova juu ya pendeleo yenye tumekuwa nayo ya kupitisha miaka mingi ya maisha yetu mu utumishi wa wakati wote. Niko pia mwenye shukrani sana kwa Yehova kwa kunipatia bibi mwenye upendo na muaminifu mwenye nimetumika naye mu hii miaka yote.

Karibuni nitaeneza miaka 70 na kwa hiyo sitakuwa tena mwalimu na mwangalizi wa muzunguko. Lakini ile hainivunje moyo. Juu ya nini? Juu ninaamini kabisa kama jambo yenye inamutukuza Yehova ni kumutumikia kwa kiasi na kumusifu kwa moyo wenye kuchochewa na upendo na shukrani. (Mik. 6:8; Mk. 12:32-34) Ili kumutukuza Yehova, haiko lazima tukuwe na pendeleo fulani ya pekee.

Wakati ninafikiria migao yenye nimetumikia, ninatambua kama haiko juu nilikuwa mutu wa maana kupita wengine njo nilipata ile migao, na haiko juu nilikuwa na uwezo fulani wa pekee. Lakini ni juu Yehova alinionyesha fazili zake zenye hazistahiliwe. Alinipatia ile migao hata kama nilikuwa na uzaifu mbalimbali. Ninajua kwamba ni kwa musaada wa Yehova tu njo nimeweza kutimiza ile migao. Ni mu ile njia njo uzaifu wangu umetukuza nguvu za Mungu.—2 Ko. 12:9.

a Habari kuhusu maisha ya Raimo Kuokkanen yenye kichwa, “Tuliazimia Kumtumikia Yehova,” ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 4, 2006.

b Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme njo imekamata nafasi ya ile masomo.