Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

Uendelee Kutembea mu “Njia ya Utakatifu”

Uendelee Kutembea mu “Njia ya Utakatifu”

“Kutakuwa njia kubwa kule, . . . Njia ya Utakatifu.”​—ISA. 35:8.

WIMBO 31 Utembee Pamoja na Mungu!

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Wayahudi wenye waliishi Babiloni walipaswa kukamata uamuzi gani muzito? (Ezra 1:2-4)

 MUFALME alitoa tangazo! Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho mu Babiloni kwa miaka 70 hivi, walikuwa sasa huru kurudia mu inchi yao Israeli. (Soma Ezra 1:2-4.) Ni Yehova tu njo alifanya ile iwezekane. Juu ya nini tunasema vile? Juu kwa kawaida, Wababiloni hawakukuwa naachilia huru waamishwa wao. (Isa. 14:4, 17) Lakini, wakati mufalme mwenye alikuwa natawala mu Babiloni alitoshwa ku kiti, mufalme mwenye alianza kutawala pa nafasi yake aliambia Wayahudi warudie mu inchi yao. Kwa hiyo, kila Muyahudi, zaidi sana vichwa vya familia, alipaswa kukamata uamuzi: Kutoka Babiloni ao kubakia. Pengine haikukuwa mwepesi kuamua. Juu ya nini?

2 Juu wengi walikuwa walishazeeka, haikukuwa mwepesi kwao kufanya ile safari ya murefu. Na juu Wayahudi wengi walizaliwa mu Babiloni, walikuwa hawayaishi fasi ingine, waliona Israeli kuwa muji wa mababu zao. Pengine Wayahudi fulani walifikia kuwa matajiri sana mu Babiloni. Kwa hiyo, haingekuwa mwepesi kwao kuacha nyumba zao za muzuri ao biashara yenye walikuwa nafanya juu waende mu inchi yenye hawakujua.

3. Wayahudi waaminifu wenye wangerudia Israeli wangepata baraka gani?

3 Wayahudi waaminifu walijua kama ikiwa wanajikaza kabisa kurudia mu Israeli wangepata baraka mingi sana. Baraka kubwa sana yenye wangepata ni kurudisha ibada safi. Hata kama mu Babiloni mulikuwa mahekalu ya wapagani zaidi ya 50 ya Wababiloni, hamukukuwa hata hekalu moya ya Yehova. Na hamukukuwa hata mazabahu kwenye Waisraeli wangetolea zabihu zenye Sheria ya Musa iliomba na hamukukuwa makuhani wenye walipaswa kutoa zile zabihu. Zaidi ya ile, mu ule muji, watu wenye walikuwa naabudu miungu ya uongo walikuwa wengi sana kuliko wale wenye walitii Yehova ao kanuni zake. Kwa hiyo, maelfu ya Wayahudi wenye walikuwa namuogopa Mungu walikuwa natazamia kwa hamu kurudia mu inchi yao ili warudishe ibada safi.   

4. Yehova aliahidi kama angefanyia nini Wayahudi wenye wangerudia mu Israeli?

4 Safari ya kutoka Babiloni kuenda Israeli haikukuwa mwepesi, na ingekamata karibu miezi ine. Lakini, Yehova aliahidi kama atatosha vizuizi vyote vyenye vingefanya Waisraeli wasirudie muzuri. Isaya aliandika hivi: “Mufungue njia ya Yehova! Mufanye njia kubwa yenye kunyooka katika jangwa kwa ajili ya Mungu wetu. . . . Udongo wenye matuta-matuta unapaswa kufanywa kuwa tambarare, na udongo wenye majiwe-majiwe utakuwa bonde tambarare.” (Isa. 40:3, 4) Wazia hii jambo: Njia kubwa yenye kunyooka inapita mu jangwa. Kusema kweli, wale wenye wangetembea mule wangeifurahia! Ingekuwa mwepesi zaidi kwao kutembea mu ile njia kubwa yenye kunyooka kuliko kupanda milima na vilima ao kushuka mu mabonde. Tena, wangetembea mbio zaidi.

5. Njia kubwa ya mufano yenye ilikuwa kati ya Babiloni na Israeli ilipewa jina gani?

5 Leo, jina ao namba fulani njo inatambulishaka njia kubwa halisi. Njia kubwa ya mufano yenye Isaya alizungumuzia ilikuwa pia na jina. Aliandika hivi: “Kutakuwa njia kubwa kule, ndiyo, njia yenye kuitwa Njia ya Utakatifu. Mwenye haiko safi hatapita kwenye njia hiyo.” (Isa. 35:8) Ile ahadi ilikuwa na maana gani kwa Waisraeli? Na iko na maana gani kwetu leo?

MAANA YA “NJIA YA UTAKATIFU”​—ZAMANI NA LEO

6. Juu ya nini ile njia iliitwa takatifu?

6 Njia kubwa iliitwa “Njia ya Utakatifu.” Ile ni jina ya muzuri sana! Juu ya nini iliitwa takatifu? Juu mutu mwenye “haiko safi,” ni kusema, Muyahudi yeyote mwenye alikuwa na mwenendo mubaya, muabudu-sanamu, ao mutu mwenye alikuwa nafanya zambi zingine nzito hangeruhusiwa kuwa kati ya taifa ya Israeli. Wayahudi wenye wangerudia wangefanywa kuwa “watu watakatifu” kwa Mungu wao. (Kum. 7:6) Lakini, ile haikumanisha kama wale wenye walitoka Babiloni hawakukuwa na lazima ya kufanya mabadiliko ili kumufurahisha Yehova.

7. Ni mabadiliko gani yenye Wayahudi fulani walipaswa kufanya? Leta mufano.

7 Sawa vile tuliona, Wayahudi wengi walizaliwa mu Babiloni, na wengi walikuwa walishazoea namna fulani ya kufikiri ya Wababiloni na kanuni zao. Miaka mingi kisha kikundi ya kwanza ya Wayahudi kurudia Yerusalemu, Ezra alifikia kujua kama Wayahudi fulani walioa wanamuke wapagani. (Kut. 34:15, 16; Ezr. 9:1, 2) Kisha, Gavana Nehemia alishangaa wakati aliona kama watoto wenye walizaliwaka mu Israeli hawakujifunzaka hata luga ya Wayahudi. (Kum. 6:6, 7; Ne. 13:23, 24) Zamani, Biblia iliandikwa zaidi sana mu Kiebrania. Sasa, juu wale watoto hawakujua ile luga, namna gani wangejifunza kumupenda Yehova na kumuabudu? (Ezr. 10:3, 44) Kwa hiyo, wale Wayahudi walipaswa kufanya mabadiliko makubwa. Lakini, ingekuwa mwepesi zaidi kwao kufanya ile mabadiliko mu Israeli, mwenye ibada safi ilikuwa inarudishwa pole kwa pole.​—Ne. 8:8, 9.

Kuanzia 1919 K.K.Y., mamilioni ya wanaume, wanamuke, na watoto wametoka mu Babiloni Mukubwa na wameanza kutembea mu “Njia ya Utakatifu” (Ona fungu ya 8)

8. Juu ya nini mambo yenye ilitokea zamani iko pia na maana fulani kwetu leo? (Ona picha ku jalada.)

8 Watu fulani wanaweza kuwaza kama ‘ile yote ilikuwa tu mambo ya kufurahisha sana.’ ‘Lakini, ile mambo yenye ilifikia Wayahudi zamani, iko na maana fulani kwetu leo?’ Ndiyo, juu mu maana fulani, tuko natembea mu “Njia ya Utakatifu.” Ikuwe tuko watiwa-mafuta ao “kondoo wengine,” tunapaswa kubakia mu “Njia ya Utakatifu.” Ile njia itatusaidia tuendelee kumuabudu Yehova sasa na wakati wenye kuya, wakati Ufalme wa Mungu utafanya dunia ikuwe muzuri sana. b (Yoh. 10:16) Kuanzia 1919 K.K.Y., mamilioni ya wanaume, wanamuke, na watoto wametoka mu Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo, na wameanza kutembea mu ile barabara ya mufano. Pengine uko kati yao. Watu walianza kutembea mu ile barabara kumepita miaka 100 hivi, lakini wengine walianzaka kuitayarisha miaka mingi sana mbele ya pale.   

KAZI YA KUTAYARISHA BARABARA

9. Kulingana na Isaya 57:14, kazi ya kutayarisha “Njia ya Utakatifu” imefanywa namna gani?

9 Juu Wayahudi watoke mu Babiloni, Yehova alitosha vizuizi. (Soma Isaya 57:14.) Tuseme nini kuhusu “Njia ya Utakatifu” leo? Mamia ya miaka mbele ya 1919, Yehova alianza kutumia wanaume wenye kumuogopa juu wasaidie watu wengine watoke mu Babiloni Mukubwa. (Linganisha na Isaya 40:3.) Wale wanaume walifanya kazi ya maana ya kutayarisha barabara, ni kusema, barabara ya kiroho juu ya kusaidia watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri watoke mu Babiloni Mukubwa na waingie mu paradiso ya kiroho ili kumuabudu Yehova pamoya na watu wake. Tuzungumuzie mambo yenye ile kazi ya “kutayarisha barabara” inatia ndani.

Mamia ya miaka mbele ya 1919 K.K.Y., wanaume wenye kumuogopa Mungu walianza kusaidia watu wengine ili watoke mu Babiloni Mukubwa (Ona fungu ya 10-11)

10-11. Kazi ya kuchapisha na kutafsiri Biblia ilisaidia namna gani ujuzi wa Biblia uenee? (Ona pia picha.)

10 Kazi ya kuchapisha. Kopi za Biblia zilifanywa kwa mukono miaka fulani mbele, mupaka mwaka wa 1450 hivi. Ile kazi ilikamata wakati mingi. Ilikuwa nguvu kupata kopi za Biblia na zilikuwa bei sana. Lakini, wakati mashine ya kuchapisha ilianza kutumiwa juu ya kufanya kopi za Biblia, ilikuwa mwepesi zaidi kuchapisha Biblia mingi na kuzipatia watu.

11 Kazi ya kutafsiri. Kwa miaka mingi, Biblia ilipatikana tu mu Kilatini. Ni watu wenye walisoma sana tu njo walikuwa naelewa ile luga. Lakini, wakati kazi ya kuchapisha ilianza kufanywa sana, wanaume wenye walimuogopa Mungu walijikaza kuitafsiri mu luga mingi zenye watu walikuwa naongea. Kwa hiyo, wasomaji wa Biblia walianza kulinganisha mambo yenye walifundishwa na viongozi wa dini na mambo yenye Biblia inafundisha kabisa.

Wanaume wenye kumuogopa Mungu walianza kusaidia watu wengine ili watoke mu Babiloni Mukubwa (Ona fungu ya 12-14) c

12-13. Leta mufano wenye unaonyesha namna wanafunzi waaminifu wa Biblia walianza kuonyesha wazi mafundisho ya uongo mu miaka ya 1835.

12 Vichapo vya kusaidia kujifunza Biblia. Kusoma Neno ya Mungu kulisaidia wanafunzi waangalifu wajifunze mambo mingi. Lakini, viongozi wa dini walikasirika wakati waliona wale wanafunzi wanaanza kufundisha wengine mambo yenye walijifunza. Kwa mufano, mu miaka ya 1835, hesabu fulani ya wanaume waaminifu ilianza kutolea watu trakte zenye zilionyesha wazi mafundisho ya uongo ya makanisa mbalimbali.

13 Mu miaka ya 1835, Henry Grew, mwanaume mwenye kumuogopa Mungu, alitolea watu trakte yenye kuzungumuzia hali ya wafu. Mu ile trakte alitumia Maandiko ili kuonyesha kama kutokufa ni zawadi kutoka kwa Mungu, hakuna mutu mwenye anazaliwaka na ile zawadi, sawa vile makanisa mingi ilikuwa inafundisha. Mu 1837, mutumishi George Storrs alipata kopi ya ile trakte wakati alikuwa anatembeza train. Aliisoma, na akafikia kuwa hakika kama alipata kweli ya maana. Aliamua kuanza kuambia wengine mambo yenye alijifunza. Mu 1842, alitoa hotuba ya muzuri yenye sehemu mingi, yenye kichwa: “Uchunguzi​—Je, Waovu Ni Wasioweza Kufa?” Maandishi ya George Storrs ilimusadia kijana Charles Taze Russell.

14. Kazi ya kutayarisha barabara ya kiroho yenye ilifanywa zamani ilisaidia namna gani Ndugu Russell na wanafunzi wenzake wa Biblia? (Ona pia picha.)

14 Kazi ya kutayarisha barabara ya kiroho yenye ilifanywa zamani ilisaidia namna gani Ndugu Russell na wanafunzi wenzake wa Biblia? Wakati walikuwa wanajifunza, walichunguza diksionere fulani za Biblia, concordances, na tafsiri mbalimbali za Biblia zenye zilifanywaka mbele ya wakati wao. Zaidi ya ile, utafiti wa Biblia wenye Henry Grew, George Storrs, na wengine walifanyaka uliwasaidia pia. Uchunguzi wenye Ndugu Russell na wanafunzi wengine walifanya uliwasaidia waunge mukono kazi ya kutayarisha barabara ya kiroho kwa kutoa vitabu na trakte mingi zenye kuzungumuzia mambo yenye Biblia inafundisha.

15. Ni mambo gani ya maana yenye ilifanyika mu 1919?

15 Mu 1919, Babiloni Mukubwa haikukuwa tena na mamlaka juu ya watu wa Mungu. Mu ile mwaka, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” alianza kufanya kazi juu ya kusaidia watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri waanze kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” (Mt. 24:45-47) Kazi ya “kutayarisha barabara” yenye ilifanywa zamani ilisaidia wale wenye walianza kutembea mu njia kubwa wamujue Yehova muzuri zaidi na makusudi yake. (Mez. 4:18) Walianza pia kuishi kulingana na mapenzi ya Yehova. Lakini, Yehova hakutazamia watu wake wafanye mabadiliko yote mara moya. Kuliko kufanya vile, alianza kuwasafisha pole kwa pole. (Ona kisanduku “ Yehova Anasafisha Watu Wake Pole kwa Pole.”) Wazia namna siye wote tutakuwa na furaha wakati tutamufurahisha Mungu mu mambo yote!​—Kol. 1:10.

“NJIA YA UTAKATIFU” HAIYAFUNGWA

16. Ni kazi gani yenye imefanywa mu “Njia ya Utakatifu” kuanzia 1919? (Isaya 48:17; 60:17)

16 Juu barabara iendelee kuwa muzuri, inaombaka kuitengeneza kila mara. Kuanzia 1919, kazi yenye kufanywa mu “Njia ya Utakatifu” ingali inaendelea juu ya kusaidia watu wengi kadiri inawezekana watoke mu Babiloni Mukubwa. Kisha mutumwa muaminifu na mwenye busara kuwekwa, alianza kutumika. Na mu 1921, alitoa kichapo ya kusaidia wale wenye wanapendezwa wajifunze kweli yenye kuwa mu Biblia. Ile kichapo inaitwa La Harpe de Dieu, na ku mwisho walifikia kufanya kopi karibu milioni sita mu luga 36, na wengi walijifunza kweli kupitia ile kichapo. Hivi karibuni, tulipata kichapo ya mupya na ya muzuri yenye kuitwa Furahia Maisha Milele! ya kutusaidia kuongoza mafunzo ya Biblia. Mu hizi siku za mwisho, Yehova anaendelea kutumia tengenezo yake ili kutupatia maagizo yenye kutoka mu Neno yake juu tuendelee kutembea mu “Njia ya Utakatifu.”​—Soma Isaya 48:17; 60:17.

17-18. “Njia ya Utakatifu” itatufikisha wapi?

17 Tunaweza kusema kama wakati mutu anakubali kujifunza Biblia, anapata nafasi ya kuanza kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” Watu fulani wanatembeaka kidogo tu mu ile njia kubwa kisha wanaiacha. Wengine wanaazimia kuendelea kutembea mule mupaka wafike ku mwisho wa safari yao. Njo wapi?

18 Kwa wale wenye kuwa na tumaini ya kuenda mbinguni, “Njia ya Utakatifu” itawafikisha mu “paradiso ya Mungu” mbinguni. (Ufu. 2:7) Kwa wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi ku dunia, ile njia kubwa itawafikisha ku mwisho wa utawala wa miaka 1000 wa Kristo, wakati watu wote watakuwa wakamilifu. Leo kama uko natembea mu ile njia, tafazali, usiangalie nyuma na usiiache mupaka ufike ku mwisho wa safari yako, ni kusema, mu dunia mupya. Tunakutakia “safari njema.”

WIMBO 24 Tuende ku Mulima wa Yehova

a Yehova aliita njia kubwa ya mufano yenye ilitoka Babiloni mupaka Israeli kuwa “Njia ya Utakatifu.” Yehova alifungula pia njia kwa ajili ya watu wake leo? Ndiyo! Kuanzia 1919 K.K.Y., mamilioni ya watu walianza kutoka mu Babiloni mukubwa na kuanza kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” Siye wote tunapaswa kuendelea kutembea mu ile njia mupaka itufikishe ku mwisho wa safari yetu.

c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu Russell na wanafunzi wenzake walitumia vichapo vya kusaidia kujifunza Biblia vyenye vilifanywaka mbele ya wakati wao.