Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

Namna ya Kufanya Sala Zetu Zikuwe Muzuri Zaidi

Namna ya Kufanya Sala Zetu Zikuwe Muzuri Zaidi

“Mumwange mioyo yenu mbele yake.”​—ZB. 62:8.

WIMBO 45 Mawazo ya Moyo Wangu

KIFUPI YA HABARI a

Kila mara tunaweza kumukaribia Yehova katika sala na kutafuta muongozo wake mu maisha yetu ya kila siku (Ona fungu ya 1)

1. Yehova anaomba waabudu wake wafanye nini? (Ona pia picha.)

 TUNAWEZA kusali kwa nani wakati tuko na lazima ya faraja na muongozo? Tunajua jibu ya ile ulizo. Tunaweza kusali kwa Yehova Mungu. Ile njo jambo yenye anatuomba tufanye. Anapenda tusali kila mara, ni kusema, ‘tusali bila kuacha.’ (1 Te. 5:17) Tunaweza kusali kwake na kutafuta muongozo wake mu maisha yetu ya kila siku. (Mez. 3:5, 6) Juu ni Mungu mukarimu, hatuambie ni mara ngapi tunaweza kusali kwake.

2. Tutaona nini mu hii habari?

2 Tunasamini sana zawadi ya sala. Lakini, juu tunakuwaka na mambo mingi ya kufanya, inaweza kuwa nguvu kupata wakati wa kusali. Tena, tunaweza kuona kama ni lazima tufanye sala zetu zikuwe muzuri zaidi. Jambo ya kufurahisha, tunaweza kupata vitia-moyo mingi na muongozo mu Biblia. Mu hii habari, tutaona namna tunaweza kupanga wakati wa kusali kwa kuchunguza mufano wa Yesu. Tutaona mambo tano ya maana yenye tunaweza kutia mu sala zetu ili zikuwe muzuri zaidi.

YESU ALIPANGA WAKATI WA KUSALI

3. Yesu alielewa nini kuhusu sala?

3 Yesu alielewa kama Yehova anakuwaka anasamini sala. Zamani, mbele akuye ku dunia aliona namna Baba yake alijibia sala za wanaume na wanamuke waaminifu. Kwa mufano, Yesu alikuwa pembeni ya Baba yake wakati alijibia sala ya Hana, Daudi, Eliya, na wengine, zenye walitoa kwa moyo wote. (1 Sa. 1:10, 11, 20; 1 Fa. 19:4-6; Zb. 32:5) Njo maana Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali kila mara na kwa uhakika!​—Mt. 7:7-11.

4. Sala za Yesu zinatufundisha nini?

4 Kupitia sala zake, Yesu aliwekea wanafunzi wake mufano. Mu utumishi wake, alisali kila mara. Alipaswa kupanga wakati wa kusali juu kila mara alikuwa na mambo mingi ya kufanya na alizungukwa na watu wengi. (Mk. 6:31, 45, 46) Alikuwa nalamuka asubui sana juu apate nafasi ya kuwa yeye peke ili kusali. (Mk. 1:35) Kwa zaidi ya mara moya, alisali usiku wote mbele ya kukamata uamuzi fulani wa maana. (Lu. 6:12, 13) Na usiku mbele akufe, alisali tena na tena mbele amalize sehemu ya nguvu ya mugao wake hapa ku dunia.​—Mt. 26:39, 42, 44.

5. Tunaweza kufanya nini ili kumuiga Yesu?

5 Mufano wa Yesu unatufundisha kama, hata ikiwa tuko na mambo mingi ya kufanya tunapaswa kupanga wakati wa kusali. Sawa vile Yesu, tunaweza kupanga wakati wa kusali, kwa mufano, tunaweza kulamuka asubui sana ao kulala nyuma kidogo usiku. Kama tunafanya vile, tunaonyesha Yehova kama tunasamini ile zawadi ya pekee. Dada Lynne anakumbuka namna alikuwa mwenye shukrani wakati alijifunza kwa mara ya kwanza juu ya pendeleo ya sala. Anasema hivi: “Wakati nilijifunza kama naweza kusali kwa Yehova wakati wowote, ile ilinisaidia nimuone kuwa rafiki yangu wa karibu sana na nipende kufanya sala zangu zikuwe muzuri zaidi.” Bila shaka, wengi kati yetu wanaonaka vile. Kwa hiyo, tuone mambo tano ya maana yenye tunaweza kutia mu sala zetu.

MAMBO TANO YA MAANA YENYE TUNAWEZA KUTIA MU SALA

6. Kulingana na Ufunuo 4:10, 11, Yehova anastahili kupokea nini?

6 Umusifu Yehova. Mu maono yenye kushangaza, mutume Yohana aliona wazee 24 mbinguni na wako namuabudu Yehova. Walimusifu na kusema kama anastahili kupokea “utukufu na heshima na nguvu.” (Soma Ufunuo 4:10, 11.) Malaika waaminifu wako pia na sababu mingi za kumusifu na kumuheshimia Yehova. Wako mbinguni pamoya naye na wamefikia kumujua muzuri. Wanaona sifa zake kupitia mambo yenye anafanya. Wakati wanaona namna Yehova iko natenda, ile inawachochea kumusifu.​—Yob. 38:4-7.

7. Tunaweza kumusifu Yehova juu ya mambo gani?

7 Siye pia tunapenda kumusifu Yehova mu sala zetu, kuonyesha mambo yenye tunapenda na mambo yenye tunafurahiaka kwake. Wakati unasoma na kujifunza Biblia, ujikaze kujua sifa za Yehova zenye unapendaka sana. (Yob. 37:23; Ro. 11:33) Kisha, umuambie namna unajisikiaka juu ya zile sifa. Tunaweza pia kumusifu juu anatusaidiaka na juu anasaidiaka pia ndugu na dada zetu Wakristo. Kila mara anatuhangaikiaka na anatulindaka.​—1 Sa. 1:27; 2:1, 2.

8. Ni sababu gani zenye zinafanya tumushukuru Yehova? (1 Watesalonike 5:18)

8 Umushukuru Yehova. Tuko na sababu mingi za kumushukuru Yehova mu sala. (Soma 1 Watesalonike 5:18.) Tunaweza kumushukuru juu ya jambo yoyote ya muzuri yenye tuko nayo. Zaidi ya ile, zawadi yote ya muzuri inatokaka kwake. (Yak. 1:17) Kwa mufano, tunaweza kumushukuru juu ya dunia na juu ya vitu vya muzuri vyenye aliumba. Tunaweza pia kumushukuru juu ya uzima wetu, familia yetu, marafiki wetu, na tumaini yetu. Na tunapenda pia kumushukuru Yehova juu anaturuhusu tukuwe marafiki wake.

9. Juu ya nini ni muzuri kumushukuru Yehova?

9 Inaweza kuwa muzuri kujikaza sana ili kufikiria sababu zenye zinatufanya siye kipekee tumushukuru Yehova. Tunaishi mu dunia yenye watu wengi hawakuwake na shukrani. Mara mingi watu wanahangaikia mambo yenye wanapenda kuliko kuhangaikia mambo yenye wanaweza kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye wako nayo. Kama na siye tunaanza kuwa vile, tutakuwa nasali Yehova juu tu ya kumuomba mambo fulani. Juu ya kuepuka ile, tunapaswa kuendelea kumushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye anatufanyiaka.​—Lu. 6:45.

Kumushukuru Yehova kunaweza kutusaidia kuvumilia (Ona fungu ya 10)

10. Namna gani kumushukuru Yehova kulisaidia dada moya avumilie? (Ona pia picha.)

10 Kuwa wenye shukrani kunaweza kutusaidia kuvumilia magumu. Fikiria mufano wa Kyung-sook, wenye kupatikana mu habari yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 1, 2015. Walimupata na kansere ya mapafu. Alisema hivi: “Ile magumu ya afya ilinivunja moyo sana. Nilisikia sawa vile nilipoteza kila kitu na niliogopa sana.” Nini njo ilimusaidia kuvumilia? Alisema kama, kila usiku mbele ya kuenda kulala, alikuwa naenda ku sehemu ya yulu ya nyumba yao na kusali kwa sauti ili kumushukuru Yehova juu ya mambo tano yenye alimufanyia ile siku. Ile ilimufanya atulie na ilimuchochea aonyeshe upendo wake kwa Yehova. Alifikia kuelewa kama Yehova anasaidiaka watumishi wake waaminifu wakati wa majaribu na kama baraka zenye tunapataka ni mingi zaidi kuliko majaribu. Sawa vile Kyung-sook, tuko na sababu mingi za kumushukuru Yehova hata kama tuko mu magumu. Kumushukuru Yehova katika sala kunaweza kutusaidia kuvumilia magumu na kuendelea kuwa wenye kutulia.

11. Juu ya nini wanafunzi wa Yesu walikuwa na lazima ya uhodari kisha yeye kurudia mbinguni?

11 Umuombe Yehova uhodari wa kuhubiri. Wakati kidogo tu mbele Yesu arudie mbinguni, alikumbusha wanafunzi wake mugao wao wa kutoa ushahidi juu yake “katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8; Lu. 24:46-48) Wakati kidogo kisha pale, viongozi Wayahudi walifunga mitume waaminifu, Petro na Yohana, na kuwapeleka mbele ya Sanhedrini. Kisha waliwakataza kuhubiri na hata waliwaogopesha. (Mdo. 4:18, 21) Petro na Yohana walitenda namna gani?

12. Kulingana na Matendo 4:29, 31, wanafunzi walifanya nini?

12 Kisha viongozi wa dini ya Wayahudi kuogopesha wanafunzi, Petro na Yohana walisema hivi: “Kama ni jambo lenye kuwa sawa mbele ya macho ya Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko kumusikiliza Mungu, muamue ninyi wenyewe. Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.” (Mdo. 4:19, 20) Kisha Petro na Yohana kufunguliwa, wanafunzi walisali kwa Yehova ili kufanya mapenzi yake. Walisali hivi: “Uwezeshe watumwa wako waendelee kutangaza neno lako bila woga wowote.” Yehova alijibia ile sala ya kutoka ku moyo.​—Soma Matendo 4:29, 31.

13. Mufano wa Jin-hyuk unaweza kutufundisha nini?

13 Tunaweza pia kuiga wanafunzi wa Yesu kwa kuendelea kuhubiri hata kama wenye mamlaka wanatukataza kufanya vile. Fikiria mufano wa ndugu Jin-hyuk, mwenye alikatala kuingia mu kazi ya jeshi. Mu gereza, walimupatia kazi ya kuhangaikia wafungwa fulani wenye walifungwa mu chumba wao peke. Lakini hawakumuruhusu kuongea nao jambo yoyote yenye haihusiane na ile kazi na walimukataza hata kuongea nao juu ya Biblia. Alimuomba Yehova amupatie uhodari na hekima juu aweze kuhubiri mu kila nafasi yenye inajitokeza. (Mdo. 5:29) Anasema hivi: “Yehova alijibia sala zangu kwa kunipatia uhodari na hekima ya kuanzisha mafunzo mingi ya Biblia ya dakika tano. Kisha, usiku nilikuwa naandika barua zenye nilipatia wafungwa siku ya kufuata.” Siye pia tuko hakika kama Yehova atatusaidia kutimiza utumishi wetu. Sawa vile Jin-hyuk, tunaweza kumuomba Yehova uhodari na hekima.

14. Unaweza kufanya nini wakati uko napambana na magumu? (Zaburi 37:3, 5)

14 Umuombe Yehova akusaidie ili uvumilie magumu. Wengi kati yetu wako napambana na magumu ya kimwili ao ya kihisia, magumu ya kupoteza mupendwa wao, magumu fulani mu familia, mateso, ao magumu ingine. Na mambo sawa vile, magonjwa ya kuambukiza na vita imefanya ikuwe nguvu kuvumilia magumu mingi kati ya ile. Umufungulie Yehova moyo wako. Umuambie hali yako sawa vile tu unaweza kumuambia rafiki yako wa karibu sana. Ukuwe hakika kama Yehova “atatenda kwa ajili yako.”​—Soma Zaburi 37:3, 5.

15. Namna gani sala inaweza kukusaidia ‘uvumilie chini ya taabu’? Leta mufano.

15 Kuendelea kusali kutakusaidia ‘uvumilie chini ya taabu.’ (Ro. 12:12) Yehova anajua mambo yenye watumishi wake wako napambana nayo. “Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.” (Zb. 145:18, 19) Kristie, painia mwenye kuwa na miaka 29 aliona ile jambo kuwa ya kweli. Bila kutazamia, alianza kugonjwa magonjwa ya nguvu sana. Ile ilifanya ashuke moyo sana. Kisha, aliambiwa kama mama yake alikuwa na ugonjwa wenye ungemufikisha tu ku kifo. Kristie anasema hivi: “Nilisali sana kwa Yehova juu anipatie nguvu yenye nilikuwa nayo lazima kila siku. Nilijikaza kuheshimia programu ya kiroho kwa kuhuzuria mikutano na kufanya funzo ya pekee.” Anasema tena hivi: “Mu ile wakati ya nguvu, sala njo ilinisaidia nivumilie. Nilijua kama kila mara Yehova alikuwa pamoya na miye na ile njo ilinisaidia nitulie. Hata kama magumu yangu ya afya haikuisha palepale, Yehova alijibia sala zangu kwa kunipatia amani ya moyo.” Tusisahau hata kidogo kama ‘Yehova anajua namna ya kukomboa kutoka katika jaribu watu wenye ushikamanifu kwake.’​—2 Pe. 2:9.

Ili kupinga jaribu, (1) umuombe Yehova akusaidie, (2) utende kulingana na sala zako, na (3) utie nguvu uhusiano wako pamoya na Yehova (Ona fungu ya 16-17)

16. Juu ya nini tunapaswa kumuomba Yehova atusaidie ili tupinge jaribu?

16 Umuombe Yehova akusaidie ili upinge jaribu. Juu hatukamilike, kila mara tunapaswa kupinga jaribu ya kufanya mambo ya mubaya. Shetani iko nafanya yake yote ili ikuwe nguvu kwetu kufanya vile. Juu ya kuchafua akili yetu, anatumia mambo ya kujifurahisha ya mubaya. Ile mambo inaweza kufanya akili yetu iyale mawazo ya mubaya, ni kusema, mawazo yenye itatuchafua na yenye inaweza kutuchochea kufanya zambi nzito.​—Mk. 7:21-23; Yak. 1:14, 15.

17. Juu tupinge jaribu tunaweza kufanya mambo gani ili kutenda kulingana na sala zetu? (Ona pia picha.)

17 Tuko na lazima ya musaada wa Yehova kama tunapenda kupinga jaribu ya kufanya mambo ya mubaya. Yesu alitia hii maneno mu sala yake ya mufano: “Usituingize katika jaribu, lakini utukomboe na ule muovu.” (Mt. 6:13) Yehova anapenda kutusaidia, lakini tunapaswa kumuomba afanye vile. Tunapaswa pia kutenda kulingana na sala zetu. Tunapaswa kufanya yetu yote ili kuepuka kusoma na kusikiliza habari yenye kuwa na mawazo ya mubaya yenye inaenea mu hii dunia ya Shetani. (Zb. 97:10) Tunaweza kujaza akili yetu na mawazo ya muzuri kwa kusoma na kujifunza Biblia. Kuhuzuria mikutano na kuhubiri kutalinda pia mawazo yetu. Na Yehova anatuahidi kama hataacha tujaribiwe kupita vile tunaweza kuvumilia.​—1 Ko. 10:12, 13.

18. Siye wote tunapaswa kufanya nini?

18 Juu tuendelee kuwa waaminifu kwa Yehova mu hizi siku za mwisho zenye kuwa nguvu, tunapaswa kusali sana. Kila siku upange wakati wa kufanya sala ya kutoka ku moyo. Yehova anapenda ‘tumwange mioyo yetu mbele yake’ katika sala. (Zb. 62:8) Umusifu Yehova na umushukuru juu ya mambo yote yenye anakufanyiaka. Umuombe akupatie uhodari wa kuhubiri. Umuombe akusaidie uvumilie magumu yoyote na upinge majaribu yoyote yenye unaweza kupata. Usiruhusu jambo ao mutu yeyote akuzuie kusali kwa Yehova kila mara. Sasa, Yehova anajibiaka sala zetu namna gani? Habari yenye kufuata itazungumuzia ile ulizo ya maana.

WIMBO 42 Sala ya Watumishi wa Mungu

a Tunapenda sala zetu zikuwe sawa vile barua yenye mutu anaandikia rafiki yake wa karibu sana kwa moyo wote. Lakini, kila mara haikuwake mwepesi kupata wakati wa kusali. Na inaweza kuwa nguvu kujua ni mambo gani yenye tutatia mu sala. Hii habari itazungumuzia hii mambo mbili ya maana.